Mauaji ya watu 3 Ilala - Dar

Mauaji ya watu 3 Ilala - Dar

Sikuwahi kuwaza kulipiza kisasi kwa mambo ya wivu wa kimapenzi - ikitokea nikahisi kuibiwa naomba mungu aniepushe na hasira

Kuibiwa hakika unaibiwa, ila kuibiwa kidharau ndio inaudhi, inabidi ajitahidi usijue pale anapochezesha nje, pia asile hela zako nyingi
 
taarifa hii ilitoka kama breaking news leo asb around sa tatu ila walisema wamekufa wawili!so sad!
 
Hii mitandao ingekuwa yangu ningeifunga, mtu anashindwa kuonyesha uhodari wa kugundua siri ya mauaji, kisha akajuza watu, ni kuropoka tu mradi umechangia. Walioanzisha hii mitandao wanatupima werevu wetu na ujinga wetu kisha wanatugawa halafu, wanatu Iraq na kutuLibya. Oneni fahara kupelekwa kaa makondo
 
Watu watatu,wameuwawa maeneo ya ilala bungoni kwa risasi.
Ilikuwa ni kama sinema ambapo alitokea kijana mmoja akashuka kwenye tex huku kashika bastola, alienda katika geti lililo karibu na hotei mpya ya M.M na kujibanza, gafla geti lilifunguliwa na gari kutoka ndani likiwa na watu wa nne, wanawake 3 na dereva mmoja mwanaume. Jamaa akiwa kajibanza alianza kushambulia ile gari na kuwaua watu wawili dereva na mwanamke mmoja na kuwajeruhi wengine wawili na kisha yeye kijipiga risasi na kufa hapo hapo.

Imeelezwa kuwa kati ya waliojeruhiwa ni mama mzazi na huyo msichana alieuliwa, pia msichana ni mdogo wake (hivyo wote ni mama na watoto wake wawili) ila mwanaume aliekuwa anaendesha gari hajajulikana alikuwa ni nani..

Imeelezwa kuwa yalikuwa ni mambo ya kimapenzi!
attachment.php


attachment.php



Ati muuaji ni mfanyabiashara wa magari! vijana, utajili na mauaji!
 
Barubaru,

Yaani hawa Mods wenu humu nadhani hawapendi asilan kuambiwa kweli na wako biased pita kiasi kwa kikundi/members fulani humu! Dah!

Yaani mpaka ile thread aloanzisha yule kanjanja wao Yeriko Yohana Msambila ya kudai ati "anatishiwa" kuuliwa na Mbunge Zitto Kabwe...pia wameifuta/wameifungia! Duh! Yaani hawa Mods kwa sasa wanachosha mno!

Ahsanta.

Ahlan wa sahalan Gombesugu.

Kwani hata ile Thread ya Yericko kumwita Al Akhiy Mohamed said Gaidi si aliokolewa na Mods pia.

Kikubwa ni kuwa ukweli na bayana zetu zinamfikia na pasi na shaka attaacha kutaka kupata umaarufu kwa kupandia migongoni mwa watu wengine.

Pole sana Yericko.
 
Hatari sana. Maisha ya binadamu hayana thamani bila hofu ya Mungu.


Mungu atusaidie sana

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Huyu jamaa muuaji ni jiran yangu hapa kitangiri jeshin mwanza kiufupi alikuwa na jeuri sana. Wiki iliyopita kidogo anigonge na gari kisa mbwembwe na speed ambazo hazina maana.
 
Picha kama la Ufoo Saro vile!

Kijana kwa jina la Gabriel Munisi (27) (mtoto wa kanali mstaafu) ambapo katika sakata hili yeye ndiyo muuwaji! Taarifa ni kwamba, huyu kijana alikuwa akimsomesha dem wake huko Turkey....."makubaliano yao yalikuwa...kwakuwa mimi sikusoma, bora wewe nikusomeshe ili kwa pamoja tukishaoana, tuje kulea watoto.....Gebo akimwambia mchumba wake"!

Baada ya kumaliza kusoma huko uturuki, na kurudi TZ ....demu akamchenjia mshikaji hamataki tena....kisa kapata mchumba mwingine..(mzava)....! Wambea wanasema, j3 dem alimpita jamaa gebo kama hamjui vile, achilia mbali matusi na maneno ya kashfa ya dem kwa mshikaji (muuaji) siku za hivi usoni!

Jamaa ishu zake ni kuchuka ndinga Dar na kwenda kuziuza mkoa fulani kanda ya ziwa, nadhani alipata tetesi kuwa demu wake anasepa leo to USA bila hata kumuaga...sasa sijui ndiyo na huyo mzva.....na alikuwa anasindikizwa [sijui] hapo siwezi pasemea! Nafikiri kwa hali hii, mshikaji Gebo akaamua afanye MAGAZIJUTO tunayo yasikitikia sasa!
 
Picha kama la Ufoo Saro vile!

Kijana kwa jina la Gabriel Munisi (27) (mtoto wa kanali mstaafu) ambapo katika sakata hili yeye ndiyo muuwaji! Taarifa ni kwamba, huyu kijana alikuwa akimsomesha dem wake huko Turkey....."makubaliano yao yalikuwa...kwakuwa mimi sikusoma, bora wewe nikusomeshe ili kwa pamoja tukishaoana, tuje kulea watoto.....Gebo akimwambia mchumba wake"!

Baada ya kumaliza kusoma huko uturuki, na kisha kurudi TZ ....demu akaanza kumchenjia mshikaji na kuwa hamataki tena....eti kisa amepata mchumba mwingine..(mzava)....! Wambea wanasema, j3 dem alimpita jamaa gebo kama hamjui vile, achilia mbali matusi na maneno ya kashfa ya dem kwa mshikaji (muuaji) siku za hivi usoni via simu!

Jamaa, ishu zake ni kuchuka ndinga Dar na kwenda kuziuza mkoa fulani kanda ya ziwa, nadhani alipata tetesi kuwa demu wake anasepa leo to USA bila hata kumuaga...sasa sijui ndiyo na huyo mzva sielewi.....na alikuwa anasindikizwa [sijui] hapo siwezi pasemea! Nafikiri kwa hali hii, mshikaji Gebo akaamua afanye MAGAZIJUTO tunayo yasikitikia sasa!
 
maisha yanaenda kasi sana wana jamvi tusipokuwa makini mwisho wa mwaka huu kuna kuwa na mambo mengi sana ya kustajaabisha tuwe makini na mienendo yetu
 
Back
Top Bottom