Mauzauza ya EPA

Scenario 2
Tukisema alikua na biashara ingine, Tungependa kuifahamu ina mtaji kiasi gani na aliupata wapi. Pili mrahaba aliokuwa anaupata kutoka kwenye kampuni alilipa kodi????? Je hiyo company/hiyo biashara ingine auditing report zake zinaonyesha faida ama hasara?????? kama Faidi je zililipa kodi???? Je walideclare hiyo biashara yao wakati wakiwa serikalini????

Sasa kumbe tunakubaliana kuwa hapo kuna mambo mengi hatujui! Sasa kwanini unakua unakimbilia kuwahukumu?
 
Watuhumiwa EPA kurejeshewa fedha
Neema Mgonja
Daily News; Thursday,December 04, 2008 @21:15

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imeamuru baadhi ya washitakiwa katika kesi za ufisadi waliokuwa wametoa fedha taslimu kwa ajili ya kupata dhamana, warudishiwe fedha zao.

Mawakili wa washitakiwa katika kesi inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Hezron Mwankenja, waliomba kwa vile tayari Mahakama Kuu ilishalegeza masharti ya dhamana dhidi ya mshitakiwa mmoja Iman Mwakyosa, basi uamuzi huo utekelezwe kwa washitakiwa wote.

Katika kesi hiyo, washitakiwa ni wanne, Rajab Maranda, Esther Mary Komu, Mwakyosa na Bosco Kimela, ambao wote walishitakiwa kwa madai ya kuiba Sh milioni 207. Mawakili wa washitakiwa hao, Makaki Masatu aliomba kwa vile tayari Mahakama Kuu imelegeza masharti kwa Mwakyosa, ni vyema wateja wengine pia wakalegezewa masharti hayo.

Mwakyosa ametoka kwa masharti ya kutoa fedha taslimu Sh milioni 26 au hati ya thamani ya kiasi hicho. Awali katika kesi hiyo, Mwakyosa na wenzake waliamriwa kila mtu kutoa Sh milioni 104 fedha taslimu ili wapate dhamana. Uamuzi huo ulimwia mgumu Mwakyosa na hakutimiza masharti hayo, hali iliyomlazimu apeleke maombi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kuomba kulegezewa masharti ili aweze kutoa hati.

Ombi hilo lilikubaliwa na mahakama hiyo na kupunguza kiasi cha fedha kutoka Sh milioni 104 hadi Sh milioni 26 au kutoa hati ya thamani ya kiasi hicho. Jana kesi hiyo ilipokwenda kwa ajili ya kutajwa, Hakimu Mwankenja alikubaliana na maombi hayo ya washitakiwa na akaamuru mahakama kuwarudishia fedha zao washtakiwa ambao tayari walishatoa fedha taslimu na wako nje kwa dhamana.

“Kutokana na maombi ya mawakili, naamuru washitakiwa wengine nao warudishiwe fedha zao ili watoe kiasi ambacho kimetajwa na Mahakama Kuu,” alisema Mwankenja. Washitakiwa ambao walishatoa zaidi ya Sh milioni 100 na kupata dhamana ni Maranda, Komu na Kimela.

Kutokana na amri hiyo, washitakiwa hao sasa kila mmoja atarudishiwa fedha zake zote na watatoa hati au Sh milioni 26. Jana Maranda na Bosco waliwasilisha hati, ila ni hati ya Bosco pekee ilipokelewa wakati hati aliyowasilisha Maranda haikuwa na barua kuthibitisha hati hiyo, hivyo mahakama kutoikubali hadi pale itakapoambatanisha na barua. Esther kwa upande wake, wakili wake hakuwapo hivyo mahakama ilimwelekeza kuwa awasilishe hati hiyo siku kesi hiyo itakapoenda kusikilizwa Januari 20.
 
Watuhumiwa EPA kurejeshewa fedha
Neema Mgonja
Daily News; Thursday,December 04, 2008 @21:15

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imeamuru baadhi ya washitakiwa katika kesi za ufisadi waliokuwa wametoa fedha taslimu kwa ajili ya kupata dhamana, warudishiwe fedha zao.

Mawakili wa washitakiwa katika kesi inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Hezron Mwankenja, waliomba kwa vile tayari Mahakama Kuu ilishalegeza masharti ya dhamana dhidi ya mshitakiwa mmoja Iman Mwakyosa, basi uamuzi huo utekelezwe kwa washitakiwa wote.

Katika kesi hiyo, washitakiwa ni wanne, Rajab Maranda, Esther Mary Komu, Mwakyosa na Bosco Kimela, ambao wote walishitakiwa kwa madai ya kuiba Sh milioni 207. Mawakili wa washitakiwa hao, Makaki Masatu aliomba kwa vile tayari Mahakama Kuu imelegeza masharti kwa Mwakyosa, ni vyema wateja wengine pia wakalegezewa masharti hayo.

Mwakyosa ametoka kwa masharti ya kutoa fedha taslimu Sh milioni 26 au hati ya thamani ya kiasi hicho. Awali katika kesi hiyo, Mwakyosa na wenzake waliamriwa kila mtu kutoa Sh milioni 104 fedha taslimu ili wapate dhamana. Uamuzi huo ulimwia mgumu Mwakyosa na hakutimiza masharti hayo, hali iliyomlazimu apeleke maombi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kuomba kulegezewa masharti ili aweze kutoa hati.

