Mauaji ya Patrice Lumumba 1961

Mauaji ya Patrice Lumumba 1961

Unapoandika jina lake tafadhali weka na heshima aliyobatizwa kama Son of Africa
Moyo wangu unapata simanzi kila nikisikia akitajwa.
Niliwahi kuhadithiwa na mzee wa kinyarwanda ambaye kwa wakati huo wa mauaji yake alikua DRC. Inahuzunisha mnoo, alifanyiwa kila aina ya mateso na udhalilishaji. May Allah rest his soul in jannah. Amin!
 
Unapoandika jina lake tafadhali weka na heshima aliyobatizwa kama Son of Africa
Moyo wangu unapata simanzi kila nikisikia akitajwa.
Niliwahi kuhadithiwa na mzee wa kinyarwanda ambaye kwa wakati huo wa mauaji yake alikua DRC. Inahuzunisha mnoo, alifanyiwa kila aina ya mateso na udhalilishaji. May Allah rest his soul in jannah. Amin!
...alisemaje huyo Mzee mkuu...ni vema ukatuambia na sisi ili tujue kiongozi
 
MAJASUSI WAANZA KUMSHUGHULIKIA LUMUMBA - 4


Ijumaa, Julai 15, majeshi ya Umoja wa Mataifa yaliwasili Congo. Julai 16, baada ya kukutana na Lumumba, mwakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN) Congo, Ralph Bunche, aliripoti, “Lumumba alikuwa kama kichaa na alitenda mambo kwa tabia za kitoto.” Lumumba na Bunche hawakuelewana vizuri.
Baada ya hali kuzidi kuwa mbaya, Jumapili ya Julai 17 Lumumba alitishia kuwa atayaita majeshi ya Urusi ili yasaidie kuyaondoa majeshi ya Umoja wa Mataifa kama watashindwa kuyaondoa majeshi ya Ubelgiji ndani ya saa 72.
Hali ya utulivu na amani ilipozidi kudorora Congo katika zile siku chache baada ya uhuru, Lumumba aliwatishia Umoja wa Mataifa kuwa atayaita majeshi ya Urusi ili yamsaidie kulinda amani Congo na kujikuta akirushiana maneno na Bunche.
Jumamosi Julai 9, 1960, ikiwa ni siku tisa tangu ijipatie uhuru, Serikali ya Congo ilibadili jina la jeshi kutoka ‘Force Publique’ na kuwa ‘Armee Nationale Congolaise’ (ANC). Baraza la Mawaziri lilimteua Victor Lundula, mwafrika aliyepigana katika Vita Kuu II ya Dunia, kuwa jenerali wa kwanza mkuu wa majeshi ya Congo na kuchukua nafasi ya Jenerali Emile Robert Alphonse Janssens ambaye alikuwa Mbelgiji.
Lumumba alimteua pia Joseph-Desire Mobutu kuwa mmoja wa mawaziri wadogo katika ofisi ya Waziri Mkuu, kama kanali na mnadhimu mkuu wa ANC.
Kitabu ‘The Congo: From Leopold to Kabila: A People’s History’ cha Georges Nzongola-Ntalaja katika ukurasa wa 98 kinasema uteuzi wa watu hao wawili Lundula na Mobutu ulitolewa vibaya.
“Lundula hakuwa na sifa zinazohitajiwa kuendesha jeshi la nchi, hususan jeshi jipya. Na kwa Mobutu, Lumumba alifanya kosa kubwa kwa kuamini tu kwamba ana uwezo wa kusimamia jeshi kwa vile aliweza kuwasimamia watu wachache waliomzunguka.”
Kitabu hicho kinasema “(Lumumba) hakusikiliza uvumi uliosambaa uliodai Mobutu alikuwa wakala wa majasusi wa Ubelgiji na Marekani. Kwa kumteua Mobutu kushika wadhifa huo, tayari (Lumumba) alikuwa amemchagua Yuda wake mwenyewe.”
Mwandishi wa historia, Didier Ndongala Mumbata, alilifafanua zaidi katika kitabu ‘Patrice Lumumba, Ahead of His Time’. Mumbata anaandika kuwa matukio ya kati ya Julai na Septemba 1960 yalibadili sana uhusiano wa Lumumba na baadhi ya mawaziri wake na wanasiasa wenzake. Alionekana kupigana vita mwenyewe.
Mambo yalipokuwa mazuri alizungukwa na marafiki na ‘wapongezaji’ wengine wa kweli na wa uongo. Mambo yalipokwenda mrama alijikuta yuko mwenyewe.
Mobutu, ambaye alikuwa rafiki yake wa karibu na ambaye awali alimteua kuwa msaidizi wake katika chama chake cha MNC, kisha akamwingiza serikalini baada ya kuwa waziri mkuu wa kwanza wa Congo, na baadaye akamfanya kuwa mnadhimu mkuu wa jeshi la Congo, alimsaliti na kujiunga na kambi ya Joseph Kasavubu. Wote wawili, Kasavubu na Mobutu walishiriki kwa kiasi kikubwa kumwangusha na kumuua Lumumba.
Familia ya Lumumba ilimjua sana Mobutu. Lumumba alikutana na Mobutu wakati yeye (Mobutu) akisomea uandishi wa habari mjini Brussels, Ubelgiji.
Mobutu na Lumumba walikuwa na matamanio yaliyokaribia kufanana. Walitamani kuona Congo iliyo na umoja, walichukia kutawaliwa na wageni. Kwa ushawishi wa Lumumba, Mobutu aliingia katika siasa za Congo kupitia MNC. Mobutu alifanya kazi kama katibu muhtasi wa Lumumba. Yeye ndiye aliyeamua nani aonane na Lumumba na kwa muda gani.
Mwandishi Mumbata anasema kwa ujumla Mobutu ndiye aliyekuwa anapanga ratiba yote ya shughuli za kisiasa za Lumumba.
Nyumbani kwa Lumumba kulikuwa kama nyumbani kwa Mobutu kwa sababu aliweza kwenda huko wakati wowote kadri alivyotaka na alikuwa akijihudumia vyakula na vinywaji kadri alivyoweza.
Sehemu kubwa ya maisha yake ya kikazi siku za mwanzo za harakati za siasa za Congo kuelekea siku ya uhuru, Mobutu alikaa nyumbani kwa Lumumba. Hii ilimfanya awe karibu zaidi na Lumumba kuliko mwanasiasa yeyote duniani.
Katika ukurasa wa 2562 wa kamusi ‘The 20th Century Go-N: Dictionary of World Biography, Volume 8’ iliyohaririwa na Frank Magill, inasimuliwa kuwa Lumumba alimwamini sana Mobutu.
Mwandishi Didier Mumbata anasimulia: “Lumumba aliwaamini watu kirahisi, na haraka. Alikuwa mwema, alikuwa akimwambia mkewe kuwa Mobutu alikuwa rafiki yake sana na nyumbani kwake (Lumumba) ni nyumbani kwa Mobutu.
Lumumba alijua fika kuwa Mobutu alihitaji sana fedha kuikimu familia yake, lakini alikuwa akimwambia asijaribu kuisaliti Congo na watu wake kwa sababu ya fedha. Lakini Mobutu, kama alivyokuwa Yuda kwa Yesu (Kristo), alikuja kumsaliti rafiki yake huyo kwa Wabelgiji na Wamarekani.”
Hata hivyo, lilipokuja suala la kupata msaada wa kijeshi kutoka Urusi ili isaidie kuyaondoa majeshi ya Ubelgiji nchini Congo, ndipo Rais Kasavubu na Mobutu walipoungana kumpinga Lumumba.
Lumumba alipoona hapati msaada wa haraka kutoka majeshi ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa, Julai 17, 1960 alitishia kuyaita majeshi ya Urusi ili yasaidie kuyaondoa ya Umoja wa Mataifa kama watashindwa kuyaondoa majeshi ya Ubelgiji ndani ya saa 72.
Baadaye siku hiyo, Lumumba alitoa tishio jingine. Akasema ikiwa majeshi ya Umoja wa Mataifa hayatayaondoa majeshi ya Ubelgiji kabla ya Julai 20, watalazimika kuyaita majeshi ya Urusi kuwaondoa wao.
Julai 22, malori 100 ya kijeshi kutoka Urusi yaliwasili Congo, lakini hayakukabidhiwa jeshi la Umoja wa Mataifa. Katika Mkutano wa Usalama wa Taifa (NSC) nchini Marekani, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA), Allen Dulles, aliwaambia wenzake mkutanoni kuwa alihisi “Lumumba amenunuliwa na Wakomunisti”. Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Rais Dwight Eisenhower.
Julai 27, akiwa Umoja wa Mataifa, kwa mara nyingine Lumumba aliomba msaada Umoja wa Mataifa, Marekani na Urusi.
Alipozuru Washington, Lumumba alikwenda kukutana na Waziri Mdogo wa Mambo ya Nje wa Marekani, Douglas Dillon, ambaye baadaye alidai kuwa Lumumba ni “mwendawazimu” na kwamba “ni mgumu kushughulika naye.”
Agosti 1, akizungumza mbele ya Umoja wa Mataifa, Lumumba alimshutumu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dag Hammarskjold, kwa kuyakatalia majeshi ya Umoja wa Mataifa kuishambulia Katanga.
Agosti 7, Lumumba alikwenda kwa siri Ghana alikokutana na Rais Kwame Nkrumah kuzungumza suala la nchi hizo kuungana.
Agosti 8 Jimbo la Kasai Kusini nalo likatangaza kujitenga na Congo. Juma moja baadaye, Lumumba aliomba msaada wa kijeshi kutoka Urusi kudhibiti majimbo ya Katanga na Kasai yaliyojitenga.
Kesho yake, Agosti 16, Urusi wakatangaza kuwa huenda Congo wakahitaji kupatiwa jeshi la nje kuleta hali ya amani. Lumumba akasisitiza kuwa majeshi ya Umoja wa Mataifa yaondoke Congo.
Agosti 18 Urusi wakatuma kwenda Congo ndege 10 za kivita zenye rangi ya jeshi la Congo.
Baada ya kurejea Congo akitokea Marekani, Lumumba aliwaambia Rais Kasavubu na Mkuu wa Majeshi yake, Joseph Mobutu, kwamba ameamua sasa kuyaita majeshi ya Urusi.

Kasavubu na Mobutu walimkatalia. Lakini Lumumba alikuwa ameshafanya uamuzi. Aliita majeshi ya Urusi ambayo yangemsaidia kuzuia kujitenga kwa jimbo la Kasai Kusini. Alifanikiwa, lakini mara baada ya mapigano kumalizika yalifuatiwa na mauaji ya watu zaidi ya 1,000 na wengine wapatao 250,000 kuyakimbia makazi yao.
Mara moja wakala wa CIA nchini Congo, Larry (Lawrence) Devlin, akatuma ripoti Washington ikidai kuwa Lumumba anajiandaa kufanya mapinduzi ya Kikomunisti.
Mradi wa kwanza wa CIA wa kumshughulikia Lumumba ulianza mapema Agosti 1960 na ulipewa jina la ‘Operation Wizard’. Sehemu moja ya utekelezaji wa mpango huo ni kuwahonga waandishi wa habari wa ndani na nje ya Congo ili waandike habari mbaya za Lumumba, kufadhili maandamano ya kumpinga, na kuhonga wanasiasa watofautiane naye. Mpango huo ulisimamiwa na mkuu wa CIA nchini Congo, Larry Devlin na watu wake.
Katika kitabu ‘Shadow Warfare: The History of Africa’s Undeclared Wars’ cha Larry Hancock, aliyekuwa akiandika muhtasari wa mkutano huo ni Robert Johnson. Dulles alikaririwa akisema, “Kwa Lumumba, tunakabiliana na mtu wa aina ya Castro au mbaya kuliko Castro.”
Siku chache baadaye, kwa mujibu wa kitabu ‘The Assassination of Lumumba’ cha Ludo de Witte, Agosti 26 “Allen Dulles, mkuu wa CIA, alituma telegramu kwenda ofisi za CIA za Leopoldville chini ya Larry Devlin: Telegramu hiyo ilisomeka “Kuondolewa kwa Lumumba madarakani lazima kuwe jambo la lazima na la haraka ... Lazima lipewe kipaumbele cha kwanza katika shughuli zetu.”
Baadaye siku hiyo hiyo Dulles alituma ujumbe mwingine kwenda Congo uliosomeka: “Sasa ni uhakika kwamba iwapo (Lumumba) ataendelea kushikilia wadhifa wake (Uwaziri Mkuu) Ukomunisti utatawala ... Kung’olewa kwake lazima kupewe kipaumbele.”
Itaendelea…!
 
Lumumba aponyoka, CIA washindwa kumuua kwa sumu-6



Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) lilituma ‘ujumbe wa sumu’ kwenda Congo kwa ajili ya kumuua Waziri Mkuu wa kwanza wa nchi hiyo, Patrice Emery Lumumba. Ujumbe huo kwenda kwa aliyekuwa mkuu wa CIA, Congo, Lawrence (Larry) Raymond Devlin, ulipelekwa na wakala wa CIA aliyeitwa Sidney Gottlieb
Kwa mujibu wa uchunguzi uliochapishwa na Madeleine G. Kalb katika kitabu ‘The Congo Cables: The Cold War in Africa-From Eisenhower to Kennedy’, ulimwambia Devlin hivi: “Atajitangaza kama Joe kutoka Paris... ni muhimu uonane naye haraka mara atakapokupigia simu. Atajitambulisha kwako kikamilifu na kukueleza kazi aliyokuja kuifanya.”
Ndipo jioni ya Jumatatu ya Septemba 26, Gottlieb aliwasili Congo. Devlin, aliyekuwa anafanya kazi ya ujasusi kwa mwamvuli wa ofisa wa ubalozi wa Marekani Congo, aliondoka ofisini kwake kwenda kukutana na mgeni wake.
Walipokuwa kwenye gari la Devlin, Gottlieb alimweleza kuwa “nimekuja Congo kukupa maelekezo kuhusu operesheni moja muhimu.”
Kitabu ‘Poisoner in Chief: Sidney Gottlieb and the CIA Search for Mind Control’ cha Stephen Kinzer kinasema Gottlieb aliwahi kuifanyia majaribio sumu yake kwa wafungwa, watumiaji dawa za kulevya, wagonjwa mahospitalini, washukiwa wa upelelezi, raia wa kawaida na hata wafanyakazi wenzake, na kote huko, alisema, alifanikiwa.
Gottlieb alikuja kujulikana kuwa ni ofisa pekee wa CIA aliyebeba sumu kutoka Amerika kwenda kumuua kiongozi wa nchi nyingine katika bara la Afrika.
Akiwa nyumbani kwa Devlin katika ubalozi wa Marekani mjini Leopoldville, ndipo Gottlieb alipomfahamisha Devlin kuwa alikuwa amebeba vifaa vyenye sumu ya kumuua Waziri Mkuu Lumumba.
“Mungu wangu,” alishangaa Devlin. “Nani aliyeidhinisha hii operesheni?” Alihoji.
“Ni Rais (Dwight) Eisenhower,” alijibu Gottlieb. “Nilikuwapo wakati akiidhinisha, lakini Dick Bisell alisema Eisenhower anataka Lumumba aondolewe madarakani.” Wakati huo Dwight David “Ike” Eisenhower ndiye alikuwa Rais wa Marekani na Bisell alikuwa ofisa wa CIA aliyeshughulikia miradi mikubwa.
Gottlieb na Devlin wote walijikuta wameacha kuongea kwa dakika kadhaa. Devlin akawasha kwanza sigara kabla hajaendelea kuongea. Baadaye kidogo Gottlieb akavunja ukimya uliotawala.
“Ni jukumu lako kufanya operesheni hii, ni yako peke yako,” Gottlieb alimwambia Devlin. “Maelezo ni yako, lakini lazima (operesheni) iwe safi, ifanyike kwa namna ambayo hakuna kitu kinachoweza kuacha nyuma alama yoyote ya kuihusisha serikali ya Marekani.” Kisha akamkabidhi kasha la sumu alilotoka nalo Marekani.
“Chukua hii,” alimwambia. “Kwa kilichomo humu ndani kikitumika hakuna mtu atakayejua kamwe kuwa Lumumba aliuawa.”
Baada ya hapo Gottlieb akaanza kumpa Devlin maelezo na maelekezo ya namna ya kufanya. Ingeweza kuwekwa kwenye kitu chochote ambacho kingeugusa mdomo wa Lumumba—iwe ni mswaki au chakula, na hapo kazi ingekuwa imemalizika.
Sumu hiyo haikutengenezwa kwa namna ya kuua haraka, lakini kifo kingekuja baada ya saa kadhaa. Alimwambia pia kwamba hata kama kungefanyika uchunguzi wa sababu za kifo, kile ambacho kingeonekana ni zile sababu za kawaida tu.
Hata hivyo ilishindikana, hawakuweza kumwekea sumu kwa kile ambacho John Jacob Nutter alikisema katika kitabu chake, ‘The CIA’s Black Ops: Covert Action, Foreign Policy, and Democracy’, kwamba “Hata kuweka sumu kwenye chakula chake ilikuwa shida sana kwa sababu CIA haikuwa na mawakala ambao wangeweza kuingia jikoni kwa Lumumba.” Kwa hiyo CIA haikufanikiwa kumuua Lumumba kwa sumu.
Kwa zaidi ya miongo miwili akiwa CIA, Gottlieb alikuwa ameelekeza nguvu na akili zake zote katika utafiti wa namna ya kuanzisha mfumo wa kudhibiti akili za mwanadamu lakini alijulikana zaidi kama “mtengenezaji mkuu wa sumu katika CIA.”
Tafiti zake zilikuwa zikifanyika kwa siri kubwa kiasi kwamba alipokuja kuacha kazi mwaka 1972 aliteketeza asilimia 80 ya nyaraka zilizokuwa na ripoti mbaya. Alilazimika kuyateketeza kabla ya kuondoka kazini. Asilimia kubwa ya nyaraka hizo inahususu kazi za Gottlieb.
Anne Collins, katika ukurasa wa 30 wa kitabu chake, ‘In the Sleep Room: The Story of the CIA Brainwashing Experiments in Canada’, anaandika kuwa nyaraka hizo zilikuwa na taarifa mbaya kiasi kwamba maelfu ya kurasa za nyaraka “ziliharibiwa kwa amri ya watu wawili: Mkurugenzi wa CIA Richard Helms, aliyestaafu mwaka 1973 na Dk Sidney Gottlieb, ambaye alihusika zaidi na nyaraka hizo.”
Ilidaiwa kuwa nyaraka hizo zingewekwa wazi zingezua kashfa kubwa zaidi duniani na huenda ingeufungulia ulimwengu sababu za kuifungulia mashtaka CIA kwa ukatili dhidi ya wanadamu.
Kitabu ‘Top Secret Government Archives: Missing Files and Conspiracy Paper Trails’ cha mwandishi wa habari za utafiti, Nick Redfern, kinaandika: “Kama tulivyoona, wakati hofu ilipotanda ndani ya CIA kwamba itajulikana kwa watu wa nje [ya CIA] mradi wa CIA [dhidi ya utu], mkurugenzi wa shirika hilo, Richard Helms na Sidney Gottlieb waliandaa mpango wa kuziteketeza moja kwa moja nyaraka hizo.
Nyaraka hizo zilijulikana pia kama ‘Mpango wa CIA wa kudhibiti akili za wanadamu’.
Sehemu ya mradi huo ulikuwa ni kufanya majaribio juu ya ubongo wa mwanadamu kwa kuendeleza dawa ambazo zingeweza kutumiwa kudhoofisha uwezo wa mtu wa kudhibiti akili yake ili atamke yale asiyokusudia kuyatamka.
Mradi huo na mingine mingi iliandaliwa chini ya Ofisi ya Ushauri wa Kisayansi ya CIA kwa kuratibiwa na Maabara ya Vita ya Kibaiolojia ya Jeshi la Marekani.
Nick Redfern anaendelea: “Kumbuka kuteketezwa nyaraka hizo kulivyofanikiwa; ni kwa kuzimwaga kwenye tanuri, mwaka 1973, katika kituo cha kumbukumbu cha CIA, kilichokuwa Warrenton, Virginia. Kwanini hili jambo lilikuwa la muhimu? Kwa sababu kugundulika siri zilizokuwa kwenye nyaraka hizo kungeonyesha ukatili dhidi ya mwanadamu uliofanywa na shirika...”
Hata hivyo, wakati watu wengi waliokuja kujulishwa kuwa ndugu zao walilishwa sumu iliyotengenezwa na Sidney Gottlieb, walianza kufungua mashtaka mmoja baada ya mwingine alianza kuitwa katika mahakama mbalimbali za nchini Marekani.
Wakati baadhi ya kesi hizo ziliendelea na nyingine zikiwa kwenye upelelezi, Gottlieb alifariki dunia Jumatano ya Machi 10, 1999 Jijini Washington.
Itaendelea…

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lumumba aponyoka, CIA washindwa kumuua kwa sumu-6



Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) lilituma ‘ujumbe wa sumu’ kwenda Congo kwa ajili ya kumuua Waziri Mkuu wa kwanza wa nchi hiyo, Patrice Emery Lumumba. Ujumbe huo kwenda kwa aliyekuwa mkuu wa CIA, Congo, Lawrence (Larry) Raymond Devlin, ulipelekwa na wakala wa CIA aliyeitwa Sidney Gottlieb
Kwa mujibu wa uchunguzi uliochapishwa na Madeleine G. Kalb katika kitabu ‘The Congo Cables: The Cold War in Africa-From Eisenhower to Kennedy’, ulimwambia Devlin hivi: “Atajitangaza kama Joe kutoka Paris... ni muhimu uonane naye haraka mara atakapokupigia simu. Atajitambulisha kwako kikamilifu na kukueleza kazi aliyokuja kuifanya.”
Ndipo jioni ya Jumatatu ya Septemba 26, Gottlieb aliwasili Congo. Devlin, aliyekuwa anafanya kazi ya ujasusi kwa mwamvuli wa ofisa wa ubalozi wa Marekani Congo, aliondoka ofisini kwake kwenda kukutana na mgeni wake.
Walipokuwa kwenye gari la Devlin, Gottlieb alimweleza kuwa “nimekuja Congo kukupa maelekezo kuhusu operesheni moja muhimu.”
Kitabu ‘Poisoner in Chief: Sidney Gottlieb and the CIA Search for Mind Control’ cha Stephen Kinzer kinasema Gottlieb aliwahi kuifanyia majaribio sumu yake kwa wafungwa, watumiaji dawa za kulevya, wagonjwa mahospitalini, washukiwa wa upelelezi, raia wa kawaida na hata wafanyakazi wenzake, na kote huko, alisema, alifanikiwa.
Gottlieb alikuja kujulikana kuwa ni ofisa pekee wa CIA aliyebeba sumu kutoka Amerika kwenda kumuua kiongozi wa nchi nyingine katika bara la Afrika.
Akiwa nyumbani kwa Devlin katika ubalozi wa Marekani mjini Leopoldville, ndipo Gottlieb alipomfahamisha Devlin kuwa alikuwa amebeba vifaa vyenye sumu ya kumuua Waziri Mkuu Lumumba.
“Mungu wangu,” alishangaa Devlin. “Nani aliyeidhinisha hii operesheni?” Alihoji.
“Ni Rais (Dwight) Eisenhower,” alijibu Gottlieb. “Nilikuwapo wakati akiidhinisha, lakini Dick Bisell alisema Eisenhower anataka Lumumba aondolewe madarakani.” Wakati huo Dwight David “Ike” Eisenhower ndiye alikuwa Rais wa Marekani na Bisell alikuwa ofisa wa CIA aliyeshughulikia miradi mikubwa.
Gottlieb na Devlin wote walijikuta wameacha kuongea kwa dakika kadhaa. Devlin akawasha kwanza sigara kabla hajaendelea kuongea. Baadaye kidogo Gottlieb akavunja ukimya uliotawala.
“Ni jukumu lako kufanya operesheni hii, ni yako peke yako,” Gottlieb alimwambia Devlin. “Maelezo ni yako, lakini lazima (operesheni) iwe safi, ifanyike kwa namna ambayo hakuna kitu kinachoweza kuacha nyuma alama yoyote ya kuihusisha serikali ya Marekani.” Kisha akamkabidhi kasha la sumu alilotoka nalo Marekani.
“Chukua hii,” alimwambia. “Kwa kilichomo humu ndani kikitumika hakuna mtu atakayejua kamwe kuwa Lumumba aliuawa.”
Baada ya hapo Gottlieb akaanza kumpa Devlin maelezo na maelekezo ya namna ya kufanya. Ingeweza kuwekwa kwenye kitu chochote ambacho kingeugusa mdomo wa Lumumba—iwe ni mswaki au chakula, na hapo kazi ingekuwa imemalizika.
Sumu hiyo haikutengenezwa kwa namna ya kuua haraka, lakini kifo kingekuja baada ya saa kadhaa. Alimwambia pia kwamba hata kama kungefanyika uchunguzi wa sababu za kifo, kile ambacho kingeonekana ni zile sababu za kawaida tu.
Hata hivyo ilishindikana, hawakuweza kumwekea sumu kwa kile ambacho John Jacob Nutter alikisema katika kitabu chake, ‘The CIA’s Black Ops: Covert Action, Foreign Policy, and Democracy’, kwamba “Hata kuweka sumu kwenye chakula chake ilikuwa shida sana kwa sababu CIA haikuwa na mawakala ambao wangeweza kuingia jikoni kwa Lumumba.” Kwa hiyo CIA haikufanikiwa kumuua Lumumba kwa sumu.
Kwa zaidi ya miongo miwili akiwa CIA, Gottlieb alikuwa ameelekeza nguvu na akili zake zote katika utafiti wa namna ya kuanzisha mfumo wa kudhibiti akili za mwanadamu lakini alijulikana zaidi kama “mtengenezaji mkuu wa sumu katika CIA.”
Tafiti zake zilikuwa zikifanyika kwa siri kubwa kiasi kwamba alipokuja kuacha kazi mwaka 1972 aliteketeza asilimia 80 ya nyaraka zilizokuwa na ripoti mbaya. Alilazimika kuyateketeza kabla ya kuondoka kazini. Asilimia kubwa ya nyaraka hizo inahususu kazi za Gottlieb.
Anne Collins, katika ukurasa wa 30 wa kitabu chake, ‘In the Sleep Room: The Story of the CIA Brainwashing Experiments in Canada’, anaandika kuwa nyaraka hizo zilikuwa na taarifa mbaya kiasi kwamba maelfu ya kurasa za nyaraka “ziliharibiwa kwa amri ya watu wawili: Mkurugenzi wa CIA Richard Helms, aliyestaafu mwaka 1973 na Dk Sidney Gottlieb, ambaye alihusika zaidi na nyaraka hizo.”
Ilidaiwa kuwa nyaraka hizo zingewekwa wazi zingezua kashfa kubwa zaidi duniani na huenda ingeufungulia ulimwengu sababu za kuifungulia mashtaka CIA kwa ukatili dhidi ya wanadamu.
Kitabu ‘Top Secret Government Archives: Missing Files and Conspiracy Paper Trails’ cha mwandishi wa habari za utafiti, Nick Redfern, kinaandika: “Kama tulivyoona, wakati hofu ilipotanda ndani ya CIA kwamba itajulikana kwa watu wa nje [ya CIA] mradi wa CIA [dhidi ya utu], mkurugenzi wa shirika hilo, Richard Helms na Sidney Gottlieb waliandaa mpango wa kuziteketeza moja kwa moja nyaraka hizo.
Nyaraka hizo zilijulikana pia kama ‘Mpango wa CIA wa kudhibiti akili za wanadamu’.
Sehemu ya mradi huo ulikuwa ni kufanya majaribio juu ya ubongo wa mwanadamu kwa kuendeleza dawa ambazo zingeweza kutumiwa kudhoofisha uwezo wa mtu wa kudhibiti akili yake ili atamke yale asiyokusudia kuyatamka.
Mradi huo na mingine mingi iliandaliwa chini ya Ofisi ya Ushauri wa Kisayansi ya CIA kwa kuratibiwa na Maabara ya Vita ya Kibaiolojia ya Jeshi la Marekani.
Nick Redfern anaendelea: “Kumbuka kuteketezwa nyaraka hizo kulivyofanikiwa; ni kwa kuzimwaga kwenye tanuri, mwaka 1973, katika kituo cha kumbukumbu cha CIA, kilichokuwa Warrenton, Virginia. Kwanini hili jambo lilikuwa la muhimu? Kwa sababu kugundulika siri zilizokuwa kwenye nyaraka hizo kungeonyesha ukatili dhidi ya mwanadamu uliofanywa na shirika...”
Hata hivyo, wakati watu wengi waliokuja kujulishwa kuwa ndugu zao walilishwa sumu iliyotengenezwa na Sidney Gottlieb, walianza kufungua mashtaka mmoja baada ya mwingine alianza kuitwa katika mahakama mbalimbali za nchini Marekani.
Wakati baadhi ya kesi hizo ziliendelea na nyingine zikiwa kwenye upelelezi, Gottlieb alifariki dunia Jumatano ya Machi 10, 1999 Jijini Washington.
Itaendelea…

Sent using Jamii Forums mobile app
Heri ya mwaka mpya mkuu bado tunakusubiri
 
OPERESHENI BARRACUDA ILIVYOMUUA LUMUMBA - 01


Alhamisi ya Juni 30, 1960, Congo ilijipatia uhuru kutoka kwa Ubelgiji. Waziri Mkuu Patrice Emery Lumumba akiwa na miaka 35, akawa kiongozi wa jamhuri hii mpya. Lakini hali ya amani na utulivu ikatoweka muda mfupi baadaye. Kikosi cha majeshi ya waasi kikazua vurugu kiasi kwamba Ubelgiji ilipeleka jeshi lake kulinda raia wake.

Siku chache baadaye, Jumatatu ya Julai 11, ya mwaka huo, Jimbo la Katanga, lililokuwa likiongozwa na Moise Kapenda Tshombe likajitenga. Umoja wa Mataifa ukaingilia kati kwa kutuma jeshi la kulinda amani.

Jumanne ya Januari 17, 1961, miezi sita tu baada ya uhuru wa Congo, Patrice Lumumba aliuawa katika Jimbo la Katanga. Februari 13, maofisa wa Jimbo la Katanga wakatangaza kifo cha Lumumba, lakini hakuna aliyewaamini. Hata wao hawakuziamini taarifa walizotoa. Lawama zikaanza kumiminika kutoka pande zote za dunia.

Urusi iliwashutumu mabeberu na kuitaka Marekani iondoe watu wake Congo, pia ikamtaka aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dag Hammarskjold, kujiuzulu kwa sababu alionekana kuwa kibaraka wa wakoloni.

Katika jiji la Moscow nchini Urusi watu waliandamana baada ya kupata taarifa za kuuawa kwa Lumumba. Katika jiji la Beijing, China, kulifanyika maandamano makubwa ya watu waliokadiriwa kuwa zaidi ya 100,000. Katika nchi mbalimbali raia walivamia balozi za Ubelgiji na kufanya uharibifu.

Ndani ya mwaka mmoja tangu kuuawa kwa Lumumba, Umoja wa Mataifa ulifanya uchunguzi na baadaye ikabainika kuwa hata Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) lilishiriki katika njama za kumuua Lumumba.

Katika ukurasa wa 198 wa kitabu “The African Liberation Struggle: Reflections” cha Godfrey Mwakikagile, jasusi wa Marekani, Stephen Andrew Lucas, ambaye alikuja Tanzania na kufundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alikuwa Congo na kufanya kazi chini ya mkuu wa CIA, Larry Devlin, wakati Lumumba alipokamatwa na kuuawa. Mwingine aliyekuwa Congo na baadaye akaenda Zanzibar ni Frank Carlucci.

Pamoja na Lumumba walikuwako wengine wawili waliokamatwa na kuuawa pamoja naye; Joseph Okito (alikuwa Naibu Spika wa Bunge la Congo) na Maurice Mpolo (alikuwa Waziri wa Vijana na Michezo). Watatu hao walisafirishwa kwa ndege kutoka Kinshasa hadi mji mkuu wa Kalonji wa Bakwanga (sasa unaitwa Mbuji-Mayi).

Wakiwa kwenye ndege aina ya DC-3, wote watatu waliteswa kikatili na walinzi wa Congo. Ndege ilipowasili anga la Bakwanga, rubani hakuweza kutua kwa sababu uwanjani hapo kulikuwa kumetapakaa matanki ya ujazo wa galoni 55.

Rubani aliamua kwenda kutua Uwanja wa Elisabethville (sasa Lubumbashi), na ndege ilipotua, Lumumba alikuwa anakaribia kuzirai kutokana na maumivu.

Ndani ya ndege walikuwa wakiteswa mbele ya Kamishna wa Ulinzi wa Congo, Ferdinand Kazadi na Kamishna wa Mambo ya Ndani wa Congo, Jonas Mukamba. Walipofikishwa Lubumbashi walipelekwa kwenye nyumba jirani na Uwanja wa Ndege wa Luano na kuendelea kuteswa.

Lumumba, ambaye uso wake uliharibiwa kiasi cha kutotambulika kutokana na vipigo na nguo zake zikiwa zimetapakaa damu, alisimamishwa kwenye kichuguu kikubwa huku akimulikwa na taa za magari.

Kwa amri ya Moise Tshombe, rais wa jimbo la Katanga ambaye naye alikuwa akipokea maelekezo kutoka Brussels, Lumumba aliteswa. Kikosi cha mauaji kilimtoa Lumumba katika nyumba alimokuwa akiteswa na kumsafirisha kwa mwendo wa dakika 45 hadi Katanga.

Hapo aliuawa na kikosi cha mauaji kwa kupigwa risasi kwa amri ya Kapteni wa Ubelgiji, Julien Gat. Aliyemfyatulia risasi ni askari wa Ubelgiji, kanali Carlos Huyghe. Mwingine aliyeshiriki kuwafyatulia risasi na kuwaua Okito na Mpolo ni kapteni Julien Gat.

KUPOTEZA USHAHIDI.
Baada ya kuuawa kwa risasi, miili ya watatu hao ilizikwa eneo walilouawa. Kwa hofu kwamba kaburi la Lumumba lingegundulika na baadaye lingeweza kugeuzwa kuwa eneo la heshima, Wabelgiji na vibaraka wao waliamua kupoteza ushahidi ambao ungeweza kuelekeza uliko mwili wake.

Jumatano ya Januari 18, ikiwa ni siku moja baada ya mauaji hayo, miili ya kina Lumumba ilifukuliwa na kupelekwa ndani zaidi msituni na kuzikwa upya karibu na mpaka wa Rhodesia (Zimbabwe) na Congo.

Usiku wa Jumapili ya Januari 22 ndugu wawili wa Ubelgiji Kamishna wa Polisi wa Ubelgiji, Gerard Soete na ndugu yake walikwenda tena kufukua miili ya Lumumba, Okito na Mpolo. Safari hii walikuwa na shoka na misumeno.

Waliikatakata miili hiyo vipande vipande kabla ya kuyeyusha mabaki yake kwa tindikali iliyokuwa imejaa kwenye pipa la petroli la lita 200. Baadaye Soete alikiri kwamba alitumia koleo kung’oa meno mawili ya Lumumba kwa ajili ya ukumbusho.

OPERESHENI BARRACUDA.
Katika kitabu cha “Encyclopedia of leadership: A-E” (ukurasa 925), George R. Goethals na Georgia Sorenson wanasema mpango wa kumuua Lumumba uliitwa ‘Operesheni Barracuda’ na uliandaliwa na Marekani, hususan CIA, ndipo Lumumba akakamatwa na Kanali Mobutu Oktoba 10, 1960.

Katika kikao kilichofanyika jijini Washington, Marekani iliamriwa Lumumba aondolewe madarakani na awekwe kiongozi ambaye angekubali kulinda maslahi ya Wamarekani nchini Congo.

Maagizo hayo yakatumwa kwa mkuu wa CIA nchini Congo, Lawrence Raymond Devlin. CIA wakaunganisha nguvu zao na Ubelgiji.

Agosti 1960, msaada wa kijeshi kutoka Urusi uliingia Congo, jambo ambalo halikuwapendeza Wamarekani na Wabelgiji. Ilikuwa lazima Lumumba aondoke kwa gharama zozote.

Ndipo wakamshawishi Rais wa Congo, Joseph Kasavubu, lakini waligonga mwamba. Devlin akaripoti taarifa hizo makao makuu ya CIA jijini Langley, Marekani, Agosti 24, 1960.

Dk Sidney Gottlieb, mtaalamu wa dawa, akapewa maagizo ya kutafuta sumu ya kumuua Lumumba na isijulikane kuwa Marekani imehusika, na iwe ni dawa ambayo chanzo chake ni Afrika.
ITAENDELEA
hiki kisa cha kifo cha Lumumba huwa naona kinautata mwingi, kwanini walitumia nguvu nyingi sana kumpoteza na kupoteza ushahidi wa kifo chake!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
IMG_2629.JPG

alizikwa hapo na badae kufukuliwa, hayo matofali yalipo ndipo lilikua kaburi lake


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom