Jhounne
JF-Expert Member
- Jul 12, 2018
- 1,093
- 2,564
YaaniMtu huyu alihukumiwa adhabu kali sana, aliteswa sana mpaka kuuliwa kwake, na baada ya kumuua wakaona haitoshi wakamtia kwenye tindikali.
YaaniMtu huyu alihukumiwa adhabu kali sana, aliteswa sana mpaka kuuliwa kwake, na baada ya kumuua wakaona haitoshi wakamtia kwenye tindikali.
Mabeberu walaaniwe!Mtu huyu alihukumiwa adhabu kali sana, aliteswa sana mpaka kuuliwa kwake, na baada ya kumuua wakaona haitoshi wakamtia kwenye tindikali.
...alisemaje huyo Mzee mkuu...ni vema ukatuambia na sisi ili tujue kiongoziUnapoandika jina lake tafadhali weka na heshima aliyobatizwa kama Son of Africa
Moyo wangu unapata simanzi kila nikisikia akitajwa.
Niliwahi kuhadithiwa na mzee wa kinyarwanda ambaye kwa wakati huo wa mauaji yake alikua DRC. Inahuzunisha mnoo, alifanyiwa kila aina ya mateso na udhalilishaji. May Allah rest his soul in jannah. Amin!
Mkuu mbona mi naona tatizo lilikua kwetu waafrika, yaani mmepewa uhuru badala ya kukaa na kupanga mambo ya nchi mnaanza kugombania madaraka. kweli akili ya Mwanfrika haibadiliki,Mabeberu walaaniwe!
Akimaliza tupe ya babako MobutuTunasubiri
Heri ya mwaka mpya mkuu bado tunakusubiriLumumba aponyoka, CIA washindwa kumuua kwa sumu-6
Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) lilituma ‘ujumbe wa sumu’ kwenda Congo kwa ajili ya kumuua Waziri Mkuu wa kwanza wa nchi hiyo, Patrice Emery Lumumba. Ujumbe huo kwenda kwa aliyekuwa mkuu wa CIA, Congo, Lawrence (Larry) Raymond Devlin, ulipelekwa na wakala wa CIA aliyeitwa Sidney Gottlieb
Kwa mujibu wa uchunguzi uliochapishwa na Madeleine G. Kalb katika kitabu ‘The Congo Cables: The Cold War in Africa-From Eisenhower to Kennedy’, ulimwambia Devlin hivi: “Atajitangaza kama Joe kutoka Paris... ni muhimu uonane naye haraka mara atakapokupigia simu. Atajitambulisha kwako kikamilifu na kukueleza kazi aliyokuja kuifanya.”
Ndipo jioni ya Jumatatu ya Septemba 26, Gottlieb aliwasili Congo. Devlin, aliyekuwa anafanya kazi ya ujasusi kwa mwamvuli wa ofisa wa ubalozi wa Marekani Congo, aliondoka ofisini kwake kwenda kukutana na mgeni wake.
Walipokuwa kwenye gari la Devlin, Gottlieb alimweleza kuwa “nimekuja Congo kukupa maelekezo kuhusu operesheni moja muhimu.”
Kitabu ‘Poisoner in Chief: Sidney Gottlieb and the CIA Search for Mind Control’ cha Stephen Kinzer kinasema Gottlieb aliwahi kuifanyia majaribio sumu yake kwa wafungwa, watumiaji dawa za kulevya, wagonjwa mahospitalini, washukiwa wa upelelezi, raia wa kawaida na hata wafanyakazi wenzake, na kote huko, alisema, alifanikiwa.
Gottlieb alikuja kujulikana kuwa ni ofisa pekee wa CIA aliyebeba sumu kutoka Amerika kwenda kumuua kiongozi wa nchi nyingine katika bara la Afrika.
Akiwa nyumbani kwa Devlin katika ubalozi wa Marekani mjini Leopoldville, ndipo Gottlieb alipomfahamisha Devlin kuwa alikuwa amebeba vifaa vyenye sumu ya kumuua Waziri Mkuu Lumumba.
“Mungu wangu,” alishangaa Devlin. “Nani aliyeidhinisha hii operesheni?” Alihoji.
“Ni Rais (Dwight) Eisenhower,” alijibu Gottlieb. “Nilikuwapo wakati akiidhinisha, lakini Dick Bisell alisema Eisenhower anataka Lumumba aondolewe madarakani.” Wakati huo Dwight David “Ike” Eisenhower ndiye alikuwa Rais wa Marekani na Bisell alikuwa ofisa wa CIA aliyeshughulikia miradi mikubwa.
Gottlieb na Devlin wote walijikuta wameacha kuongea kwa dakika kadhaa. Devlin akawasha kwanza sigara kabla hajaendelea kuongea. Baadaye kidogo Gottlieb akavunja ukimya uliotawala.
“Ni jukumu lako kufanya operesheni hii, ni yako peke yako,” Gottlieb alimwambia Devlin. “Maelezo ni yako, lakini lazima (operesheni) iwe safi, ifanyike kwa namna ambayo hakuna kitu kinachoweza kuacha nyuma alama yoyote ya kuihusisha serikali ya Marekani.” Kisha akamkabidhi kasha la sumu alilotoka nalo Marekani.
“Chukua hii,” alimwambia. “Kwa kilichomo humu ndani kikitumika hakuna mtu atakayejua kamwe kuwa Lumumba aliuawa.”
Baada ya hapo Gottlieb akaanza kumpa Devlin maelezo na maelekezo ya namna ya kufanya. Ingeweza kuwekwa kwenye kitu chochote ambacho kingeugusa mdomo wa Lumumba—iwe ni mswaki au chakula, na hapo kazi ingekuwa imemalizika.
Sumu hiyo haikutengenezwa kwa namna ya kuua haraka, lakini kifo kingekuja baada ya saa kadhaa. Alimwambia pia kwamba hata kama kungefanyika uchunguzi wa sababu za kifo, kile ambacho kingeonekana ni zile sababu za kawaida tu.
Hata hivyo ilishindikana, hawakuweza kumwekea sumu kwa kile ambacho John Jacob Nutter alikisema katika kitabu chake, ‘The CIA’s Black Ops: Covert Action, Foreign Policy, and Democracy’, kwamba “Hata kuweka sumu kwenye chakula chake ilikuwa shida sana kwa sababu CIA haikuwa na mawakala ambao wangeweza kuingia jikoni kwa Lumumba.” Kwa hiyo CIA haikufanikiwa kumuua Lumumba kwa sumu.
Kwa zaidi ya miongo miwili akiwa CIA, Gottlieb alikuwa ameelekeza nguvu na akili zake zote katika utafiti wa namna ya kuanzisha mfumo wa kudhibiti akili za mwanadamu lakini alijulikana zaidi kama “mtengenezaji mkuu wa sumu katika CIA.”
Tafiti zake zilikuwa zikifanyika kwa siri kubwa kiasi kwamba alipokuja kuacha kazi mwaka 1972 aliteketeza asilimia 80 ya nyaraka zilizokuwa na ripoti mbaya. Alilazimika kuyateketeza kabla ya kuondoka kazini. Asilimia kubwa ya nyaraka hizo inahususu kazi za Gottlieb.
Anne Collins, katika ukurasa wa 30 wa kitabu chake, ‘In the Sleep Room: The Story of the CIA Brainwashing Experiments in Canada’, anaandika kuwa nyaraka hizo zilikuwa na taarifa mbaya kiasi kwamba maelfu ya kurasa za nyaraka “ziliharibiwa kwa amri ya watu wawili: Mkurugenzi wa CIA Richard Helms, aliyestaafu mwaka 1973 na Dk Sidney Gottlieb, ambaye alihusika zaidi na nyaraka hizo.”
Ilidaiwa kuwa nyaraka hizo zingewekwa wazi zingezua kashfa kubwa zaidi duniani na huenda ingeufungulia ulimwengu sababu za kuifungulia mashtaka CIA kwa ukatili dhidi ya wanadamu.
Kitabu ‘Top Secret Government Archives: Missing Files and Conspiracy Paper Trails’ cha mwandishi wa habari za utafiti, Nick Redfern, kinaandika: “Kama tulivyoona, wakati hofu ilipotanda ndani ya CIA kwamba itajulikana kwa watu wa nje [ya CIA] mradi wa CIA [dhidi ya utu], mkurugenzi wa shirika hilo, Richard Helms na Sidney Gottlieb waliandaa mpango wa kuziteketeza moja kwa moja nyaraka hizo.
Nyaraka hizo zilijulikana pia kama ‘Mpango wa CIA wa kudhibiti akili za wanadamu’.
Sehemu ya mradi huo ulikuwa ni kufanya majaribio juu ya ubongo wa mwanadamu kwa kuendeleza dawa ambazo zingeweza kutumiwa kudhoofisha uwezo wa mtu wa kudhibiti akili yake ili atamke yale asiyokusudia kuyatamka.
Mradi huo na mingine mingi iliandaliwa chini ya Ofisi ya Ushauri wa Kisayansi ya CIA kwa kuratibiwa na Maabara ya Vita ya Kibaiolojia ya Jeshi la Marekani.
Nick Redfern anaendelea: “Kumbuka kuteketezwa nyaraka hizo kulivyofanikiwa; ni kwa kuzimwaga kwenye tanuri, mwaka 1973, katika kituo cha kumbukumbu cha CIA, kilichokuwa Warrenton, Virginia. Kwanini hili jambo lilikuwa la muhimu? Kwa sababu kugundulika siri zilizokuwa kwenye nyaraka hizo kungeonyesha ukatili dhidi ya mwanadamu uliofanywa na shirika...”
Hata hivyo, wakati watu wengi waliokuja kujulishwa kuwa ndugu zao walilishwa sumu iliyotengenezwa na Sidney Gottlieb, walianza kufungua mashtaka mmoja baada ya mwingine alianza kuitwa katika mahakama mbalimbali za nchini Marekani.
Wakati baadhi ya kesi hizo ziliendelea na nyingine zikiwa kwenye upelelezi, Gottlieb alifariki dunia Jumatano ya Machi 10, 1999 Jijini Washington.
Itaendelea…
Sent using Jamii Forums mobile app
hiki kisa cha kifo cha Lumumba huwa naona kinautata mwingi, kwanini walitumia nguvu nyingi sana kumpoteza na kupoteza ushahidi wa kifo chake!!OPERESHENI BARRACUDA ILIVYOMUUA LUMUMBA - 01
Alhamisi ya Juni 30, 1960, Congo ilijipatia uhuru kutoka kwa Ubelgiji. Waziri Mkuu Patrice Emery Lumumba akiwa na miaka 35, akawa kiongozi wa jamhuri hii mpya. Lakini hali ya amani na utulivu ikatoweka muda mfupi baadaye. Kikosi cha majeshi ya waasi kikazua vurugu kiasi kwamba Ubelgiji ilipeleka jeshi lake kulinda raia wake.
Siku chache baadaye, Jumatatu ya Julai 11, ya mwaka huo, Jimbo la Katanga, lililokuwa likiongozwa na Moise Kapenda Tshombe likajitenga. Umoja wa Mataifa ukaingilia kati kwa kutuma jeshi la kulinda amani.
Jumanne ya Januari 17, 1961, miezi sita tu baada ya uhuru wa Congo, Patrice Lumumba aliuawa katika Jimbo la Katanga. Februari 13, maofisa wa Jimbo la Katanga wakatangaza kifo cha Lumumba, lakini hakuna aliyewaamini. Hata wao hawakuziamini taarifa walizotoa. Lawama zikaanza kumiminika kutoka pande zote za dunia.
Urusi iliwashutumu mabeberu na kuitaka Marekani iondoe watu wake Congo, pia ikamtaka aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dag Hammarskjold, kujiuzulu kwa sababu alionekana kuwa kibaraka wa wakoloni.
Katika jiji la Moscow nchini Urusi watu waliandamana baada ya kupata taarifa za kuuawa kwa Lumumba. Katika jiji la Beijing, China, kulifanyika maandamano makubwa ya watu waliokadiriwa kuwa zaidi ya 100,000. Katika nchi mbalimbali raia walivamia balozi za Ubelgiji na kufanya uharibifu.
Ndani ya mwaka mmoja tangu kuuawa kwa Lumumba, Umoja wa Mataifa ulifanya uchunguzi na baadaye ikabainika kuwa hata Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) lilishiriki katika njama za kumuua Lumumba.
Katika ukurasa wa 198 wa kitabu “The African Liberation Struggle: Reflections” cha Godfrey Mwakikagile, jasusi wa Marekani, Stephen Andrew Lucas, ambaye alikuja Tanzania na kufundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alikuwa Congo na kufanya kazi chini ya mkuu wa CIA, Larry Devlin, wakati Lumumba alipokamatwa na kuuawa. Mwingine aliyekuwa Congo na baadaye akaenda Zanzibar ni Frank Carlucci.
Pamoja na Lumumba walikuwako wengine wawili waliokamatwa na kuuawa pamoja naye; Joseph Okito (alikuwa Naibu Spika wa Bunge la Congo) na Maurice Mpolo (alikuwa Waziri wa Vijana na Michezo). Watatu hao walisafirishwa kwa ndege kutoka Kinshasa hadi mji mkuu wa Kalonji wa Bakwanga (sasa unaitwa Mbuji-Mayi).
Wakiwa kwenye ndege aina ya DC-3, wote watatu waliteswa kikatili na walinzi wa Congo. Ndege ilipowasili anga la Bakwanga, rubani hakuweza kutua kwa sababu uwanjani hapo kulikuwa kumetapakaa matanki ya ujazo wa galoni 55.
Rubani aliamua kwenda kutua Uwanja wa Elisabethville (sasa Lubumbashi), na ndege ilipotua, Lumumba alikuwa anakaribia kuzirai kutokana na maumivu.