Ombi hilo lilikubaliwa na mahakama hiyo na kupunguza kiasi cha fedha kutoka Sh milioni 104 hadi Sh milioni 26 au kutoa hati ya thamani ya kiasi hicho. Jana kesi hiyo ilipokwenda kwa ajili ya kutajwa, Hakimu Mwankenja alikubaliana na maombi hayo ya washitakiwa na akaamuru mahakama kuwarudishia fedha zao washtakiwa ambao tayari walishatoa fedha taslimu na wako nje kwa dhamana.

“Kutokana na maombi ya mawakili, naamuru washitakiwa wengine nao warudishiwe fedha zao ili watoe kiasi ambacho kimetajwa na Mahakama Kuu,” alisema Mwankenja. Washitakiwa ambao walishatoa zaidi ya Sh milioni 100 na kupata dhamana ni Maranda, Komu na Kimela.

Kutokana na amri hiyo, washitakiwa hao sasa kila mmoja atarudishiwa fedha zake zote na watatoa hati au Sh milioni 26. Jana Maranda na Bosco waliwasilisha hati, ila ni hati ya Bosco pekee ilipokelewa wakati hati aliyowasilisha Maranda haikuwa na barua kuthibitisha hati hiyo, hivyo mahakama kutoikubali hadi pale itakapoambatanisha na barua. Esther kwa upande wake, wakili wake hakuwapo hivyo mahakama ilimwelekeza kuwa awasilishe hati hiyo siku kesi hiyo itakapoenda kusikilizwa Januari 20.

Huyu Hakimu kesha likoroga jee hao watuhumiwa watakuwa na imani nae kupata fair trial ?
 
Babu wewe naoye unazidi kuboa

umeshindwa vipi kutuletea orodha badala ya hizi articles?

Acha hizo wewe! Kama huna la kusema la maana ni bora ukae kimya. Tumechoshwa na vituko vyako visivyokwisha. Wewe unajifanya ni mtetezi wa copy rights wakati huo huo unaweka movies ambazo huna copy rights za kuziweka hapa. Kama una swali kuhusu article hii lielekeze kwa mwandishi wa habari hii, jina na gazeti analofanyia kazi vyote vimekuwa included.
 
Inakuaje hizi nyumba walizoweka thamani zilikuwa MILLION 5 wakati wananunua SERIKALINI na leo hii baada ya miaka mitano zina thamani YA MAMILLION?

It doesn't make any sense at all. WHO WAS THE APPRAISER? MKAPA?
 
Inakuaje hizi nyumba walizoweka thamani zilikuwa MILLION 5 wakati wananunua SERIKALINI na leo hii baada ya miaka mitano zina thamani YA MAMILLION?

It doesn't make any sense at all. WHO WAS THE APPRAISER? MKAPA?

Kuna utata mkubwa kuhusu tathmini ya mali hizo kama ilifanywa na wataalamu katika mambo ya valuation. Hata katika majiji yenye gharama kubwa za maisha kama New York, London na Paris n.k. nyumba haziappreciate haraka kiasi hicho. Naona wakubwa walishaamua kuwakingia kifua. Kuna dalili ya hii kesi itajaa usanii wa hali ya juu na matokeo yake jamaa kuonekana hawana hatia. Maana si kitu cha kawaida hata kidogo Waziri wa mambo ya ndani kuwatembelea watuhumiwa wakiwa rumande na maelezo aliyoyatoa hayakuwaridhisha Watanzania wengi wanaofuatilia sakata la mafisadi hawa. Tusubiri tuone mwelekeo wa kesi hii.
 
...kama ambavyo viongozi wote wanavyotakiwa kuorodhesha mali zao?

Date::12/4/2008
Kambi ya upinzani wahoji mabilioni ya Mramba, Yona
Na Salim Said
Mwananchi

SIKU chache baada ya mawaziri wa zamani, Basil Mramba na Daniel Yona, kutolewa gerezani kwa kuwasilisha hati za mali zenye thamani ya jumla ya Sh6.2 bilioni kama dhamana, wapinzani wameeleza kushtushwa na kiwango hicho cha mali kumilikiwa na watumishi wa serikali.

Hati za mali za Mramba, ambaye pamoja na Yona wameshtakiwa kwa makosa ya kutumia vibaya ofisi wakati wakiwa mawaziri, ni zile za nyumba yake na za washirika wake zenye thamani ya Sh3.14 bilioni, wakati hati za mali za Yona zilikuwa ni nyumba zake tatu zenye thamani ya jumla ya Sh3 bilioni.

Kiwango hicho cha thamani za mali kimewashtua wanasiasa wa upinzani.

Baadhi ya viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) na chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wamehoji uhalali wa mtumishi wa umma kumiliki mali yenye thamani ya zaidi ya Sh3 bilioni.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam, viongozi wa Chadema na CUF walisema mshahara wa mtumishi wa umma unaeleweka.

