Matokeo Kidato IV: Utata mtupu!

Matokeo Kidato IV: Utata mtupu!

Hakuna wakati taifa letu limechanganyikiwa kama sasa. Fikiria walioidhinisha matokeo ndio wanaotengua wakingali madarakani. Ilikuwaje Lukuvi atoe tamko la wizara ya elimu wakati waziri husika na naibu wake wako. Mimi nilidhani walishajiuzulu. Mwenyekiti wa NECTA na Katibu mtendaji kama wanajiamini na elimu zao na wangependa kutunza heshima zao waondoke madarakani kabla matokeo mapya hajatangazwa vinginevyo wote ni wahuni 2
umemaliza kila kitu mdau
 
Bado sijui hii aibu tutaifuta vipi na Mungu ni wa ajabu kila siku wanazidi kuumbuana wenyewe hadi raha sometimes japo inakera.
 
Bongo kila kitu ni siasa tuu hakuna hata aibu!!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
samahani mkuu.umemaliza kidato cha nne mwaka gani? Viwango vya juu! Umetumia vigezo gani? Umewahi hata kuona moja ya mtihani wa necta mwaka jana? uspumbuzike na hoja za wanasiasa. Heri yao ambao hawajashikiwa akili zao na wanasiasa uchwara!

hapo kwenye rangi naona unatafuta cheche kwa moderator.
 
Tatizo la nchi hii ni kuingiza siasa hata kwenye mambo yasiyo husiana na siasa
 
Alikuwa na majibu kabla ya kuanza kazi ya uchunguzi kwenye tume.
In fwakt, iyo tume ilitakiwa iwe na mtu mmoja tu!
Huyohuyo mwenyekiti, huyo katibu, huyo mjumbe, huyohuyo nafasi zooooote.!
Na Mtu huyo ni Prof. Mchome (I doubt huu uprofesa wa kibongo, bora hata maji marefu aliamua kujipa)

Mkuu hapa bongo Prof. akiamua kujiingiza kwenye siasa inabidi awe tayari kuuvua Uprof. wake!
 
Baadhi wa wasomi wa kibongo (kama hawa akina Prof. Mukandala), hawaitendei haki kabisa nnchi hii!
 
Kikao cha kupitisha Viwango Vipya vya Ufaulu vilivyotumika kwa Kidato cha Nne kilihusisha Wizara ya Elimu na Ufundi,NECTA na TCU. Nyaraka za kikao hicho kilichofanyika Disemba mwaka jana,zinaonesha kuwa kikao husika kilikuwa chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dr.Shukuru Kawambwa na Katibu wa Kikao alikuwa Naibu wake Bwana Phillipo Mulugo.

Kwa upande wa NECTA,waliwasilishwa na Mwenyekiti wake Prof.Rwekaza Mukandala na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo,Dr.Joyce Ndalichako.Pia alikuwepo Mjumbe kutoka Mamlaka ya Vyuo Vikuu nchini-TCU ambaye alikuwa ni Prof. Sifuni Ernest Mchome (ambaye baadaye akawa Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Ufaulu wa Kidato cha Nne!)

Kikao hicho kiliidhinisha kutumika kwa viwango hivyo vipyakwa kidato cha nne na cha sita. Wajumbe wote wa Mkutano walikubaliana na viwango vipya na matumizi yake kwa kidato cha nne 2012.

Habari zaidi zimeripotiwa katika Mwananchi la leo

Je, kuchunguza na kutaka kubadili matokeo haya si dharau zilizopitiliza kwa watanzania? Je, ni halali kwa Prof.Mchome kuhudhuria kikao na halafu kuongoza Tume ya Kuchunguza? Watanzania tumedharauliwa,sasa tuchukue hatua gani? Nani mtanzania muungwana atawaamini watu hawa kwasasa?
Made in Tanzania.
 
Kikao cha kupitisha Viwango Vipya vya Ufaulu vilivyotumika kwa Kidato cha Nne kilihusisha Wizara ya Elimu na Ufundi,NECTA na TCU. Nyaraka za kikao hicho kilichofanyika Disemba mwaka jana,zinaonesha kuwa kikao husika kilikuwa chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dr.Shukuru Kawambwa na Katibu wa Kikao alikuwa Naibu wake Bwana Phillipo Mulugo.

Kwa upande wa NECTA,waliwasilishwa na Mwenyekiti wake Prof.Rwekaza Mukandala na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo,Dr.Joyce Ndalichako.Pia alikuwepo Mjumbe kutoka Mamlaka ya Vyuo Vikuu nchini-TCU ambaye alikuwa ni Prof. Sifuni Ernest Mchome (ambaye baadaye akawa Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Ufaulu wa Kidato cha Nne!)

Kikao hicho kiliidhinisha kutumika kwa viwango hivyo vipyakwa kidato cha nne na cha sita. Wajumbe wote wa Mkutano walikubaliana na viwango vipya na matumizi yake kwa kidato cha nne 2012.

Habari zaidi zimeripotiwa katika Mwananchi la leo

Je, kuchunguza na kutaka kubadili matokeo haya si dharau zilizopitiliza kwa watanzania? Je, ni halali kwa Prof.Mchome kuhudhuria kikao na halafu kuongoza Tume ya Kuchunguza? Watanzania tumedharauliwa,sasa tuchukue hatua gani? Nani mtanzania muungwana atawaamini watu hawa kwasasa?

kawambwa team chura anapenda maji lakini cyo ya moto
 
Jamani mataTizo yote Haya ya kiutendaji ya waliopewa madaraka waliowengi ni MAtokeo ya elimu yetu ya tz. Curriculum ndiyo inataka mtu awe hivyo,muongo, fisadi ,aajiriwe, atoe&apokee rushwa ili afaidi yeye tu. Ubinafsi mbele.
 
Kama ndivyo ilivyotokea bado naendelea kushikiria msimamo wangu kwamba kuna ulazima viwango vya zamani vitumike......it's wasn't fair at all! Mitihani imefanyika somewhere around October - November huku wahusika wakuu (wanafunzi wakiwa wanafahamu wazi kwamba grading ipo hivi!! Mitihani wameshafanya, wametulia nyumbani wanasubiria matokeo; huku nyuma wapuuzi wachache wanakaa na kuweka viwango vipya....NO, UNACCEPTABLE! Narudia, wengi wetu tunatamani kila wakati tupate sababu ya kuilaumu serikali; hapa wasilaumiwe kwa kurudisha viwango vipya bali walaumiwe kwa kutumia viwango vipya kinyemela (bila wahusika waathirika wakuu) kufahamu! Tuache ubinfasi wa kujiona tumeshavuka mto! Hapa JF nafahamu kuna wanafunzi wengi wa vyuo vikuu! Assume, tangu unaingia First Year unafahamu (say) C inaanzii 50-64; na umefanya paper unafahamu hivyo ndivyo viwango! Hatimae unarudishiwa paper yako, unakuta umepata 52; unapumua kidogo coz' unafahamu umepata C. Matokeo yanawekwa notice board, unakuta somo husika umewekewa D; unakuja kuhoji unaambiwa mara baada ya mitihani kwisha; board ilikaa na kuweka viwango vipya ambavyo C inaanzia 55-69! Let's be honest here...hivi kweli huko vyuoni kungekalika?! Yaani from nowhere, muambiwe viwango vibadilishwa tena kimya kimya! HAPANA, HILI HALIKUBALIKI! Hao wote waliokaa na kupitisha maamuzi sio waathirika wa moja kwa moja, waathirika wa moja kwa moja ni wanafunzi waliohusika na wazazi/walezi wao!

cc JokaKuu
 
Last edited by a moderator:
Obwato hakuna haki yoyote kwa mwanafunzi kuwekewa kiwango kidogo cha ufaulu huu ni udhalilishaji kwa mwanafunzi mwenyewe, na kama kweli tunataka kutengeneza taifa la watu washindani kwenye nyanja za ajira na kujiajiri ni bora tukamaintain viwango hivyo vikubwa ili tutoe mazao bora! kuwawekea viwango vidogo vya ufaulu ni kuwadanganya wanafunzi wenyewe kuwa wao ni bora na wanapofika kwenye ushindani na wengine wanaonekana vilaza tu! Just thinking outside the Box!

Mkuu uko sahihi kabisa. Mimi binafsi siamini kwamba wanafunzi hawa wengi eti wamefeli kwa sababu alama zilibadilishwa. Kwa nini sasa hawakupata alama za juu ili wafaulu? Sababu za kufeli ziko wazi lakini kwa kuogopa aibu na kuonekana wameshindwa kufanya kazi zao ndo wameamua kujishikiza kwenye hilo la alama. Aibu tupu!
 
Wazimu wa namna yeyote ile unawezekana Tanzania na watu walio wengi watauvumilia kazi kwelikweli!
 
Back
Top Bottom