KERO Mawakala Selcom Tanzania hatupati Kamisheni ya kuuza Huduma ya Umeme

KERO Mawakala Selcom Tanzania hatupati Kamisheni ya kuuza Huduma ya Umeme

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Tunawaandikia kama mawakala wenu tukitoa malalamiko yetu rasmi kuhusu huduma za umeme (LUKU) na controller number, ambapo kwa muda mrefu hakuna kamisheni inayolipwa kabisa huku makato ya miamala yakiendelea kufanyika.

Sisi kama mawakala:
  • Tunaweka mtaji wetu binafsi
  • Tunahudumia wateja na kubeba lawama zote za changamoto za mfumo
  • Tunakatwa makato ya miamala papo hapo
Lakini hakuna faida yoyote inayobaki kwa wakala, hata TZS 100.

Hali hii inatufanya tujiulize kwa haki kabisa:
Je, tunafanya kazi kwa manufaa ya nani kama wakala halipwi?

Pia, hata pale ambapo kamisheni hulipwa mwisho wa mwezi, bado:
  • Makato yanaendelea kila siku
  • Hakuna uwazi wa kutosha kwenye rate card ya huduma hizi
Tunaomba kwa heshima:

1. Ufafanuzi rasmi wa muundo wa kamisheni (commission structure) kwa huduma za umeme na controller number
2. Marekebisho ya haraka ili angalau kuwe na kamisheni ya msingi kwa wakala
3. Au maelekezo rasmi kama huduma hizi hazina kamisheni kabisa.
 
Dawa n kuacha kufanya hayo malipo
 
Tunaomba kwa heshima:

1. Ufafanuzi rasmi wa muundo wa kamisheni (commission structure) kwa huduma za umeme na controller number
2. Marekebisho ya haraka ili angalau kuwe na kamisheni ya msingi kwa wakala
3. Au maelekezo rasmi kama huduma hizi hazina kamisheni kabisa.
Mkuu anaestahiri kuwapa nyinyi
Kamisheni ni nani?
 
Back
Top Bottom