Mkuu wa Idara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa CUF, Ismail Jussa alisema ingawa dhamana ni haki yake, lakini Yona ameushangaza umma kumiliki mali yenye thamani hiyo ya fedha.

"Kimsingi, dhamana ni haki yao lakini tatizo linakuja pale mtumishi wa umma anapoweza kujidhamini mwenyewe kwa mali yenye thamani ya mabilioni ya shilingi," alionyesha mshangao Jussa.

Kwa mujibu wa Jussa, kitendo cha waziri huyo mstaafu kujidhamini kwa mali ya mabilioni hayo kinaweka maswali mengi dhidi ya viongozi wa serikali.

Jussa, ambaye ni mwanasheria kitaaluma, pia alihoji kasi ya kusikilizwa kwa rufaa yao wakati kuna watu wengi wamekata rufaa, lakini bado wanaendelea kusota rumande bila rufaa zao kusikilizwa haraka.

“Mimi, kama mwanasheria sioni tatizo la kupewa dhamana, lakini rufaa yao na ile ya serikali dhidi ya walimu inaibua maswali mengi ambayo majibu yake ni magumu kuhusiana na uhuru wa mahakama,” alisisitiza Jussa.

Naye afisa habari wa Chadema, David Kafulila alisema haiwezekani kwa mtumishi wa umma kumiliki mali za namna hiyo.

“Hizo mali za Sh2.9 bilioni ni sehemu tu ya mali za Yona... kachomoa tu kidogo ili ziweze kumtoa nje, lakini alizipata kwa mshahara gani hata kama ni waziri,” alihoji Kafulila.

Alisema mazingira kama hayo ya kutatanisha kwa kiongozi kumiliki mali za thamani hiyo, ndiyo yaliyovifanya vyama vya upinzani nchini kutaka uhakiki wa mali zote za viongozi wa serikali pamoja na akaunti zao za benki, lakini walikataliwa.

Kafulila alitoa mfano wa waziri wa zamani wa miundombinu, Andrew Chenge ambaye alijiuzulu kutokana na kuhusishwa na kashfa ya ununuzi wa rada na kubainika kuwa ana akaunti yenye dola 1 milioni nje ya nchi, akisema ndilo lililojitokeza kwa mawaziri hao wawili.

“Kama mtu anaweza kumega sehemu tu ya mali yake yenye thamani ya 2.9 bilioni na kutoa kama dhamana mahakamani, kwa nini asiziite Sh.1 bilioni vijisenti,” alihoji Kafulila.

“Tunataka uhakiki wa mali za viongozi wa serikali kufanyika ili kugundua madudu ya kifisadi,” alisema Kafulila.

Aliongeza kwamba rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa alitangaza mali zake wakati anaingia madarakani, lakini aliondoka kimyakimya huku Rais Jakaya Kikwete akingia kimyakimya pasipo kujulikana mali zake.

Labda tume ya maadili inaweza kutoa jibu kama ziliorodheshwa ama ala.
 
Kuna utata mkubwa kuhusu tathmini ya mali hizo kama ilifanywa na wataalamu katika mambo ya valuation. Hata katika majiji yenye gharama kubwa za maisha kama New York, London na Paris n.k. nyumba haziappreciate haraka kiasi hicho. Naona wakubwa walishaamua kuwakingia kifua. Kuna dalili ya hii kesi itajaa usanii wa hali ya juu na matokeo yake jamaa kuonekana hawana hatia. Maana si kitu cha kawaida hata kidogo Waziri wa mambo ya ndani kuwatembelea watuhumiwa wakiwa rumande na maelezo aliyoyatoa hayakuwaridhisha Watanzania wengi wanaofuatilia sakata la mafisadi hawa. Tusubiri tuone mwelekeo wa kesi hii.

BAK hakuna lisilowezekaa TZ. Usishange pale majengo hayohayo yatakapo depreciate in value ikifikia kulipa property tax!
 
Jamani nimesoma nikiwa kwenye gari,kati ya magazeti ya leo kwamba wale wanaotuhumiwa wezi wa pesa zetu bot
wameambiwa kwenda kuchukua baadhi ya pesa kama walivyolalamika dhamana zao zilikuwa kubwa sana ...mbona aijaniingia tusaidiane kwa mlioona,,mi nilishasema hii ni cinema
mwisho .......*********
 
..masharti ya dhamana yanatakiwa yawe the same across the board.

..haiwezekani wengine watoe fedha taslimu, wakati wengine wanaruhusiwa kuwasilisha assets, au dhamana yao inakuwa calculated deferently frm the rest.
 
tatizo ya Asset za Nyumba ni kwenye valuation, kama hii habari inavyo onyesha
Milk factory owner opposes sale of his house
FAUSTINE KAPAMA
Daily News; Thursday,December 04, 2008 @21:15

The owner of Musoma Dairy Milk Factory, Dr Gideon Warioba Mazara, has opposed the sale of his 750m/- worth of his house and application for his detention in prison for allegedly failing to honour a court’s decree for payment of 136m/- loan with interests.

His advocate, Mr Mabere Marando, filed an application at the High Court’s Commercial Division, seeking orders to set aside the sale of his residential house situated at Musoma Municipality, which fetched a mere 75,100,000/-, contrary to the law of the land. The law requires that a house furnished as security should be sold at not less than 25 percent of its market value.

The house situated on Plot Number 7, Medium Density, Nyabisarye area comprising Title Number 5722 L.R. MWA, was sold last year in favour of Eurafrican Bank (T) Limited to satisfy a court’s decree of 196,133,538/62. Mr Marando has also filed a notice to show cause why Dr Mazara and his wife Keja Esther Mazara, who were guarantors of loan, should not be held responsible.

Hearing of the both applications was to take off on Wednesday before Judge Katherine Oriyo. The parties, however, agreed to address the court by filing written submissions. The judge, therefore, ordered advocate Dilip Kesaria, for the bank, to file on December 12, his submissions on the application for imprisonment and objection to the notice to show cause.

While Mr Marando, the judge ordered, would reply on January 9, and subsequently file his submissions in support of the notice to show cause why his client should not be committed to jail for failure to settle the loan the bank had extended to Musoma Diary Limited. The judge said she would give her ruling on the matter on March 3, next year.

It is alleged that Musoma Diary Limited took an overdraft facility of 100m/- from the bank long before its receivership. Thereafter, the company was placed under receivership. However, Dr Mazara continued to pay the loan using his personal fund since he and his wife were the guarantors of the loan, who had offered their residential houses as security.

Last year the bank decided to auction the house to recover the said loan. According to affidavits filed in court, at the time of sale of the house, the market value of the house was 750m/- and the forced sale value was 600m/-. The best reasonable price at that time was, therefore, 600m/-. Surprisingly, however, the house was sold at 75m/- only.

It is alleged that the decree holder (bank) did not give notice to the judgement debtors (Musoma Diary Limited, Dr Mazara and his wife) that amount obtained from sale could not satisfy the decree and a year later filed the application for their detention in prison.

Dr Mazara stated in one of his affidavits that after the sale of the house he complained to the court broker as to why the property was sold at a throw away price of 75m/-, while its value exceeded 600m/- and such sale did not satisfy the full claimed amount in the decree. He stated that the court broker informed him that once the security is sold the claim would be deemed to have been satisfied and whatever loss that remains was the business of the decree holder that is why the bank never demanded him to pay the balance.



Pia Nakumbuka Nyumba ya Cheo ilikuwa Valued at 600Mill, lakini iliuzwa kama 70Million
 
Nimeshtushwa na thamani ya mali zisizohamishika ambazo Mh. Yona na Mwenzake Mramba, waliziwekana kama rehani dhidi ya uhuru wao katika kesi inayowakabili ya matumizi mabaya ya madaraka yao.

Kilichinishtua sio uwezekano wa Mtanzania kuwa na mali nyingi kiasi hiki, la! Ila haijaniingia akilini namna gani mtumishi wa umma anaweza kupata mali nyingi kiasi hiki kutoka katika mshahara ama posho.

Je, walikuwa wafanyabiashara kabla ya kuwa mawaziri au kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi wa umma? Kuna mwenye kujua hilo?.....Naambatanisha.


Yona ajidhamini Wazomewa na kadamsanina waandishi wetu WAZIRI wa zamani wa Madini na Nishati, Daniel Yona, jana Jumanne, alikuwa kivutio na gumzo kubwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, alipojidhamini kwa mali zake mwenyewe zenye thamani ya Sh. bilioni 3.69 ili kuepukana na adha ya kurejea rumande ya Keko.

Wakati Yona alijidhamini kwa mali zake mwenyewe, Basil Mramba ambaye anashitakiwa naye kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka yao na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh. bilioni 11, alijidhamini kwa mali zake, kampuni na mali za watu wengine wawili, Hatibu Senkoro na Harun Mohammed zinazofikia Sh. bilioni 3,146,660,000.

Mmoja wa wadhamini hao wa Mramba, Senkoro sasa anafanya kazi katika kampuni ya Barrick ya Canada lakini yenye kuendesha migodi duniani kote ukiwamo wa dhahabu wa Geita aliko Senkoro. Kabla ya kujiunga na Barrick aliongoza kwa miaka mingi kampuni ya TDFL iliyokuwa ikuhusika na masuala ya fedha.

Mbele ya Hakimu Mkazi Hezron Mwankenja, Yona ambaye ni mshitakiwa wa pili kupitia mawakili wake, Stanslaus Boniface na Frederick Manyanda, aliwasilisha hati ya kwanza ya nyumba yenye namba 57467 yenye thamani ya Sh. milioni 443.

Hati ya pili iliyowasilishwa na waziri huyo wa zamani ilikuwa ya nyumba yenye namba 59935 yenye thamani ya Sh. bilioni 2.2 na ya tatu yenye namba 57230 yenye thamani ya Sh. 420,300,000. Nyumba zote hizo ziko Makongo Juu, Dar es Salaam.

Mapema kupitia kwa mawakili hao hao, Mramba ambaye ni mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, aliwasilisha hati ya nyumba yenye namba 42578 iliyoridhiwa na Senkoro yenye thamani ya Sh. milioni 397.

