MBATIA kufukuzwa Ubunge?

MBATIA kufukuzwa Ubunge?

ccm (bunge) imeunda kamati kuipitia mitaala aliyoiwasilisha waziri ili kwa vyovyote ije na taarifa kuwa mitaala ipo na ni swafi na Mbatia kaongopa.
swali ni kwa nini waziri alikuwa kaibana hiyo mitaala kibindoni wakati wa kuwasilisha kwake - mitaala kaimelemetesha au kai-blandish tu pale na kudai italetwa. mbona tunaona na kushuhudia spika akiwa mkali kutaka mbunge mwernye document crucial aiweke mezani kwake - ilishindikana nini kwa hili.
mitaala ni kitu academic hakitakiwi kiwe siri - mtu anatakiwa anainigia website ya elimu na anaikuta..
kaaaaazi kwelikweli
 
hebu tusaidie wewe sasa; mitaala ni nini?

soma makala ya mkumbo kwenye gazeti nililokuambia ameeleza kila kitu. Kama watu hautaelewa nitakuja na maelezo kutoka kwa wataalam mahiri wa mitaala hapa nchini,prof osaki,prof njabiri,prof chonjo etc
 
bado Mbatia yuko sahihi; muda aliotaka Mtaala wa Elimu uwasilishwe Bungeni aukuonekana; kwa maana haukuwepo kabisa tangu awali; sasa huu uliowasilishwa juzi kuna uwezekano mkubwa umeandaliwa fastafasta ili kuliondolewa Taifa aibu.

Na hicho ndiyo walichokifanya.Inachukua masaa mangapi kukwenda hata shule moja pale Dodoma na kuleta nakala kama kweli Mtaala wenyewe ulikuwepo.Si ni lazima usambazwe shule zote Tanzania au ulikuwa kwenye Kabati la Katibu Mkuu na kama ndivyo unawezaje kusema ulikuwepo ili hali hapo mashuleni ambako ndiko waliko walimu na wanafunzi hakuna nakala ?

Tuache Porojo na Usanii hali ya Tanganyika hii inazidi kuwa mbaya.Kuchezea Elimu ni hatari na athari zake zimekwisha anza kuonekana tunawalisha watoto wetu Uongo na uzandiki kuwa kuna Nchi ilipata Uhuru 1961 na Nchi hii ilikuwa inaitwa Tanzania Bara.

Viongozi wetu wengi 90% wanachowaza ni matumbo yao na familia yao na wanajisahau kuwa wote tuko dunia na ardhi moja ya Tanzania kama Mungu atapenda iendelee kuwepo maana ninachokiona sisi kama Binadamu tushaichoka.
 
Kwamaana hii,Mh Mbatia atakuwa sahihi hakuna kitu kinaitwa mtaala au kimeandika mtaala.Mh MBATIA aliuliza je ni mtaala gani unatumika hapa nchi.?

mbatia alikuwa sawa kusema hakuna document yoyote inayoitwa mtaala kakini hayuko sahihi kusema kwamba tanzania hakuna mitaala
 
Sidhani kama kuna mitaala Tanzania,ukitaka kujua ipo ama haipo angalia mtoto wako anachosema shule,iwe shule za St Kayumba au za English medium wanazoziita academy.Hivi kweli mtoto wa darasa la pili au la tatu unamfundisha sayansi mtoto huyu ataweza?Kwa madarasa haya matatu tunategemea mtoto afundishwe ABC za kusoma,kuandika,hesabu na lugha.Mtoto huyu ana masoma zaidi ya saba kwa mantiki ya kawaida anaweza?Je wanasaikolojia wanasemaje kuhusu hili.Nimeona madaftari ya watoto wa chini ya darasa la nne masomo yao ni magumu kwa kiwango cha mtoto.
Sikuwahi kufundishwa hayo yote mpaka akili ilipokomaa yaani darasa la nne.Je tunadumaza au kupandisha elimu yetu?Kwa ufupi Wizara ya elimu hakuna mitaala na kama ipo basi ni kwa ajili ya show off na siyo kwa ajili ya kupandisha elimu yetu.Maana kila shule inatumia vitabu vyake tofauti na shule nyingine.
 
