Matokeo Kidato IV: Utata mtupu!

Matokeo Kidato IV: Utata mtupu!

Kama ndivyo ilivyotokea bado naendelea kushikiria msimamo wangu kwamba kuna ulazima viwango vya zamani vitumike......it's wasn't fair at all! Mitihani imefanyika somewhere around October - November huku wahusika wakuu (wanafunzi wakiwa wanafahamu wazi kwamba grading ipo hivi!! Mitihani wameshafanya, wametulia nyumbani wanasubiria matokeo; huku nyuma wapuuzi wachache wanakaa na kuweka viwango vipya....NO, UNACCEPTABLE! Narudia, wengi wetu tunatamani kila wakati tupate sababu ya kuilaumu serikali; hapa wasilaumiwe kwa kurudisha viwango vipya bali walaumiwe kwa kutumia viwango vipya kinyemela (bila wahusika waathirika wakuu) kufahamu! Tuache ubinfasi wa kujiona tumeshavuka mto! Hapa JF nafahamu kuna wanafunzi wengi wa vyuo vikuu! Assume, tangu unaingia First Year unafahamu (say) C inaanzii 50-64; na umefanya paper unafahamu hivyo ndivyo viwango! Hatimae unarudishiwa paper yako, unakuta umepata 52; unapumua kidogo coz' unafahamu umepata C. Matokeo yanawekwa notice board, unakuta somo husika umewekewa D; unakuja kuhoji unaambiwa mara baada ya mitihani kwisha; board ilikaa na kuweka viwango vipya ambavyo C inaanzia 55-69! Let's be honest here...hivi kweli huko vyuoni kungekalika?! Yaani from nowhere, muambiwe viwango vibadilishwa tena kimya kimya! HAPANA, HILI HALIKUBALIKI! Hao wote waliokaa na kupitisha maamuzi sio waathirika wa moja kwa moja, waathirika wa moja kwa moja ni wanafunzi waliohusika na wazazi/walezi wao!

cc JokaKuu
NasDaz,

..lakini NECTA ni chombo cha serikali pia.

..umesahau kwamba mtendaji mkuu wa necta anateuliwa na raisi??

..binafsi nadhani students were not supposed to fail that much hata kama grading scheme[madaraja]imebadilishwa.

..naamini wanafunzi wameathirika kiasi kile kwasababu wengi wao wanafaulu at borderline.

cc: Kichuguu, Kitila Mkumbo, @Kubwajinga, Nyani Ngabu
 
NasDaz,

..lakini NECTA ni chombo cha serikali pia.

..umesahau kwamba mtendaji mkuu wa necta anateuliwa na raisi??

..binafsi nadhani students were not supposed to fail that much hata kama grading scheme[madaraja]imebadilishwa.

..naamini wanafunzi wameathirika kiasi kile kwasababu wengi wao wanafaulu at borderline.

cc: Kichuguu, Kitila Mkumbo, @Kubwajinga, Nyani Ngabu
JokaKuu,
You're right, NECTA ni chombo cha serikali! Lakini kuwa chombo cha serikali hakuhalalishi wao kufanya mambo ya hovyo hovyo yakaachwa yapite kwavile tu mambo hayo yamefanywa na mamlaka inayotambulika na kwa baraka za serikali! Na kimsingi hoja yangu haisimami kwavile tu wanafunzi wamefeli; ninachosimamia mimi ni kwamba kilichofanyika hakikuwa right! Inawezekana kabisa katika kubadilisha Grading NECTA hawalazimiki kuutaarifu umma au inawezekana kabisa kwamba NECTA wana mamlaka ya kubadilisha GRADING hata siku rasmi ya kuanza kusahihisha mitihani yenyewe; lakini hata kama wana mamlaka hayo, bado si sahihi kufanya jambo linaloakisi maisha ya watu kihuni huni namna hiyo!

JokaKuu, na ndio maana nilipata kuwauliza hata nyie wasomi, hivi umeshafanya UE yako huku unafahamu kabisa kwamba (say) C inaanzia 50-64, na wewe paper unapata 52 lakini unakuta umewekewa D na unapohoji, unajibiwa kwamba last week tumebadilisha Grading(kinyemela) na sasa C inaanzia 55! Je, ungekubali uache mambo yapite kirahisi rahisi tu?!

Suala la grading ni sensitive issue ambayo wahusika ni lazima walifahamu in advance na ndio maana hata kwenye University Prospectus unakuta Grading zimewekwa mle! Mtu unaanza First Year, unafahamu kabisa kwamba nikipata marks fulani; hiyo ni A or B or anything like that! Sasa kama kitu ni sensitive kiasi hicho, watu wachache hamuwezi kuamka na kuanza grading mpya bila wadau kufahamu! Kwa mfano, taarifa ya Mwananchi wanasema makubaliano ya kubadilisha grading yalifanyika December.....what does it mean? Yaani wakati mitihani imeshaanza kusahishwa, tena wakati hata wasahishaji wanafahamu kwamba grading zipo hivi na hivi; huku nyuma, waheshimiwa wachache wanaamua vinginevyo! No, sio sahihi kabisa!

Ikiwa tuta-entertain suala la NECTA kupandisha viwango kinyemela na kuona wapo right; sijui tutakuwa na mamlaka gani ya kuwasimanga siku wakiamua tena kushusha viwango kinyemela!!

Nakubaliana na hoja yako kwako kwamba " students were not supposed to fail that much hata kama grading scheme[madaraja]imebadilishwa", lakini kama nilivyosema hapo awali, iwe wamefeli sana au wamefaulu sana; bado haikuwa sahihi!
 
Tanzania yetu eeeh yote yanapatikana tu hapa kwingineko wamedurufu kwetu
 
JokaKuu,
You're right, NECTA ni chombo cha serikali! Lakini kuwa chombo cha serikali hakuhalalishi wao kufanya mambo ya hovyo hovyo yakaachwa yapite kwavile tu mambo hayo yamefanywa na mamlaka inayotambulika na kwa baraka za serikali! Na kimsingi hoja yangu haisimami kwavile tu wanafunzi wamefeli; ninachosimamia mimi ni kwamba kilichofanyika hakikuwa right! Inawezekana kabisa katika kubadilisha Grading NECTA hawalazimiki kuutaarifu umma au inawezekana kabisa kwamba NECTA wana mamlaka ya kubadilisha GRADING hata siku rasmi ya kuanza kusahihisha mitihani yenyewe; lakini hata kama wana mamlaka hayo, bado si sahihi kufanya jambo linaloakisi maisha ya watu kihuni huni namna hiyo!

Suala la grading ni sensitive issue ambayo wahusika ni lazima walifahamu in advance na ndio maana hata kwenye University Prospectus unakuta Grading zimewekwa mle! Mtu unaanza First Year, unafahamu kabisa kwamba nikipata marks fulani; hiyo ni A or B or anything like that! Sasa kama kitu ni sensitive kiasi hicho, watu wachache hamuwezi kuamka na kuanza grading mpya bila wadau kufahamu! Kwa mfano, taarifa ya Mwananchi wanasema makubaliano ya kubadilisha grading yalifanyika December.....what does it mean? Yaani wakati mitihani imeshaanza kusahishwa, tena wakati hata wasahishaji wanafahamu kwamba grading zipo hivi na hivi; huku nyuma, waheshimiwa wachache wanaamua vinginevyo! No, sio sahihi kabisa!

Ikiwa tuta-entertain suala la NECTA kupandisha viwango kinyemela na kuona wapo right; sijui tutakuwa na mamlaka gani ya kuwasimanga siku wakiamua tena kushusha viwango kinyemela!!

Nakubaliana na hoja yako kwako kwamba " students were not supposed to fail that much hata kama grading scheme[madaraja]imebadilishwa", lakini kama nilivyosema hapo awali, iwe wamefeli sana au wamefaulu sana; bado haikuwa sahihi!