Aliwasilisha hati nyingine yenye namba 44755 Kitalu namba 138 Kitalu C ya Harun Mohammed yenye thamani ya Sh. bilioni 1,226,200,000.

Mramba pia aliwasilisha hati namba 7217 ya Kitalu 53 Msasani mali ya kampuni ya Kilimanjaro Mine Limited yenye thamani ya Sh. 976,420,000 na hati ya nyumba yake mwenyewe namba 40268 Kitalu namba 446 iliyopo Kawe, Dar es Salaam yenye thamani ya Sh. 547,400, 000.

Baada ya kupokea hati zote za washitakiwa zilizowasilishwa kupitia kwa mawakili wao, Hakimu Mwankenja alisema kwamba washitakiwa baada ya kushindwa kutimiza sharti la awali la kila mshitakiwa kulipa fedha taslimu Sh bilioni 3.9 walikwenda kwenye mahakama ya juu (Mahakama Kuu) kuomba kulegezwa kwa sharti hilo.

Sharti hilo lililegezwa kwa kutakiwa kila mshitakiwa kutoa hati za mali zenye thamani ya Sh bilioni 2.9, sharti ambalo washitakiwa walikuwa wametimiza kwa kuwasilisha hati hizo.

Hakimu Mwankenja alisema baada ya hati hizo kuhakikiwa na waendesha mashitaka, mawakili wa utetezi na Mahakama yenyewe na kwa kuwa hakukuwa na upande wowote uliowasilisha pingamizi kuhusiana na hati hizo, Mahakama iliridhia washitakiwa, ambao walikuwa chini ya ulinzi, waachiwe kwa dhamana hadi kesi itakapotajwa tena.

Baada ya kutoka kwa dhamana, washitakiwa hao watatakiwa kurejea mahakamani Januari 2 mwakani wakati kesi yao itakapotajwa. Kabla ya tarehe hiyo kuafikiwa na Hakimu Mwankenja, mawakili wa utetezi walijaribu bila mafanikio kuishawishi Mahakama ipange kesi hiyo itajwe Januari 5 mwakani.

Mbali na sharti la kila mmoja kuwasilisha hati za mali zenye thamani ya Sh bilioni 2.9, washitakiwa hao kila mmoja alitakiwa kusalimisha mahakamani hati zake za kusafiria na asitoke nje ya mkoa wa Dar es Salaam bila ya kibali cha Mahakama.

Kwa kupata dhamana jana ilikuwa ni furaha kubwa kwa mawaziri hao waandamizi wa zamani katika serikali ya Awamu ya Tatu, chini ya Rais Benjamin Mkapa. Dhamana hiyo ilitolewa wakati juzi watuhumiwa hao walikuwa wamekwama kuipata kutokana na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu kusema kwamba haikutoa hati ya watuhumiwa hao kuletwa mahakamani.

Kutokana na sababu hiyo Mahakama hiyo ilishindwa kushughulikia suala la kukamilisha dhamana yao iliyolegezwa masharti na Mahakama Kuu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Jaji Njengafibili Mwaikugile wa Mahakama Kuu, Dar es Salaam Ijumaa iliyopita alitoa amri ya kurekebishwa mara moja kwa sharti lililokuwa likiwataka watuhumiwa hao kila mmoja kutoa fedha taslimu Sh bilioni 2.9 ili wapate dhamana badala yake alisema kisheria mtuhumiwa anatakiwa apate dhamana kwa kutoa kiasi cha fedha au kuwasilisha hati ya mali yenye thamani sawa na kiwango hicho.

Baada ya amri hiyo ndipo juzi Jumatatu walipofikishwa Mahakama ya Kisutu ambako waligonga mwamba kwa kuwa Mahakama hiyo haikuwa na taarifa ya kuletwa kwao. Ilisema ilikuwa na taarifa ya kuletwa kwao jana Jumanne.

Hali haikuwa ya kawaida mahakamani hapo jana Jumanne baada ya washitakiwa hao kuletwa na kupata dhamana kwani pilika pilika za watu wa kawaida na wapiga picha wa vyombo mbalimbali za kutaka kushuhudia jinsi wanavyorudi ‘uraiani’ vilifanya eneo la Mahakama kuwa na vituko vya kukimbia hapa na pale.

Kwa takriban saa moja watu hao na wapiga picha walikimbia kutoka sehemu ya mbele ya Mahakama hadi ya nyuma kutafuta ni sehemu ipi kati ya hizo watakapotokea baada ya kutolewa kwenye chumba cha Mahakama walikopatiwa dhamana.

Hatimaye walitolewa kupitia mlango wa mbele. Patashika ya wapiga picha ilikuwa kubwa na washitakiwa hao walimulikwa na taa za kamera mfululizo kiasi cha Mramba ambaye kipindi chote cha kesi akiwa nje ya Mahakama alikuwa ‘bubu’ akiwa chini ya ulinzi, jana sauti yake ilisikika kwa mara ya kwanza akiwa ‘huru.’

“Pigeni zote, pigeni zote,” alisema Mramba akiwahimiza wapiga picha kuendelea kupata picha zake zinazomuonyesha anatoka mahakamani baada ya kupata dhamana.

