Mateso na unyanyasaji wa wafanyakazi kiwanda cha Fujian Mkuranga (Kisemvule)

Hiki si ndio like kiwanda kilichofungwa kutokana na mazingira mabovu ya kufanyia kazi kilichosababisha vifo vya wafanyakazi wawili? Kilifunguliwaje tena kabla ya hayo mazingira kurekebishwa? Na hili la wafanyakazi kupigwa limekaaje? Huu ni utumwa kwa kigezo Cha uwekezaji
Naam, ndo hicho hicho mkuu,

Watu wanapitia magumu mule ndani,
 
Wasaidiwe na nani?

Asili ya "Ngozi Nyeusi" ni UBINAFSI.

Sio kwamba wahusika hawafahamu shida za wafanyakazi wa kitanzania kwenye viwanda kama hivyo, nakuhakikishia wanajua kwa asilimia 100 ila hawachukuliwi hatua yoyote sababu hawajali madhila yanayowakuta either sababu ni kwamba They don't care( haiwaongezei wala kuwapunguzia chochote) au ni kwamba wanapewa pesa kukaa kimya (Ubinafsi).

Huu ndio ukweli mchungu.
Ndo wanaotuumiza Sana, watu wanatakiwa kusaidia Ila wao wanaamua kuwa upande wa watesi yaani wachina
 
Hiki si ndio like kiwanda kilichofungwa kutokana na mazingira mabovu ya kufanyia kazi kilichosababisha vifo vya wafanyakazi wawili? Kilifunguliwaje tena kabla ya hayo mazingira kurekebishwa? Na hili la wafanyakazi kupigwa limekaaje? Huu ni utumwa kwa kigezo Cha uwekezaji
Kwani ambaye aliekuwa anaonekana mchawi sini Magufuli ambaye hayupo kwa sasa? Wacha nchi ifunguliwe ushenzi uendelee hichi ndicho ambacho CCM inakipenda ufisadi na ushetani na uonevu kwa wananchi huku kundi dogo likineemeka na bakshishi
 
Ttizo linakuja m2 anaona akiacha kazi atapat kazi kwengin wap lakin weng wanaumia sana kweny viwanda.
Watanzania kujitoa muhanga wanaonaga ni swala la watu flani tu wao haliwahusu na kwa unafiki unaweza ukajitoa muhanga ila shukurani zao itakuwa ni vijembe na kejeli tu na kuitwa kiherehere😅
 
Wasaidiwe na nani?

Asili ya "Ngozi Nyeusi" ni UBINAFSI.

Sio kwamba wahusika hawafahamu shida za wafanyakazi wa kitanzania kwenye viwanda kama hivyo, nakuhakikishia wanajua kwa asilimia 100 ila hawachukuliwi hatua yoyote sababu hawajali madhila yanayowakuta either sababu ni kwamba They don't care( haiwaongezei wala kuwapunguzia chochote) au ni kwamba wanapewa pesa kukaa kimya (Ubinafsi).

Huu ndio ukweli mchungu.
Mkuu ni ubinafsi mim ndo maana huwez niambia mambo ya uzalendo nikakuelewa
 
Ukitaka kujua Watanzania tuna ujinga mwingi nenda kwenye viwanda vya wachina na wahindi hivi visovyo na majina makubwa uone ni jinsi gani watanzania wanateswa na ujira kidogo.
 
Najiuliza, ni shida au kutojitambua ndio kinachopelekea haya !!??
 
Najiuliza, ni shida au kutojitambua ndio kinachopelekea haya !!??
Shida mzee kuna watu wamesota kutafuta ajira za kueleweka hawaoni mwanga wanaamua kujitosa huko.

Na pia ni kutojitambua kwa viongozi wa serekali.
 
Back
Top Bottom