Mambo haya yakithibitika mbatia atajiuzuru,yeye sio mjinga hadi aseme HAKUNA MTAALA RASIMI WA ELIMU:-

1.SHARTI MITAALA HIYO IWE NI MITAALA RASMI YA ELIMU.

2.HIYO MITAALA ITHIBITIKE KUWA SIO RASIMU ILIYOANDALIWA 2012.

3.HIYO MITAALA IWE RASMI SIYO YA JUMLA.

Tunafahamu kwamba Tanzania wajanja ni wengi wanaweza kuchapa hiyo mitaala hata usiku wa manane,lakini mwisho wao umekaribia sana,Mbatia yuko sahihi HAKUNA MITAALA RASMI YA ELIMU TANZANIA.Isipokuwa RASIMU ya mtaala huo ndiyo ilishandaliwa tangu 2012.
 
sramble umejiambulisha kwenye thread moja wapo kwamba ni mwalimu na uko na M.A nijitambulishe kwako na mbele ya wana jf mi ni curriculum specilist,nakuomba usome makala ya mkumbo kwenye gazeti la raia mwema la leo uone jinsi unavyopotosha watu kuhusu hili suala la mitaala. Nilieleza pia kwenye thread yako ya jmosi iliyopita kuhusu suala hili la mitaala, naomba uwe professional zaidi ukiwa unasoma makala ya mkumbo kwani huo ndo ukweli kuhusu sakata hili la mitaala


mkumbo namfahamu ni mhadhiri na mkuu wa kitivo cha elimu pale duce chang'ombe. ni msomi na namheshimu. makala yake nimeisome katika raia mwema la wiki hii ukurasa wa 8 na 9. mbona ninayo yasema ndiyo aliyoyaandika. sijatofautiana nae hata kidogo. kasema nchi yetu ina mitalaa na kasema mihutasari hutokana na mitalaa. huwezi kuwa na muhtasari bila ya kuwa na mtalaa. hebu isome kisha unieleze wapi nimetofautiana nae. wewe kama curriculum specialist (jpo katika ngazi za elimu sijawahi sikia cheo hiki kitaaluma!) nieleze wapi nimepotosha watu kuhusu mambo ya mitalaa au mitaala!
 
Kama mtaala ulikuwep,o kwa nini imemchukua waziri muda mrefu kuuleta bungeni. Mtaala ni document ambayo anagalau wadau na viongozi wa elimu wanatakiwa kuwa nao. Pale Dodoma, kuna maofisa elimu wa mkoa,wilaya, nk. Ningetumaini wangekuwa nao.Kwa hiyo waziri alipotakiwa aulete lilikuwa ni swala la kuwaambia wasaidizi wake wamletee huo mtaaala. Lakini inaonekana mtaala upo wizarani kwa kiongozi fulani kwa matumizi yake, na si ya elimu ya watanzania.Ndo maana umechelewa kuletwa bungeni.Kama ulikuwepo hasa. Otherwsise umekuwa compiled faster kumaliza tatizo la Mbatia.
 
"BAADHI ya walimu wa shule za msingi wilaya za Korogwe na Moshi wamelalamikia mabadiliko ya mara kwa mara ya mitaala kwa shule za msingi pamoja na idadi kubwa ya masomo kwa wanafunzi wa madarasa ya chini, kuwa yamekuwa yakiwachanganya wanafunzi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti hivi karibuni walisema mabadiliko ya mara kwa mara kwa mitaala yanayofanywa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi bila maandalizi yamekuwa chanzo cha vikwazo cha kufanya vizuri kwa sekta hiyo."

Uliripoti mtandao wa http://www.thehabari.com/?p=21453 NA HAKIELIMU Agust 2012.

Sasa ikiwa mtaala haupo,Ina maana hawa waalimu na wanafunzi walikuwa wakichanganywa na kitu ambacho hakipo huku serikali nayo ikiwa inalaumiwa kubadilishabadilisha kitu ambacho hakipo? yaani mambo mengine mimi yananipa raha kweli!
 
Mitaala: http://hakielimu.org/files/publications/nani haumua watoto wetu wajifunze.pdf

Mtaala kwa kuzingatia mambo 12.
• Kile kinachofundishwa shuleni
• Seti ya masomo
• Maarifa
• Programu ya masomo
• Seti ya vitu vya kujifunza
• Orodha ya kozi
• Seti ya malengo ya ufanyaji kitu
• Kozi ya kujifunza
• Kila kitu kinachoendelea shuleni, ukijumuisha mambo yanayofanyika nje ya darasa, usimamizi, na uhusiano kati ya mtu mmoja na mwingine
• Kila kitu kinachopangwa na wafanyakazi shuleni
• Mjumuiko wa uzoefu mbalimbali anaoupata mwanafunzi awapo shuleni
• Kile ambacho mwanafunzi hukipata kikiwa ni matokeo ya kuwa shuleni

sasa haya hapa juu tunayo kweli? na kama ni kweli tunayo kwa nini basi iwe inabadilika badilika mara kwa mara na nani ana jukumu kisheria la kufanya mabadiliko haya?

au serikali imepeleka bungeni Muhtasari wa ufundishaji.
 
soma makala ya mkumbo kwenye gazeti nililokuambia ameeleza kila kitu. Kama watu hautaelewa nitakuja na maelezo kutoka kwa wataalam mahiri wa mitaala hapa nchini,prof osaki,prof njabiri,prof chonjo etc
unadhani hili suala ili kueleweka linataka maprofesa!
 
Mitaala: http://hakielimu.org/files/publications/nani%20haumua%20watoto%20wetu%20wajifunze.pdf

Mtaala kwa kuzingatia mambo 12.
• Kile kinachofundishwa shuleni
• Seti ya masomo
• Maarifa
• Programu ya masomo
• Seti ya vitu vya kujifunza
• Orodha ya kozi
• Seti ya malengo ya ufanyaji kitu
• Kozi ya kujifunza
• Kila kitu kinachoendelea shuleni, ukijumuisha mambo yanayofanyika nje ya darasa, usimamizi, na uhusiano kati ya mtu mmoja na mwingine
• Kila kitu kinachopangwa na wafanyakazi shuleni
• Mjumuiko wa uzoefu mbalimbali anaoupata mwanafunzi awapo shuleni
• Kile ambacho mwanafunzi hukipata kikiwa ni matokeo ya kuwa shuleni

sasa haya hapa juu tunayo kweli? na kama ni kweli tunayo kwa nini basi iwe inabadilika badilika mara kwa mara na nani ana jukumu kisheria la kufanya mabadiliko haya?

au serikali imepeleka bungeni Muhtasari wa ufundishaji.



mitaala na mihutasari iliyopo hapa nchini imekidhi vigezo hivi vyote. tatizo labda ni nyenzo za kufundishia lakini haya yote yameandikwa na kuchambuliwa kiufasaha
 
ru.

Mtaala wa elimu umewakilishwa na kuundiwa Tume ya wabunge 6 itakayodhibitisha mtaala huo chini ya mama Magreth Sitta.

Tugemee nini kama itathibitishwa kwamba mtaala huo upo???
Samahani kama ninarudia posting hii, kuna kitu inabidi kijadiliwe kwa kina hapo. Tume ya wabunge inaundwa kuthibitisha mtaala. Hivi tumefikia kiwango cha kuunda tume kuthibitisha nyaraka zinazotoka serikalini- na hasa mtaala unaotakiwa uwe ulikuwa unatumika? Shule zipo, walimu wapo, wanafunzi wapo, wizara ya elimu ipo- kwa ufupi Elimu ipo kwenye motion nchini. Kwa hiyo tulitegemea serikali ikisema mtaala ni huu, iwe hivyo.
Kitendo cha BUNGE kuunda tume kuverify mtaala wa serikali ni tusi. Bunge haliiamini serikali katika suala hili. Kwa ufupi Bunge limeungana na Mbatia kuamini kuwa serikali haina mtaala. Serikali ingekuwa na mtaala (ambao aliuonyesha wajiri wakati anajibu hoja ya Mbatia) sidhani kama waziri asingemuonyesha Spika. Na spika asinge kuwa na mashaka na mtaala huo kama tuonavyo sasa.
Aghhhr!
 
mitaala na mihutasari iliyopo hapa nchini imekidhi vigezo hivi vyote. o labda ni nyenzo za kufundishia lakini haya yote yameandikwa na kuchambuliwa kiufasaha
sasa kama huna nyezo za kufundishia utasemaje una mitaala? ni sawa na kuandika mambo kwenye makaratasi then who cares wanafunzi wanapata nini at the end of the day.
 
nimemuona MAMA POROJO nikakumbuka siku akiripoti vurugu za cdm Singida/Igunga na jinsi akina Mnyika walivyokuwa wamepanga vijana wa kuua wanaccm kabla maaskari hawajatoa ushahidi kuwa Mwigulu Nchemba ndiye aliyepanga na kuratibu hizo vurugu zilizopelekea mauaji!
Endelea mama
 
Tatizo sio kuwa na mitaala tu. je iliyopo ni mizuri? na je hata hiyo iliyowasilishwa ilikuwapo kabla? inafaa?
Sidhani kama amewasilisha mitaala ambayo ni published. Ninachojua amewasilisha rasmu ya mitaala ya elimu ya Tanzania. Hiyo published curriculum document ya Tanzania haikuwahi kuwepo, tangu ile ya Elimu ya kujitegemea ilipo perish. So iwe na itakavyokuwa, kama kweli waziri amewasilisha mitaala halisi basi tutataka atupe na ISBN namba ya publication ya hiyo mitaala na si draft.
 
Huyo Kawambwa wenu me simuamini hata kidogo,mijitu misanii sanii tu kazi yao kubwa kutuhadaa,Mbati hawezi kujiuzuru kwa usanii wa serikali.
 
sasa kama huna nyezo za kufundishia utasemaje una mitaala? ni sawa na kuandika mambo kwenye makaratasi then who cares wanafunzi wanapata nini at the end of the day.

tumia akili. mtaala ni maandishi siyo vitu halisi. instructional materials (learning / teaching aids) hutajwa kwenye mitaala. tofautisha mambo mawili. acha hoja za kitoto. mitaala ipo. kupungua au kukosekana kwa vifaa vya kufundishia mashuleni hilo ni suala lingine. tumia ubongo acha uvivu dogo.
 
Kwani ni wangapi magamba wenzako wamewajibika kwa madudu waliotufanyia watanganyika?
MBATIA aliapa bungeni kwamba Waziri wa Elimu atakapowakilishwa mtaala wa elimu atajiuzulu ubunge kwani haupo tangu tupate uhuru.

Mtaala wa elimu umewakilishwa na kuundiwa Tume ya wabunge 6 itakayodhibitisha mtaala huo chini ya mama Magreth Sitta.

Tugemee nini kama itathibitishwa kwamba mtaala huo upo???

My Take:

Nilimsikia MBATIA kwa kinywa chake akitoa ahidi na kuapa kupitia TBC live kutoka bungeni kwamba ataachia ngazi.

Mdomo nyumba ya maneno. Huwezi kuisukuma gari ukiwa ndani ya gari.

Mbatia hilo unalo timiza ahadi yako endapo itathibitishwa kwamba ulilidanganya bunge na Watanzania. Kama atagoma kujiuzulu basi bunge litumie busara kumfukuza ubunge ili ahadi yake itimie.
 
Back
Top Bottom