ShesRise_1
JF-Expert Member
- Aug 21, 2025
- 17,749
- 42,229
- Thread starter
- #41
Sikujua kama sijaeleweka japo naona kuna walioelewaHoja gani mkuu 'ShesRise', maana naona umechanganya maharage, makande, njegere, wali,n.k., ndani ya dishi hilo moja.
Maana yako ya "muuaji" ni nini?
Nikikulipa ujira unifikishie mzigo wangu nyumbani kwangu, mzigo ni wako au ni wangu?
Labda ingesaidia kidogo kufafanua mada yako ili ieleweke kwa wepesi.
Mimi ngoja nikupe mfano halisi kabisa:
Mzee Ally Mohamed Kibao aliyeuliwa kikatili kabisa.
Muuaji alikuwa ni aliyetoa amri huyo mzee auwawe; au hao wavuta bangi waliotoa roho yake na kuharibu maiti?
Ngoja nishauri: unapoandika mada kama hii, haisaidii kitu kutumia maneno meeeengi sana kama ulivyofanya hapa. Ingetosha tu kutumia mistari michache tu bila ya kumchosha msomaji wako, na kumchanganya akili.
Asante kwa maoni🙏🙏🙏
