Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemshukia Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi maarufu Sugu kikimtaka asijisumbue kuchukua fomu ya kutetea nafasi hiyo mwaka 2015 kwasababu anachezea ubunge wake kutokana na kutumia muda mwingi kuchochea vurugu na maandamano badala ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Jiji la Mbeya.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Hapo kwenye red. Hivi kazi ya mbunge ni kuwaletea maendeleo wananchi??? Anapata wapi hizo pesa za kutekeleza miradi ya maendeleo? Au wabunge wanakusanya kodi kwenye majimbo yao siku hizi? Nadhani huu ni upotoshaji mkubwa ambao umekuwa ukifanywa kila siku na CCM. Serikali ndio inayokusanya kodi na ndio inawajibika kutekeleza miradi ya maendeleo katika nchi (including jimbo la mbunge).
Kazi ya mbunge inabaki ni kuhakikisha(kusimamia) serikali katika kuhakikisha inatekeleza mipango yake ya maendeleo na pia kukusanya kero za eneo husika na kuziwakilisha serikalini ili ziweze kufanyiwa kazi. Pia mbunge anawajibu kuhamasisha ushiriki wa wananchi wa jimbo lake(hata wale ambao hawakumpigia kura) kushiriki katika shughuli mbali mbali za maendeleo.
Nje ya hapo hata kama mbunge atakuwa mzuri kiasi gani lakini serikali ikaacha kutimiza wajibu wake basi hayo maendeleo itakuwa ndoto tu. Serikali haiwezi kujitoa katika kupeleka maendeleo kwa wananchi wake au kuurusha huu mzigo kwa mbunge.