Mbeya: CCM na Shitambala wamshukia Sugu

babalao 2

JF-Expert Member
Apr 6, 2012
5,398
3,244
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemshukia Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi maarufu Sugu kikimtaka asijisumbue kuchukua fomu ya kutetea nafasi hiyo mwaka 2015 kwasababu anachezea ubunge wake kutokana na kutumia muda mwingi kuchochea vurugu na maandamano badala ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Jiji la Mbeya.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (Nec), Sambwee Shitambala, amesema hayo jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari ikiwa ni siku mbili baada ya Sugu kumshambulia Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillip Mulugo kwa madai kwamba ana elimu ya kuungaunga.

Shitambala ambaye kabla ya kujiunga na CCM alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya, alisema Sugu tangu achaguliwe kazi yake kubwa imekuwa ni kuchochea vurugu, maandamano na kukashifu viongozi wa CCM na serikali na kusahau jukumu lake la msingi la kuwaletea maendeleo wapiga kura wake.

"Sugu anajisahau kuwa ubunge Mbeya amepewa kama zawadi kwa muda, mimi ndiye baba yake niliyempigia kampeni hadi akapata ubunge, elimu yake ya darasa la 12 asiitumie kukashifu viongozi wa CCM na serikali ambao wana elimu zaidi yake," alisema Shitambala.

Alisema hata hivyo hamshangai Sugu kujikita katika kuchochea vurugu kwasababu uwezo wake wa kufikiri mambo ya kuwaletea maendeleo wananchi waliomchagua umefikia kikomo sababu ubunge ameupata kama zawadi. Shitambala alisema kipimo kizuri kwa mbunge wa Mbeya mjini ni kuangalia katika kampeni za chaguzi ndogo alizoshiriki kupiga kampeni katika wilaya za Chunya, Kyela na Mbozi, zote Chadema wameshindwa.

"Sugu ameshafeli kisiasa sababu ameshindwa kutumikia wananchi, asiwe na haja ya kuchukua fomu kuwania mwaka 2015 atapa aibu, CCM Mbeya mjini tunatamani 2015 ifike hata leo Sugu ashuhudie tunavyompiga chini kwa kishindo,"alisema Shitambala.

Alisema mbunge wa Mbeya mjini lazima atambue kuwa wananchi walimchagua ili aweze kuwatatulia kero mbalimbali zinazowakabili lakini siyo kuchochea vurugu ambazo zinasababisha Jiji la Mbeya kukosa utulivu.

Hata hivyo Mbilinyi (CHADEMA), alisema hatishwi na kauli za viongozi wa CCM wanaodai majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani Mbeya, likiwamo la Mbeya Mjini yatarejeshwa mwaka 2015.


CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Shitambala ninamweshimu sana. Hata mzee wa upako ikimuonaga Mwanasheria huyu hawez kusema lolote. Sugu kama anaweza amjibu mwanasheria huyo kama alivyo mjibu Mlugo. 96% huyu jamaa ndiye aliyemweka Sugu pale.
 
Shitambala ninamweshimu sana. Hata mzee wa upako ikimuonaga Mwanasheria huyu hawez kusema lolote. Sugu kama anaweza amjibu mwanasheria huyo kama alivyo mjibu Mlugo. 96% huyu jamaa ndiye aliyemweka Sugu pale.

Kumsaidia mtu sio sababu ya kumtangaza kuwa umemsaidia.
Unajua nini kilimtoa Shitambala CHADEMA?
 
Shitambala ninamweshimu sana. Hata mzee wa upako ikimuonaga Mwanasheria huyu hawez kusema lolote. Sugu kama anaweza amjibu mwanasheria huyo kama alivyo mjibu Mlugo. 96% huyu jamaa ndiye aliyemweka Sugu pale.
Sugu tumemchagua wana Mbeya mjini kwa mapenzi yetu kwake. Shitambala hata kama ulimuweka Sugu, hukuingia mawazoni mwa wana mbeya mjini kumchagua kwa lazima. nina imani wana mbeya sio wajinga wa kununuliwa kwa kanga na kofia kama zamani ili watoe kura. Sugu piga kazi tupo nyuma yako. peoplezzzzzzz
 
Kama kuna mtu aliyeishiwa kisiasa hapa mbeya basi ni huyu jamaa anayeitwa shitambala!aliuza jimbo la mbeya vijijini mara2,na kama haitoshi akanunuliwa na kuhamia magamba.hizo ni hasira baada kuzomewa sana mwanjelwa!
 
Hivi Sitambala hayumo humu nimuulize maswali?

Cc - [MENTION]BAPUPEGHE[/MENTION]
 
Shitambala ninamweshimu sana. Hata mzee wa upako ikimuonaga Mwanasheria huyu hawez kusema lolote. Sugu kama anaweza amjibu mwanasheria huyo kama alivyo mjibu Mlugo. 96% huyu jamaa ndiye aliyemweka Sugu pale.

Kwa kuwa yeye ndie aliyemzawadia huo ubunge hakuona hizo kasoro za sugu?je huyo wa CCM naye atamzawadia?
 
Shitambala acha kujisumbua au kwa sababu na wewe umepewa zawadi ya UNEC.
 
Huyu shitambala haeleweki kiasi cha kutia shaka uanasheria wake kwani hajui kujenga hoja.Tunasikia soko la Mwanjelwa lilicheleweshwa kukamilika vile mkandarasi alipewa tenda kiccm,bado chama chake ndicho kinakusanya kodi halmashauri ya jiji kwa ajili ya kuleta maendeleo na zaidi hii ni mara ya kwanza mbunge wa upinzani kuonesha uhai wa siasa za Mbeya bungeni na nje ya bunge.Je, kuna majukumu gani na kwa ground zipi ambapo Mhe.Mbilinyi hatekelezi ili kuleta maendeleo?
 
Shitambala ninamweshimu sana. Hata mzee wa upako ikimuonaga Mwanasheria huyu hawez kusema lolote. Sugu kama anaweza amjibu mwanasheria huyo kama alivyo mjibu Mlugo. 96% huyu jamaa ndiye aliyemweka Sugu pale.

huyu jamaa shitambala naye si aligombea mbeya vijijini mbona alishindwa???? alimuwekaje sugu kama yeye mwenyewe alishindwa kujiweka??? acheni unafiki, plz muwage wakweli na unazi muwekage pembeni, huyo bwn anatwanga maji kwny kinu wanabaki kutapatapa.
 
Back
Top Bottom