Mawaziri watakiwa kurudi Dar na Kurejesha magari Wizarani

Sina uhakika lakini sidhani kama mawaziri wanaweza kushitakiwa kwa makosa ya kiutendaji yaliyofanywa na watendaji katika wizara zao au taasis zilizoko chini ya wizara zao.

Upotevu wa fedha ulioko kwenye report ya CAG unahusu utendaji. Na nivyema mkatambua kuwa baadhi ya upotevu huo ni wa miaka 3 iliyopita wakati hata mawaziri husika walikya hawaja chaguliwa.

Pia ikumbukwe kuwa wengine kama Maige hawakutuhumiwa na CAG bali report za kamati za bunge.

Report hizi haziwezi kumpeleka mtu mahakamani hadi pale vyombo vinavyohusika vitafanya uchunguzi na kubaini kama tuhuma hizo ni za kweli au la.

Hapo ni kweli kwa sababu kulingana na sheria za Tanzania zipo Taasisi hususan polisi, Uhamiaji na Takukuru ambazo ndizo zenye mamlaka ya kufanya chunguzi za makosa ya kijinai na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa baada ya kujiridhisha kuwa upo ushahidi usio na mashaka unaowahusisha watuhumiwa, ripoti za CAG na Kamati za bunge zinaweza kusaidia katika uchunguzi wa tuhuma husika na haziwezi kutumika kwa asilimia 100 kama ushahidi. Aidha maofisa wa ofisi ya CAG na wajumbe wa kamati za Bunge wanaweza kuwa mashahidi wa Jamhuri lakini hawawezi kufungua kesi mahakamani. Ni muhimu wanaJF kulielewa hili!
 
Kuna taarifa za kuaminika kwamba JK atatangaza baraza jipya la mawaziri punde,lakini ameiomba mamlaka husika kuwafungulia mashitaka mawaziri wake wote waliotajwa na ndg LUDOVIC UTOUH kama
wabadhilifu wakubwa wa mipesa ya wa tz..na tayari ameshawapiga pini mawaziri wote wasitoke nje ya Dar.
Mh JK ameamua kuchukua uamuzi wa kuwashitaki mawaziri wake ili kukinusuru
Chama na kasheshe la uchaguzi mkuu ujao.
Bado nafatilia na kama kuna taarifa mpya ntawajuza.

Suala la kuwapeleka Watu Mahakamani ni suala la TAKUKURU NA DPP WAKE!! Sasa raisi Katoka wapi tena Hapo? Ndio Tusema Takukuru wanakula Mshahara Bure Hadi Raisi aseme? Duh Tanzania Raha kwelikweli!!
 
kama hivyo hali itakuwa mbaya sana tanzania maana mkulo, mkuchika, ngereja ndio walikuwa washika pembe wakati jk anaingia kwenye urahisi na ndio walipeleka hela za kampeni dodoma kweli tusubiri tuone nini kitatokea
 
Sina uhakika lakini sidhani kama mawaziri wanaweza kushitakiwa kwa makosa ya kiutendaji yaliyofanywa na watendaji katika wizara zao au taasis zilizoko chini ya wizara zao.

Upotevu wa fedha ulioko kwenye report ya CAG unahusu utendaji. Na nivyema mkatambua kuwa baadhi ya upotevu huo ni wa miaka 3 iliyopita wakati hata mawaziri husika walikya hawaja chaguliwa.

Pia ikumbukwe kuwa wengine kama Maige hawakutuhumiwa na CAG bali report za kamati za bunge.

Report hizi haziwezi kumpeleka mtu mahakamani hadi pale vyombo vinavyohusika vitafanya uchunguzi na kubaini kama tuhuma hizo ni za kweli au la.
You're quite right
 
Back
Top Bottom