VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Najua kila jambo lako. Nimekutangulia kila ulipopita. Kuanzia shule, JKT, Chuo Kikuu na hata kule kwenye Kitengo. Nakufahamu hadi kuishiwa hamu. Nakujua nje na ndani kuliko maboga niliyoyaotesha uani. Ndugu Mbatia umepotea.
Ukawasiliana na wakuu wa chama na Serikali. 'Ukaombwa' upewe 'kazi maalum' ya kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wamwaka huu. Ukaambiwa kuwa mwaka huu ni zamu yako tukibeba chama chetu, na chama chetu kitagharimia kila jambo. Kwamba utawazeshwa ili uweze.
Ukaitwa Ikulu. Ukathibitisha kukubali na kusisitiziwa ahadi ya Ubunge uliyopewa tangu mwanzo kwa jimbo utakalolitaka. Na ukaahidiwa kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Ukaahidiwa na mambo lukuki matamumatamu. Tayari umeshaanza kazi. Kazi yako inaendelea vyema kabisa.
Ndugu Mbatia, ahadi ya Ubunge itakutesa sana. Itakutesa hadi ukumbuke siku ile ulipojiunga kule na kuambiwa yale. Utakumbuka jinsi ulivyoaminika kisiasa kuwa wewe ni mpinzani na hata kupata nafasi huko. Utakumbuka na kujuta kwa kujianika kirahisi.
Time will tell!
Tujihadhari na ugonjwa wa Corona!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha, Tanzania)
Ukawasiliana na wakuu wa chama na Serikali. 'Ukaombwa' upewe 'kazi maalum' ya kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wamwaka huu. Ukaambiwa kuwa mwaka huu ni zamu yako tukibeba chama chetu, na chama chetu kitagharimia kila jambo. Kwamba utawazeshwa ili uweze.
Ukaitwa Ikulu. Ukathibitisha kukubali na kusisitiziwa ahadi ya Ubunge uliyopewa tangu mwanzo kwa jimbo utakalolitaka. Na ukaahidiwa kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Ukaahidiwa na mambo lukuki matamumatamu. Tayari umeshaanza kazi. Kazi yako inaendelea vyema kabisa.
Ndugu Mbatia, ahadi ya Ubunge itakutesa sana. Itakutesa hadi ukumbuke siku ile ulipojiunga kule na kuambiwa yale. Utakumbuka jinsi ulivyoaminika kisiasa kuwa wewe ni mpinzani na hata kupata nafasi huko. Utakumbuka na kujuta kwa kujianika kirahisi.
Time will tell!
Tujihadhari na ugonjwa wa Corona!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha, Tanzania)