Matokeo Kidato cha sita: Lengo limetimia!

Matokeo Kidato cha sita: Lengo limetimia!

kwan jaman mnacholalamika nn? kwan div 4 nao mnawahesabu kwenda vyuo vikuu? kama sikosei vyuo vikuu mwisho div 3 ya point 15

Hata TCU pia wana BRN, kwa sasa Cut-off Point ni 2.5 ambao ni Full vilaza.
 
Nafikiri mabadiliko yaliyo fanywa hasa kwa A level si mabaya sana ukilinganisha na O level japo sikuona sababu ya kubadilisha Kwa A leve!

Lakini ninacho jiuliza utaratibu wa kuwapa mikopo utakuwaje? Na cut off ya vyuo itabadilishwa?
 
it makes sense kumbuken waliofanya mtihani wa acsee walifaulu csee kwahyo mnaoshangaa matokeo haya basi mna lenu binafsi.inawezekana mnachanganya politics na elimu.
 
Sijaona hata makosa hapo;
Nilitegemea big results kuliko hata hapo alipofikia binti yangu.

Ninaona shule zetu za kidumu na mfagio wamejitahidi sana;

HONGERA SANA WAALIMU WOTE WA "A" LEVEL KWA SHULE ZA SERIKALI.
Mamndenyi Hongera sana!
 
Last edited by a moderator:
Hakika yametimia ni usanii mtupu wanachezea viwango vya ufaulu ili kuwachanganya watu yaani kila siku mabadiliko lakini kweli lengo limetimia
 
Mijitu mingine sifuri kabisa unataka watu wafeli ndio uone elimu inapanda? Kama panya anafundishwa na anagraduate na degree yake itashindikana nini kwa binaadamu? wacha watu wasome uwatoke ujinga. Ni mzigo mkubwa kwa taifa ikiwa mchezo wa mama joyce ungeendelea. Asante serikali kwa kujenga vyuo vingi ili elimu iwe tunu ya taifa watanzania wote waipate.
 
Mijitu mingine sifuri kabisa unataka watu wafeli ndio uone elimu inapanda? Kama panya anafundishwa na anagraduate na degree yake itashindikana nini kwa binaadamu? wacha watu wasome uwatoke ujinga. Ni mzigo mkubwa kwa taifa ikiwa mchezo wa mama joyce ungeendelea. Asante serikali kwa kujenga vyuo vingi ili elimu iwe tunu ya taifa watanzania wote waipate.
Mkuu mama Joyce alikuwa na mchezo gani? Mie nilidhani kiwango kimepanda kwa sababu mwaka huu alama za madaraja yote kuanzia A mpaka D zimeshushwa sana na ndiyo maana hata idadi ya pointi za I hadi III zimebanwa sana maana kama I ingebaki pointi 3-9 basi waliopata I wangeweza kufika asilimia 50
 
Sijaona hata makosa hapo;
Nilitegemea big results kuliko hata hapo alipofikia binti yangu.

Ninaona shule zetu za kidumu na mfagio wamejitahidi sana;

HONGERA SANA WAALIMU WOTE WA "A" LEVEL KWA SHULE ZA SERIKALI.
Mamndenyi si jambo la kushangilia hata kidogo,mimi kama mwalimu inanisikitisha sana Elimu inavurugwa, kwa wenye ufahamu ndo wataweza kung'amua nini kinaendelea kwenye hii Elimu.Nenda vyuoni kajionee mwanachuo hajui kuandika essay ili mradi siku zinasonga huko vyuoni ni aibu huku ngazi ya chini ndio kilio, mitihani imevuja kuanzia kuanzia necta mwaka jana siye tunajionea mengi nyie endeleeni kushangilia uozo.
 
Last edited by a moderator:
Wahusika wa mitaala na mitihani ya kidato cha nne na sita,kuanzia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi hadi Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA),wanapaswa kujipongeza. Lengo limetimia. Katika matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa leo, asilimia zaidi ya 90 ya watahiniwa wamefaulu. Matokeo makubwa sasa!

Daraja la kwanza ingawa limepunguzwa kutoka 3-9 hadi 3-7 limesheheni;daraja la pili lipo la kutosha;daraja la tatu limejaa;la nne lina watu bwerere na sifuri zimepungua mno (si zaidi ya 650). Jipongezeni kwa matokeo haya kwakuwa mmetimiza lengo. Hongereni!

Furahini mkijua kuwa elimu yetu ndiyo inazidi kuvurugika. Kuanzia wanafunzi wenyewe,wazazi/walezi na washika dau wengine hawajui hata kukokotoa madaraja na hata alama. Hawajui kwanini daraja la kwanza limeishia alama 7 na si 9.Hawajui kwanini kuna A-D za General Studies. Hawajui kama kwenye daraja husika kama kumehesabiwa General Studies na BAM au la.Lakini,wanasheherekea matokeo.

Vyuo navyo vitawekwa njia panda. Itabidi uundwe utaratibu mpya wa 'cut-off points' ili kuendana na matokeo haya. Yote haya yanafanyika ili ionekane kuwa elimu yetu inapaa kwa kuwa na ufaulu wa juu: zaidi ya asilimia 90. Lengo kubwa ni kuonyesha umma wa watanzania na dunia kwa ujumla kuwa elimu yetu na watahiniwa wetu sasa ni moto wa kuotea mbali. Safari hii hamtapigiwa kelele wala kuundwa Kamati. Mmefaulisha vyema sasa.

Lakini,mambo ni tofauti. Wahusika mjipongeze huku mkijiuliza kama kweli mko sahihi kuichora elimu ya nchi hii hivi mnavyofanya.....
Jamani watanzania tumelogwa au mbona tunapenda kulalamika vitu bila kufahamuau kusoma... Acha upotoshaji kijana., mitandao ya kijamii isitumike kueneza uongo kiasi hiking jamani...necta wametoa miongozo VP uliisoma.. Na TCU pia ulisoma kijana..,necta kuna watu smart sana Dr msonde na Mr salum ni watu makini sana..wale hawawezi kiyumbishwa kisiasa.,
 
Hakika yametimia ni usanii mtupu wanachezea viwango vya ufaulu ili kuwachanganya watu yaani kila siku mabadiliko lakini kweli lengo limetimia
Wanafunzi wali pass mitihani necta exam ya form 4 kuanzia 3 C...so unategema hao watu watafeli.,
 
Wanafunzi wali pass mitihani necta exam ya form 4 kuanzia 3 C...so unategema hao watu watafeli.,
Mkuu nimekuelewa kuwa zamani hata waliokuwa wanapata F zote walikuwa wanaenda A-Level isipokuwa kwa kundi hili walianza kuchukua wale wenye ufaulu wa kuanzia C tatu ndiyo maana wamefanya wonders!!!
 
Jamani watanzania tumelogwa au mbona tunapenda kulalamika vitu bila kufahamuau kusoma... Acha upotoshaji kijana., mitandao ya kijamii isitumike kueneza uongo kiasi hiking jamani...necta wametoa miongozo VP uliisoma.. Na TCU pia ulisoma kijana..,necta kuna watu smart sana Dr msonde na Mr salum ni watu makini sana..wale hawawezi kiyumbishwa kisiasa.,

We unachekesha
 
Namkumbuka dada Joyce Ndalichako, sijui alienda wapi yule dada? Ana msimamo wa viwango kumzidi hata kaka Mukandala.

i hate tanzanian profesa wana njaa sana hawa watu wengi hawana msimamo mbele ya wanasiasa hata kama ni kuzalilisha taaluma zao kazi kusumbua watu na sup
 
hii ndo BRN kila eneo matokeo makubwa sasa. Hadi wakulima mikoa flani inayo lima pamba ,wakulima mbegu zao hazijaota mpaka sasa
.wameingia hasara mno na mbegu hizo zimetoka kwenye kwenye
kituo cha utafiti cha kilimo cha Ukiliguru......
BRN ipo on work now.
 
kuna watu humu wanabwabwaja tu vyuo mara wata disco ,mara hawapati kazi !watajiajiri nyie shida yenu nini kwani kuna mtu kaokotwa mtaani na kupewa matokeo acheni wivu wa kike.
 
Back
Top Bottom