Mauaji ya visasi

Ninao wengi wa kuwalipa kisasi kiasi kwamba naishia kucheka na kusema acha ninywe bia maisha yaendelee. Hakika nimeamini nina hasira kali sana na Mungu ameota mbegu kuu njema ndani yangu.

Si muda sahihi wa kusema neno bali nashukuru yale mema niliyoyaongeza baada ya kusoma visa na simulizi kadhaa mahali hapa. Shukrani sana.
Ukijipa muda utagundua kuwa mtu anaekukosea kwa makusudi na bila kujali hisia zako akiwa na dhamira mbaya huwa anaishia pabaya pia. Hakuna mwanadamu mwenye jeuri kuliko nguvu za ulimwengu ambazo zinasimamiwa na MUNGU.

So ni vema kujipa muda, mtu amekufanyia ubaya kwa kusudi then kubali yaishe kisasi muachie MUNGU. Unaweza dhania kumkata na panga au kumchoma kisu itakuwa ni adhabu kali kwake kumbe wala ile sio kitu ila mkabidhi kwa aliyemuumba atawajibishwa huko.

Aiseeee maisha yanapoanza kumnyoosha mtu aliyekukosea na kukuumiza kiasi kwamba unakaa chini unajiuliza hivi MUNGU anaona ukorofi unaofanyiwa ama la? Kazi ya kunyooshwa ikianza utatamani kumpigia MUNGU magoti amuonee huruma. Wewe kaa kimya mwache ajifanye mjanja. Mkalie mbali na kata nae mazoea na mawasiliano basi. Dunia ikianza kumfunza mtu wa hivyo aiseee hakuna wa kuamulia. Maana ukishika panga ukataka kumkata watu wanaweza ingilia akatetewa, au ukisema umtumie wajuba wamdhuru still anaweza escape au ukajagundulika msala ukakurudia, au ukamwekea figisu watu wanaokuheshimu wakakusihi umsamehe. Ila Maisha sasa yakianza kumnyoosha mtajikuta ni ninyi wawili tu ndio mkitazamana mnajua kuwa sasa muda wa malipo umefika na nani analipia hesabu yake ya madhambi aliyomkosea mwenzake.

Hii kitu hata katika mahusiano ipo sana. Mwanaume au mwanamke anamuacha mwenzake kipindi ambacho hakukuwa na sababu yoyote ya msingi na kulikuwa na utulivu tu au anamfanyia mwenzake matukio ya kuvunja moyo na kuumiza hisia kwa makusudi kabisa then anategemea mwenzake ataelewa tu na kupuuzia maisha yaendelee. Watu wa hivi huko wanakokwenda MUNGU huwa anawapa wanachotaka ila anawanyima wanachostahili sababu unachostahili ndicho kitakupa furaha ila unachotaka kitakufanya ujiskie vizuri kwa muda tu then baadae balaa linaanza.


S
 
Mzee akitukanwa sana kwakweli... Ilihitaji uvumilivu wa kiwango cha juu mno kutofanya alichofanya mzee
Ila me nadhani miaka hiyo hakukuwa na mawakili wazuri, huyu mzee amekosea sana kwa namna huyo marehemu RC alivyomkosea heshima eneo lake. Huwezi kwenda eneo la mtu na kuanza kumtusi mbele ya familia yake hata mimi ningemzabua makofi.

Kimsingi hapo huyo mzee alitakiwa kupewa mvua ya miaka kadhaa kama sio maisha. Ila kumnyonga ni kumtendea dhambi kubwa sana huko anapokwenda roho yake imefunga kwa huzuni anaonekana ni mtu mbaya kwa kosa la kusababishiwa. Kuna muda hawa viongozi au watu fulani wenye mamlaka huwa wanatafuta kuadhibiwa kwa makusudi.
 
Ila me nadhani miaka hiyo hakukuwa na mawakili wazuri, huyu mzee amekosea sana kwa namna huyo marehemu RC alivyomkosea heshima eneo lake. Huwezi kwenda eneo la mtu na kuanza kumtusi mbele ya familia yake hata mimi ningemzabua makofi.