Chifu,

Unataka kumaanisha kwamba grading system mpya ndiyo chanzo cha kufeli vibaya kwa kidato cha nne 2012?!?
 
mwaka 2011 -dv 4 na 0 ni 90%
mwaka 2012 - dv 4 na 0 ni 93%
serikali- vitumike viwango vya 2011
wanafunzi & vilaza wengine - hah hah hah hah afadhali kiwango cha kufaulu kitapanda.
Mimi- hah hah hah hah hah hah endeleeni kuota.
 
Chifu,

Unataka kumaanisha kwamba grading system mpya ndiyo chanzo cha kufeli vibaya kwa kidato cha nne 2012?!?
Mkuu wangu,
mbona nimeshaeleza wazi kwamba hoja ya msingi sio kufeli sana au kidogo; hoja ya msingi ni kwamba haikuwa right kubadilisha grading wakati mechi imeshachezwa na kumalizika!!

Kama kubadilisha grading kueathiri au hapana, nimeshalisema hili siku za nyuma, nikafanya hadi analysis ya matokeo ya baadhi ya shule kwa kipindi cha mwaka 2010, 2011 na 2012! Siwezi kuyarudia yale coz' yalikuwa maelezo marefu sana.....But all in all, sababu yoyote itakayotajwa kama chanzo, excluding grading ni sababu ambayo imekuwepo nchini kwa miaka kadhaa sasa; so why 2012?! Katika maelezo yale nikahoji; ikiwa chanzo ni vitabu, mishahara midogo, mahabara, n.k; mbona hata shule zile zisizo na common problems(kv Feza Boys, Marian Girls n.k) nazo wamefeli ikiwa utaamua kulinganisha matokeo ya shule hizo ya mwaka 2012 na yale ya 2011 na 2010?!

Hapo, nikaona lazima patakuwa na COMMON PROBLEM(S) kwa both; private na government schools ambayo katu haiwezi kuwa suala la maabara, maslahi or anything like that! By the way, kwangu hoja ya maabara naona ndo wala haiwezi kuwa sababu coz' kama ingekuwa sababu basi wanafunzi ingekuwa wanafaulu masomo yasiyohitaji maabara!
 
NasDaz,

..mimi nadhani wananchi tunapaswa kuambiwa ukweli about who knew what and when.

..imeelezwa kwamba vikao vya maamuzi ya kubadili grading system vinahusisha watendaji wa necta na wizara.

..sasa ktk mazingira hayo kwanini taarifa hizo hazikufika mashuleni na kwa wanafunzi?

..mimi panahitajika kufanyika mabadiliko makubwa necta na wizarani. hivi tutakuwa taifa la aina gani huko mbele ya safari?
 
Last edited by a moderator:
NasDaz,

..mimi nadhani wananchi tunapaswa kuambiwa ukweli about who knew what and when.

..imeelezwa kwamba vikao vya maamuzi ya kubadili grading system vinahusisha watendaji wa necta na wizara.

..sasa ktk mazingira hayo kwanini taarifa hizo hazikufika mashuleni na kwa wanafunzi?

..mimi panahitajika kufanyika mabadiliko makubwa necta na wizarani. hivi tutakuwa taifa la aina gani huko mbele ya safari?
Sasa ikiwa maamuzi ya kubadili grading yalifanyika December 2012; hao wanafunzi wangepata saa ngapi taarifa hizo wakati wahusika (watahiniwa 2012) walikuwa wameshafanya mitihani na kuwa majumbani kwao!!? Inawezekana mashuleni taarifa zilifika lakini zilifika wakati grading mpya zimeshatumika! Katika hali ya hali kawaida, nilitarajia suala la new grading lingefanyika na kutangazwa kwa wadau/wanafunzi angalu miezi kabla ya mitihani!

Suala la kufanya mabadiliko makubwa wizarani na NECTA, naunga mkono kwani inavyoelekea mambo yanaendeshwa "Biz as usual!"
 
Sasa ikiwa maamuzi ya kubadili grading yalifanyika December 2012; hao wanafunzi wangepata saa ngapi taarifa hizo wakati wahusika (watahiniwa 2012) walikuwa wameshafanya mitihani na kuwa majumbani kwao!!? Inawezekana mashuleni taarifa zilifika lakini zilifika wakati grading mpya zimeshatumika! Katika hali ya hali kawaida, nilitarajia suala la new grading lingefanyika na kutangazwa kwa wadau/wanafunzi angalu miezi kabla ya mitihani!

Suala la kufanya mabadiliko makubwa wizarani na NECTA, naunga mkono kwani inavyoelekea mambo yanaendeshwa "Biz as usual!"
NasDaz,

..kama ni hivyo wahusika wizarani na necta wanapaswa kuchukuliwa hatua.

..uamuzi sensitive kama huo unafanyika na hakuna mtu serikalini anachukua hatua za kuusitisha??

..hii nchi iko inajiendesha yenyewe kwa kweli. we dont have a government.
 
Last edited by a moderator:
NasDaz,

..kama ni hivyo wahusika wizarani na necta wanapaswa kuchukuliwa hatua.

..uamuzi sensitive kama huo unafanyika na hakuna mtu serikalini anachukua hatua za kuusitisha??

..hii nchi iko inajiendesha yenyewe kwa kweli. we dont have a government.
@JokaKuu,
Dakika chache zilizopita nilikuwa natafuta source ya habari ya mtoa mada hapo juu! Baada ya kupekuwa pekuwa, nimeikuta hapa: Ripoti ya Elimu bungeni yaibua utata - Kitaifa - mwananchi.co.tz .

Hakika baada ya kusoma, nikajikuta namchukia Kawambwa ghafla! Nimejikuta nikimchukia ghafla kv ni hivi majuzi tu nilimuona kupitia TV akisema kwamba yeye hana sababu za kuwajibika! Lakini ukisoma habari hiyo, utakuja kugundua tatizo ni Wizara na NECTA! Hata hivyo, NECTA nawaona ndo wana nafasi kubwa zaidi katika hili kv wao ni professional na mambo mengi NECTA walikuwa wanapeleka mapendekezo wizarani na Wizara kutoa maamuzi!! Aidha, kuna jambo ambalo limenishangaza kwenye taarifa hiyo ambayo Mwananchi imenukuu kutoka kwenye nyaraka ambazo ziliambatanishwa kwenye gazeti la Jamhuri! Aya zilizoniacha mdomo wazi ni pamoja na:

"Tafadhali rejea kikao kilichofanyika tarehe 10/12/2012 katika ukumbi wa mikutano wa wizara kuhusu somo tajwa hapo juu (Maagizo ya kuhusu utaratibu wa matumizi ya viwango vya ufaulu katika mitihani ya kidato cha nne na sita).

"Viwango vya ufaulu vilivyopendekezwa na Baraza la Mitihani la Tanzania vitumike kwa mitihani ya Kidato cha Nne 2012 na Kidato cha Sita kwa mwaka 2012 tu.

Ukisoma aya za kwanza, ndipo unakuja ku-conclude kwamba kumbe ni kweli maamuzi ya kubadilisha Grading System yalifanyika December wakati imeshafanywa na bila shaka hata kusahisha ilikuwa imeshamalizika! Hapa ndipo waheshimiwa wakakubaliana kutumika mfumo mpya!

Lakini aya iliyonishitua zaidi ni hii hapa:
"Viwango vya ufaulu vilivyopendekezwa na Baraza la Mitihani la Tanzania vitumike kwa mitihani ya Kidato cha Nne 2012 na Kidato cha Sita kwa mwaka 2012 tu. msisitizo kwenye UNDERLINED ITALIC BOLD! Kwanini iwe kwa mwaka 2012 tu? Ina maana walitaka kuujaribu mfumo waone itakuwa vipi wakishatumia mfumo husika?! Kama ndivyo, hii maana yake ni nini? Yaani unafanya intermediate surgical practices kwa mwanadamu?!

Kutokana na haya, ndipo ninapozidi kupata nguvu na hoja yangu kwamba jambo lililofanyika halikubaliki hata kidogo!!! Hata hivyo, nimeridhishwa na serikali kwa kugundua kwamba walikosea na kuamua kurudi nyuma....


 
NasDaz,

..nimesoma gazeti la mwananchi.

..Prof.Mchome, mwenyekiti wa tume ya kuchunguza matokeo, alikuwepo kwenye kikao cha wizarani kuzungumzia mfumo mpya wa madaraja!!
 
Last edited by a moderator:
Kikao cha kupitisha Viwango Vipya vya Ufaulu vilivyotumika kwa Kidato cha Nne kilihusisha Wizara ya Elimu na Ufundi,NECTA na TCU. Nyaraka za kikao hicho kilichofanyika Disemba mwaka jana,zinaonesha kuwa kikao husika kilikuwa chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dr.Shukuru Kawambwa na Katibu wa Kikao alikuwa Naibu wake Bwana Phillipo Mulugo.

Kwa upande wa NECTA,waliwasilishwa na Mwenyekiti wake Prof.Rwekaza Mukandala na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo,Dr.Joyce Ndalichako.Pia alikuwepo Mjumbe kutoka Mamlaka ya Vyuo Vikuu nchini-TCU ambaye alikuwa ni Prof. Sifuni Ernest Mchome (ambaye baadaye akawa Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Ufaulu wa Kidato cha Nne!)

Kikao hicho kiliidhinisha kutumika kwa viwango hivyo vipyakwa kidato cha nne na cha sita. Wajumbe wote wa Mkutano walikubaliana na viwango vipya na matumizi yake kwa kidato cha nne 2012.

Habari zaidi zimeripotiwa katika Mwananchi la leo

Je, kuchunguza na kutaka kubadili matokeo haya si dharau zilizopitiliza kwa watanzania? Je, ni halali kwa Prof.Mchome kuhudhuria kikao na halafu kuongoza Tume ya Kuchunguza? Watanzania tumedharauliwa,sasa tuchukue hatua gani? Nani mtanzania muungwana atawaamini watu hawa kwasasa?
Bro hoja ya ina mantiki kwa mambo mawili.
Kwanza waziri alishiriki kuleta fujo hii. Aliidhinisha mabadiriko MABAYA. Ndiyo maana tuliomba ajiudhuru.
Pili, Mchome kuchunguza alichoidhinisha kimsingi haikubakiki. Hapa wa kulaumiwa ni Wazuri mkuu Pinda. Hapa kweli alipinda.
HOJA YA MSINGI KABISA ni kuwa vigezo vya ufaulu vimerudi kama zamani kwenye D=21. Huu ndiyo usawa maana SOTE tulipimwa kwa kigezo hicho. Hongereni kuturushia vigezo vya zamani.
 
NasDaz,

..nimesoma gazeti la mwananchi.

..Prof.Mchome, mwenyekiti wa tume ya kuchunguza matokeo, alikuwepo kwenye kikao cha wizarani kuzungumzia mfumo mpya wa madaraja!!

Binafsi nilkuwa bado cjalisoma! Hilo suala la Mchome nalo nimejiuliza kidogo hususani maoni yake kwa Mwananchi yanayoonesha as if yeye hausiki! Hata hivyo, baada ya kutafakari kidogo, nikajiridhisha kwamba huenda Role ya Mjumbe wa TCU (kama Profesa Mchome) si role ya kimaamuzi bali inawezekana anaenda pale kama muangaliaji tu! Na hata ukiangalia panel, unaona kabisa kwamba huenda role ya TCU pale si kubwa sana kwani wakati Wizara na NECTA wametoka mjumbe zaidi ya mmoja; TCU ni Mchome peke yake!!

Katika hili, bila shaka kinachotokea ni kwamba, Key Player NECTA anaanzisha grading system in advance; anafanya evaluation zote za mfumo (let's call it SWOT analysis ya mfumo husika)! Wakisharidhika kwamba everything is OK, wanatoa pendekezo serikalini la kubadilisha mfumo! Hapo ndipo kunakuwa na kikao kati ya NECTA na Serikali ambapo bila shaka NECTA watakuwa wanaeleza strengths na weakness ya kile wanachopendekeza! Lakini kwavile TCU nao ni wadau, ndipo bila shaka wanapokuja kualikwa huku kila kitu kikiwa kimeshakuwa engineered na NECTA wenyewe....hawa ndio wenye mamlaka! Serikali kwa upande wake, ndie mwenye haki na wajibu wa kukataa au kuruhusu kwa marekebisho yoyote yanayopendekezwa na wataalamu wake kutoka NECTA lakini sizani kama TCU wana power hiyo!

So, wakati sina shaka hata kidogo na role ya NECTA na ile ya Wizara kuhusu suala hili, huku nikiwa sina uhakika wa role ya (mjumbe wa) TCU basi najikuta nakosa ubavu wa kumshutumu moja kwa moja Profesa Mchome hata kama nae alikuwapo kwenye panel.
 
Hapa ni kweli kabisa inaonyesha kama prof. Mchome aliitwa just for his information; na hata ukiangalia roles za tcu isingempa strength ya kutoa hoja za kulikataa wazo hilo, kwa sababu yeye hana mitaala wala hatungi hio mitihani, pengine necta waliweka hoja za kuanzisha utaratibu wa kutahini kwa maswali mepesi kiasi ya kwamba wahisi ni lazima kupandisha grade refer mitihani ya darasa la saba maswali kuchagua yote. Pia prof. Mchome yawezekana alitoa maoni hasi kwa misingi ya kutoshirikishwa mapema wadau wote ikiwa ni pamoja na mashule lakini hoja ikapingwa! Hali ambayo imepelekea sasa wamuone kama "jiwe lililokataliwa na waashi" na ndio maana tatizo la msingi ameliona mapema kabisa. But all in all makosa makubwa hapa ni maamuzi ya kubadili grade bila ya kuandaa wadau muhimu kabisa ambao ni walimu na wanafunzi wenyewe, tukumbuke kutokana na mfumo wetu wa elimu ambao tunalazimika kusoma masomo mengi hata ambayo hayatakuwa katika combination zetu, inabidi ujipange sana katika muda ili upate kusoma zaidi combination then yale ya zaidi unagonga kwa wastani wa kufaulu mathalani c hivi sasa hapa kama mtu anabadilishiwa grade wakati hajui maana yake alilosomea A anaweza kuangukia B au C sasa habari gani kwa yale aliyosomea C kama sio F.
 
Kufeli kwa wanafunzi hakutokani na grading system, bali ni kunaonyesha kuwa wanafunzi hawakuandaliwa vizuri. Tufikie wakati tuwe tunakubali makosa. Tunaposhindwa kukubali makosa basi tunakuwa tunaendelea kuyakubali na kuendela na njia hiyo hiyo mbovu.
 
NasDaz,

..nilivyoelewa mimi ni kwamba necta ilitoa mapendekezo. kikao kikaitishwa kujadili mapendekezo, Prof.Mchome na wengine walihudhuria kikao hicho. baadaye wizara ilitoa maagizo kimaandishi kwamba necta waendelee na zoezi la kubadili mfumo wa madaraja.

..pia kuna kitu nimejifunza kutokana na makala ya mwananchi, and i hope I am correct. Nilivyoelewa ni kwamba tofauti ya mfumo mpya na ule wa zamani ni kwamba huu mpya unatumia "fixed grading." Mfumo wa zamani nilivyoelewa mimi ni kwamba yale madaraja yalikuwa kama yana "float"; kwamba A,B,C, etc inaweza kubadilika kulingana na kufaulu/kufeli kwa wanafunzi.

..kuna mambo mengine pia kama ya ratio ya maendeleo ya darasani vs mtihani wa kitaifa ktk kuamua final grade ya mwanafunzi. mambo yote hayo yamebadilika ktk mfumo mpya. wananchi tunapaswa kuelezwa tofauti ya mifumo hiyo miwili kabla hatujaambiwa kwanini mmoja ni bora kuliko mwingine.

..naungana na Kichuguu kusema kwamba wanafunzi wetu hawajawiva sawasawa. mwanafunzi mzuri anaweza kufeli ikiwa tu mtihani utatungwa kutokana na SYLLABUS tofauti, not kutokana na kuwa graded ktk madaraja tofauti.

CC: fier, Nyani Ngabu, Mzalendo Mkuu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom