Mbeya: CCM na Shitambala wamshukia Sugu

Mbeya: CCM na Shitambala wamshukia Sugu

CCM na shitmbara hawana jipya mbeya, ninanavyo wafahamu ndugu zangu wa mbeya wakisema no ni no
 
huyu jamaa shitambala naye si aligombea mbeya vijijini mbona alishindwa???? alimuwekaje sugu kama yeye mwenyewe alishindwa kujiweka??? acheni unafiki, plz muwage wakweli na unazi muwekage pembeni, huyo bwn anatwanga maji kwny kinu wanabaki kutapatapa.
Umeond eeh! Kwanza naona huyu mjinga shitambala bado hatujui vizur wana mbeya. Aje agombee aone.
 
Shitambala ninamweshimu sana. Hata mzee wa upako ikimuonaga Mwanasheria huyu hawez kusema lolote. Sugu kama anaweza amjibu mwanasheria huyo kama alivyo mjibu Mlugo. 96% huyu jamaa ndiye aliyemweka Sugu pale.
kwa hiyo kura yake moja ndio iliyompa ubunge?
 
ubunge kweli pipi hata sugu kaupata huyo hata ukisikiliza michango yake bungeni hamna kitu ni utumbo tu kweli CHADEMA mnatuchezea watanzania
 
wewe chitambala kweli chitambala ilikuaje kama mtu unasema ni darasa la 12 kwanini sasa ulimpigia debe wakati uliona uwezo wake ni mdogo? Huo ndiyo unafiki mkubwa wa nyie wana siasa wa CCM,so ulimpigia debe huku ukijua anauwezo mdogo? ina maana hata ndani ya chama mnaweza kumpigia debe mtu tena hata kama kiongozi mkubwa na huku mkijua kumbe ana uwezo mdogo! hicho ni kiwango cha juu kabisa cha Unafiki na usaliti mkubwa na ndiyo maana sisi wengine hatuwaamini wala hatutaki kuwasikiliza kabisa! sasa ona kitambala asivyo weza hata kufukiri anakuja kusema mbele za watu at the of the day anaonekana hajui hata kufikiri vizuri. Hata hivyo Rais Reagan wa Marekani alikua hana elimu ya degree lakini uliza alichoifanyia marekani, je jacob zuma wa South africa alisoma mpaka la ngapi? hata sekondary hakusoma lakini anaongoza taifa kubwa na wanamkubari, Hivyo point ya kwamba Sugu ni darasa la 12 ni ya kijinga kusemwa na Mtu anae dai yeye ni Mwanasheria huku akishindwa kufikiri vitu vidogo tu.
 
Eti anasema alimuweka sugu jimbo la mbeya mjini?cjampata sawasawa ina maana yy alipiga kura za kichawi?aliiangia mioyoni mwa wanambeya mjini na kuhakikisha wanachgua Sugu?
Me namshauri shitambala aaache ushamba na siasa za zamani,WAPIGA KURA MBEYA MJINI ndio waliomuweka SUGU hapo alipo na wao ndio watakao mtoa hapo na sio yy mnafiki.
 
Huyu mwanasheria anawazimu, hivi ni nani kamwambia kuna direct relationship kati ya level ya education na uongozi? huu ndio upuuzi unaowafanya wasomi wetu badala ya kubaki vyuoni kuandaa viongozi, wanaishia kukimbilia bungeni. Angalia leo hii prof mahiri darasani kama Muhongo alivyochemsha na kutia kichefuchefu kwenye swala la Mtwara. Mimi mpiga kura wa mbeya ninayeishi dar, nilimchagua sugu kama yeye na kama CDM, pengine angesimama huyu mamluki mwanashjeria ningepigia chama na sisi yeye kwa kuwa hana quality yoyote ya uongozi. Hivi mmewasahau wabunge wa southern highland mara tu baada ya uhuru wakina mzee yule wa Rungwe hivi walikua wana degree ngapi? sugu na mzee wa upako wanatuwakilisha sisi mara elfu kumi ya wakina shitambalaa na mulugu. Wewe jiulize umepataje UNEC wa chama kikongwa kama CCM kwa kuingia uanachama kwa kipindi cha less than 3 years? hii ni kawaida kweli? waliokitetea chama miaka yote hiyo hawapo? si ndio uko kupewa tu, sasa ulifikiri ukisema wewe juu ya sugu tutakuona babu kubwa? angekua mwanasheria mahiri angeingia bongo ndio kwenye hela, yeye akubali tu kuwa ni mwanasheria lakini hakuna umahiri wowote, wakina mahiri tumewaona, wakina Kimongono, Safari, Mgongolwa wanafanya mambo, wewe unafanya kibarua tu, Sugu hakuna wakukutisha, hapa swala sio kisomo, ni namna gani unaweza kulitumikia taifa lako, mulugu hukumtukana umemuelezea ni mtu gani, kwani je si kweli kwamba hajua Tanzania ni muungano wa nchi zipi? kwani hili ulisema wewe, small brain can never be changed by accumulating certificates, huhitaji kufika chuo kikuu kuwa na akili
 
Nahisi kama mnaendelea kuchezea akili za watu hapa vile, Shitambala alikua anagombea Mbeya Vijijini na alikua akiendelea na kampeni zake ili naye aingie Bungeni, sasa hapo ilikuaje achangia hizo % ulizoweka hapo mkuu, unaweza kuwa busy na chungu cha mwenzio while huna hakika na chungu chako? Guys let us by serious for sometimes, Chitambala tunajua kua alishinda uchaguzi ule kule vijijini lakini kiu na tamaa ya pesa akamfikisha hapo alipo leo, mikutano ya Sugu na Mbeya yake wote huwa tunaiona, watu wa Mbeya waliisha tamka kuwa Rais wao ni Sugu, kama issue ya maandamano, mbona kila wakati hua yanasababishwa na serikali yenyewe, rejea maandamano ya wamachinga wakati ule, mkono wa Sugu pale ulikua wapi? Kwanza alikua zake Dodoma, nakumbuka hadi jeshi liliingilia kati lakini Sugu alipofika tu from dodoma, mambo yakawa sawa, Wasomi type ya Shitambala ndio janga lenyewe la taifa, hawaelezi kiini cha tatizo, huangalia matumbo yao then na ubongo wanahamishia huko huko tumboni, Bora Form 4 ya Sugu kuliko degree za akina Shitambala, Mchemba, Nape na hata Amini! Sijaona impact za elim zao kwa nchi au hata sehemu ambazo wanakotoka, Nendeni Singida anakotoka bwana Chemba mwone.

Mkuu labda anataka kusema kukosa kwake ubunge ni kwa kuwa alichukua jukumu la kumuuza Sugu kwa wananchi kuliko kwake mwenyewe. Ofcourse haiwezi kuwa kweli!
 
Shitambala ninamweshimu sana. Hata mzee wa upako ikimuonaga Mwanasheria huyu hawez kusema lolote. Sugu kama anaweza amjibu mwanasheria huyo kama alivyo mjibu Mlugo. 96% huyu jamaa ndiye aliyemweka Sugu pale.

wapiga kura ndo wamemuweka Sugu pale.
Dua la kuku hili.
 
Kumbe huyo shitambala anataka kuwa KING MAKER wa mbeya hata Rostam aziz alijaribu kisha akasema ni siasa uchwara watu wameamka alifikiri ataenda na wengi ccm kumbe hola.
 
Hawa ndio watakaoamua, sio maneno ya jukwaani!

Mbeya.jpg
 
shitambala alishalogwa huyo hana lolote jipya.Linauza kura za watu kisa tumbo!!! Ole wake wacha makamanda tumuibukie.
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemshukia Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi maarufu Sugu kikimtaka asijisumbue kuchukua fomu ya kutetea nafasi hiyo mwaka 2015 kwasababu anachezea ubunge wake kutokana na kutumia muda mwingi kuchochea vurugu na maandamano badala ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Jiji la Mbeya.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (Nec), Sambwee Shitambala, amesema hayo jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari ikiwa ni siku mbili baada ya Sugu kumshambulia Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillip Mulugo kwa madai kwamba ana elimu ya kuungaunga.
Shitambala ambaye kabla ya kujiunga na CCM alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya, alisema Sugu tangu achaguliwe kazi yake kubwa imekuwa ni kuchochea vurugu, maandamano na kukashifu viongozi wa CCM na serikali na kusahau jukumu lake la msingi la kuwaletea maendeleo wapiga kura wake.
“Sugu anajisahau kuwa ubunge Mbeya amepewa kama zawadi kwa muda, mimi ndiye baba yake niliyempigia kampeni hadi akapata ubunge, elimu yake ya darasa la 12 asiitumie kukashifu viongozi wa CCM na serikali ambao wana elimu zaidi yake,” alisema Shitambala.
Alisema hata hivyo hamshangai Sugu kujikita katika kuchochea vurugu kwasababu uwezo wake wa kufikiri mambo ya kuwaletea maendeleo wananchi waliomchagua umefikia kikomo sababu ubunge ameupata kama zawadi. Shitambala alisema kipimo kizuri kwa mbunge wa Mbeya mjini ni kuangalia katika kampeni za chaguzi ndogo alizoshiriki kupiga kampeni katika wilaya za Chunya, Kyela na Mbozi, zote Chadema wameshindwa.
“Sugu ameshafeli kisiasa sababu ameshindwa kutumikia wananchi, asiwe na haja ya kuchukua fomu kuwania mwaka 2015 atapa aibu, CCM Mbeya mjini tunatamani 2015 ifike hata leo Sugu ashuhudie tunavyompiga chini kwa kishindo,”alisema Shitambala.
Alisema mbunge wa Mbeya mjini lazima atambue kuwa wananchi walimchagua ili aweze kuwatatulia kero mbalimbali zinazowakabili lakini siyo kuchochea vurugu ambazo zinasababisha Jiji la Mbeya kukosa utulivu.
Hata hivyo Mbilinyi (CHADEMA), alisema hatishwi na kauli za viongozi wa CCM wanaodai majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani Mbeya, likiwamo la Mbeya Mjini yatarejeshwa mwaka 2015.

CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
njaa mbaya sana
 
Sugu akuwekwaa shitambala ni wananchi wa mbeya mjini ndio waliomchagua,na waondoe wazo la kurudisha jimbo la mbeya mjini wakae wakijua kuna kizazi kipya kitakachopiga kura 2015 ambao hawajui ccm ni nini zaidi ya cdm..
 
Mkuu moja ya hoja ya kukosana na CDM huyu Advocate Shitambala ilikuwa ni kukubali matokeo ya jimbo alilogombea kupindishwa na hatimaye jimbo likachukuliwa na CCM,so kwa mujibu wa CDM Shitambala alishinda jimbo lile kiuhalali lakini akahongwa na ccm kukubali matokeo yapindishwe.

My take: Sugu alikosea sana kumzodoe Mulugo kwa kiwango chake cha elimu wakati yeye hata hiyo Digrii ya kuungaunga hana. Siasa za Bongo bana raha sana eti elimu ya darasa la 12 dah!!!!

Nikuulize Mwili Nyumba, vipi kuhusu Waheshimiwa Majimarefu, Komba, Lukuvi, n.k? Kwa maoni yangu Sugu yuko juu
 
Back
Top Bottom