Matumizi mabaya ya IDs za Wakongwe wa JF, wanasema Gudume yupo Twitter

GuDume

JF-Expert Member
Jan 18, 2015
6,652
14,247
Wanasema "hata akienda juu Kapungu hafikii kwa Mungu" ndiyo. Sisi wazee wa zamani tumekutana na mengi hadi kufika umri huu...kutekwa kisiasa,kiuchumi na kimapenzi pia. Lakini tumeweza ku survive katika jamii yenye kujawa watu na viumbe visivyo vya kawaida. Hivyo wanaotumia IDs zetu bado hawawezi kuwa sisi.

Duniani hatupo peke yetu. Ni ukweli ulio na utupu, uso fichika. Kuna watu na waso watu. Tumechanganyika wote kwenye kapu moja. Na JF imekuwa kama kokoro. Inakamata kila kitu na hatimaye kuvua samaki na waso samaki. So ni jukumu la kila member kujenga utulivu wa akili.

Binafsi kwa siku lazima asubuhi na usiku nipitie JF kujua nini kimejiri ulimwenguni.

Kumeibuka matumizi yasofaa ya IDs za members wakongwe humu ndani katika mitandao mingine ya Kijamii. Mfano mara kadhaa kuna watu wanasema Gudume yupo Twitter. Hapana. Sina account ya jina langu Twitter na mtu yeyote anayetumia jina hili nitamke tu kuwa huyo ni tapeli kama wale wanaosema "ile ela itume kwenye number ii"

Gudume anabaki JF akifurahi na wanaofurahi na kulia na waolia. Wapo wazee wenzangu humu tunaendelea kusomana na kubadilishana mawazo. Naamini tutafikia hatua siku moja hadi ya kubadilishana mademu " ashakum si matusi" maana pia inachosha kila mara kubadilishana mawazo tu.
 
As long as ni fake id sidhani kama ina madhara kwako..

Mfano, kuna akina Juma wengi duniani, anayetumia Juma kule Facebook haimaanishi akitokea mtu Twitter akajiita Juma awe ni yule wa Facebook..

Hivyo relax mzee wetu...
 
Members wengi maarufu huku ndio waliochangamsha Tweeter! Sometimes IDs za huku zinatumika kule na members wa huku hata kama si yule yule!
 
Gudume tupo na wewe kipindi cha nyuma aisee ulichangamsha MMU. Kwa niaba ya wanaJf tunaomba uwe unaandika atleast nyuzi 1 per day.
 
Sijui kwa nini sijawahi hata kufikiria kufunguwa account Twitter?

Ni kama Telegram licha ya kusifiwa usalama wake bado hata sijawahi kufikiria kudownload hiyo app.
 
Sijui kwa nini sijawahi hata kufikiria kufunguwa account Twitter?

Ni kama Telegram licha ya kusifiwa usalama wake bado hata sijawahi kufikiria kudownload hiyo app.
Na kama mpaka leo hujafungua akaunti twitter nakushauri usijiunge tu. Miaka ya nyuma kidogo kundi la wajinga lilikuwa facebook, twitter ikawa na werevu.
Lakini sasa hivi lile kundi la wajinga limehamia twitter kiasi werevu wanazidiwa sasa.
OGOPA SANA KUNDI LA WAJINGA, WAKIAMUA WANAKUCHAGULIA HATA RAIS AMBAYE HATAKIWI
 
Na kama mpaka leo hujafungua akaunti twitter nakushauri usijiunge tu. Miaka ya nyuma kidogo kundi la wajinga lilikuwa facebook, twitter ikawa na werevu.
Lakini sasa hivi lile kundi la wajinga limehamia twitter kiasi werevu wanazidiwa sasa.
OGOPA SANA KUNDI LA WAJINGA, WAKIAMUA WANAKUCHAGULIA HATA RAIS AMBAYE HATAKIWI
Hilo kundi haliwezi kuishi Sasa, ndio mtaji muhimu wa Ccm.
 
Na memes na kuchambana na kutukanana. Twitter haiwezekani kabisa kuwa na mjadala wa maana.
Kwahiyo Twitter na Instagram kwa kina michambo city hamna tofauti?

Sasa tuiprotect JF kwa nguvu zote maana nayo imevamiwa na vijana wa hovyo.

Mods wangekuwa wanatumia siku maalum za kufuta uchafu na takataka zote zilizojazwa JF na kuzitupa kwenye trash bin.

Mtu unaingia hata hujui uende jukwaa gani ni takataka zimejaa kila jukwaa.
 
Back
Top Bottom