Ndani ya ndege walikuwa wakiteswa mbele ya Kamishna wa Ulinzi wa Congo, Ferdinand Kazadi na Kamishna wa Mambo ya Ndani wa Congo, Jonas Mukamba. Walipofikishwa Lubumbashi walipelekwa kwenye nyumba jirani na Uwanja wa Ndege wa Luano na kuendelea kuteswa.
Lumumba, ambaye uso wake uliharibiwa kiasi cha kutotambulika kutokana na vipigo na nguo zake zikiwa zimetapakaa damu, alisimamishwa kwenye kichuguu kikubwa huku akimulikwa na taa za magari.
Kwa amri ya Moise Tshombe, rais wa jimbo la Katanga ambaye naye alikuwa akipokea maelekezo kutoka Brussels, Lumumba aliteswa. Kikosi cha mauaji kilimtoa Lumumba katika nyumba alimokuwa akiteswa na kumsafirisha kwa mwendo wa dakika 45 hadi Katanga.
Hapo aliuawa na kikosi cha mauaji kwa kupigwa risasi kwa amri ya Kapteni wa Ubelgiji, Julien Gat. Aliyemfyatulia risasi ni askari wa Ubelgiji, kanali Carlos Huyghe. Mwingine aliyeshiriki kuwafyatulia risasi na kuwaua Okito na Mpolo ni kapteni Julien Gat.
KUPOTEZA USHAHIDI.
Baada ya kuuawa kwa risasi, miili ya watatu hao ilizikwa eneo walilouawa. Kwa hofu kwamba kaburi la Lumumba lingegundulika na baadaye lingeweza kugeuzwa kuwa eneo la heshima, Wabelgiji na vibaraka wao waliamua kupoteza ushahidi ambao ungeweza kuelekeza uliko mwili wake.
Jumatano ya Januari 18, ikiwa ni siku moja baada ya mauaji hayo, miili ya kina Lumumba ilifukuliwa na kupelekwa ndani zaidi msituni na kuzikwa upya karibu na mpaka wa Rhodesia (Zimbabwe) na Congo.
Usiku wa Jumapili ya Januari 22 ndugu wawili wa Ubelgiji Kamishna wa Polisi wa Ubelgiji, Gerard Soete na ndugu yake walikwenda tena kufukua miili ya Lumumba, Okito na Mpolo. Safari hii walikuwa na shoka na misumeno.
Waliikatakata miili hiyo vipande vipande kabla ya kuyeyusha mabaki yake kwa tindikali iliyokuwa imejaa kwenye pipa la petroli la lita 200. Baadaye Soete alikiri kwamba alitumia koleo kung’oa meno mawili ya Lumumba kwa ajili ya ukumbusho.
OPERESHENI BARRACUDA.
Katika kitabu cha “Encyclopedia of leadership: A-E” (ukurasa 925), George R. Goethals na Georgia Sorenson wanasema mpango wa kumuua Lumumba uliitwa ‘Operesheni Barracuda’ na uliandaliwa na Marekani, hususan CIA, ndipo Lumumba akakamatwa na Kanali Mobutu Oktoba 10, 1960.
Katika kikao kilichofanyika jijini Washington, Marekani iliamriwa Lumumba aondolewe madarakani na awekwe kiongozi ambaye angekubali kulinda maslahi ya Wamarekani nchini Congo.
Maagizo hayo yakatumwa kwa mkuu wa CIA nchini Congo, Lawrence Raymond Devlin. CIA wakaunganisha nguvu zao na Ubelgiji.
Agosti 1960, msaada wa kijeshi kutoka Urusi uliingia Congo, jambo ambalo halikuwapendeza Wamarekani na Wabelgiji. Ilikuwa lazima Lumumba aondoke kwa gharama zozote.
Ndipo wakamshawishi Rais wa Congo, Joseph Kasavubu, lakini waligonga mwamba. Devlin akaripoti taarifa hizo makao makuu ya CIA jijini Langley, Marekani, Agosti 24, 1960.
Dk Sidney Gottlieb, mtaalamu wa dawa, akapewa maagizo ya kutafuta sumu ya kumuua Lumumba na isijulikane kuwa Marekani imehusika, na iwe ni dawa ambayo chanzo chake ni Afrika.
ITAENDELEA
siasa za zamani zilikua ngumu sana kwa mtu mweusi hasa zikienda kinyume na siasa za wazungu.Mtu huyu alihukumiwa adhabu kali sana, aliteswa sana mpaka kuuliwa kwake, na baada ya kumuua wakaona haitoshi wakamtia kwenye tindikali.