Maumivu makali

Maumivu makali

Mimi ni dada wa miaka 38 nina watoto 3 kwenye ndoa nina miaka 13, mume wangu ana umri miaka 52.

Mwaka huu mwanzoni nilifuma sms kwenye simu ya mume wangu akijibu sms ya mchepuko.

Ni hivi mchepuko alimwandikia kwamba ana mimba yake, yeye akajibu kwamba sio mimba yake siku ambayo walikutana yeye akumaliza (sijui alikuwa na mana gani). Hiki kitu kimeniumiza sana moyo.

Nilikuwa nina uhakika kwamba anachepuka lakini nikajipa moyo anatumia condom. Baada ya kufuma hiyo sms ndio nikaamini kwamba ana kwenda bila kinga. Hiki kitu kinaniumiza sana moyo sijui nifanye nini ili nisahau, ukizingatia magojwa yalivyo mengi! Inatisha kwelikweli.

Naomba ushauri nitumia njia gani ili nikifute kwenye mawazo yangu.

Mwathirika.


Pole sana mpendwa, hizo ni changamoto tu ila zisikuumize bali zikufunze ujue tatizo lilipo kisha ulitatue. Usikimbie wala uckacrike kwani unazidi kumpa go ahead.
Cha mcngi yajibu haya maswali;
1. Akija nyumbani toka kazini huwa unampokeaje? Unampa mda kidogo wa kumsalimia na kujua mawili matatu aliyoyapitia tangu atoke asubui?

2. Baada ya hapo unampa huduma gani kuondoa uchovu, eg maji ya kuoga, kuandaa msosi nk

3. Mawasiliano yenu yakoje, we ni mtu mbishi, wa kupiga kelele akikosea, ama wa kununa ovyo?

4. Ukiwa na jambo la kimapenzi ama la kimaendeleo unamshirikishaje? Faragha ama ni mtu wa kubeba moyoni?

5. Je kwenye tendo takatifu unajumuika vip, unajiandaa vp na usafi wako kwa ujumla ukoje?

6. Unafahamu vtu gani anapenda? Anavipata vyote? Su unajitahidi kiasi gani kujua flavour zake?

7. Unaufahaamu mchepuko wake, ukoje ukijilinganisha nae? Unajiweka sawa kama awali ama cku hizi mambo mengi?


8. Baada ya tukio hilo, tabia yako imekuaje hapo ndani?

9. Je, wewe ama yeye, kuna anayetumia kilevi?

10. Je, unamshirikidhs Mungu wako msmbo haya na kuomba hekima?


Ni hayo tu kwa sasa, ila all in all, stay calm, be humble and wise in all tou talk and do. Pia acha kuhoji nafsi yako sana juu ya hili kwani ndo maumivu yanaongezeka.

Iambie akili au moyo tulia ni maisha.

Usikae mda mrefu bila kula kuepuka matatizo mengine.

Safari bado ni ndefu hivyo funga tumbo, jikaze, wanao wasijue sana au kabisa.


Stay Alive! And may God give you strength.
 
Hahahahhahahahah acha nicheke kwanza

Ni hivi niliolewa 2010 na mwanaume niliyempenda kwa moyo wote.

Ndoa ikawa tamuuuuu sanaaa tamu kweli (nilikuwa nawaambia rafiki zangu mume wangu hata aje mwanamke ameumbwa vipi hajavaa nguo hata moja hatamtamani, nilimuamini sana na before marriage tulishakaa kama miaka mitano hivi so nilijiaminisha).

Basi bwana mambo yakabadilika weeee hadi ikafika muda mume nyumbani harudi hata wiki ila kazini yupo muda wote. Iliendelea hivyo hadi tukatengana (nakata story)

Basi baadae tukasuluhishwa pale tukarudiana (simu pia ilichangia hadi tukatengana), basi maisha yakaendelea ila ule upendo ukawa umepungua kwa upande wangu, mume akajitahidi sana kunirudisha kawaida akawa mtulivu kweli kweli taratibu (na wanawake tulivyo) nikajikuta narudisha upendo vile vile japo kuna muda nakuwa na wasi wasi.

(Tuokoe muda), kuna siku nikawa naumwa nimelala nimeshindwa hata kupika nikampigia simu kumwambia, akarudi kama saa 3 usiku kakuta nimelala, tumesalimiana kaniuliza unaendeleaje na vitu kama hivyo, baadae pale kitandani akakaa ila hatazamani na mimi akawa busy na simu hadi saa tano (me nilipitiwa na kausingizi ka homa) nashtuka nakuta mtu yupo busy bado, akaniomba maji ya kuoga ki ukweli sikuwa naweza hivyo nikamuomba ajiandalie alichukia kwa sababu nilimzoesha ni lazima ni muandalie maji na lazima tuoge wote hata kama nimeshaoga ila akaanda akaenda kuoga.

Mimi nikawa naitamani sana ile simu, nikaishika yeye yupo bafuni, yaani kufungua tu kwenye sms nakutana na chatting moja mataa (baby, honey swty darling majina yote yale mazuri mazuri unayoyajua) ila kubwa zaidi ni sms za pitia ofisini nikuone mwanaume ndo anamtumia mwanamke nimekumiss nahitaji kufanya mapenzi na ww, your so sweet na vitu kama hivyo mwisho kabisa wakamalizana na hii, "kesho saa tisa basi tukutane kule kule wewe tangulia ukifika niambie" (nilivyofika hapa nilipona nikawa mzima kabisaa).

Basi mume katoka kuoga nikamuuliza, jibu lake sasa hahahahahahahah "alikwambia ushike simu yangu nani umeyataka" (nililia sana zaidi ya sana haielezeki kumbuka me nilikuwa naumwa nipo kitandani yeye ndo anafanya hayo). Niliumia sana.

Nikajitahidi nijidai mkali nikaishia kupewa maneno ya kuumiza zaidi.

Kweli Mungu yupo. Nilijikuta nawaza niamke nisali tu, basi hivyo hivyo huku nalia nikaingia kuoga nikapata udhu vizuri nikaswali (me ni muslim), niliswali huku machozi yanatoka, niliamua kumlilia Mungu nilitumia muda mrefu sana hadi pale moyo wangu ulivyopoa.

Nilivyoridhika nikapanda kitandani yeye alivyoona ninaswali akalala, basi nikajiandaa kulala ila kabla nikamuamsha nikamshika mkono nikamwambia "nisamehe mume wangu", akaniuliza kwanini nikamjibu "kwa sababu nimeshika simu yako nisingeshika haya yote yasingetokea, nisamehe sana, nakupenda mume wangu".

Mh machozi yakamtoka akaniambia nisamehe pia mke wangu, nikamjibu nimekusamehe na moyo wangu mweupe, sina kinyongo na wewe, akaniambia nakupenda mke wangu hawa nawapotezea muda tu ndio maana nimekuoa wewe, nikamjibu najua mume wangu na nakuahidi sitashika simu yako tena. Baada ya HAPO SIKUSHIKA SIMU YAKE TENA NA SITASHIKA SIMU YA MWANAUME TENA

Ila baadae tuliachana. So kushika simu ya mtu ni kujitafutia matatizo, mwanaume ukigundua hajatulia unaamua tu au kumvumilia (ndo ile kwa shida na raha) au kuachana nae ila kushika simu unajiumiza na ukimuuliza anaweza kukujibu ukahisi dunia nzima inakuona unavyojibiwa

kwenye hii post kuna sehemu nimecheka hadi machoz ila pole aiseee. hawa viumbe wanadamu both ke na me ni shidaaaaa
 
Hahahahah wapi hapo?

pale ulipojitahid kuwa mkali hahahahah

hiv nikuulize maana ishapita muda; si kuna wakat ukikumbuka huwa unacheka??
maana mie michoz haikukauka mapema
 
pale ulipojitahid kuwa mkali hahahahah

hiv nikuulize maana ishapita muda; si kuna wakat ukikumbuka huwa unacheka??
maana mie michoz haikukauka mapema

Teh teh, kuna muda nacheka saaanaaaa
 
Teh teh, kuna muda nacheka saaanaaaa

cheka tu LUV maana hakuna namna. yaan kila nikikumbuka nacheka. nahis ka nakuon Vile ulivyojiandaa gafla ukanyweaaa.
mbavu zangu mieeee
 
cheka tu LUV maana hakuna namna. yaan kila nikikumbuka nacheka. nahis ka nakuon Vile ulivyojiandaa gafla ukanyweaaa.
mbavu zangu mieeee

Hahahahahah haya bwana, umenifanya nicheke aiseee
 
Back
Top Bottom