Mawaziri Kupanguliwa

Mawaziri Kupanguliwa

Nchi hii sijui inalaana gani kila kukicha mabadiliko hii inamfanya anaeteuliwa ashawishike kufanya vitu vya ajabu make anajua kesho anatenguliwa.mi najiuliza huyo anaetenguliwa sina uhakika kama analipwa stahiki zake.na kama analipwa serikali inapata hasara gani make teuzi sasa ni kila mwezi.nchi ya ajabu sana hii.
 
mama ikimpendeza angeaza fagio lake kwa mzee wa skafu yule wa kutokea Singida! Mfumko wa bei na tozo unatishia maisha ya mtanzania!
Huyo hamtoi kabisaa, wee dili zitapigwaje??
 
Hii ndio taarifa mpya iliyotolewa na Gazeti bomba la Raia Mwema .

Kwamba Muda mfupi ujao baadhi ya Waheshimiwa Mawaziri wanaweza kuwa Raia wa kawaida kama tulivyo sisi wengine , hasa baada ya nafasi zao kujazwa na Wazalendo wengine .

Usiondoke JF .
Ndoto za Sukuma gang
 
Wanagawana ulaji ".....wewe mpishe kidogo mwenzio afyonze asali, pumzika kidogo wakati tunakutafutia sehemu nyingine tamu...." Sisi huku tynakenua meno eti anapanga safu mpya...kama ni safu mpya na yeye inabidi apangwe maana maji yameishamzidi kimo.

Dotto Biteko mara hii hitoboi japo umejitahidi kupaka rangi manyoya yako ili ufanane nao!
 
Raia mwema inatumia fursa za akili za waswahili za kuombeana mabaya kufanya biashara.
 
Mi naomba kuuliza je hao wanaotenguliwa huwa wanapewa kiinua mgongo au malipo yoyote au huwa wana nusu mshahara kama wastafu au ikoje?

Isije ikawa tunapoteza mamilioni ya pesa kuhudumia mizigo
Kila mfanyakazi pamoja na wanasiasa wanakuwa na mafao wakipumzishwa wanalipwa, ila watumishi wa umma (sio wanasiasa) hata wakitumbuliwa madaraka, wanaendelea kulipwa misharaha na stahiki zao bila hata ya kufanya kazi. Wako wengi benchi huko makao makuu wanasoma magazeti kutwa wakisubiri kupangiwa kazi zingine, ili mradi hawakufukuzwa kazi. Kwa Mtumishi wa umma, kutumbuliwa sio sawa na kufukuzwa kazi.
 
Back
Top Bottom