kitendo cha kusema ulikuwa na uhakika kwamba anachepua mpaka hapo ushaonyesho udhaifu mkubwa sana na wa ajabu...kama ulikuwa na uhakika anachepuka ilibidi uanze kutibu tatizo hilo ili asichepuka ikiwa ni pamoja na kumuonyesha kuwa ajue kuwa umeshajua anachepuka...ila we unaomba ushauri baada ya kugundua anafanya bila kinga, ina maana kwamba kuchepuka ulikuwa umeshahalalisha ila kujua kuwa hatumii kinga ndo umeshtuka!! haya ni maajabu, hakikisha mmeo hachepuki, rudisha mapenzi ya dhati, ili aanze kusahau wa nje, mi sitoshangaa akikuletea mtoto, we unajua mmeo anachepuka afu unakaa kimya.....acha kujishusha hadhi yako kiasi hicho mbele ya mmeo. suala ni dhibiti asichepuke, kwahiyo wataka si uliotuomba ushauri tukushauri namna ya kumuambia mmeo atumie kinga akiwa anachepuka! kama umejua anachepuka na umeangalia tu leo washtuka kujua hatumii kinga, safari ijayo atahamia hukohuko...acha kulea tatizo hili ktk familia yako, matokeo yake ni makubwa sana anaweza akahamishia huduma zote kwa mchepuo.ushauri nasema dhibiti mmeo asichepuke kabisaaaa