Baada ya Kenya kuendesha shughuli za serikali kwa miezi 5 bila mawaziri (isipokuwa wale wachache walioteuliwa kabla ya muafaka) wala waziri mkuu, tumejifunza nini? Kuna umuhimu wowote wa kuwa na hawa watu wanaoitwa mawaziri? Wamepata hasara gani kutokana na kutokuwepo watu hao? Mojawapo ya faida waliyopata ni kuwa wamepata savings ya ile gharama ambayo wangetumia kuwahudumia mawaziri kwa miezi hiyo mitano! Je kuna faida zaidi? Nadhani yaliyotokea Kenya ni fursa nzuri ya kutafakari upya umuhimu wa hawa tunaowaita mawaziri. Wakuu mnasemaje?