Mateso na unyanyasaji wa wafanyakazi kiwanda cha Fujian Mkuranga (Kisemvule)

Apr 15, 2021
82
123
Amani na upendo kwenu nyote!

Kwanza nikiri wazi Mimi nimefanyakazi ktk kiwanda hiki katika vitengo mbalimbali jikoni, nondo na skrepa toka 2018 Hadi 2021 oktoba nikaacha kazi, jamaa na rafiki zangu wanaendelea kutaabika na kupata mateso mpaka sasa.

Katika kiwanda hiki Kuna MATESO NA UNYANYASAJI MKUBWA SANA KWA WAFANYAKAZI. Kiwanda hiki kinazalisha Nondo, kipo wilaya ya Mkuranga kata ya Vikindu ktk eneo la Kisemvule. Kiwanda hiki kinamilikiwa na Wachina.

Wafanyakazi karibu vitengo vyote wanateseka sana, wachina wanatesa Sana wafanyakazi!

Kupigwa wafanyakazi, kukatwa mshahara, kunyimwa stahiki zao wapato Ajali na kufukuza hovyo wafanyakazi.

Kuhusu kupiga wafanyakazi hii ni kero kubwa sana hasa ktk kitengo cha jikoni na kitengo cha mafundi umeme.

Malalamiko yashapelekwa labour zaidi ya mara tatu, wamekuja Mara moja tu, baada ya hapo Hali ikaendelea vilevile, kibaya zaidi wale Wachina wakazidisha ukatili na wanajisifu wanatoa tu pesa na hakuna cha kuwafanya.

Wapo waliokatika mikono, miguu, na majeraha mengine lkn hawajapewa haki yao.

Tunaomba serikali iingilie kati haraka haya mateso na manyanyaso wanayopitia Watanzania wenzetu.

Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya ndani, Waziri wa kazi, Waziri wa Uwekezaji na mbunge wa Mkuranga Mheshimiwa Ulega mtusaidie , watu wanakuwa watumwa kwenye nchi yao.

Mchina wa umeme na jikoni ndo vinara wakutesa na kupiga wafanyakazi.

Uwekezaji na wawekezaji tunawapenda lkn haya mateso tunaomba sana yafanyiwe kazi.
 
Mimi najiulizaga ivi kuna hajjagani ya kuwaitamkuu wa wilaya wa mkoa Kwa mahakama zina maana gani kwenye hii nchii
 
Dah,Kama ni kweli,huu ni ujinga na upuuzi kabisa Yani nchi yetu lakini bado tunahenyeshwa kama wageni...
 
Hiki si ndio like kiwanda kilichofungwa kutokana na mazingira mabovu ya kufanyia kazi kilichosababisha vifo vya wafanyakazi wawili? Kilifunguliwaje tena kabla ya hayo mazingira kurekebishwa? Na hili la wafanyakazi kupigwa limekaaje? Huu ni utumwa kwa kigezo Cha uwekezaji.
 
Nunua Saa zenye camera urekodi tukio mkipigwa kisha lirushe kwenye media kama ushahidi
 
Kuna wakati jitahidini mfanye kitu ili wawe na heshima kwa watanzania.....
Kabisa !!!
Hata hivyo mambo mengine yanatokana na Kuendekeza Njaa, Kutojitambua, Ubinafsi, Kuogopa the so called foreigners na Uoga wa maisha.
 
Poleni ila watanzania always ni waoga na wanasubiri wahanga wawasafishie njia,amka mtanzania hii nchi ni yako, fanyeni maandamano kudai haki zenu,upuuzi huu hapo SA hawa wachina wamenyooka, maana wale wazulu nao hawakawi kulianzisha.
 
Wasaidiwe na nani?

Asili ya "Ngozi Nyeusi" ni UBINAFSI.

Sio kwamba wahusika hawafahamu shida za wafanyakazi wa kitanzania kwenye viwanda kama hivyo, nakuhakikishia wanajua kwa asilimia 100 ila hawachukuliwi hatua yoyote sababu hawajali madhila yanayowakuta either sababu ni kwamba They don't care( haiwaongezei wala kuwapunguzia chochote) au ni kwamba wanapewa pesa kukaa kimya (Ubinafsi).

Huu ndio ukweli mchungu.
 
Back
Top Bottom