Alikuwa akihimiza hivyo wakati anaelekea kupanda kwenye gari la kifahari lililokuwa limeegeshwa mbele ya lango kuu la Mahakama. Bila shaka gari hilo lilikuwa tayari kumpeleka nyumbani kuungana na familia yake iliyomkosa kwa wiki nzima baada ya kulazimika ‘kulala’ mapema kila siku akiwa rumande ya Keko.

Kama ilivyokuwa Jumanne ya wiki iliyopita wakati waliposhindwa sharti la kuwasilisha kila mmoja fedha taslimu bilioni 2.9 hivyo kulazimika kwenda Keko, kulikuwa na kundi la watu lililoonyesha hasira za wazi dhidi yao licha ya kuwapo askari na makachero mahakamani hapo.

Wakati Jumanne iliyopita Mramba na Yona walisindikizwa kwa kelele za ‘wezi hao, wezi,’ jana kila mmoja kwa wakati wake alisindikizwa kwa kelele za ‘mwizi huyo, mwizi huyo,’ gari lake lilipoondoka kwa kasi katika eneo la Mahakama.

Gari la kwanza kuondoka lilikuwa ni lile lililombeba Yona na la pili lilikuwa lililombeba Mramba na kufuatia na mengine ambayo bila shaka yalikuwa ni ya wana familia wa familia za washitakiwa hao wawili.

Mramba na Yona wote kwa pamoja wameshitakiwa kwa kuibeba kampuni ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Washington DC, Marekani ambayo ilikuwa ikifanya kazi ya uhakiki wa mapato ya madini ya dhahabu nchini.

Mawaziri hao wawili Jumanne ya wiki iliyopita walisomewa mashitaka yao na waendesha mashitaka kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Hezron Mwankenja, kukiwa na ulinzi mkali wa makachero na askari magereza wenye silaha.

Pamoja na kutoa upendeleo wa kuongeza mkataba wa kampuni hiyo ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation, Mramba na Yona wakiwa Waziri wa Fedha na Waziri wa Nishati na Madini, ilidaiwa waliisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh. bilioni 11 kutokana na kusamehe kodi kampuni hiyo kinyume cha sheria.

Makosa hayo yalielezwa mahakamani hapo kutendwa katika kipindi cha mwaka 2002 na mwaka 2007, ambako Mramba aliandaa na kutoa matoleo ya Gazeti la Serikali (GN) yenye namba 423/2003, 424/2003, 497/2004, 498/2004, 377/2005 na 378/2005 ambayo yalilenga kutoa msamaha wa kodi kwa Alex Stewart (Assayers) Government BC uliofikia kiwango cha Sh 11,752,350,148/- bila kuzingatia sheria ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Kwa mamlaka yao na nafasi zao, Mramba na Yona walidaiwa mahakamani hapo kwamba bila kuzingatia wajibu wao waliokabidhiwa na serikali waliingia mkataba ulioisababishia serikali hasara ya Sh 11,752,350,148/- kutokana na kampuni hiyo ya uhakiki wa dhahabu.

Ilidaiwa kwamba Mramba kupitia matoleo mbalimbali ya Gazeti la Serikali amewezesha kutolewa kwa msamaha wa kodi ya mapato iliyopaswa kulipwa na kampuni hiyo ya Alex Stewart kinyume cha sheria ya Kodi ya Mapato.

Kwa mujibu wa maelezo ya waendesha mashitaka hao, Mramba anadaiwa alitumia vibaya madaraka yake kwa kudharau ushauri wa TRA waliomtaka kutokubali kutoa msamaha wa kodi ya mapato kwa kampuni hiyo ya kigeni ambayo ililalamikiwa sana kwa kumega mapato ya dhahabu nchini.

Mawaziri hao wa zamani walituhumiwa pia kudharau maelekezo ya kamati ya ushauri ya serikali ambayo ilipendekeza kupelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali mkataba wa Alex Stewarts na badala yake waliongeza muda wa mkataba wa kampuni hiyo bila kuzingatia suala la kupitia upya ada iliyokuwa ikilipwa kwa kampuni hiyo na hivyo kuiingizia serikali hasara.

Katika kuongeza mkataba huo, Mramba na Yona walidaiwa kutumia vibaya madaraka yao kwa kumshirikisha Dk. Enrique Segura wa Alex Stewarts katika kuingia naye mkataba wa nyongeza ya miaka miwili kuanzia Juni 14, 2005 hadi Juni 23, 2007 bila kuzingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2002 na Sheria ya Madini ya mwaka 2002.

Mashitaka dhidi ya watuhumiwa hao yalifuatia kibali kilichotolewa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) Elieza Feleshi kutoa kibali kwamba viongozi hao waandamizi wametumia vibaya madaraka yao na wamesababisha hasara kwa mamlaka husika.
 
Nyumba ya 750million yauzwa 75million, ndio mambo hayo.
Milk factory owner opposes sale of his house
FAUSTINE KAPAMA
Daily News; Thursday,December 04, 2008 @21:15

Milk factory owner opposes sale of his house

The owner of Musoma Dairy Milk Factory, Dr Gideon Warioba Mazara, has opposed the sale of his 750m/- worth of his house and application for his detention in prison for allegedly failing to honour a court’s decree for payment of 136m/- loan with interests.

His advocate, Mr Mabere Marando, filed an application at the High Court’s Commercial Division, seeking orders to set aside the sale of his residential house situated at Musoma Municipality, which fetched a mere 75,100,000/-, contrary to the law of the land. The law requires that a house furnished as security should be sold at not less than 25 percent of its market value.

The house situated on Plot Number 7, Medium Density, Nyabisarye area comprising Title Number 5722 L.R. MWA, was sold last year in favour of Eurafrican Bank (T) Limited to satisfy a court’s decree of 196,133,538/62. Mr Marando has also filed a notice to show cause why Dr Mazara and his wife Keja Esther Mazara, who were guarantors of loan, should not be held responsible.

Hearing of the both applications was to take off on Wednesday before Judge Katherine Oriyo. The parties, however, agreed to address the court by filing written submissions. The judge, therefore, ordered advocate Dilip Kesaria, for the bank, to file on December 12, his submissions on the application for imprisonment and objection to the notice to show cause.

While Mr Marando, the judge ordered, would reply on January 9, and subsequently file his submissions in support of the notice to show cause why his client should not be committed to jail for failure to settle the loan the bank had extended to Musoma Diary Limited. The judge said she would give her ruling on the matter on March 3, next year.

It is alleged that Musoma Diary Limited took an overdraft facility of 100m/- from the bank long before its receivership. Thereafter, the company was placed under receivership. However, Dr Mazara continued to pay the loan using his personal fund since he and his wife were the guarantors of the loan, who had offered their residential houses as security.

Last year the bank decided to auction the house to recover the said loan. According to affidavits filed in court, at the time of sale of the house, the market value of the house was 750m/- and the forced sale value was 600m/-. The best reasonable price at that time was, therefore, 600m/-. Surprisingly, however, the house was sold at 75m/- only.

It is alleged that the decree holder (bank) did not give notice to the judgement debtors (Musoma Diary Limited, Dr Mazara and his wife) that amount obtained from sale could not satisfy the decree and a year later filed the application for their detention in prison.

Dr Mazara stated in one of his affidavits that after the sale of the house he complained to the court broker as to why the property was sold at a throw away price of 75m/-, while its value exceeded 600m/- and such sale did not satisfy the full claimed amount in the decree. He stated that the court broker informed him that once the security is sold the claim would be deemed to have been satisfied and whatever loss that remains was the business of the decree holder that is why the bank never demanded him to pay the balance.

View Visitor's comments on this Story
 
Mwanahalisi, masahihisho kidogo SIO WEZI WA EPA, bali ni WATUHUMIWA WIZI WA EPA, na fomula ya dhamana iko kwenye sheria lakini Hakimu mmoja tu pale Kisutu alishindwa kuisoma vizuri hio sheria na hivyo kupelekea watu kuamini masharti ya dhamana yamelegezwa! Ingekuwa ni nchi nyingine Hakimu Mwankenja angeshughulikiwa kwa kusababisha mchanganyo wa mawazo kwa wananchi, na pengine watuhumiwa wangeweza pia kumdai fidia kwa mateso yasiyo ya lazima aliyowasababishia, riba watakayotoa kwa waliowakopesha mapesa yote yale! Usibweteke tu hawa ni watuhumiwa hatujawapata wezi wetu, najua tutawapata tu!
 
Inakuaje hizi nyumba walizoweka thamani zilikuwa MILLION 5 wakati wananunua SERIKALINI na leo hii baada ya miaka mitano zina thamani YA MAMILLION?

He! Kumbe ni nyumba zetu ndizo zimewatoa lupango!!!
 
Wakuu,
Kinachowashangaza hapa ni kitu gani lakini?..
Hivi kweli mlikuwa hamfahamu kwamba tulikuwa tunaibiwa miaka yote, leo mnakuja shangaa kiasi cha fedha inachozungumziwa hapa..
Toka mwaka 2001/2 kama sikosei nimekuwa nikipiga vita habari ya viongozi kujilimbikiza mali wakiwa madarakani. Sioni kipya kabisa zaidi ya ukweli huu kuwa wazi kwenu, jambo ambalo wengi toka enzi za Nyenzo, Bcs hawakuamini kuwa tunaibiwa isipokuwa mimi ni Mjamaa, niliyekunywa maji ya Uhuru - Mwalimu.
Nitarudia kusema hakuna viongozi matajiri duniani kama viongozi wa nchi maskini hasa zile zilizoingia Ubepari wakati wananchi wake wote ni maskini.

Ubepari una mwanzo na mwanzo wake ni Mtaji, sasa ikiwa wananchi wote maskini huo mtaji utatoka wapi?..nakumbuka maneno ya mwalimu kuwa tunachofanya ni kugawana Umaskini..Utajiri wetu ni sinia la Pilau siku ya maulidi..na mfumo mzima wa mageuzi yetu ya uchumi ni Darwin's nightmare!
China sio wajinga kuingia Ubepari kwa tahadhari na kuyaweka maslahi ya taifa mbele ya Ubepari wenyewe - Watu na Mazingira, bado ni somo kubwa la kuanzia...

Mimi I hope kukamatwa kwa hawa jamaa Yona na Mramba ni mwanzo wa kumvuta Shark mkubwa - MKAPA, nje ya hapo hakuna jipya - Utajiri wa viongozi hawa sii mgeni kwa wale wanaowafahamu..
 
Imetolewa mara ya mwisho: 07.12.2008 0006 EAT

• Baada ya Mramba, Yona kuonja jela...Wasomi wasema 'ni zamu ya' Mgonja

*Wadai ndiye mtaalamu 'anafahamu' zaidi
*Wasisitiza sheria haibagui, haina uhasama

Na Reuben Kagaruki

MAGWIJI wa sheria wamehoji jinsi ambavyo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Bw. Gray Mgonja, alivyosalimika sakata ambalo aliyekuwa waziri wake, Bw. Basil Mramba, alikamatwa na kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya kutumia ofisi yake vibaya na kulisababishia taifa upotevu wa zaidi ya sh bilioni 11.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, mwanasheria maarufu nchini, Profesa Abdallah Safari, alisema haiingi akilini kuona Katibu Mkuu ambaye ni mtaalam, akiachwa kwenye kesi hiyo.

Alipoulizwa kama ni sahihi kwa Bw. Mgonja kutohusishwa kwenye mashitaka yanayomkabili, Bw. Mramba alidai wadhifa wa uwaziri ni wa kisiasa na mtendaji ni katibu mkuu ndio maana yanaibuka maswali mengi.

Kuhusu kauli za baadhi ya ndugu wa washitakiwa hao, Bw. Mramba na Bw. Daniel Yona kuwa nyuma yao wapo watu wengi wanaostahili kuchukuliwa hatua, Profesa Safari ilionekana kukubaliana nao.

Alisema ufisadi katika akaunti ya EPA ni sehemu ya vitendo hivyo, kwa kuwa kuna ufisadi wa aina nyingi uliofanyika nchini. "Ufisadi mkubwa uliofanyika ni kuchukua nyumba za Serikali na kuziuza, wanapolalamika wanayajua haya," alisisitiza Profesa Safari.

Akizungumzia hilo, Mhadhiri wa Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Sengondo Mvungi, alisema kuna makosa ambayo Bw. Mramba alitenda na anaweza kushitakiwa peke yake na inawezekana yakawepo makosa ambayo wanaweza kushitakiwa wote.

Alisema ili kubaini hilo hapo ndipo unahitajika uandishi wa habari za uchunguzi. Alisema ili kujua kama Bw. Mgonja anatakiwa kuunganishwa na Bw. Mramba inabidi waandishi wa habari wasiishie kusoma hati ya mashitaka iliyopo mahakamani.

"Baada hapo mnachotakiwa kufanya ni kuchunguza ili kuona makosa aliyofanya Mramba yanamhusisha na Mgonja au hapana," alisisitiza.

Dkt. Mvungi alisisitiza kuwa tuhuma dhidi ya viongozi hao hazikuanzishwa na CCM bali viongozi wa vyama vya upinzani, hivyo ni rahisi kufuatilia ili kujua kama makosa yanayokabili Bw. Mramba anamhusisha na aliyekuwa katibu mkuu wake.

Hata hivyo alisema ana uhakika tuhuma ya ununuzi wa rada itabeba wengi. Alitaja tuhuma nyingine za ufisadi ambazo ana imani zitabeba watu wengi kuwa ni pamoja na ile ya ununuzi wa ndege ya Rais, mkataba wa IPTL, Kiwira na EPA.

Alipoulizwa kama ni sahihi kwa kesi ya Bw. Mramba na Yona kufunguliwa katika mahakama ya Kisutu, Dkt. Mvungi alisema sheria imeelekeza kuwa zipo kesi zinazotakiwa kuanzia mahakama za chini au mahakama za juu.

Dkt. Mvungi alipoulizwa kama ni sahihi kuwashitaki watuhumiwa wa EPA waliorejesha fedha walizokuwa wamejichotea alijibu; "Utawala wa sheria hauwezi kutendea wananchi tofauti na wala Rais hawezi kubagua."

Alisisitiza kuwa Rais ana mamlaka ya kusamehe watu waliokwisha kuhukumiwa na mahakama na sio wale wanaokabiliwa na tuhuma. Dkt. Mvungi alipoulizwa kama kufikishwa mahakamani kwa Bw. Mramba na Bw. Yona kunaweza kuamsha chuki na uhasama ndani ya jamii alijibu;

"Watendaji wa umma wanapopewa nyadhifa za kuongoza, wanapewa kwa sababu ya usafi wao, wanapo boronga sheria haiwezi kuwaachia kwa kuogopa uhasama."

Mwezi uliopita mawaziri wawili wa zamani Bw. Mramba na Bw. Yona, walifikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya kusababisha upotevu wa zaidi ya Sh bilioni 11.

Mawaziri hao walikaa rumande kwa siku kadhaa na wiki hii walipata dhamana na kurejea uraiani.
 
Back
Top Bottom