Kimsingi hapo huyo mzee alitakiwa kupewa mvua ya miaka kadhaa kama sio maisha. Ila kumnyonga ni kumtendea dhambi kubwa sana huko anapokwenda roho yake imefunga kwa huzuni anaonekana ni mtu mbaya kwa kosa la kusababishiwa. Kuna muda hawa viongozi au watu fulani wenye mamlaka huwa wanatafuta kuadhibiwa kwa makusudi.
Uko sahihi sana, hivi ndugu hawawezi kuifufua hii kesi na kukata rufaa?
 
Ukijipa muda utagundua kuwa mtu anaekukosea kwa makusudi na bila kujali hisia zako akiwa na dhamira mbaya huwa anaishia pabaya pia. Hakuna mwanadamu mwenye jeuri kuliko nguvu za ulimwengu ambazo zinasimamiwa na MUNGU.

So ni vema kujipa muda, mtu amekufanyia ubaya kwa kusudi then kubali yaishe kisasi muachie MUNGU. Unaweza dhania kumkata na panga au kumchoma kisu itakuwa ni adhabu kali kwake kumbe wala ile sio kitu ila mkabidhi kwa aliyemuumba atawajibishwa huko.

Aiseeee maisha yanapoanza kumnyoosha mtu aliyekukosea na kukuumiza kiasi kwamba unakaa chini unajiuliza hivi MUNGU anaona ukorofi unaofanyiwa ama la? Kazi ya kunyooshwa ikianza utatamani kumpigia MUNGU magoti amuonee huruma. Wewe kaa kimya mwache ajifanye mjanja. Mkalie mbali na kata nae mazoea na mawasiliano basi. Dunia ikianza kumfunza mtu wa hivyo aiseee hakuna wa kuamulia. Maana ukishika panga ukataka kumkata watu wanaweza ingilia akatetewa, au ukisema umtumie wajuba wamdhuru still anaweza escape au ukajagundulika msala ukakurudia, au ukamwekea figisu watu wanaokuheshimu wakakusihi umsamehe. Ila Maisha sasa yakianza kumnyoosha mtajikuta ni ninyi wawili tu ndio mkitazamana mnajua kuwa sasa muda wa malipo umefika na nani analipia hesabu yake ya madhambi aliyomkosea mwenzake.

Hii kitu hata katika mahusiano ipo sana. Mwanaume au mwanamke anamuacha mwenzake kipindi ambacho hakukuwa na sababu yoyote ya msingi na kulikuwa na utulivu tu au anamfanyia mwenzake matukio ya kuvunja moyo na kuumiza hisia kwa makusudi kabisa then anategemea mwenzake ataelewa tu na kupuuzia maisha yaendelee. Watu wa hivi huko wanakokwenda MUNGU huwa anawapa wanachotaka ila anawanyima wanachostahili sababu unachostahili ndicho kitakupa furaha ila unachotaka kitakufanya ujiskie vizuri kwa muda tu then baadae balaa linaanza.


S
Webale sana sana 🙏🙏🙏👍👍
 
Imetusikitisha sana ni jirani yangu kiboshoroad apa.inatia hasira sana
Ndio kwanza natoka msibani...na bila shaka nitausindikiza msiba mpaka kaskazin... yes visas...na kisa kipo hivi...

Ilikuwa siku ya jumapili usiku nipo pub flan napiga kilaji huku nasubiria vitasa vya mandonga...akatokea dogolas yupo na rafiki yake...wakanipa hi thn wakajongea kwenye meza yao na nikamuita muhudum nikamwambia wasikilize wale...basi akawasikiliza nikawaanzishia vinywaji vya kama 25,000 hivi...na mim nikawa na jamaa yangu tunazipasua bia na k vant..

Ilipofika mida ya saa tano usiku...nikawa nimechoka so nikaenda zangu lala...Asubuh ya jumatatu nasikia taarifa za msiba dada mmoja kauwawa na kubakwa..kudadis kumbe ni mke wa mdogo wangu sio wa damu lakin nimempita umri...

Jana nikaenda msiban na nikakutana na dogo na akaanza nisimulia kisa kilivyo tokea...

Nikamuuliza ilikuwaje..akaniambia pale ulinipo niacha..tulihama bar na kuhamia bar nyingine...ambayo hyo bar ipo karibu na kwao..sasa kuna jamaa alitokea na ni jiran yao na wamekua wote...akamwambia mwana amnunulie bia kwel dogo akamnunulia bia 2...mchiz akanywa akasepa kumbe mchiz ana jamaa yake hapo washapanga kuwa kwa kuwa dogo yupo hapa basi mkewe atakuwa nyumban peke yake so lazima akampige machine kwan anamtamanig muda mrefu...

Akamuacha jamaa yake pale amlie rada dogo yy akaenda nyumban kwa dogo akavunja mlango...akamkuta mke wa dogo na mtt kama wa miaka 7 wa kike...akamtia ngum mke wa dogo kumtoa wenge...akaanza kumkaba na kumvua ngoa sasa yule mke wa dogo ikasemekana akakosa pumzi ...jamaa akala mzigo mid kama ya saa tisa usiku

Kaka yake na dogo akawa anarudi gafla anakutana na mtu anatoka mbio...na anajigonga ukutan sasa yy akajua ni mwiz akaanza mkimbiza bila kujua mchiz kafanya unyama gan ndan...akamkimbiza sana lakin hakufanikiwa kumkamata lakin alimihis kama ni mtu fulan...hivyo akarud home akakuta umeme umekatika...sasa anaita shemej wala haitiki...akakutana na mtoto wa dogo...akamwambia mama kavamiwa na kaka fulan akawa anampiga...kwenda chumban anamkuta shemeji yake kama kazimia na damu nyingi kitandan...sasa nyumba yao ipo karibu na kituo cha polisi na hata hospital ya rufaaa ipo karibu na kwao...

Kaka mtu akambeba mtoto kwenda nae polis kutoa taarifa...huku nyuma dogo anarud nyumban...yupo na jamaa yake anakuta mazingira ambayo hayaelewi...anaingia chumban anakutana na mke wake hajielewi...anamtafuta mtt hamuon...ikabid ambebe mkewe kumpeleka hospital...mke anachukuliwa vipimo taarifa inatoka amefariki...jamaa anawaza kama wamemuua mke basi na mtt atakuwa wanemuua kupoteza ushahid...sasa daktar wakamwambia aende polis kureport tukio...anaenda polis anakutana na kaka yake pamoja na mtoto wake

Dogo anafika kituon anamwambia kaka yake wameniulia mke...kaka yake anamwambia hyo mtu nimekutana nae na nimemkimbiza...dogo akauliza amevaaje..akamwambia amevaa mabuti na kofia...dogo akavuta hisia na kumwambia kaka yake au ni muddy?? Kaka mtu akamwambia atakuwa ni yy caz alihis hicho kitu lakin hakuwa na uhakika

Wakatoka na defender pale mpaka eneo la tukio...polis wakachukua picha na mlangon kuna alama ya viatu alivyo kuwa anauvunja...

Wakaenda mpaka kwa kina muddy ni nyumba ya pili tu ni jiran sana..

Wakagonga na kuna mtu akafungua polis wakahoji muddy yupo jamaa akawa mbishi akapigwa rungu moja tuu...akasema muddy anakaa chumba cha tatu...polis dogo na kaka yake...wakagonga sana mlango bila mafanikio...ikabid wauvunje..muddy anaamka anajifanya ametoka usingizin na hajui lolote...

Polis wakamuhoji viatu vyako vipo wap...akawaonesha lakin baada ya upekuz zaid wakakuta ameficha lile buti...kwel ni yy..wakamwambia umechukua nn nyumba ya hapo jiran akatoa simu na suti...dogo anajua paswed ya mkew..kuiweka ikafunguka..pemben kulikuwa na shoka dogo akachukua akataka kumkata kata muddy na polis walimdhibit asifanye ivo..

Wakamchukua muddy kwa mahojiano zaidi...dogo analia tu muda wote...jana walimuhoji taarifa ya habari...kumuuliza kama walikuwa na bifu na muddy akanijibu hapana lakin kuna rafik yake muddy aliiba mtaani na dogo alimuona so alienda kureport polis na wakamueka ndan week mbili..na alivyotoka akamwambia dogo nitakuonesha...sasa ndio wakaungana na muddy kufanya malipiz...
 
Una shida zako tu bro. Mbona mambo yapo straight tu ila uzushi ni mwingi unaowapotosha vijana mnaokurupuka bila kutafakari. Kuna vitabu vingi ambavyo vinaeleza maisha ya Adam na Hawa na Mmandenyi anasema kitabu cha "Legends of Jews " ndicho kinachosema eti nyoka alimlala Hawa wakazaa Kaini. Huo ni upotoshaji, sasa nyoka(Shetani) ni Roho itawezaje kuzaa na Hawa(Mwili). Huo ni uongo ni sawa na uzushi "eti majini yanazaa na wanadamu"
Mamandenyi kaingizwa Chaka vibaya Sana na yey kaenda kichwa kichwa Google kitu gani yaani kuamini kila kitu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Leo tarehe 25/12/2018, siku ya Krismasi, ni miaka 47 imepita toka Mnyalukolo, SAID ABDALLAH SIULANGA MWAMWINDI, ammimimie risasi na kumuua aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Iringa, marehemu Dr. WILBERT KLERUU. Mauaji hayo yaliyokea tarehe 25/12/1971 kijijini Mkungugu, Isimani, Iringa.


Dr. WILBERT KLERUU alikuwa ni mzaliwa wa Mwika, Kilimanjaro ambaye alikuwa ni mmoja wa Watanzania wachache wakati huo waliokuwa na shahada ya uzamivu(PHD) ya uchumi wa kijamaa.


Dr. KLERUU alikuwa ni kipenzi cha Baba wa Taifa, Mwalimu JK NYERERE, kutokana na weledi na utendaji wake usio na mfano. Mwanazuoni mwa mwaka 1971, DR.

.KLERUU alikuwaamehamishiwa mkoani Iringa kutokea Mtwara.


Dr. KLERUU alikuwa ni kiongozi machachari sana na ilikuwa kawaida kwake na alikuwa hana hiana kuwafokea hadharani watumishi wa umma wazembe. Kwa hakika, Dr. KLERUU alikuwa mbabe sana. Akiwa Iringa, kuna wakati gari yake ilipigwa "overtake" na gari hilo lililompiga"-overtake" likamziba kwa mbele.

Kufumba na kufumbua, Dr. KLERUU alishuka kama komandoo na kwenda kumuwasha vibao dreva wa gari hilo! Dr. KLERUU, mara kwa mara, alipenda kuwafokea watu kwa kuwaambia "Hamnijui Mimi? Kawaulizeni watu wa Mtwara" na yeye hakuwa mtu wa kukaa ofisini kama viongozi wengi wa wakati huo, bali alijumuika na wananchi na kufanya nao shughuli za maendeleo bega kwa bega ambapo ilikuwa ni kawaida kwake kushika jembe kwa masaa kadhaa bila kula!.


Kipindi hicho kulikuwa na kampeni kubwa ya kuwafanya wananchi walime mashamba ya pamoja na hivyo wakulima waliokuwa na mashamba makubwa walinyang'anywa, kitendo ambacho hakikuwapendeza Wanyalukolo waliokuwa matajiri wenye mashamba makubwa ya mahindi.


Dr. KLERUU alihamishiwa Iringa ili akatekeleze mpango huo wa serikali na alipofika tu akatangaza kwamba mashamba yote binafsi yanapaswa kuwa ya ujamaa kufikia Novemba 1971.






Bw. MWAMWINDI alihamia eneo la Mkungugu, Isimani mwaka 1954 akitokea Iringa mjini alikokuwa dreva. Alianza kilimo kidogo kidogo hatimaye akawa na mashamba makubwa ya mahindi ya hekari takriban 160. Akawa analima mashamba yake kwa trekta katika eneo hilo ambalo awali lilikuwa ni pori. Kipindi hicho, hakukuwa na sehemu Tanzania iliyokuwa ikizalisha mahindi mengi kama Isimani.


Jumamosi ya tarehe 24/12/1971, Dr. KLERUU alitembelea mashamba mbalimbali maeneo ya Tarafani, Igulu na Ndolela kuhamasisha kilimo cha pamoja. Kesho yake, Jumapili ya tarehe 25/12/1971, Dr. KLERUU( ambaye hakuwa na Jumapili wala skukuu) aliendelea na shughuli hizo za kutembelea mashamba muda wa saa 11 jioni, Dr. KLERUU alifika kwenye shamba la MWAMWINDI na kumkuta akilima kwa trekta lake.

Pamoja nae kulikuwa na mtoto wake(Mohamed) na watu wawili aliowaajiri( Yadi Chaula na Charles Mwamalata), Bw. Joseph Kusava ambaye ni mkwe wake pamoja na wake zake waliokuwa wakishirikiana nae kulima siku hiyo. Dr. KLERUU alifika shambani hapo akiendesha gari lake binafsi aina ya Peugeot 404 rangi ya bluu na ubavuni ikiwa imeandikwa RC-Iringa. Baada ya kushuka alimfuata moja kwa moja MWAMWINDI na kuanza kumuhoji maswali mengi kwanini hataki mashamba yake yawe ya ujamaa. Akamwambia "Unafanya nini hapo?"Shuka shenzi we".

MWAMWINDI akamuuliza "kwanini unanitukana?" Dr. KLERUU akamjibu "Funga mdomo wako, n'ge n'ge n'ge nini? Kwanini nawaambia hamsikii? Blood fool". Katika eneo hilo walikuwa wao wawili tu kwani watu wengine walikuwa mbali kidogo. Dr. KLERUU aliyekuwa na kawaida ya kutembea na kifimbo kidogo akakitumia kumchomachoma nacho MWAMWINDI.


MWAMWINDI akafura sana hivyo akaanza kwenda ndani kupitia eneo la makaburi ya baba yake na ndugu wengine huku Dr. KLERUU akimfuata na alipoyaona makaburi akasema "Tazama unaendelea kujenga nyumba za kudumu". MWAMWINDI akamjibu "Hizi sio nyumba, ni mahali ninapozika ndugu zangu". Dr. KLERUU akajibu "Ni mahali unapozikia mirija wenzio, mbwa we!".


Mnyalukolo MWAMWINDI akawaamehamaki sana. Akasema "Swela", akaingia ndani akachukua gobore akatoka nalo nje na kumfyatulia risasi Dr. KLERUU ambaye alianguka na kufariki hapohapo!!! MWAMWINDI aliuchukua mwili wake akauweka kwenye buti ya gari ya Mkuu huyo wa Mkoa, akachukua na kofia ya Pama ya Mkuu wa Mkoa akaivaa yeye na kuanza safari ya kilometa 40 kwenda Iringa mjini.


Mjini Iringa, watu walishangaa kuona gari ya Mkuu wa mkoa inapita upande wa kulia kwa vile mtaa wa Jamatini ulikuwa ni "One way" lakini wakahisi huenda Mkuu wa mkoa ana dharura. Saa 1 jioni, MWAMWINDI akafika kituo kikuu cha polisi akaenda moja kwa moja kaunta akamkuta PC MBETA KASONDA na kukwambia "Ebu nenda kwenye buti ukaitoe mbwa yenu nimeishaiua" na kumkabidhi bunduki pamoja na funguo za gari. PC KASONDA hakuamini macho yake alipouona mwili wa Dr. KLERUU ukiwa umetapakaa damu. Dr. KLERUU alikuwa amevaa ovaroli nyeusi na miwani. Hivyo, mara moja PC KASONDA akamuweka MWAMWINDI chini ya ulinzi.

Mtu mwingine aliyekuwepo kituoni hapo ni mzee DAVID BUTITINI(ambaye alikuwa askari polisi na baadaye kada wa CCM Iringa). Tarumbeta likapulizwa na askari wakakusanyika na kupewa rasmi taarifa ya kifo hicho cha Mkuu wao wa mkoa na gari lake likahifadhiwa nyuma ya kituo cha polisi. Askari wanne wakaenda kuleta kitanda cha magurudumu toka hospitali na hatimaye mwili wa Dr. KLERUU ukapelekwa "mortuary". Kesho yake, siku ya jumatatu, mji mzima wa Iringa uligubikwa na simanzi kubwa.


Kuna kundi la watu ambao walikuwa wakimchukia sana Dr. KLERUU kutokana na aina ya uongozi wake hivyo lilipopata tu taarifa za kifo chake wakanunua makreti ya bia usiku huohuo na kuanza kunywa kwa kushangilia hadharani! Msako ulipoanza usiku huohuo, jamaa hao walikuwa wa kwanza kukamatwa!.


Mzee BUTININI ambaye pia alikuwa Mtwara wakati DR. KLERUU alipokuwa Mkuu wa Mkoa, anakiri kuwa ni kweli DR. KLERUU alikuwa mtu wa shoka- "Ni kweli hata kule Mtwara alionekana mtemi sana mwenye kuhimiza mambo kwa nguvu. Lakini lazma muelewe maeneo ya Mtwara yalikuwa ya vita na tulikuwa tukiwasaidia ndugu zetu wa Frelimo hivyo kule kulihitaji mtu kama DR. KLERUU. Mtwara DR. KLERUU hakukumbana na upinzani ila Iringa hali ilikuwa tofauti. Kwa mawazo yangu, Dr. KLERUU alipaswa kwanza kujifunza juu ya mila na desturi za watu wa Iringa. Maana watu wa Iringa ni watu wa Iringa tu."


Mauaji hayo ya Dr. KLERUU yalimsikitisha sana Mwalimu NYERERE, wakuu wa mikoa na wananchi mbalimbambali. Lilikuwa ni tukio lililoongelewa nchi nzima. Majirani na wazee wengi waliokuwa wakilima pamoja na MWAMWINDI walisombwa na vyombo cha usalama na kumwekea ndani kuisaidia polisi ambapo walikuwa wakikamatwa na kusafirishwa usiku kwa ndege za jeshi. Takribani watu 30 walikamatwa wakiwemo wazee maarufu kama IBRAHIM KHALILI, PESAMBIL, MURSALI na wengineo na kupelekwa sehemu mbalimbali za nchi mf Shinyanga, Mwanza na Zanzibar. Cha kusikitisha ni kwamba ndugu zao hawakujua wamepelekwa wapi! Aidha, nyumbani kwa MWAMWINDI huko Mkungugu kukawa kunalindwa na askari wa FFU muda wote.


Kitendo cha kukamatwa majirani na marafiki wa MWAMWINDI kilileta uhasama mkubwa baina ya ndugu wa majirani hao na familia ya MWAMWINDI.


Ikabidi mwanae (AMANI MWAMWINDI)(21) alazimike kutafuta kibali cha DC Iringa kwenda gereza la Dodoma alikokuwa anashikiliwa MWAMWINDI. Alipoganikiwa kukipata alikwenda na akamueleza hali hiyo ambayo ilimsukitisha sana Mzee MWAMWINDI. AMANI akamshauri baba yake aandike barua kwa Rais NYERERE, nae akafanya hivyo siku hiyohiyo. Katika barua hiyo, MWAMWINDI alimueleza Mwalimu kwamba yeye ndiye aliyemuua Dr. KLERUU hivyo wengine hawahusiki hivyo waachiwe. Baada ya kupita siku kadhaa, wazee hao majirani wakaachiwa na kurejea kijijini hapo, Isimani. Hata hivyo, tafrani hiyo iliyokuwaimewakumba ikafanya wengi wahame eneo hilo kwani waliishaona "togwa limeingia nzi"!.

Upelelezi wa mauaji hayo ulienda haraka na MWAMWINDI akafunguliwa kesi ya mauaji ya kukusudia Mahakama kuu. Kesi ilipoanza kusikilizwa, ilivuta hisia za watu wengi na umati wa watu uliokuwa ukitamalaki kila siku mahakamani ulikuwa "si wa nchi hii!.


Tarehe 2/10/1972, baada ya mashahidi wa pande zote kutoa ushahidi wao akiwemo RPC wa Iringa (Abubakar Hassan) aliyetoa ushahidi upande wa MWAMWINDI kwamba hakuwa na taarifa kwamba Mkuu huyo wa Mkoa angetembelea eneo hilo ndio maana hakumpa "Police escort", Jaji GABRIEL CHIKE ONYIUKE toka Nigeria(aliyehudumu Tanzania toka 1970-1973) alimtia MWAMWINDI hatiani na kumuhukumu kunyongwa hadi afe. Hii ilikuwa ni baada ya kuukataa utetezi wake kwamba alitenda kosa hilo baada ya kurukwa na akili na pia alikasirishwa "provoked" na marehemu, Mh. Jaji aliona kwamba ingawa ni kweli MNYALUKOLO wa kawaida huwa si mtu wa mchezo-mchezo anapodhihakiwa hasa mbele za wake zake lakini kitendo cha MWAMWINDI cha kwenda ndani kufuata bunduki kilionesha, pasina shaka, kwamba aliua kwa kudhamiria.
Adhabu hiyo ya kifo ilitekelezwa mara moja kwani Mwalimu NYERERE alisaini hati ya kifo cha MWAMWINDI

. Hayo hiyo, ilikuwa ni moja ya hati tatu za vifo zilizosainiwa na Mwalimu NYERERE kuidhinisha kunyongwa kwa binadamu katika uongozi wake wa miaka 24 katika taifa hili.


Kesi hii ilikuwa ya aina yake na haikuchukua hata mwaka mmoja toka tukio kutokea na adhabu kutolewa tofauti na kesi nyingine za mauaji ambazo, kwa kawaida, huchukua miaka mingi kabla ya hukumu kutolewa. Kesi hii ilichukua miezi kumi tu.


Baada ya msiba, familia ya DR. KLERUU ilirudi Kilimanjaro. Hata hivyo, Mwalimu NYERERE na KARUME na baadae ABDU JUMBE walikuwa karibu sana na mjane wa DR. KLERUU na wakawasomesha wanawe nchini Urusi na Bulgaria. Aidha, viongozi wengine waliwatia moyo na kuwafariji sana mf. Marehemu Mzee RASHID KAWAWA na mama GETRUDE MONGELA. Dr. KLERUU aliacha watoto wanne ambao ni Eva, Andrew, Carmen na Edwin.


Mwezi Machi 2014, familia ya DR. KLERUU na ya MWAMWINDI zilikutana kwa furaha ili kusameheana kwa tukio hilo. Bi. EVA KLERUU(60) ambaye ni mtoto mkubwa wa Dr. KLERUU na Bw. AMAN MWAMWINDI(67) (aliyekuwa Meya wa mji wa Iringa) walifanya jambo hilo la kihistoria na hivyo kuyaishi kivitendo maandiko ya vitabu vitakatifu yatutakayo wanadamu kusameheana. Picha hii chini inawaonesha wawili hao wakiwa na bashasha baada ya tendo hilo la kihistoria na lisilo la kawaida.


Mnara wa DR. KLERUU umejengwa kwenye "mji" wa MWAMWINDI mahali ambapo alipigwa risasi . Nyumba ya Mkuu wa Mkoa DR. KLERUU bado ipo. Picha hizi hapa chini zinamuonesha Mnyalukolo MWAMWINDI baada ya kujisalimisha polisi pamoja na nyumba ya DR. KLERUU.


REST IN PEACE:


1. Dr. W. KLERUU

2. S. A. MWAMWINDI
Mkuu sijona nyumba ya kleru

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
HV mkuu mtu akiuwa au kuona mauaji je unaweza kukaha muda wote had kufa pasipo kujulikana Kama ulihusika na Jambo fln au itafika muda mtu kufa kabla ya matendo yake kuwa adharani ?

Inonesha kuwa kila tukio la mauwaji halipiti. Hvhv tu bill kujulikana

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
sio kweli ukiua bila kutumia akili ndio lazima ukamatwe tu...lakini wapo wauaji ambao wanaua kwa kupanga mauaji hao bwana hawakamatwi...ng'oooo
 
Kaini kumuua mdogo wake, kisa kikuu siyo sadaka but ni mwanamke aliyepaswa kuolewa na mdogo wake


Kaini siyo mtoto wa Adam ?

Visa vya mauaji ni vingi na miaka hii vimezidi

Just go ...
Aise! Kuna Bible version ya shetani ishatoka ama?
 
Ila me nadhani miaka hiyo hakukuwa na mawakili wazuri, huyu mzee amekosea sana kwa namna huyo marehemu RC alivyomkosea heshima eneo lake. Huwezi kwenda eneo la mtu na kuanza kumtusi mbele ya familia yake hata mimi ningemzabua makofi.

Kimsingi hapo huyo mzee alitakiwa kupewa mvua ya miaka kadhaa kama sio maisha. Ila kumnyonga ni kumtendea dhambi kubwa sana huko anapokwenda roho yake imefunga kwa huzuni anaonekana ni mtu mbaya kwa kosa la kusababishiwa. Kuna muda hawa viongozi au watu fulani wenye mamlaka huwa wanatafuta kuadhibiwa kwa makusudi.
Issue sio kutokuwa na mawakili,bali ni mfumo wa katiba iliyopo,ulioupa mhimili mmoja madaraka zaidi( deep state)
Hivi hujui kuwa Rais wa wakati huo aliwaita majaji wote na kuwapa maelekezo ya kufanya dhidi ya kesi zote dhidi ya serikali kuhusu operation vijiji? Na ilikuwa Mwamwindi lazima anyongwe? Kiasi Cha jaji mmoja kujiuzulu,kwa kutotaka kuinajisi taaluma yake?
Mimi hushangaa kwa baadhi ya watu kudai magufuli alikuwa dikteta hivi wangekuwepo kipindi Cha awamu ya Kwanza wangesemaje?
 
Uko sahihi sana, hivi ndugu hawawezi kuifufua hii kesi na kukata rufaa?
Ukate rufaa miaka hamsini baada ya mtu kunyongwa? Ili iweje? Ingekuwa wanasiasa Kama sugu na lema ambao walifungwa kwa maelekezo kutoka juu Kama ilivyokuwa kwa Mwamwindi pia aliyehukumiwa kunyongwa pia kwa maelekezo ya Rais wa wakati huo na kusaini hati ya kunyongwa harakaharaka ingekuwa sawa,ukate rufaa ili mtu afufuliwe au?
 
Ila me nadhani miaka hiyo hakukuwa na mawakili wazuri, huyu mzee amekosea sana kwa namna huyo marehemu RC alivyomkosea heshima eneo lake. Huwezi kwenda eneo la mtu na kuanza kumtusi mbele ya familia yake hata mimi ningemzabua makofi.

Kimsingi hapo huyo mzee alitakiwa kupewa mvua ya miaka kadhaa kama sio maisha. Ila kumnyonga ni kumtendea dhambi kubwa sana huko anapokwenda roho yake imefunga kwa huzuni anaonekana ni mtu mbaya kwa kosa la kusababishiwa. Kuna muda hawa viongozi au watu fulani wenye mamlaka huwa wanatafuta kuadhibiwa kwa makusudi.
Hilo ni kosa la kuua bila kukusudia(manslaughter) baada ya mtu kuwa provoked lakini kwa maelekezo kutoka juu likawa kosa la kuua kwa kukusudia ili kuufavor utawala wa wakati huo
 
Ukate rufaa miaka hamsini baada ya mtu kunyongwa? Ili iweje? Ingekuwa wanasiasa Kama sugu na lema ambao walifungwa kwa maelekezo kutoka juu Kama ilivyokuwa kwa Mwamwindi pia aliyehukumiwa kunyongwa pia kwa maelekezo ya Rais wa wakati huo na kusaini hati ya kunyongwa harakaharaka ingekuwa sawa,ukate rufaa ili mtu afufuliwe au?
Hapana familia ipate fidia ya haki
 
Back
Top Bottom