Askofu Gwajima, nakushauri usigombee tena ubunge wa Kawe

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,860
12,293
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Brother "G", huu ninaokupa ni ushauri mzuri ambao utakusaidia kukulindia heshima yako nusu uliyobaki nayo sasa hivi.

Kumbuka Jimbo la Kawe ndio Jimbo namba 1 au 2 nchini kuwa na
1. Wasomi wengi.
2. Viongozi wengi wa Serikali, waliopo madarakani na wastaafu.
3. Wakuu wengi wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, waliopo madarakani na wastaafu.
4. Maspika wabunge wastaafu.
5. Baadhi ya wakuu wa vyama vya siasa.
6. Na raia wengine ambao wana uelewa mkubwa wa mambo.

Hivyo basi hayo makundi niliyoyataja hapo juu, hayatokuwa tayari kukurudisha bungeni ukaendelee kupiga pesa kupitia Jimbo hili again.

Ahadi ulizotoa mwaka 2020, mpaka sasa ni miaka mi3 ndani ya ofisi haujatimiza hata 15% ya kile ulichoahidi. Kwa kukusaidia tu, ngoja nikupe baadhi ya maeneo ambayo kama CCM wakikupitisha kugombea basi askofu "G" utaangukia pua mchana kweupe.

A. Mtaa wa SALASALA.

Toka uingie bungeni mwaka 2020, hadi leo hakuna kitu chochote cha maana ambacho ushaifanyia Salasala.
Barabara iliyopo ni moja tu ile inayotoka mbuyuni alafu inakunja pale katika ofisi ya serikali ya mtaa, inapita kwa spika wa bunge na kwenda kuishia mbele kidogo.

Maeneo mengine ni hovyo. Barabara zingine zilizobaki zote mbovu, hazipitiki kwa gari, baskeli wala bodaboda. japo mtaa upo katika eneo zuri kijiografia, hali ya hewa tamu na upepo mwanana kutoka mbezi beach unapanda hadi juu, ardhi safi ambayo haina milima milima ya hovyo nk. Miundo mbinu ya maji, umeme pia bado ni kikwazo kwa baadhi ya maeneo.

B. Mtaa wa MADALE

Huko nako ndo usiseme, yani hata ile barabara ya Madale imekosa wa kuisimamia. Imekuwa kama vile njia ya kupitia ng'ombe kwenda malishoni. Japo eneo lina hadhi ya kishua kama Salasala lkn usimamiaji wa miundo mbinu umekuwa hakuna, hadi kupelekea watu sasa wanajijengea hovyo kama mwananyamala kisiwani au vingunguti.

Maeneo ambayo umeyaacha katika Jimbo ni mengi, haina haja ya kuyataja yote, ila unachotakiwa kujua ni kwamba 2025 hautapita katika ubunge hata ukija na porojo gani.

Kama unataka uendelee na ubunge basi una options mbili.
1. Kufanyia kazi changamoto zote za miundombinu ya Jimbo angalau kwa 60% alaf zilizobaki utamaliza katika kipindi cha pili cha 2025 to 2030.

2. Au ukagombea katika majimbo mengine kama vile Temeke, Mbagala au Ukonga ambayo yana idadi kubwa ya waswahili.

Uchaguzi ujao wana Kawe watamchagua mtu mwenye uwezo wa kweli wa kuleta maendeleo Kawe, bila kujali ni wa chama tawala au upinzani.
 
Huyo hata hakuwahi kuchaguliwa, alipewa ushindi wa kura za kwenye begi, nilishangaa sana pale nilipoona Gwajima ameshinda kwa kura zaidi ya elfu themanini jimbo la Kawe, nikasema hawa wajinga hata kuiba hawajui, waliiba mpaka wakapitiliza.
 
Huyo hata hakuwahi kuchaguliwa, alipewa ushindi wa kura za kwenye begi, nilishangaa sana pale nilipoona Gwajima ameshinda kwa kura zaidi ya elfu themanini jimbo la Kawe, nikasema hawa wajinga hata kuiba hawajui, waliiba mpaka wakapitiliza.
Ikipatikana njia ya kudhibiti wizi wao, hawa wahuni wanaweza kuzidiwa wabunge hata na chama cha mzee Rungwe.
 
Huyo hata hakuwahi kuchaguliwa, alipewa ushindi wa kura za kwenye begi, nilishangaa sana pale nilipoona Gwajima ameshinda kwa kura zaidi ya elfu themanini jimbo la Kawe, nikasema hawa wajinga hata kuiba hawajui, waliiba mpaka wakapitiliza.
Huyu jamaa hakuwa chaguo la wana Kawe. Hata hivyo angekuwa mjanja angeleta maendeleo ya kweli, ili kutengeneza mazingira ya kukubalika katika chaguzi zijazo.
 
Hakupigiwa Kura na wana Kawe bali alipigiwa Kura na Nduguye ( sasa Hayati ), Wakurugenzi na Wasimamizi.

Hakuna na hayupo mwana Kawe Mpumbavu ( Fool ) angeweza kumpa Kura yake Gwajima.

Kipenzi cha wana CCM Kawe alikuwa ni Furaha Dominic ( Mpwa wa Hayati ) na siyo huyo ( huyu ) tuliyelazimishwa Kumpenda na Kumuamini wakati amejaa Unafiki na Usanii mwingi sana.
 
Habari zenu wanaJF wwenzangu,

Brother "G", huu ninaokupa ni ushauri mzuri ambao utakusaidia kukulindia heshima yako nusu uliyobaki nayo sasa hivi.

Kumbuka Jimbo la Kawe ndio Jimbo namba 1 au 2 nchini kuwa na
1. Wasomi wengi.
2. Viongozi wengi wa Serikali, waliopo madarakani na wastaafu.
3. Wakuu wengi wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, waliopo madarakani na wastaafu.
4. Maspika wabunge wastaafu.
5. Baadhi ya wakuu wa vyama vya siasa.
6. Na raia wengine ambao wana uelewa mkubwa wa mambo.

Hivyo basi hayo makundi niliyoyataja hapo juu, hayatokuwa tayari kukurudisha bungeni ukaendelee kupiga pesa kupitia Jimbo hili again.

Ahadi ulizotoa mwaka 2020, mpaka sasa ni miaka mi3 ndani ya ofisi haujatimiza hata 15% ya kile ulichoahidi. Kwa kukusaidia tu, ngoja nikupe baadhi ya maeneo ambayo kama CCM wakikupitisha kugombea basi askofu "G" utaangukia pua mchana kweupe.

A. Mtaa wa SALASALA.

Toka uingie bungeni mwaka 2020, hadi leo hakuna kitu chochote cha maana ambacho ushaifanyia Salasala.
Barabara iliyopo ni moja tu ile inayotoka mbuyuni alafu inakunja pale katika ofisi ya serikali ya mtaa, inapita kwa spika wa bunge na kwenda kuishia mbele kidogo. Maeneo mengine ni hovyo japo mtaa upo katika eneo zuri kijiografia, hali ya hewa tamu na upepo mwanana kutoka mbezi beach unapanda hadi juu, ardhi safi ambayo haina milima milima ya hovyo nk. Miundo mbinu ya maji, umeme pia bado ni kikwazo kwa baadhi ya maeneo.

B. Mtaa wa MADALE

Huko nako ndo usiseme, yani hata ile barabara ya Madale imekosa wa kuisimamia. Imekuwa kama vile njia ya kupitia ng'ombe kwenda malishoni. Japo eneo lina hadhi ya kishua kama Salasala lkn usimamiaji wa miundo mbinu umekuwa hakuna, hadi kupelekea watu sasa wanajijengea hovyo kama mwananyamala kisiwani au vingunguti.

Maeneo ambayo umeyaacha katika Jimbo ni mengi, haina haja ya kuyataja yote, ila unachotakiwa kujua ni kwamba 2025 hautapita katika ubunge hata ukija na porojo gani.

Kama unataka uendelee na ubunge basi una options mbili.
1. Kufanyia kazi changamoto zote za miundombinu ya Jimbo angalau kwa 60% alaf zilizobaki utamaliza katika kipindi cha pili cha 2025 to 2030.

2. Au ukagombea katika majimbo mengine kama vile Temeke, Mbagala au Ukonga ambayo yana idadi kubwa ya waswahili.

Uchaguzi ujao wana Kawe watamchagua mtu mwenye uwezo wa kweli wa kuleta maendeleo Kawe, bila kujali ni wa chama tawala au upinzani.
Hutaki kwenda Marekani ?
 
Habari zenu wanaJF wwenzangu,

Brother "G", huu ninaokupa ni ushauri mzuri ambao utakusaidia kukulindia heshima yako nusu uliyobaki nayo sasa hivi.

Kumbuka Jimbo la Kawe ndio Jimbo namba 1 au 2 nchini kuwa na
1. Wasomi wengi.
2. Viongozi wengi wa Serikali, waliopo madarakani na wastaafu.
3. Wakuu wengi wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, waliopo madarakani na wastaafu.
4. Maspika wabunge wastaafu.
5. Baadhi ya wakuu wa vyama vya siasa.
6. Na raia wengine ambao wana uelewa mkubwa wa mambo.

Hivyo basi hayo makundi niliyoyataja hapo juu, hayatokuwa tayari kukurudisha bungeni ukaendelee kupiga pesa kupitia Jimbo hili again.

Ahadi ulizotoa mwaka 2020, mpaka sasa ni miaka mi3 ndani ya ofisi haujatimiza hata 15% ya kile ulichoahidi. Kwa kukusaidia tu, ngoja nikupe baadhi ya maeneo ambayo kama CCM wakikupitisha kugombea basi askofu "G" utaangukia pua mchana kweupe.

A. Mtaa wa SALASALA.

Toka uingie bungeni mwaka 2020, hadi leo hakuna kitu chochote cha maana ambacho ushaifanyia Salasala.
Barabara iliyopo ni moja tu ile inayotoka mbuyuni alafu inakunja pale katika ofisi ya serikali ya mtaa, inapita kwa spika wa bunge na kwenda kuishia mbele kidogo. Maeneo mengine ni hovyo japo mtaa upo katika eneo zuri kijiografia, hali ya hewa tamu na upepo mwanana kutoka mbezi beach unapanda hadi juu, ardhi safi ambayo haina milima milima ya hovyo nk. Miundo mbinu ya maji, umeme pia bado ni kikwazo kwa baadhi ya maeneo.

B. Mtaa wa MADALE

Huko nako ndo usiseme, yani hata ile barabara ya Madale imekosa wa kuisimamia. Imekuwa kama vile njia ya kupitia ng'ombe kwenda malishoni. Japo eneo lina hadhi ya kishua kama Salasala lkn usimamiaji wa miundo mbinu umekuwa hakuna, hadi kupelekea watu sasa wanajijengea hovyo kama mwananyamala kisiwani au vingunguti.

Maeneo ambayo umeyaacha katika Jimbo ni mengi, haina haja ya kuyataja yote, ila unachotakiwa kujua ni kwamba 2025 hautapita katika ubunge hata ukija na porojo gani.

Kama unataka uendelee na ubunge basi una options mbili.
1. Kufanyia kazi changamoto zote za miundombinu ya Jimbo angalau kwa 60% alaf zilizobaki utamaliza katika kipindi cha pili cha 2025 to 2030.

2. Au ukagombea katika majimbo mengine kama vile Temeke, Mbagala au Ukonga ambayo yana idadi kubwa ya waswahili.

Uchaguzi ujao wana Kawe watamchagua mtu mwenye uwezo wa kweli wa kuleta maendeleo Kawe, bila kujali ni wa chama tawala au upinzani.
Na wewe ni Mstaafu wa kada ipi?
 
Hakupigiwa Kura na wana Kawe bali alipigiwa Kura na Nduguye ( sasa Hayati ), Wakurugenzi na Wasimamizi.

Hakuna na hayupo mwana Kawe Mpumbavu ( Fool ) angeweza kumpa Kura yake Gwajima.

Kipenzi cha wana CCM Kawe alikuwa ni Furaha Dominic ( Mpwa wa Hayati ) na siyo huyo ( huyu ) tuliyelazimishwa Kumpenda na Kumuamini wakati amejaa Unafiki na Usanii mwingi sana.
Nakubaliana na wewe kwa 100%

Hata hapo juu kwenye post namb #5 kuna mdau nilimwambia the same thing 👇
Huyu jamaa hakuwa chaguo la wana Kawe. Hata hivyo angekuwa mjanja angeleta maendeleo ya kweli, ili kutengeneza mazingira ya kukubalika katika chaguzi zijazo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom