Mauaji yaliyojaa utata

Mauaji yaliyojaa utata

NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Tano.
Todd Lewis, muigizaji aliyekuwa na jina kubwa duniani alikuwa akitoka katika Uwanja wa Kikapu wa Stapple Center kuangalia mechi ambayo iliwakutanisha wenyewe, La Lakers ikiongozwa na Shaq O’ Neil ambayo ilikuwa ikipambana na Chicago Bulls.
Alikuwa ameamua kusafiri kutoka jijini New York mpaka Los Angeles kwa ajili ya kuangalia mechi hiyo. Alipenda mchezo wa kikapu na hakutaka kabisa kukosa mchezo huo ambao ulikuwa ukizikutanisha timu kongwe, kali ambazo zilikuwa na nguvu mno katika kipindi hicho.
Nje ya uwanja huo, watu wengi walikuwa wakimsubiri, alikuwa na jina kubwa, ukiachana na mastaa wengi wa mchezo wa kikapu, pia siku hiyo Todd alikuwa gumzo kubwa, ndani ya uwanja huo, watu wengi walitaka kupiga naye picha, pale alipokuwa amekaa, watu walimsogelea na kuanza kujifotoa picha kadhaa na mpaka mchezo huo unamalizika, kulikuwa na watu wengi waliopata nafasi ya kupiga naye picha.
Wengine hawakuridhika, hata walipokuwa wakitoka, bado mashabiki walikmfuata Todd, walitaka kupiga naye picha huku wengine wakitaka kusainiwa vitabu vyao.
Hayo yalikuwa maisha ya usupastaa, walimheshimu kwa kuwa aliifanya kazi yake ipasavyo, wengi walipenda kutazama filamu zake, kwa kifupi, Todd aliwavutia watu wengi mno.
Alipomaliza kuwasainia watu vitabu vyao na hata kupiga nao picha, kama kawaida akaifuata gari yake ya kifahari, Ferrari nyekundu na kisha kuingia, kilichofuata ni kuanza safari ya kuelekea hotelini kabla ya kurudi New York alipokuwa akiishi siku inayofuata.
Akaliwasha gari hilo na kuondoka mahali hapo. Moyo wake ulijisikia faraja, hakuamini kwamba mwisho wa siku angekuwa na umaarufu mkubwa kama aliokuwa nao katika kipindi hicho.
Katika kipindi cha nyuma alipokuwa akianza, mambo yalikuwa magumu mno, alipambana usiku na mchana lakini mwisho wa siku, alifanikiwa kuwa kama alivyokuwa, hakukuwa na kitu kingine kilichokuwa kikiendelea zaidi ya kukusanya fedha na kuwa nazo zaidi ya zile alizokuwa nazo.
Wakati safari ikiendelea na kuyakuta makutano ya Barabara za St. Barnaba na Morovian ambayo ilikuwa ikienda mpaka katika Mtaa wa Butterfly uliokuwa umbali kama wa kilometa tatu, akashtuka baada ya kuona gari moja likija kwa kasi nyumba yake, lilikwenda mbele yake kwa mwendo wa kasi na kisha kusimama kwa katikati ya barabara, tena kiubavuubavu.
Kama haukuwa umakini wake mkubwa, basi angeweza kuligonga gari hilo. Kwa ustadi mkubwa, Todd akafunga breki na kisha kusimama, alibaki akihema kwa nguvu, mbele yake ilionekana ajali kubwa ambayo pasipo kutumia uwezo wake basi angeweza kuligonga gari hilo.
Huku akijiuliza ni kitu gani kinaendelea, wanaume wawili wakateremka kutoka kwenye ile gari na kuanza kuelekea kule alipokuwa. Hakujua watu hao walikuwa wakina nani na walihitaji nini kutoka kwake.
Mahali hapohakukuwa na magari, ilikuwa usiku sana na magari hayakuwa yakipita mara kwa mara, hasa katika barabara hiyo ya magari yaendayo kasi. Akashindwa kuliwasha gari lake, watu wale walikwenda kwa kasi mpaka pale lilipokuwa gari lake, wakamwambia afungue mlango vinginevyo wangempiga risasi humohumo.
Hakuwa na jinsi, hakutaka kupinga, kitu cha kwanza kabisa, akashusha kioo cha mbele cha mlango wa upande mwingine, mwanaume mmoja akaingia na kumwamuru aendeshe mpaka sehemu waliyotaka wao waelekee.
“Naomba uniache, kama unataka gari chukua,” alisema Todd huku akitetemeka.
“Unadhani sisi tunataka gari?” aliuliza mwanaume huyo huku akiwa na bastola mkononi mwake.
“Hata kama unataka kiasi chochote cha fedha, nitakupa, naomba uniache...” alisema Todd, tayari machozi yakaanza kububujika mashavuni mwake.
Mwanaume yule mwingine akapita upande wa pili, akaufungua mlango na kumshusha Todd kisha kumpeleka katika gari lao walilokuja nalo huku yule mwingine akiachwa katika gari lile kwa ajili ya kuondoka nalo.
Kila kitu kilichokuwa kikifanyika mahali hapo, kilifanyika kwa haraka sana, tukio zima lilichukua sekunde arobaini na tano tu, tayari wakaondoka huku wakiwa na Todd ndani ya gari.
“Naombeni mniacheee...” alisema Todd.
“Hutakiwi kupiga kelele...” alisema mwanaume mmoja huku akimnyooshea bastola.
“Nimefanya nini? Naombeni msiniue..” alisema Todd.
“Kwani kila anayeuawa kuna baya amelifanya? Hakuna kitu kama hicho, kuwa mpole,” alisema mwanaume huyo.
Baada ya hapo, hawakutaka kuongea kitu chochote kile, wakaondoka naye huku garini wakiwa kimya, kwani hata Todd naye aliyetaka kuzungumza maneno mengi aeleweke na hivyo kuachwa, aliambiwa akae kimya kwani suala la kumuua lisingeweza kuzuilika hata kidogo.
Walikwenda mpaka katika barabara nyingine ya Queen Elizabeth I ambayo ilikuwa ikienda moja kwa moja mpaka kwenye jumba la makumbusho ya Lincoln, hawakufika huko, wakakata kulia na kisha kuchukua barabara nyingine ambayo iliwapeleka mpaka katika sehemu ambayo haikuwa na watu, giza lilitawala, gari likasimamishwa mahali hapo.
“Naomba mnisamehe....”
“Halafu?”
“Niondoke, nitawalipa kiasi cha fedha chochote mnacholkitaka....”
“Halafu?”
“Naomba mnisamehe...”
Hawakutaka kupoteza muda, saa zao zilionyeshwa kwamba tayari ilikuwa ni saa nane za usiku hivyo walitakiwa wafanye haraka, wamuue na kisha kuendelea na mambo yao.
Walichokifanya ni kumkaba kooni, tena kwa nguvu kuhakikisha anakufa na kisha kufanya kile walichoambiwa kukifanya. Mwanaume mmoja mwenye nguvu ndiye aliyetumika kumuua Todd ndani ya gari hilo.
Dracula hakutaka kwenda katika lile gari kwani aliamini kwamba vijana wale wangefanya kama jinsi alivyowapa maagizo, kweli wakafanya. Kilichofuata baada ya kuhakikisha kwamba Todd amekufa ni kumchoma sindano iliyokuwa na madawa aina ya cocaine, walipomaliza, wakachukua nailo zenye unyevuunyevu ambazo kwa kutumia utaalamu wao waliweza kuweka alama za vidole za Benjamin na kisha kuziweka katika shingo ya Todd na sehemu nyingine za mwili.
“Vipi?”
“Tayari!”
“Mbebeni mkamuweke ndani ya gari lake, pia wekeni na hizi fedha,” aliagiza Dracula huku akiwapa noti ambazo zilitakiwa kuwekwa ndani ya gari hilo, vijana wale wakafanya kama walivyoagizwa, wakaubeba mwili wa Todd na kisha kuupeleka garini mwake na kuziweka noti zile.
“Tuondokeni!” alisema Dracula baada ya kumaliza kila kitu. Wakaondoka mahali hapo huku kila mmoja akiwa na furaha ya kukamilisha kazi waliyokuwa wamepewa.
****
Hakukuwa na mtu aliyeamini mara baada ya taarifa juu ya kifo cha Todd zilipotolewa katika vyombo mbalimbali vya habari nchini Marekani. Wengi walipigwa na bumbuwazi, kile walichokisikia, hakikuaminika kwao kwamba yule muigizaji, mwenye jina aliyekuwa akivuma sana kipindi hicho, Todd Lewis alikutwa amejidunga madawa ya kulevya kwakujiovadozi.
Watu wakapigiana simu, kila aliyesikia, hakutaka kukubaliana na habari hiyo kwani miongoni mwa watu waliokuwa wakifanya vizuri kipindi hicho, alikuwa huyo Todd, sasa kwa nini afe mapema hivyo? Tena mbaya zaidi alikutwa akiwa amejiovadozi madawa ya kulevya kitu ambacho kiliwachanganya watu wote kwani Todd hakuwa mtumiaji wa madawa hayo hata mara moja.
Wengi wakaenda katika Hospitali ya Calvary kujionea, huko, watu walikuwa wakilia kwani ndipo walipopata taarifa kamili kwamba muigizaji huyo alikutwa ndani ya gari yake ya kifahari ya Ferrari akiwa amejiovadozi madawa ya kulevya.
“Haiwezekani Bwana! Huyu jamaa hakuwa mlevi kabisa,” alisema jamaa mmoja.
“Ndiyo! Hata mimi nimeshangaa sana, yaani Todd awe mlevi wa madawa ya kulevya! Haiwezekani hata kidogo,” alisikika jamaa mwingine.
Kila mmoja alikuwa sahihi kabisa, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa na shaka na Todd kwamba alikuwa mtumiaji wa madawa hayo, taarifa hizo zikaendelea kusambaa kila kona mpaka ndani ya saa moja tu, dunia nzima ilijua nini kilitokea nchini Marekani.
Hofu zikaanza kutanda, taarifa zilizosema kwamba ndani ya gari la marehemu kulikutwa noti za fedha kutoka nchi mbalimbali ziliwashtua sana kwani hata siku ambayo Carter alikutwa akiwa amekufa ndani ya chumba cha hoteli, fedha kama hizo zilikutwa kitu kilichowafanya watu kuona cha kawaida ila baada ya fedha hizo kukutwa ndani ya gari hilo, wakagundua kwamba inawezekana hizo fedha zilibeba ujumbe fulani.
“Kama huyu Benjamin ndiye aliyemuua Carter, basi inawezekana akawa amemuua na Todd pia,” alisema jamaa mmoja wakati alipokuwa supamaketi, katika sehemu ya kuuzia magazeti na majarida mbalimbali.
“Inawezekana kabisa...hebu tuwasikilizie polisi tuone watasemaje,” alisema jamaa mwingine.
Hilo ndilo lililokuwa vichwani mwa watu wengi, kila aliyesikia namna gari hilo lilivyokutwa, alikuwa na uhakika kwamba muuaji alikuwa yuleyule, kijana wa chuo mwenye akili nyingi, Benjamin Saunders.
Hilo ndilo lililotokea, baada ya siku mbili, taarifa zikatolewa kwamba alama za vidole vya Benjamin vilikuta katika mwili wa Todd, yaani kabla ya kumchoma sindano, alimkaba kooni na kumuua na ndipo alipofanya mambo mengine likiwepo lile la kumchoma sindano ya madawa ya kulevya ili ionekane kwamba alikuwa amejiovadozi.
Hakukuwa na mtu aliyejua sababu ya Benjamin kuwaua watu maarufu, wengi waliuliza, kwenye mitandao wakatoa maoni yao lakini hakukuwa na mtu aliyefahamu lolote lile juu ya sababu ya Benjamin kuwaua watu maarufu na kisha kuacha noti za fedha mbalimbali karibu na miili yao.
“Ila kwa nini anawaua watu maarufu?’ aliuliza mwanamke mmoja.
“Hata mimi sifahamu! Kwanza nashangaa...”
“Halafu nasikia huyu Benjamin mwenyewe ana akili sana darasani.”
“Hata mimi nimesikia hivyohivyo na watu walipokwenda, wakakuta kweli ana akili sana, inawezekana ndiyo ikawa sababu ya kuwasumbua polisi na wananchi kumtia nguvuni,” alisema jamaa mmoja.
Bado watu walitakiwa kumtafuta Benjamin lakini hakukuwa na yeyote aliyempata, kiasi kikubwa cha fedha zaidi ya dola milioni ishirini na tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni hamsini kilitolewa lakini bado majibu yalikuwa yaleyale kwamba mitaani hakuonekana kabisa.
Maofisa wa FBI walikuwa na kazi kubwa, hakukuwa na aliyeamini kwamba mpaka muda huo Benjamin hakuwa amepatikana. Taarifa zilizopelekwa katika meza ya mkuu wa kitengo chao zilisema kwamba walitakiwa kupewa muda zaidi kwani inawezekana kulikuwa na mtu hatari ambaye alikuwa akimlinda Benjamin ili asiingie katika mikono yao.
“Kwa hiyo tumeshindwa?” aliuliza mkuu wa FBI, Bwana Connery Gibson.
“Hapana!”
“Sasa mbona hapatikani?”
“Ngoja tuendelee nadhani kuna kipindi tutampata tu.”
Hakukuwa na muda mwingine wa kupoteza, kama kusubiri, walisubiri kwa kipindi kirefu lakini hakukuwa na mafanikio yoyote yale, kuna kipindi walijiona kama kushindwa hivyo walitakiwa kuwasiliana na Shirika la Kijasusi la FBI ili wawasaidie kwani huyu Benjamin, japokuwa walijua kwamba hakuwa polisi au mtu yeyote mwenye uwezo wowote wa kijeshi lakini alikuwa mgumu mno kupatikana.
Walichokifanya ni kujiongeza tu, wakawagawa vijana wao katika miji mingine kama Los Angeles, Miami, Texas na sehemu nyingine ili kuhakikisha Benjamin anapatikana haraka iwezekanavyo.
“Nadhani hatotushinda tena, si ndiyo?”
“Tutegemee hilo mkuu!”
****
Harry alichanganyikiwa, hakuamini kile alichokuwa amekiona kwamba muigizaji maarufu duniani kwa kipindi hicho, Todd Lewis aliuawa ndani ya gari lake huku wauaji hao wakitaka kuionyeshea dunia kwamba alijiovadozi madawa ya kulevya kitu ambacho hakikuwa kweli kabisa.
Kilichomchanganya zaidi ni alama za vidole zilizopatikana ndani ya gari lile na hata katika mwili wa Todd ambazo zilionyesha kwamba ni Benjamin ndiye aliyefanya mauaji hayo.
Hapo ndipo alipoamini kwamba Benjamin hakuhusika katika mauaji, kulikuwa na watu wengine waliokuwa wakiyafanya huku wakiweka alama za vidole vyake katika kila tukio walilolifanya.
Alimwangalia Benjamin mara mbilimbili, hakuamini kilichokuwa kimetokea, alimuonea huruma sana kwamba inawezekana vipi mtu auwe na kisha kuweka alama za vidole vyake? Alimuuliza Benjamin lakini mwanaume huyo alimwambia ukweli kwamba hakujua kitu chochote kile.
“Sifahamu!” alisema Benjamin.
“Kuna kitu unajua!”
“Harry! Sifahamu chochote, huyu mzee Seppy ndiye anahusika, yaani ni lazima dunia ijue kwamba yeye ndiye anahusika, vinginevyo, nitahukumiwa kwa mauaji ambayo sikuyafanya,” alisema Benjamin.
“Tutatoa vipi taarifa polisi? Watakukamata!”
Huo ndiyo ulikuwa mtihani mwingine, hawakujua ni kitu gani walitakiwa kufanya, hawakuwa na ushahidi wa kutosha hivyo kama wangekosea sehemu moja basi lingekuwa tatizo kubwa kwao, walitakiwa kujipanga ili hata kama watakwenda kutoa taarifa polisi basi kusiwe na tatizo lolote lile.
David ndiye alikuwa na ushahidi kamili lakini bado kulikuwa na kitu kimoja kilichokuwa kikiwatatiza, kila mauaji yalipotokea, kulikuwa na fedha zilizokuwa zikiachwa, zile fedha zilimaanisha nini? Kila walichojiuliza, walikosa jibu.
“Sijui zinamaanisha nini, ila kama nikipewa muda, nitaweza kufahamu tu, kuna kitu,” alisema Benjamin huku akionekana kama mtu aliyekuwa akijifikiria sana.
“Hili ndilo la msingi, sidhani kama hata FBI watakuwa wanajua maana, huu utakuwa ni ujumbe, ujumbe gani sasa? Hebu tuhangaike mpaka tufahamu,” alisema Harry.
Wote wakakubaliana na kuingia kazini kuhakikisha wanajua kwanza maana ya zile fedha za noti zilizokuwa zikiwekwa katika mauaji yaliyokuwa yakitokea.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi
Thanks

Sent using Jamii Forums mobile app
 
shukrani Madame S, japo na mimi ni mfatiliaji wa kimya kimya siku nyingi
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Tano.
Todd Lewis, muigizaji aliyekuwa na jina kubwa duniani alikuwa akitoka katika Uwanja wa Kikapu wa Stapple Center kuangalia mechi ambayo iliwakutanisha wenyewe, La Lakers ikiongozwa na Shaq O’ Neil ambayo ilikuwa ikipambana na Chicago Bulls.
Alikuwa ameamua kusafiri kutoka jijini New York mpaka Los Angeles kwa ajili ya kuangalia mechi hiyo. Alipenda mchezo wa kikapu na hakutaka kabisa kukosa mchezo huo ambao ulikuwa ukizikutanisha timu kongwe, kali ambazo zilikuwa na nguvu mno katika kipindi hicho.
Nje ya uwanja huo, watu wengi walikuwa wakimsubiri, alikuwa na jina kubwa, ukiachana na mastaa wengi wa mchezo wa kikapu, pia siku hiyo Todd alikuwa gumzo kubwa, ndani ya uwanja huo, watu wengi walitaka kupiga naye picha, pale alipokuwa amekaa, watu walimsogelea na kuanza kujifotoa picha kadhaa na mpaka mchezo huo unamalizika, kulikuwa na watu wengi waliopata nafasi ya kupiga naye picha.
Wengine hawakuridhika, hata walipokuwa wakitoka, bado mashabiki walikmfuata Todd, walitaka kupiga naye picha huku wengine wakitaka kusainiwa vitabu vyao.
Hayo yalikuwa maisha ya usupastaa, walimheshimu kwa kuwa aliifanya kazi yake ipasavyo, wengi walipenda kutazama filamu zake, kwa kifupi, Todd aliwavutia watu wengi mno.
Alipomaliza kuwasainia watu vitabu vyao na hata kupiga nao picha, kama kawaida akaifuata gari yake ya kifahari, Ferrari nyekundu na kisha kuingia, kilichofuata ni kuanza safari ya kuelekea hotelini kabla ya kurudi New York alipokuwa akiishi siku inayofuata.
Akaliwasha gari hilo na kuondoka mahali hapo. Moyo wake ulijisikia faraja, hakuamini kwamba mwisho wa siku angekuwa na umaarufu mkubwa kama aliokuwa nao katika kipindi hicho.
Katika kipindi cha nyuma alipokuwa akianza, mambo yalikuwa magumu mno, alipambana usiku na mchana lakini mwisho wa siku, alifanikiwa kuwa kama alivyokuwa, hakukuwa na kitu kingine kilichokuwa kikiendelea zaidi ya kukusanya fedha na kuwa nazo zaidi ya zile alizokuwa nazo.
Wakati safari ikiendelea na kuyakuta makutano ya Barabara za St. Barnaba na Morovian ambayo ilikuwa ikienda mpaka katika Mtaa wa Butterfly uliokuwa umbali kama wa kilometa tatu, akashtuka baada ya kuona gari moja likija kwa kasi nyumba yake, lilikwenda mbele yake kwa mwendo wa kasi na kisha kusimama kwa katikati ya barabara, tena kiubavuubavu.
Kama haukuwa umakini wake mkubwa, basi angeweza kuligonga gari hilo. Kwa ustadi mkubwa, Todd akafunga breki na kisha kusimama, alibaki akihema kwa nguvu, mbele yake ilionekana ajali kubwa ambayo pasipo kutumia uwezo wake basi angeweza kuligonga gari hilo.
Huku akijiuliza ni kitu gani kinaendelea, wanaume wawili wakateremka kutoka kwenye ile gari na kuanza kuelekea kule alipokuwa. Hakujua watu hao walikuwa wakina nani na walihitaji nini kutoka kwake.
Mahali hapohakukuwa na magari, ilikuwa usiku sana na magari hayakuwa yakipita mara kwa mara, hasa katika barabara hiyo ya magari yaendayo kasi. Akashindwa kuliwasha gari lake, watu wale walikwenda kwa kasi mpaka pale lilipokuwa gari lake, wakamwambia afungue mlango vinginevyo wangempiga risasi humohumo.
Hakuwa na jinsi, hakutaka kupinga, kitu cha kwanza kabisa, akashusha kioo cha mbele cha mlango wa upande mwingine, mwanaume mmoja akaingia na kumwamuru aendeshe mpaka sehemu waliyotaka wao waelekee.
“Naomba uniache, kama unataka gari chukua,” alisema Todd huku akitetemeka.
“Unadhani sisi tunataka gari?” aliuliza mwanaume huyo huku akiwa na bastola mkononi mwake.
“Hata kama unataka kiasi chochote cha fedha, nitakupa, naomba uniache...” alisema Todd, tayari machozi yakaanza kububujika mashavuni mwake.
Mwanaume yule mwingine akapita upande wa pili, akaufungua mlango na kumshusha Todd kisha kumpeleka katika gari lao walilokuja nalo huku yule mwingine akiachwa katika gari lile kwa ajili ya kuondoka nalo.
Kila kitu kilichokuwa kikifanyika mahali hapo, kilifanyika kwa haraka sana, tukio zima lilichukua sekunde arobaini na tano tu, tayari wakaondoka huku wakiwa na Todd ndani ya gari.
“Naombeni mniacheee...” alisema Todd.
“Hutakiwi kupiga kelele...” alisema mwanaume mmoja huku akimnyooshea bastola.
“Nimefanya nini? Naombeni msiniue..” alisema Todd.
“Kwani kila anayeuawa kuna baya amelifanya? Hakuna kitu kama hicho, kuwa mpole,” alisema mwanaume huyo.
Baada ya hapo, hawakutaka kuongea kitu chochote kile, wakaondoka naye huku garini wakiwa kimya, kwani hata Todd naye aliyetaka kuzungumza maneno mengi aeleweke na hivyo kuachwa, aliambiwa akae kimya kwani suala la kumuua lisingeweza kuzuilika hata kidogo.
Walikwenda mpaka katika barabara nyingine ya Queen Elizabeth I ambayo ilikuwa ikienda moja kwa moja mpaka kwenye jumba la makumbusho ya Lincoln, hawakufika huko, wakakata kulia na kisha kuchukua barabara nyingine ambayo iliwapeleka mpaka katika sehemu ambayo haikuwa na watu, giza lilitawala, gari likasimamishwa mahali hapo.
“Naomba mnisamehe....”
“Halafu?”
“Niondoke, nitawalipa kiasi cha fedha chochote mnacholkitaka....”
“Halafu?”
“Naomba mnisamehe...”
Hawakutaka kupoteza muda, saa zao zilionyeshwa kwamba tayari ilikuwa ni saa nane za usiku hivyo walitakiwa wafanye haraka, wamuue na kisha kuendelea na mambo yao.
Walichokifanya ni kumkaba kooni, tena kwa nguvu kuhakikisha anakufa na kisha kufanya kile walichoambiwa kukifanya. Mwanaume mmoja mwenye nguvu ndiye aliyetumika kumuua Todd ndani ya gari hilo.
Dracula hakutaka kwenda katika lile gari kwani aliamini kwamba vijana wale wangefanya kama jinsi alivyowapa maagizo, kweli wakafanya. Kilichofuata baada ya kuhakikisha kwamba Todd amekufa ni kumchoma sindano iliyokuwa na madawa aina ya cocaine, walipomaliza, wakachukua nailo zenye unyevuunyevu ambazo kwa kutumia utaalamu wao waliweza kuweka alama za vidole za Benjamin na kisha kuziweka katika shingo ya Todd na sehemu nyingine za mwili.
“Vipi?”
“Tayari!”
“Mbebeni mkamuweke ndani ya gari lake, pia wekeni na hizi fedha,” aliagiza Dracula huku akiwapa noti ambazo zilitakiwa kuwekwa ndani ya gari hilo, vijana wale wakafanya kama walivyoagizwa, wakaubeba mwili wa Todd na kisha kuupeleka garini mwake na kuziweka noti zile.
“Tuondokeni!” alisema Dracula baada ya kumaliza kila kitu. Wakaondoka mahali hapo huku kila mmoja akiwa na furaha ya kukamilisha kazi waliyokuwa wamepewa.
****
Hakukuwa na mtu aliyeamini mara baada ya taarifa juu ya kifo cha Todd zilipotolewa katika vyombo mbalimbali vya habari nchini Marekani. Wengi walipigwa na bumbuwazi, kile walichokisikia, hakikuaminika kwao kwamba yule muigizaji, mwenye jina aliyekuwa akivuma sana kipindi hicho, Todd Lewis alikutwa amejidunga madawa ya kulevya kwakujiovadozi.
Watu wakapigiana simu, kila aliyesikia, hakutaka kukubaliana na habari hiyo kwani miongoni mwa watu waliokuwa wakifanya vizuri kipindi hicho, alikuwa huyo Todd, sasa kwa nini afe mapema hivyo? Tena mbaya zaidi alikutwa akiwa amejiovadozi madawa ya kulevya kitu ambacho kiliwachanganya watu wote kwani Todd hakuwa mtumiaji wa madawa hayo hata mara moja.
Wengi wakaenda katika Hospitali ya Calvary kujionea, huko, watu walikuwa wakilia kwani ndipo walipopata taarifa kamili kwamba muigizaji huyo alikutwa ndani ya gari yake ya kifahari ya Ferrari akiwa amejiovadozi madawa ya kulevya.
“Haiwezekani Bwana! Huyu jamaa hakuwa mlevi kabisa,” alisema jamaa mmoja.
“Ndiyo! Hata mimi nimeshangaa sana, yaani Todd awe mlevi wa madawa ya kulevya! Haiwezekani hata kidogo,” alisikika jamaa mwingine.
Kila mmoja alikuwa sahihi kabisa, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa na shaka na Todd kwamba alikuwa mtumiaji wa madawa hayo, taarifa hizo zikaendelea kusambaa kila kona mpaka ndani ya saa moja tu, dunia nzima ilijua nini kilitokea nchini Marekani.
Hofu zikaanza kutanda, taarifa zilizosema kwamba ndani ya gari la marehemu kulikutwa noti za fedha kutoka nchi mbalimbali ziliwashtua sana kwani hata siku ambayo Carter alikutwa akiwa amekufa ndani ya chumba cha hoteli, fedha kama hizo zilikutwa kitu kilichowafanya watu kuona cha kawaida ila baada ya fedha hizo kukutwa ndani ya gari hilo, wakagundua kwamba inawezekana hizo fedha zilibeba ujumbe fulani.
“Kama huyu Benjamin ndiye aliyemuua Carter, basi inawezekana akawa amemuua na Todd pia,” alisema jamaa mmoja wakati alipokuwa supamaketi, katika sehemu ya kuuzia magazeti na majarida mbalimbali.
“Inawezekana kabisa...hebu tuwasikilizie polisi tuone watasemaje,” alisema jamaa mwingine.
Hilo ndilo lililokuwa vichwani mwa watu wengi, kila aliyesikia namna gari hilo lilivyokutwa, alikuwa na uhakika kwamba muuaji alikuwa yuleyule, kijana wa chuo mwenye akili nyingi, Benjamin Saunders.
Hilo ndilo lililotokea, baada ya siku mbili, taarifa zikatolewa kwamba alama za vidole vya Benjamin vilikuta katika mwili wa Todd, yaani kabla ya kumchoma sindano, alimkaba kooni na kumuua na ndipo alipofanya mambo mengine likiwepo lile la kumchoma sindano ya madawa ya kulevya ili ionekane kwamba alikuwa amejiovadozi.
Hakukuwa na mtu aliyejua sababu ya Benjamin kuwaua watu maarufu, wengi waliuliza, kwenye mitandao wakatoa maoni yao lakini hakukuwa na mtu aliyefahamu lolote lile juu ya sababu ya Benjamin kuwaua watu maarufu na kisha kuacha noti za fedha mbalimbali karibu na miili yao.
“Ila kwa nini anawaua watu maarufu?’ aliuliza mwanamke mmoja.
“Hata mimi sifahamu! Kwanza nashangaa...”
“Halafu nasikia huyu Benjamin mwenyewe ana akili sana darasani.”
“Hata mimi nimesikia hivyohivyo na watu walipokwenda, wakakuta kweli ana akili sana, inawezekana ndiyo ikawa sababu ya kuwasumbua polisi na wananchi kumtia nguvuni,” alisema jamaa mmoja.
Bado watu walitakiwa kumtafuta Benjamin lakini hakukuwa na yeyote aliyempata, kiasi kikubwa cha fedha zaidi ya dola milioni ishirini na tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni hamsini kilitolewa lakini bado majibu yalikuwa yaleyale kwamba mitaani hakuonekana kabisa.
Maofisa wa FBI walikuwa na kazi kubwa, hakukuwa na aliyeamini kwamba mpaka muda huo Benjamin hakuwa amepatikana. Taarifa zilizopelekwa katika meza ya mkuu wa kitengo chao zilisema kwamba walitakiwa kupewa muda zaidi kwani inawezekana kulikuwa na mtu hatari ambaye alikuwa akimlinda Benjamin ili asiingie katika mikono yao.
“Kwa hiyo tumeshindwa?” aliuliza mkuu wa FBI, Bwana Connery Gibson.
“Hapana!”
“Sasa mbona hapatikani?”
“Ngoja tuendelee nadhani kuna kipindi tutampata tu.”
Hakukuwa na muda mwingine wa kupoteza, kama kusubiri, walisubiri kwa kipindi kirefu lakini hakukuwa na mafanikio yoyote yale, kuna kipindi walijiona kama kushindwa hivyo walitakiwa kuwasiliana na Shirika la Kijasusi la FBI ili wawasaidie kwani huyu Benjamin, japokuwa walijua kwamba hakuwa polisi au mtu yeyote mwenye uwezo wowote wa kijeshi lakini alikuwa mgumu mno kupatikana.
Walichokifanya ni kujiongeza tu, wakawagawa vijana wao katika miji mingine kama Los Angeles, Miami, Texas na sehemu nyingine ili kuhakikisha Benjamin anapatikana haraka iwezekanavyo.
“Nadhani hatotushinda tena, si ndiyo?”
“Tutegemee hilo mkuu!”
****
Harry alichanganyikiwa, hakuamini kile alichokuwa amekiona kwamba muigizaji maarufu duniani kwa kipindi hicho, Todd Lewis aliuawa ndani ya gari lake huku wauaji hao wakitaka kuionyeshea dunia kwamba alijiovadozi madawa ya kulevya kitu ambacho hakikuwa kweli kabisa.
Kilichomchanganya zaidi ni alama za vidole zilizopatikana ndani ya gari lile na hata katika mwili wa Todd ambazo zilionyesha kwamba ni Benjamin ndiye aliyefanya mauaji hayo.
Hapo ndipo alipoamini kwamba Benjamin hakuhusika katika mauaji, kulikuwa na watu wengine waliokuwa wakiyafanya huku wakiweka alama za vidole vyake katika kila tukio walilolifanya.
Alimwangalia Benjamin mara mbilimbili, hakuamini kilichokuwa kimetokea, alimuonea huruma sana kwamba inawezekana vipi mtu auwe na kisha kuweka alama za vidole vyake? Alimuuliza Benjamin lakini mwanaume huyo alimwambia ukweli kwamba hakujua kitu chochote kile.
“Sifahamu!” alisema Benjamin.
“Kuna kitu unajua!”
“Harry! Sifahamu chochote, huyu mzee Seppy ndiye anahusika, yaani ni lazima dunia ijue kwamba yeye ndiye anahusika, vinginevyo, nitahukumiwa kwa mauaji ambayo sikuyafanya,” alisema Benjamin.
“Tutatoa vipi taarifa polisi? Watakukamata!”
Huo ndiyo ulikuwa mtihani mwingine, hawakujua ni kitu gani walitakiwa kufanya, hawakuwa na ushahidi wa kutosha hivyo kama wangekosea sehemu moja basi lingekuwa tatizo kubwa kwao, walitakiwa kujipanga ili hata kama watakwenda kutoa taarifa polisi basi kusiwe na tatizo lolote lile.
David ndiye alikuwa na ushahidi kamili lakini bado kulikuwa na kitu kimoja kilichokuwa kikiwatatiza, kila mauaji yalipotokea, kulikuwa na fedha zilizokuwa zikiachwa, zile fedha zilimaanisha nini? Kila walichojiuliza, walikosa jibu.
“Sijui zinamaanisha nini, ila kama nikipewa muda, nitaweza kufahamu tu, kuna kitu,” alisema Benjamin huku akionekana kama mtu aliyekuwa akijifikiria sana.
“Hili ndilo la msingi, sidhani kama hata FBI watakuwa wanajua maana, huu utakuwa ni ujumbe, ujumbe gani sasa? Hebu tuhangaike mpaka tufahamu,” alisema Harry.
Wote wakakubaliana na kuingia kazini kuhakikisha wanajua kwanza maana ya zile fedha za noti zilizokuwa zikiwekwa katika mauaji yaliyokuwa yakitokea.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi
Ahsante Madame S kama jina langu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Sita.
Moyo wa Bwana Seppy haukuridhika kabisa, japokuwa aliendelea kufanya mauaji lakini uwepo wa Benjamin ulimkosesha amani kabisa. Alikosa furaha kabisa, kuna kipindi alikuwa akikaa chumbani kwake na kujifikiria sana.
Mtu huyo alikuwa muhimu sana, kila kilichokuwa kikiendelea, aliona kama Benjamin alikifahamu hivyo kama mtyu huyo asingekufa haraka iwezekanavyo basi ilikuwa ni lazima kujulikana na hivyo kumletea matatizo katika maisha yake.
Hakuwa na mfariji yeyote yule zaidi ya demu wake mwenye asili ya Urusi aliyeitwa Maria Kontekov, msichana mrefu, mrembo mwenye macho ya bluu ambayo yaliwachanganya wanaume wengi kipindi hicho.
Mara kwa mara alikuwa akionana na huyu msichana wake, alioa na kubahatika kupata watoto wawili lakini kipindi kirefu cha maisha yake alipenda kukaa na Maria zaidi ya mke wake ambaye naye umri ulikwenda sana kama alivyokuwa.
Nyumbani hakukulalika, kama alitaka kuonana na vijana wake, alikuwa na jumba jingine la kukutaniana na kupanga vitu vingine. Alipokuwa na mawazo mengi kama kipindi hicho, kimbilio lake pekee lilikuwa Maria ambaye alikuwa akitoka Urusi na kwenda Marekani, wanafanya mambo yao na kisha kurudi huko.
Fedha iliongea, Maria hakuwa akiongea chochote mbele ya Bwana Seppy, alipata chochote alichokitaka lakini kwa sharti kwamba hakutakiwa kuwa na mwanaume yeyote zaidi yake.
Hilo, kwa Maria wala halikuwa tatizo, alikuwa radhi kumridhisha mzee huyo tu kwani kitu pekee alichokihitaji kilikuwa ni fedha tu. Alipewa fedha za kutosha na hata pale ambapo alikuwa na fedha nyingi, nyingine akaongezewa, akaunti yake benki ikajaa fedha nyingi, akanunuliwa jumba la kifahari jiji Moscow nchini Urusi, akanunuliwa magari ya kifahari pamoja na kufunguliwa biashara kubwa.
Mawazo juu ya Benjamin yalipomzingua kichwani mwake, harakaharaka akamwambia Maria afike haraka iwezekanavyo nchini Marekani. Hakukuwa na umbali mkubwa kutoka Marekani mpaka Urusi lakini mzee huyo akaamua kumtumia ndege yake na hatimaye wakutane jijini New York, wazungumze kama kawaida yao na kuingia chumbani kufanya mambo yao.
Ndani ya saa tatu, tayari msichana huyo alikuwa mikononi mwake, walikuwa chumbani, wakafanya kila kitu huku muda mwingi mzee huyo akihitaji kuchuliwa mgongo wake kitu ambacho wala hakikuwa tatizo kwa Maria.
“Kuna nini mpenzi?” aliuliza Maria kwa sauti ndogo iliyojaa mahaba.
“Hakuna kitu kipenzi!”
“Hapana! Huwezi kunidanganya, ninakujua, nimekaa nawe kipindi kirefu, unapokuwa kwenye mawazo, najua, hebu niambie, tatizo nini,” alisema Maria huku akiwa kifuani mwa Bwana Seppy.
“Hakuna kitu!”
“Kweli?”
“Ndiyo mpenzi! Hebu nichue kidogo mgongo,” alisema mzee huyo, haraka sana Maria akaanza kazi hiyo.
Siku hiyo walishinda chumbani tu, Bwana Seppy alijisikia amani moyoni mwake, msichana huyo ndiye alikuwa kila kitu katika maisha yake, ilikuwa ni rahisi kugombana na mkewe ila si Maria, hata kama ungetaka kumchukiza, mtongoze Maria, alikuwa radhi kukuua ila si kama ambavyo ungemtongoza mkewe wa ndoa.
Wiki nzima Bwana Seppy hakurudi nyumbani, alikuwa akijifariji na Maria tu chumbani. Fedha ilikuwa kila kitu, ilibadilisha kila muonekano wa kitu, kile kilichokuwa hakiwezekani, ilikifanya kiwezekane, tena kwa urahisi kabisa.
Maisha yalikuwa ni ya raha na starehe, vijana wake waliendelea na kazi kubwa ya kumtafuta Benjamin huku yeye akiwa hotelini akila raha kabisa. Hakutaka kusikia lolote kuhusu familia yake, hakutaka kusikia kuhusu watoto wake, Jericho na Vanessa, kitu alichotamani kusikia ni kuhusu Maria tu.
“Umekuwa mnyonge kwa kipindi kirefu sana, naomba leo usiku unitoe mtoko,” alisema Maria kwa sauti ndogo huku akiwa kifuani mwa mzee Seppy.
“Unataka twende wapi?”
“Tukaangalie mechi ya kikapu, leo La Lakers anacheza,” alisema msichana Maria.
“Sawa! Tutakwenda kutazama, ninataka uwe na furaha kipindi chote mpenzi,” alisema mwanaume huyo.
Haraka sana Bwana Seppy akampigia simu Dracula na kumwambia kwamba siku hiyo alihitaji kwenda kuangalia mchezo wa kikapu baina ya Timu ya LA Lakers na Memphis ambazo zilitarajiwa kucheza katika mchuano mkali wa timu za Magharibi.
Hilo wala halikuwa tatizo, haraka sana Dracula akaenda kukata tiketi mbili, tena katika upande wa VIP, alipozipata akampelekea mzee huyo hotelini kitu kilichomfanya Maria kuwa na furaha sana.
“Nakupenda mpenzi,” Maria alimwambia Bwana Seppy.
“Nakupenda pia.”
Walilala mchana huo na usiku wakaamka na kuanza safari ya kwenda katika uwanja wa La Lakers, Staple Center. Ndani ya gari ulikuwa ni muda wakupeana mahaba motomoto. Japokuwa Bwana Seppy alikuwa mtu mzima kama baba yake lakini halikuwa tatizo kwa Maria kubadilishana naye mate na kufanya mambo mengine ya aibu, alifanya hivyo kwa sababu nyuma ya pazia kulikuwa na fedha.
Walipofika, wakataremka na kisha kuingia ndani. Ilikuwa vigumu kumgundua Bwana Seppy kwamba alikuwa yeye, kichwani alivalia kofia, akavaa fulana kali, jinzi na raba zilizokuwa na chata ya Nike, kwa muonekano, alionekana kama kijana mwenye miaka thelathini.
Wakaingia mpaka katika sehemu ambayo walitakiwa kukaa. Huko, ni watu wenye fedha ndiyo waliokuwa wakikaa, tiketi zao zilikuwa ni dola elfu themanini ambazo zilikuwa ni sawa na milioni mia moja sitini, na watu walilipia bila malalamiko.
Kule walipokuwa wakikaa, mbele yao kulikuwa na kioo kikubwa, walikaa kibosi na wote waliokuwa huko walikuwa na wasichana wao wadogo, ni mambo ya kifuska ndiyo yaliyokuwa yakiendelea huko.
Katika kipindi hicho, mchezaji aliyekuwa na jina ambaye alikuwa akichipukia alikuwa Paul McKenzie, miongoni mwa wachezaji waliokuwa mwiba kipindi hicho, huyu jamaa alikuwa akitisha. Alikuwa na umri wa miaka kumi na tisa tu lakini uwezo wake ulikuwa mkubwa kana kwamba alikuwa na miaka thelathini.
Mpaka katika kipindi hicho, alivunja rekodi nyingi mno na rekodi moja tu ndiyo alikuwa akiifukuzia, ya kufunga pointi nyingi kama ilivyokuwa kwa mkongwe wa mchezo huo, Michael Jordan, au MJ kama alivyojulikana na watu wengi.
Mafanikio makubwa ndiyo yaliyomfanya kujituma kila siku. Timu ya La Lakers ikapata mtu sahihi wa kuchukua nafasi ya mkali mwingine, Shaq O’Neil ambaye alistaafu kipindi kilichopita huku akiwa ameipa timu hiyo mafanikio makubwa.
Mbali na uwezo mkubwa aliokuwa nao, Paul alikuwa na sura nzuri, aliwavutia wasichana wengi, katika kipindi hicho ndicho alisemekana kuwa mwanaume mwenye sura nzuri zaidi ya wanaume wote chini ya jua. Wanawake walimpenda kwa sababu hakuwa na makuu, hakuwa na kashfa yoyote ile, kitu alichokuwa akikiangalia ni mpira wa kikapu ambao ulimpa magari, majumba ya kifahari na vitu vingine vingi, hata akaunti yake benki ilikuwa ikisomeka na kutuna kila siku.
Wakati tv kubwa iliyopachikwa ukumbini hapo ilipomuonyesha Paul kwa karibu, tena kwa kumvuta, msichana Maria akashtuka, hakuamini kama kweli duniani kulikuwa na mwanaume mwenye sura nzuri kama yule aliyemuona.
Mapigo yake ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu, akajikuta akianza kuangukia katika penzi la mwanaume huyo, hakuishia kuangalia kwenye televisheni ile tu, akayatupa macho yake uwanjani, kila aliposhika mpira, wanawake walisikika wakipiga kelele hali iliyoonyesha kwamba hata wanawake waliokuwa humo walimpenda mno.
Moyo wake ukamia mno, kwa jinsi Paul alivyokuwa mzuri, hakutaka kumuona mwanamke yeyote anakuwa naye zaidi yake yeye, hakutaka kubaki kule juu, akajifanya kuvurugwa na tumbo hivyo alitakiwa kwenda chooni, Bwana Seppy hakuwa na wasiwasi wowote ule, akamruhusu msichana huyo aende huko.
Maria akaanza kutembea kwa harakaharaka, akashuka chini mpaka kule katika viti vya chini kabisa, alitaka kumuona Paul kwa ukaribu kabisa kwani alihisi telvisheni ile ilikuwa imemdanganya, alipofika huko, akajipenyeza katikati ya watu mpaka katika kiti ambacho hakikuwa na mtu na kukaa hapo.
Macho yake yakaanza kumwangalia vizuri Paul, aliuona uzuri wa mwanaume huyo, wanawake ambao walikuwa jirani yake, muda wote walikuwa wakimsifia mwanaume huyo, tena huku wakimuita kila alipogusa mpira.
Maria alikasirika, alitamani kuwaambia wasimuite kwani alimuona kama kuwa mpenzi wake. Wakati mpira ukiwa umepigwa na kuelekea nje katika upande aliokuwa Maria na wanawake wengine.
Paul akaufuata, wanawake wote wakasimama, wakazidi kuliita jina lake, Paul akawaangalia, tabasamu pana lilikuwa usoni mwake, alipomuona msichana Maria tu, hakufanya kitu chochote zaidi ya kumkonyeza kitu kilichowafanya wanawake wote waliokuwa hapo kumuonea wivu msichana Maria, kwani kwa muonekano tu, hata naye Paul alionekana kuvutiwa naye, ila hakujua kama angeweza kuonana naye baada ya mechi hiyo kumalizika.
Je, nini kitaendelea?
Simu yangu ambayo ninaitumia kama hotspot imezingua. So tuvumiliane katika kipindi hiki kigumu kidogo.
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Saba.
Maria hakutaka kuondoka, akanogewa kukaa mahali hapo, baada ya dakika kumi na tano ndipo akakumbuka kwamba alikuwa ameaga anakwenda chooni hivyo kama angechelewa zaidi kungekuwa na tatizo, harakaharaka akasimama na kuanza kuondoka kuelekea juu alipomuacha mwanaume wake.
Alipandisha ngazi harakaharaka mpaka juu ambapo akaingia katika chumba hicho. Bwana Seppy wala hakuwa na wasiwasi, ndiyo kwanza akawa anazungumza na wazee wenzake wenye fedha, Maria akakaa katika kiti na kuendelea kuufuatilia mchezo huo.
Mawazo yake yalikuwa kwa Paul tu, kila aliposhika mpira, alitetemeka, mapigo yake ya moyo yalimdunda mno, mwanaume huyo alimtetemesha kupita kawaida.
Hata Paul mwenyewe, muda mwingi alikuwa akiangalia katika sehemu aliyokuwa Maria, pale, hakuweza kumuona, hakujua kama mwanamke huyo aliondoka au alitoka na angerudi baada ya muda fulani.
Kipindi cha kwanza kilipofika, wakiwa mapumziko, Maria alikuwa akimfuatilia Paul kwa karibu kabisa, macho ya Paul hayakutulia, alikuwa akiangalia huku na kule, kwa muonekano wake tu ilionyesha kwamba alikuwa akimtafuta mtu fulani, alitamani kujitokeza lakini alishindwa kabisa kufanya hivyo.
“Au nimfuate?” alijiuliza huku akiendelea kumwangalia mwanaume huyo.
Paul alichanganyikiwa, tayari moyo wake ulitekwa na msichana huyo, hakuwa radhi kuendelea kucheza na wakati moyo wake ulichanganyikiwa, kipindi cha pili hakuingia, alifikiria kuingia kipindi cha tatu.
Alikaa kwenye benchi lakini macho yake yaliendelea kutalii huku na kule, alitamani kumuona msichana huyo ambaye aliutetemesha moyo wake kwa kipindi hicho.
Wanawake walikuwa wakimuita lakini hakuwa na habari nao, alikuwa akimtaka msichana mmoja tu, alikuwa Maria ambaye hakujua aliondoka na kuelekea wapi na wala hakujua kama alikuwa akifuatiliwa na msichana huyo.
Mchezo uliendelea, La Lakers hawakuwa wakali kipindi hicho, staa wao alikuwa nje, ila kipindi cha tatu kilivyoingia, akaingia, timu ikapata uhai na kujikuta akifunga pointi nyingi sana.
Mpaka mchezo unamalizika, bado Paul alikuwa na mawazo tele, alishindwa kuvumilia, hakutaka kuingia chumbani kuzungumza na wachezaji wenzake, alibaki akizunguka huku na kule.
Watu wakaanza kutoka, naye akatoka uwanjani, alipofika kwenye korido tayari kwa kwenda chumbani walipokuwa wenzake, akakutana na mchezaji mwenzake wa akiba, akamfuata na kisha kumpa kikaratasi kilichokuwa na namba, alipoiangalia namba hiyo, hakuifahamu ila chini kulikuwa na jina la Maria, akaisevu na kisha kuangalia picha katika Mtandao wa Whatsapp, picha aliyokutana nayo, ilikuwa ni ya msichana huyo aliyekuwa akimtafuta sana kipindi hicho. Msichana Maria.
****
Mpaka mechi inamalizika, Maria alichanganyikiwa, hakujua ni kwa jinsi gani angeweza kuwasiliana na Paul. Hakutaka kubaki humo, alijua kwamba kama angeendelea kubaki asingeweza kuonana na mwanaume huyo, ilikuwa ni lazima ateremke ili aende akaonane naye huko huko.
Hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kumuaga Bwana Seppy kwamba anakwenda tena chooni kwani tumbo lilikuwa likimsumbua. Mzee Seppy hakuwa na tatizo, alikuwa amenogewa na maongezi na mzee mwenzake tena huku wakinywa pombe kali, akamruhusu.
Maria akaondoka kuelekea chini, huko, alimsubiri Paul lakini hakutokea, hakujua nini cha kufanya, kitu kilichomjia kichwani mwake ilikuwa ni lazima amwachie namba mwanaume huyo ili kama kumtafuta, amtafute kwani kuonana naye tayari ilionekana kuwa tatizo kubwa.
Akachukua kikaratasi, akaandika jina lake na namba yake ya simu. Kwa sababu hakumuona mwanaume huyo, alichokifanya ni kumgawia mchezaji mmoja na kumwambia kwamba ampe Paul kwani alitaka kuwasiliana naye, hilo halikuwa tatizo, mchezaji huyo akachukua kikaratasi hicho na kumuahidi kwamba angeweza kumpa.
“Naomba usisahau, nakuomba,” alisema Maria.
“Usijali! Nitaifikisha...”
“Nakuomba usikose...tafadhali nakuomba!”
“Usijali dada!”
“Nitashukuru sana!”
****
Muda wote Maria alikuwa akiiangalia simu yake, alikuwa na presha kubwa ya kuona akipigiwa na Paul na kumwambia kwamba alikuwa akimpenda kama alivyokuwa akimpenda.
Hakuwa na raha, hata ndani ya gari alikuwa kimya kabisa, moyo wake ulikuwa kwenye mawazo tele, hakumfikiria Bwana Seppy tena, mtu aliyekuwa akimfikiria alikuwa Paul tu ambaye aliuburuza vibaya moyo wake.
Bwana Seppy aliyaona mabadiliko, akajaribu kuuliza sababu ya mpenzi wake kuwa vile lakini wala hakupata jibu lolote lile, ilimuuma kwani kati ya watu ambao hakutaka kabisa awaone wakiwa na majonzi mioyoni mwao, alikuwa huyu Maria.
Alijaribu kumuuliza tatizo lilikuwa nini lakini hakupewa jibu la kuridhisha kwani msichana huyo alimwambia wazi kwamba alikuwa poa na hakukuwa na tatizo lolote lile.
Upande wa pili, bado Paul alikuwa akikiangalia kikaratasi kile, japokuwa hakuwa akimfahamu msichana huyo lakini akahisi kwamba ndiye yule aliyemuona uwanjani wakati mechi ikiendelea na ghafla akapotea.
Naye kuanzia kipindi hicho akawa na mawazo tele, alikuwa na namba lakini alihofia kuipiga na kuzungumza na msichana huyo. Alibaki akijiuliza, kujiuliza huko hakukuisha mpaka alipolala usiku.
Kesho, kitu cha kwanza kabisa kukikumbuka kilikuwa ni namba ya Maria, hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kuchukua simu yake na kuanza kumpigia simu Maria. Simu ilianza kuita, ikaita, hapohapo ikakatwa.
Mara ya kwanza alihisi kwamba ni network, alichokifanya ni kupiga tena na tena lakini majibu yalikuwa yaleyale kwamba simu ilikatwa kila alipopiga, na baadaye alipojaribu kuipiga tena, haikuwa ikipatikana kitu kilichouumiza moyo wake kupita kawaida.
****
Nahitaji kurudi nyumbani nikapumzike mpenzi,” alisema Maria huku akimwangalia Bwana Seppy usoni.
“Mbona mapema jamani! Si ulisema unakaa mwezi mzima?” aliuliza Bwana Seppy huku akionekana kushtuka.
“Kuna mambo mengi natakiwa kufanya, ila wiki ijayo nitarudi tena, si unajua mama atakuwa amenikumbuka sana,” alisema Maria.
Kwa jinsi alivyokuwa akizungumza, ilikuwa ni vigumu sana kugundua kwamba msichana huyo alikuwa na lake kichwani. Aliiona simu ngeni ikiingia, haikuwa kawaida simu ngeni kuingia katika simu yake, akajua kwamba moja kwa moja mpigaji alikuwa Paul.
Alitamani kupokea lakini ilishindikana kabisa kwani alikuwa jirani na Bwana Seppy hivyo kuikata kila ilipokuwa ikiita. Baadaye alipoona kwamba inasumbua sana na angeweza kushtukiwa, akaizima kabisa.
Moyo wake ulikuwa na furaha tele, hakukuwa na kitu kingine alichokifikiria zaidi ya kumpigia mwanaume huyo ili azungumze naye na ikiwezekana wakutane sehemu, hata kama angemuomba penzi, kwake hakuwa na kinyongo, alikuwa tayari kumpa kwani hakukuwa na mwanaume aliyekuwa akimpenda kama ilivyokuwa kwa Paul.
Alihakikisha anaondoka siku hiyo, hakutaka tena kuendelea kukaa nchini Marekani, iwe isiwe ilikuwa ni lazima kuondoka. Hilo wala halikuwa tatizo, Bwana Seppy akakubaliana naye, hivyo mchana wa siku hiyo akapanda ndege ambayo ilimrudisha mpaka nchini Mexico.
“Nitakukumbuka mpenzi,” alimwambia Bwana Seppy.
“Nitakukumbuka pia, ila usisahau kurudi wiki ijayo!”
“Nitarudi tu,” alisema Maria na kisha kummwagia mabusu mfululizo.
Wakati ndege ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Benito Juarez nchini Mexico, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumpigia simu Paul. Wakati simu inaita, moyo wake ulikuwa na presha kubwa, alitamani kuisikia sauti ya mwanaume huyo. Simu wala haikuita sana, ikapokelewa.
“Nazungumza na nani?”
“Mimi! Maria, yule binti wa uwanjani,” aliitikia Maria huku akiachia tabasamu, fikra zake zilimwambia kwamba mwanaume huyo alikuwa akimwangalia.
“Nimefurahi sana kusikia sauti yako! Kumbe upo Mexico?” aliuliza Paul kwa mshangao, kwani code ya simu ile ilionyesha kwamba mpigaji alikuwa Mexico.
“Ndiyo!”
“Ninatamani nikuone, naweza kuja?”
“Naweza!”
Walizungumza mengi, siku hiyo, Paul hakutaka kabisa kukaa nchini Marekani, kutoka hapo mpaka Mexico haikuwa mbali, siku hiyohiyo akapanda ndege na kuelekea huko ambapo alipokelewa na msichana huyo kisiri.
Hawakutaka kwenda kwenye hoteli kubwa kwani walihisi kwamba huko wangeshtukiwa mapema, kwa kuwa ilikuwa usiku, wakaenda katika hoteli ya chini, tena uswahili kabisa ambapo walikuwa na uhakika kwamba wasingeweza kugundulika kwa urahisi.
“Ninakupenda Paul,” alisema Maria huku tayari wakiwa kitandani.
“Nakupenda pia na ndiyo maana nimesafiri kuja huku, kwa ajili yako tu,” alisema Paul huku akimmwagia mabusu mfululizo msichana huyo.
“Una mchumba?” aliuliza Maria.
“Hapana! Wewe?”
“Ninaye, ni mzee mmoja hivi, sina jinsi, ilinipasa kuwa naye,” alijibu Maria.
“Kwa nini?”
“Basi tu! Maisha yalinipasa kuwa na mzee huyo.”
“Yupi?”
“Bwana Seppy!”
“Yule bilionea?”
“Ndiyo! Ila moyo wangu haupo kwake kabisa, ninakupenda Paul, ninataka uupoze moyo wangu!” alisema Maria kwa sauti ya kulalamika kimahaba.
“Akija kujua je?”
“Sidhani na ndiyo maana ninataka tufanye vitu kisiri sana.”
“Basi hakuna tatizo!”
Usiku huo ulikuwa ni usiku wa raha, hakukuwa na karaha, walianza kubusiana hapa na pale na mwisho wa siku wakajikuta wakiwa watupu kabisa, kilichofuatia ni miguno ya mahaba na kelele za chumbani kitandani humo.
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa kila kitu, mara kwa mara walikuwa wakikutana, safari za Paul kwenda nchini Mexico hazikukata, mara kwa mara alikuwa akisafiri kwenda huko.
Kwa Maria, naye alichanganyikiwa mno, kila alipopata nafasi ya kwenda nchini Marekani, alihakikisha anakutana na Paul na kufanya mambo yao kimyakimya pasipo mtu yeyote kufahamu.
Safari za Maria kwenda nchini Marekani kumuona Bwana Seppy zikaanza kupungua, kila alipoambiwa aende, akajifanya kuwa bize. Bwana Seppy akaanza kupatwa na machale, haikuwa kawaida kabisa, Maria alionekana kubadilika, alihisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea nyuma ya pazia.
Kuna kipindi aliamua kumtafuta Maria, simu yake haikuwa ikipatikana lakini alipojaribu kumtumia ujumbe katika Mtandao wa Whatsapp, meseji ilikwenda na kusomwa.
“Upo wapi?” aliuliza Bwana Seppy.
“Nyumbani!”
“Una uhakika?”
“Ndiyo mpenzi! Mama anaumwa!”
“Haupo Marekani?”
“Mimi? Marekani! Nije bila taarifa! Inawezekana vipi?” aliuliza Maria.
“Kweli upo Mexico?”
“Ndiyo mpenzi! Halafu nimekumisi sana, nataka wikiendi hii nije kukuona,” aliandika Maria.
“Sawa! Karibu,” alijibu Maria. Hakujua kama Bwana Seppy alikuwa akimfuatilia hatua kwa hatua kupitia simu yake kwa kitu kiitwacho GPS na alijua kwamba kipindi hicho hakuwa nchini Mexico, alikuwa Marekani katika Hoteli ya Greenland iliyokuwa Kaskazini mwa Jiji la New York.
Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom