Uchaguzi 2020 Mbeya na Iringa bado ngoma ngumu kwa CCM

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,050
50,997
MBEYA NA IRINGA BADO NGOMA NGUMU

Na, Robert Heriel

Kama kuna majimbo ambayo CCM itahangaika sana ni pamoja na Iringa Mjini, Mbarali, Mbeya Mjini, na Tunduma Mjini.

Kanda ya juu Kusini sasa ndio itakuwa kambi Rasmi ya Upinzani tofauti na sasa ambapo Kanda ya kaskazini mashariki yaani Arusha na Moshi Mjini.

Ni rahisi Kwa CCM kupata jimbo la la Moshi mjini na Arusha Mjini Kuliko Kuyapata Majimbo ya Iringa Mjini na Mbeya Mjini.
Sitashangaa kutokumuona Lema na mbunge atakayepeperusha bendera ya CHADEMA pale moshi mjini,

Tulia Ackson namuona kama Mpambanaji anayejaribu bahati yake, lakini uhakika ni kuwa hawezi kupata ubunge hapo Mbeya Mjini. Jimbo la Mbeya mjini ni gumu mno zaidi ya majimbo mengine. Sitashangaa Sugu akimshinda Tulia kwa kura zaidi ya elfu ishirini, hilo halitanishangaza kabisa.

Kitu pekee ambacho ninakiona katika majimbo hayo ni muitikio wa wanawake kwenye siasa pamoja na wanaume watu wazima. Nafahamu wanawake ndio wapiga kura wakubwa na watu wazima.

Mbeya Mjini na Iringa wakina mama ni wengi wanaoukubali Upinzani, kina baba ni wengi wanaoukubali upinzani. Achilia mbali vijana ambao kimsingi ndio wapinzani wenyewe lakini hawa wengi wao sio wapiga kura. Kina mama na wababa ukiona wanakusapoti basi kuwa na uhakika kwamba utashinda.

Arusha na Moshi Mjini kwa sasa inapoteza sifa yake, ni kama wameishiwa pumzi, nina uhakika jimbo moja kati ya Moshi mjini au Arusha mjini Mwaka huu lazima liende CCM. na kama Upinzani hawatakuwa makini wanaweza kupoteza majimbo yote mawili.

Kwa upande wa Mbowe pale Hai, mwaka huu atashinda lakini kwa Kura chache sana.

Majimbo mengine ambayo CCM itaonja joto la jiwe ni pamoja na Mikumi kwa Profesa Jay, Kigoma mjini, Tunduma, Tarime Vijijini, Bunda huyu atashinda kwa kura chache,

Majimbo ambayo yapo hati hati kuchukuliwa na CCM ni KAWE kwa Halima Mdee, Ubungo hili litachukuliwa asubuhi kabla magari yanayotoka Dar hayajafika morogoro. Kibamba hili nalo litachukuliwa mapema tuu.

CCM mwaka huu itachukua majimbo mengi ya Upinzani, lakini litashindwa kuchukua majimbo ya Iringa mjini na Mbeya mjini.

Kwa upande wa Jimbo la Singida mashariki alipokuwa Tundu Lisu, upinzani utachukua kwa kura chache.

Upande wa Urais, mgombea wa Upinzani, atachukua kura nyingi jimbo la Iringa Mjini, mbeya mjini, Mikumi, Kigoma mjini, kusini na kaskazini, Tarime vijijini, Bunda nusu nusu, Arusha mjini Nusu kwa Nusu, Moshi Mjini nusu kwa Nusu, Karatu mpinzani atashinda, Majimbo mengi ya Singida watagawana na CCM, Zanzibar upinzani utashinda ikiwa watasimamisha mgombea mmoja.

Kama Lisu atapitishwa na NEC atapigwa kwenye majimbo mengi na Magufuli, labda abadilishe mbinu hasa katika utoaji wa hotuba.

Ni ngumu Lisu kumshinda Magufuli lakini kama atabadili hotuba zake Lisu anaweza kushinda hata kwa kura laki moja.

Mambo ambayo Lisu lazima ayaongelee ili apewe kura na kumzidi Magufuli

1. Ajira kwa vijana na namna ya kuondoa umasikini
Lisu lazima awashawishi vijana ambao wengi kwa sasa hawana ajira, Lisu lazima atumie ushawishi mkubwa kuhakikisha anageuza nyoyo za vijana, aseme ataajiri vijana,

Hoja hii Atamzidi Magufuli kwa sababu ni wazi awamu hii Magufuli hajaajiri vijana wengi, hivyo kufanya vijana wengi kubaki mtaani wakiwa wamezubaa.

Magufuli hoja hii hawezi kuitumia kwani ataonekana anaongea uongo, tena ataonekana anawadharau vijana kwa kuongea uongo wa mchana kweupe. Najua hawezi kusema kuwa ataajiri akipewa tena, kwani vijana watamuambia kama ulishindwa kutuajiri awamu ya kwanza basi hata awamu ya pili utashindwa.

2. Nyongeza ya Mishahara, na kupanda madaraja.
Lisu anaweza akashinda, ikiwa atatoa maneno yenye kushawishi wafanyakazi na watumishi wa UMMA kuhusiana na nyongeza ya mishahara na kupanda vyeo.

Wafanyakazi wengi hawajaongezewa mishahara tangu Magufuli aingie madarakani, hakuna mtumishi anayelifurahia hili lakini watafanya nini ikiwa waliambiwa kama mshahara mdogo waache kazi.

Lisu lazima aeleze kuwa serikali isipoongeza mshahara inatengeneza mazingira hata kwa sekta binafsi kupunguza mishahara ya wafanyakazi wao.

Lisu lazima aseme kuwa endapo serikali haiajiri inasababisha thamani ya elimu kushuka, na wataalamu kulipwa ujira mdogo kwenye sekta binafsi.

Lisu lazima atoe mifano kuwa serikali inapogoma kuajiri inasababisha vijana wasomi kuwa cheap labor. Atoe mifano kuwa wapo wasomi wa ngazi ya shahada wanaolipwa laki moja, wengine wakijitolea kwenye sekta binafsi miaka nenda rudi wakisubiri ajira lakini mtoa ajira yupo kimya.

Lisu lazima azungumzie suala la vijana wa viwandani wanaolipwa chini ya laki themanini huku wakifanya kazi masaa kumi na mbili.

Hili magufuli kashindwa kulitolea maelezo, na penginde muda huo hana.

3. Unyonyaji wa wazungu
Lisu lazima azungumzie suala la makampuni ya kigeni yaliyokuja kuwekeza hapa nchini na namna yanavyolinyonya taifa hili.

Lisu hapaswi kukaa kimya kuwakemea wazungu.

Katika hili Magufuli amemzidi kwa mbali kabisa, Magufuli amejipambanua kwa kuwakemea wazungu, hata mimi namsapoti.

4. Uhuru wa Vyombo vya habari
Lisu katika hili namuona akijitahidi kulibeba, na linampa nguvu kubwa kwa watu wengi hasa wenye taaluma.

Magufuli hapa atashindwa kwani amekuwa nyuma katika hili wakati yeye anayomamlaka namba moja hapa nchini

5. Haki za Binadamu
Lisu katika hili kajidhatiti, nafikiri ni kwa vile yeye ni mwanasheria. Lisu lazima apigilie misumari kwa matukio ya kikatili ambayo yametokea nchi hii na vyombo husika havijafuatilia, matukio ya utekaji, mauaji, unyanyasaji, upendeleo miongoni mwa mambo mengine.

Lisu hili linambeba kwa watu wote wenye hofu ya Mungu, waasomi na watu wanaojua dunia ipo wapi.

Lisu atafeli katika hoja hii pale atakaposhindwa kueleza mipaka ya haki za binadamu ikiwa ni pamoja na haki ya ushoga, usagaji, umalaya, kutupa picha za uchi mitandaoni, ambapo kimsingi katika Hili Magufuli naye kajipambanua.

Lisu lazima atoke hadharani aseme kuwa tunapenda haki, lakini sio haki zinazovunja utu wa mwanadamu, aseme kuwa hataruhusu ushoga, wasagaji na wahuni kulingana na sheria za nchi yetu.

Lisu amezidiwa hapa na Magufuli kwa sababu Anashindwa kueleza kinagaubaga tena kwa ukali kuwa Ushoga ni kosa. Magufuli katika hili amemshinda. Na hili linambeba.

6. Kukemea na Kutokomeza Rushwa na Ufisadi.
Lisu lazima akemee Rushwa na Ufisadi. Lisu ni mwanasheria hivyo anajua ni kwa namna gani anaweza kulisaidia taifa hili kwa kutokomeza Rushwa na Ufisadi.

Lisu atachaguliwa na Watanzania kwa kukema Rushwa na Ufisadi.

Magufuli katika hoja ya Rushwa na Ufisadi amejidhatiti na kajitahidi kwa kiasi chake. Shida ya Magufuli ni pale ambapo hatuoni Fisadi yeyote aliyefungwa licha ya kuanzishwa kwa mahakama ya Ufisadi. Niliwahi sikia wapo waliwekwa rumande lakini baadaye waliambiwa walipe kisha watolewe. Hiyo binafsi ilinifanya nione kama igizo la kuchekesha.

Wezi wa kuku nao wangeambiwa warudishe kuku watolewe, wezi wa maduka, n.k
Hata hivyo siasa inamambo mengi, kwa umri wangu mengine pengine yakawa sio level yangu. Lakini kwa akili ya kawaida, jambo lile lilikuwa sio zuri.

7. Mahusiano Mazuri ndani ya Nchi na jumuiya za Kimataifa.
Lisu lazima aeleze kwa kina ni mahusiano yapi ayatakayo baina ya nchi yetu na mataifa mengine.

Magufuli katika hili kajidhatiti kikamilifu kuwa, yeye hana shida na taifa lolote, anahitaji uhusiano mzuri na mataifa mengine, lakini mahusiano hayo sharti yawe na maslahi kwa taifa letu. Hiyo nampa Tiki, hata mimi ningekuwa Rais ningefanya kama yeye, nchi kama inataka kukunyonya au kukulalia unaipiga mtama wa mchomvu. Lazima kuwe na mutual relationship.

Kuhusu Kuzikana, ni kweli MAGUFULI anafanya isivyo halali kutokwenda kwenye misiba ya wakubwa wenzake huko nchi za nje, lakini nami nasema sio kila msiba lazima aende, angalau msiba mmoja kwa misiba minne aende. Asipoenda kabisa inaonekana hana upendo, akienda kila msiba ataitwa Rais wa Misiba.

Kwa upande wa ndani ya nchi, Magufuli nimeshawahi kuona kwenye media viongozi kadhaa wa upinzani wakialikwa ikulu au pengine kwenda wao wenyewe. Magufuli anafanya vizuri katika hilo. Kuhusu CHADEMA kutoitwa Ikulu, kama hujaitwa IKULU na unalolote la kuongea na Rais, nini kilikuzuia, viongozi wa CHADEMA kama hamkuitwa Ikulu, mngepaswa muende ninyi. Hapa Magufuli hana makosa, vinginevyo awe aliwahi kufuatwa na viongozi wa CHADEMA akakata, kwa kweli hata mtanzania wa kawaida akisikia ataona Magufuli hajafanya vizuri.

Kuhusu Mikutano ya Kisiasa, ni kweli kabisa kuna muda wa siasa na muda wa kazi. Lakini hatuwezi kusahau kuwa wapo watu wamesomea taaluma ya siasa, yaani siasa kwao ni kazi. Kuwazuia vyama upinzani kufanya siasa kwa miaka karibu mitano wakati CCM tunawaona wakifanya mikutano yao hapa na pale haikuwa vizuri. Lisu katika hili watanzania wenye kupenda haki na wasomi watamuelewa.

8. MAENDELEO
Lisu lazima atuambie ni namna gani atatuletea maendeleo katika miundombinu, huduma za kijamii, kilimo, mawasiliano, viwanda, usafirishaji n.k

Magufuli katika hili kafanikiwa kwa asilimia kubwa. Hapa Magufuli hatatumia nguvu kubwa kwani tayari amefanya kwa kiasi maendeleo,
Magufuli kafanya yafuatayo kwa kipindi chake
1. SEKTA YA UCHUKUZI NA USAFIRISHAJI

1.1. RELI
>Kafufua reli ya kaskazini, DSM, Tanga, Moshi na Arusha. Hii niliipanda mwezi wa pili.
> Kujenga Reli ya Kisasa SGR, HII nami nimeikagua imefikia pazuri
> Kununua na kukarabati mabehewa na miundombinu ya Reli pamoja na Treni

1.2. NDEGE
> Kafufua shirika la ndege kwa kununua ndede za kisasa, Nadhani mpaka sasa Tangu aingie madarakani kanunua ndege 6.
> Kajenge Terminal 3 pale uwanja wa Julius kambarage Nyerere
> Kajenga uwanja wa Ndege Chato. Japo wapinzani wake wanakosoa vikali, lakini Chato pia ni Tanzania.

1.3. Barabara
> Magufuli kajenga barabara na kuzikarabati barabara nyingi hapa Tanzania

2. HUDUMA ZA KIJAMII
> Magufuli kajenga hospitali nyingi za wilaya na kuzikarabati. Japo kuna changamoto ya madaktari na madawa lakini atapongezwa na kila mtu muungwana kwa kufanaya hivyo.

> Magufuli chini ya serikali ya awamu yake, umeme umetambazwa kwa kiasi kikubwa vijijini, pia tatizo la umeme sio sana

> Maji, kwa sehemu kubwa hasa mjini serikali imejitahidi kuwapa wananchi maji. Lakini bado changamoto ni kubwa.

> Serikali imejitahidi kutoa elimu bure kwa ngazi ya msingi mpaka shule ya upili kidato cha nne. Pia madawati kwa sehemu za mjini kwa kiasi kikubwa. Lakini bado miundombinu ya elimu bado haijatengemaa. Lakini angalau amepagusia.

> Huduma za kipolisi, kwa kiasi kikubwa uhalifu wa unyang'anyi umepungua, vikundi vya uhalifu kama panya road, watoto wa Mbwa, vimedhibitiwa, hata changamoto ya kuel kibiti, mapango ya Amboni, Mwanza, kote kumedhibitiwa.
Kasoro kubwa ilikuwa utekaji ambapo kwa sehemu kubwa wapinzani wanaishutumu serikali.
Huduma za ulinzi imejitahidi sana, lakini kasoro ipo kwenye utekaji kwa watu wasiojulikana.

3. UTALII
3.1 Uanzishwaji wa TANZANIA SAFARI CHANEL
Kupitia chanel hii utalii wa nchi unatangazwa ndani na nje ya Tanzania, tunatangaza nchi yetu, hivyo utalii utakua. Lakini pia wapo watanzania wenzetu wamepata ajira pale.
Changamoto ya Chanel hii ni kuwa Hakuna ubunifu, mambo yanarudiwa yale yale kila siku utadhani hakuna mambo mengine. Nafahamu ubunifu uanenda sambamba na uwekezaji, serikali ihakikishe vijana wanakusanya taarifa za kuvutia ili zirushwe luningani.

3.2 Kuzipandisha hadhi mapori na kuwa hifadhi
> Serikali hii imepandisha hadhi baadhi ya mapori na kuwa hifadhi matahalani mapori ya akiba ya Burigi, Biharamulo na Kimisi. Manufaa yatakajikita katika uimarishaji wa utalii pamoja na ulinzi katika mapori hayo.
Pia kupitia upandishaji hadhi mapori hayo na kuwa hifadhi ajira zimezalishwa kwa watakaozihudumia hifadhi hizo.

Lisu hapaswi kuziponda kazi za Magufuli, katika hilo anakosea, na anatukosea watanzania hasa wale ambao hatuna mrengo wowote zaidi ya kuangalia maslahi ya nchi.

Lisu kuziponda kazi za Magufuli unapoteza baadhi ya kura kwa wale wanaoziona.

Lisu unapaswa uponde yale mapungufu aliyonayo Magufuli katika utendaji wake kwa kulitumikia taifa hili. Mimi naunga mkono mtu anayetenda haki, asiye na upendeleo.

Mtu asiye na mawe mawili ya kupimia, mtu asiye mnafiki.

Ninapenda Lisu na Magufuli washirikiane, iwe ni Lisu kashindwa au Magufuli kashindwa. Wote ni Watanzania.

Mbeya na Iringa bado kugumu

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
 
Kwa taarifa yako CHADEMA imeenea kote Tanzania hii, labda kasoro maeneo ya Pwani na Zanzibar, lakini huko Bara kote ni mali ya Chadema, subiri October utajionea.

Badala ya kusema Kanda ya Kaskazini inaenda kupotea kuwa ngome ya Chadema, ulitakiwa useme Chadema inaenda kuongeza ngome nyingine, nayo ni Nyanda za Juu Kusini.

Chama cha maajabu, kinachokua kila kukicha hata pasipo kufanya mikutano ya hadhara, hakika mbegu ikishaoteshwa ardhini hakuna wa kuizuia kuchipua.
 
Kwa taarifa yako Chadema imeenea kote Tanzania hii, labda kasoro maeneo ya Pwani na Zanzibar, lakini huko bara kote ni mali ya Chadema, subiri October utajionea.

Badala ya kusema Kanda ya Kaskazini inaenda kupotea kuwa ngome ya Chadema, ulitakiwa useme Chadema inaenda kuongeza ngome nyingine, nayo ni Nyanda za Juu Kusini.

Chama cha maajabu, kinachokua kila kukicha hata pasipo kufanya mikutano ya hadhara.

Sio kosa pale nilipoishia kusema uongeze na wewe Mkuu.

Tupo pamoja
 
Umejitahidi kueleza ila pale pa kusema huoni mafisadi wakifungwa jela Hapo umekosea kumshugulikia fisadi sio kumfunga tu ni kushughulika na Mali alizochuma kifisadi

Wengi wanalia biashara zao Magufuli kahakikisha zinakufa kifo Cha uhakika kwa kutumia mbinu za kisayansi

Wewe shahidi mafisadi mingi iliiba pesa serikalini ikajenga mihoteli na mi apartment Mbeya,Arusha, Morogoro,Dar nk ikitegemea tenda za serikali Sasa hivi mingi imefilisika na mingine kufariki dunia kwa pressure sababu serikali ilikata tenda zote

Mifisadi mingi ndio ilichangia Chadema 2015 uchaguzi huu haina pesa imeshughulikiwa barabara . Chadema waliipokea mifisadi Magufuli akaishughulikia barabara ikiwa huko huko Chadema ikarudi mingine mbio CCM ikitegemea labda atalegeza akakaza Uzi
Chadema mwaka huu haina pesa Baada ya Magufuli kuishughulikia mifisadi iliyoenda kujificha Chadema.Huko Kuna fisadi mmoja tu kabaki ambaye naye analiwa timing saaa yeyote atakiona Cha mtema kuni katulia akidhani kumetulia
 
Kwa taarifa yako CHADEMA imeenea kote Tanzania hii, labda kasoro maeneo ya Pwani na Zanzibar, lakini huko Bara kote ni mali ya Chadema, subiri October utajionea.

Badala ya kusema Kanda ya Kaskazini inaenda kupotea kuwa ngome ya Chadema, ulitakiwa useme Chadema inaenda kuongeza ngome nyingine, nayo ni Nyanda za Juu Kusini.

Chama cha maajabu, kinachokua kila kukicha hata pasipo kufanya mikutano ya hadhara, hakika mbegu ikishaoteshwa ardhini hakuna wa kuizuia kuchipua.
Mkoa wenye watu wajinga ni Dar na pwani watu wengi hawajitambui,wanawaza vigodoro,simba na yanga
 
Kiukweli umejitahidi Sana Sana kuandika uhalisia japo yapo maeneo hujayatendea haki .. chadema mikoa ya kaskazini itaendelea kupeta..na kuhusu suala la Lissu tutamshauri ajikite kwenye kuigusa jamii moja kwa moja ..ajira , kilimo , biashara na uhuru wa vyombo vya hbr ...kwa Sasa anakifanya ni kuwarudisha watanzania kwenye mode ya kiuchaguzi ...yote kwa yote nakupa big up
 
Kiukweli umejitahidi Sana Sana kuandika uhalisia japo yapo maeneo hujayatendea haki .. chadema mikoa ya kaskazini itaendelea kupeta..na kuhusu suala la Lissu tutamshauri ajikite kwenye kuigusa jamii moja kwa moja ..ajira , kilimo , biashara na uhuru wa vyombo vya hbr ...kwa Sasa anakifanya ni kuwarudisha watanzania kwenye mode ya kiuchaguzi ...yote kwa yote nakupa big up


Tupo Pamoja Mkuu
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom