Mbeya again! Soko lateketea kabisa mjini Tunduma

Mbeya again! Soko lateketea kabisa mjini Tunduma

Kwani Tz kunani? Mbona majanga yanatokea karhbia kila mwaka? Serikali imeshindwa kukabiliana nalo kabisa au haijaliona
 
wAdau habar nilizozipata ni kuwa kuwa soka la tunduma linaungua sasa iv hzi hbar nikutoka kwa mtu aliyeko huko mby tunduma soko hlo lipo karibu na police post tunduma jaman mby kunani?
 
Maduka yameteketea,bado moto unawaka kuna hatari ya soko lote kuteketea,magari ya zima moto yanajitahidi kuzima moto,waliko huko watujulishe zaidi.source ITV.
 
Soko kuu lililopo katika mji mdogo wa Tunduma uliopo mpakani mwa Tanzania na Zambia linateketea kwa moto hivi sasa. Chanzo cha moto hakijajulikana, ila inasemekana kulikuwa na matatizo ya umeume mchana wa leo, na watu wengi wa hapo sokoni walikuwa wamewasha majenereta. Juhudi za kuuzima zinaendelea, na hadi jirani wa Zambia wanasaidia kuuzima.
Source: Festo Sikagonamo wa ITV
 
kunani mbeya,na mioto ya masoko nini tafsiri yake?poleni wafanyabiashara mliofikwa na hasara.tunashukuru pia fire ya zambia kwa msaada katika kuzibiti moto huo
Source.itv breaknews
 
Sijajua kila baada ya soko kuungua huwa kinafuata nini katika eneo husika?
 
Poleni sana wana Tunduma. Mungu awe nanyi ktk huu wakati mgumu.
 
Hivi Mbeya kuna pepo la kuunguza masoko jamani? Mbona kila kukicha ni nyinyi tu?

Ni mpangilio mbovu unaosababishwa na mchanganyiko wa bidhaa mbalimbali zikiwepo za kulipuka.
 
moto mkali ulioanza Jana jumatatu jioni majira ya saa 9 alasiri umeteketeza kabisa soko kuu la mji wa Tunduma mpakani mwa Tanzania na Zambia mkoani mbeya. mji huu ambao ni maarufu kwa biashara za kimataifa una wafanya biashara wengi na Bidhaa za mamilioni ya fedha zimeteketea kabisa kwa moto ambao chanzo chake unasemekana kuwa ni moto ulioanzia katoka moja ya vibanda ndani ya soko hilo ambapo jenereta lililokuwa likifanyiwa majaribio lililipuka. (Taarifa sahihi za uhakikika wa chanzo na picha baadae kidogo). Huu ni msiba mkubwa sana. Mungu awape moyo wa uvumilivu wote waliofikwa na balaa hili.
 
It sounds like too much for only Mbeya!
All in all, poleni sana wana Tunduma kwa janga hilo!
 
Poleni waathirika. Masoko yote mkoani Mbeya yakate bima kubwa dhidi ya moto.
 
Kwa mujibu wa Michuzi blog, soko la tunduma limeteketea kwa moto, ambao chanzo chake bado hakijajulikana.
Bado system zetu za kubaliana na majanga hazijaweza kutatua kadhia hii ya moto katika masoko na mahali pengine.
Nawasilisha.
IMG00145-20111128-1718+%u002525281%2529.jpg IMG00156-20111128-1916.jpg IMG00147-20111128-1721.jpg
 
Back
Top Bottom