Kidogo-kidogo tutafika!
Mimi hasira zangu kwa CCM na Tume ya Uchaguzi sijui nizielezeje.
Na hao wasimamizi wanarubuniwa vipi lakini?Ni Njaa kali au nini?
Lazima bunge litabadili katiba hv karibuni na mambo haya ya NEC na CCM kuwa mashoga utaisha.
Mkuu BIRO Lipangalala,Jongo Mlabani,Mbasa,Kionjo,Kosovo,Katindiuka wengi wao wamekataa Elimu bure,Afya bure,Cement 5000/= na bati 5000/=.Wamechagua sisiem.
Habari zina sema Chadema imeshinda lakini mkurugenzi kapigwa mkwara akitangaza chadema imeshinda atafute sehemu ya kazi nyingine.
Hivi kweli jamani hii ni haki kweli? wamerudia kuhesabu na wakaweka za kuchakachua lkn bado wameshindwa sasa hawataki kutangaza mshindi, jamani wakilombero msikubari mlinde kura zenu ndiyo silaha yenu katika miaka mitano ijayo.
Habari hii ina ukweli na punde nimemtumia sms Dr Slaa, yule mama ameshinda ila kuna hila kama ya Ulanga Magharibi na ni kweli wanaweza kutaka kununua matokeo kama chama ila kwa Mteketa sasa yuko hoi kiuchumi. Nimeongea na mmoja ya waliojumuisha kura anasema mama kashinda kwa tofauti takribani alfu na upuuzi ila CCM WANATAKA KUCHAKACHUA. WENYE SIMU YA REGIA MPIGIENI MWAMBIENI ASIDANGANYIKE NA MAPESA ASIMAME KTK MSTARI SALAMA. MIE NAMKUBALI SANA NA UMMA WA ULANGA KILOMBERO UKO MKONONI MWAKE.
Regia asaidiwe maana tangu asubuhi yuko pale Bomani na wananchi yeye mwenyewe tayari ana takwimu za ushindi wake, nimemsihi Dr Slaa kumsaidia kwa hali mali kisiasa ili akue na kukomaa kisiasa kama kina Mdee, kilombero ametisha na sasa nguvu ya umma imsitiri atutoe kimasokimaso wana Moro, So God help us.
Mimi nasikitika sana kuwa kwani kuna nini majimbo ambayo upinzani ha hasa ule wa Chadema ukiwa unataka kushinda, matokeo ndo yanacheleweshwa vibaya mno!
Prof. alishashinda, Rejia alishashinda, yaani kichwa kinaniuma vibaya, kwanini lakini nec?????
Sehemu zetu zote matokeo kuhesabu tu, inakuwa shida, wakati kupiga kura haikuwa vile. Halafu mbona mwaka huu kura zilizoharibika nyingi sana?????
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.