JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Nimekutana na hili andiko kwenye mitandao yetu hii, naamini mamlaka zitatuambia ukweli wa hii kitu....
Anaandika Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mh. Siriel Mchembe👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿
Niimepokea taarifa kutoka kwa DC Rungwe Dkt. Vincent Anney kwamba alfajiri ya leo, Hakimu Joakim Mwakyolo wa Mahakama ya Wilaya hapa Handeni ameuawa na wananchi wenye hasira kali huko Busokelo Tukuyu/Rungwe.
Marehemu alikuwa likizo maana huko Rungwe ndipo anapotokea.
Chanzo cha kuuawa ni Mgogoro wa Ardhi kati yake na wanakijiji hicho anachotoka.
Alishindwa kesi ya ardhi Mahakama Kuu dhidi ya kijiji, lakini baada ya muda akaonekana kwenye eneo la Mgogoro akiwa ameongozana na Watu wawili.
Inadaiwa kuwa yeye na watu hao wawili kuna vitu walikuwa wanavichimbia ardhini kwenye eneo hilo la mgogoro jambo ambalo lilitafsiriwa na wanakijiji kwamba ni ushirikina.
Wananchi walipowazonga watatu hao na kuwahoji kuhusu suala hilo, ugomvi ukatokea kati yao, jambo lililopelekea mmoja wa watu waliokuwa na Hakimu huyo kuwapiga risasi wanakijiji wawili miguuni.
Baada ya hapo wananchi wakapandwa hasira na kumshambulia kwa mawe na silaha mbalimbali Hakimu huyo pamoja mmoja wa watu aliokuwa nao, huku mwingine akitoweka kuelekea kusikojulikana.
Hivyo vifo vilivyoripotiwa ni viwili. Hakimu pamoja na mmoja wa watu alikwenda nao kwenye eneo la mgogoro.
Pole sana Mhimili wetu wa Mahakama, hasa Hakimu wa Wilaya Handeni Mhe.Sabuni kwa kuondokewa na mtumishi huyu. Poleni ndugu zangu wa Handeni.
Tuwaombee pumziko la amani - Amina.
===================
TAARIFA RASMI YA MKUU WA WILAYA
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Dkt. Vincent Anney amesema “Ni tukio la kweli, Hakimu alikuwa na mgogoro na Wanakijiji, yeye si mwananchi wa Rungwe ila alinunua eneo Rungwe.
“Zamani baba yake alikuwa anaishi Rungwe akahamia Kyela, hata yeye Hakimu alizaliwa hukohuko Kyela. Hapo kati alianzisha mgogoro na wananchi akisema anataka eneo la babu yake lakini hiyo ni sehemu nyingine, si sehemu ambayo tukio limetokea.
“Eneo ambalo limesababisha auawe ni kubwa kuna karibia ekari 1000, ni msitu na ni hifadhi ambayo imekuwa ikisadia mvua, alinunua kinyemela, wananchi wakamshtaki Mahakamani.
“Akashindwa kesi, alikuwa katika harakati za kukata rufaa, kesi ikiwa imeisha akaenda shambani akiwa na watu wengine wawili akaanza kuchimbachimba, inasemakana alikuwa anachimba dawa.
“Yakatokea majibizano kati yake na Wananchi waliofika eneo hilo, akatoa bastola na kuwapiga risasi Wananchi wawili miguuni.
“Wananchi wakakasirika na kuanza kumpiga kisha kusababisha kifo chake pamoja na mmoja kati ya wale watu wawili alioongozana nao, mwingine mmoja alitokomea haijulikani alipokwenda.
“Tumeshawakamata watu kama saba hivi kutokana na tukio hilo na uchunguzi unaendelea.”
Anaandika Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mh. Siriel Mchembe👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿
Niimepokea taarifa kutoka kwa DC Rungwe Dkt. Vincent Anney kwamba alfajiri ya leo, Hakimu Joakim Mwakyolo wa Mahakama ya Wilaya hapa Handeni ameuawa na wananchi wenye hasira kali huko Busokelo Tukuyu/Rungwe.
Marehemu alikuwa likizo maana huko Rungwe ndipo anapotokea.
Chanzo cha kuuawa ni Mgogoro wa Ardhi kati yake na wanakijiji hicho anachotoka.
Alishindwa kesi ya ardhi Mahakama Kuu dhidi ya kijiji, lakini baada ya muda akaonekana kwenye eneo la Mgogoro akiwa ameongozana na Watu wawili.
Inadaiwa kuwa yeye na watu hao wawili kuna vitu walikuwa wanavichimbia ardhini kwenye eneo hilo la mgogoro jambo ambalo lilitafsiriwa na wanakijiji kwamba ni ushirikina.
Wananchi walipowazonga watatu hao na kuwahoji kuhusu suala hilo, ugomvi ukatokea kati yao, jambo lililopelekea mmoja wa watu waliokuwa na Hakimu huyo kuwapiga risasi wanakijiji wawili miguuni.
Baada ya hapo wananchi wakapandwa hasira na kumshambulia kwa mawe na silaha mbalimbali Hakimu huyo pamoja mmoja wa watu aliokuwa nao, huku mwingine akitoweka kuelekea kusikojulikana.
Hivyo vifo vilivyoripotiwa ni viwili. Hakimu pamoja na mmoja wa watu alikwenda nao kwenye eneo la mgogoro.
Pole sana Mhimili wetu wa Mahakama, hasa Hakimu wa Wilaya Handeni Mhe.Sabuni kwa kuondokewa na mtumishi huyu. Poleni ndugu zangu wa Handeni.
Tuwaombee pumziko la amani - Amina.
===================
TAARIFA RASMI YA MKUU WA WILAYA
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Dkt. Vincent Anney amesema “Ni tukio la kweli, Hakimu alikuwa na mgogoro na Wanakijiji, yeye si mwananchi wa Rungwe ila alinunua eneo Rungwe.
“Zamani baba yake alikuwa anaishi Rungwe akahamia Kyela, hata yeye Hakimu alizaliwa hukohuko Kyela. Hapo kati alianzisha mgogoro na wananchi akisema anataka eneo la babu yake lakini hiyo ni sehemu nyingine, si sehemu ambayo tukio limetokea.
“Eneo ambalo limesababisha auawe ni kubwa kuna karibia ekari 1000, ni msitu na ni hifadhi ambayo imekuwa ikisadia mvua, alinunua kinyemela, wananchi wakamshtaki Mahakamani.
“Akashindwa kesi, alikuwa katika harakati za kukata rufaa, kesi ikiwa imeisha akaenda shambani akiwa na watu wengine wawili akaanza kuchimbachimba, inasemakana alikuwa anachimba dawa.
“Yakatokea majibizano kati yake na Wananchi waliofika eneo hilo, akatoa bastola na kuwapiga risasi Wananchi wawili miguuni.
“Wananchi wakakasirika na kuanza kumpiga kisha kusababisha kifo chake pamoja na mmoja kati ya wale watu wawili alioongozana nao, mwingine mmoja alitokomea haijulikani alipokwenda.
“Tumeshawakamata watu kama saba hivi kutokana na tukio hilo na uchunguzi unaendelea.”