figganigga
Platinum Member
- Oct 17, 2010
- 26,662
- 59,100
Katika kuadhimisha miaka 33 ya Chadema mkoani Mbeya, kulipangwa kufanyika uzinduzi wa tawi la chama katika Kata ya Inyala pamoja na bonanza la kumbukizi. Hata hivyo, wakati wa uzinduzi wa kijiwe hicho, Polisi wakiongozwa na OCD wa Mbeya Vijiji walifika wakiwa na magari, wakawatawanya wananchi waliokuwa eneo la Stand ya Inyala na kuwakamata Masaga Kaloli, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Mbeya, Elisha Chonya, Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Mbeya pamoja na wanachama wengine.