Matatizo ya Flat Screen TV: Umeishakumbana nayo?

Matatizo ya Flat Screen TV: Umeishakumbana nayo?

Ya kwangu Samsung led TV flat screen 48 inches iliweka mistari katikati ikawa haionyeshi picha ni sauti tu nimeiweka stoo tu nilirudisha dukani ilikua na guarantee walinizungusha Mara subiri tuitengeneze, Mara tumeagiza sijui mkanda Dubai, Mara leta 900 tuagize screen hii umepasua! Ndo maana wino unamwagika duh! Hadi nikaamua kuichukua na kuiweka store.
Mimi nina Samsung serie 5 inchi 40 ina miaka 3 ila kuna mistari imeanza kwa chini kulia, horizontally...sijajua ni nini ila inaonyesha vizuri hiyo michirizi kwa mbali inakera
 
Mimi nina Samsung serie 5 ina miaka 3 ila kuna mistari imeanza kwa chini kulia, horizontally...sijajua ni nini ila inaonyesha vizuri hiyo michirizi kwa mbali inakera
Nenda pale Posta Freedom Electronics jengo la Harbour view wana service center 0786 000 777
 
Mi nina Boss 40" na ina kingamuzi cha bure ndani, toka 2013 haijawahi nisumbua, saiv kuna tv zinaitwa STARX LED zina king'amuzi ndani, nzuri sana na ni affordable price kuna jamaa yangu
 
Acha uongo wewe. mimi nina chogo JVC toka mwaka 2001 mpaka leo haijawahi kuleta matatizo.
Mkuu c uongo chogo za sasa hivi nyingi ni feki tofauti na za zamani, hata hivyo sijasema zote zinasumbua kwa hiyo yengua kauli yako, pia michogo quality ya picha ni mbovu, jaribu kununua flat mkuu hilo li chogo lako utaligawa tu Kwan quality ya picha ni nzuri sana,
 
Mafundi mmeridhika mmekosa ubunifu tatizo la IC kutopatikana ni la electronics karibu zote original sio tv pekee. Hamfanyi jitihada za kuagiza toka kiwandani mnakimbilia kuweka mashine za kichina Hivi ikiharibika fridge au hi fi system mtapata wapi mashine ya kuweka?
Hata nje kwa taarifa ako wanabadili kad nzma, hii ni kutokana na complications za technology ya smd.
Yan vifaa vdogo mno hutumika ambapo unahtaj mitambo mikubwa ama robots kupachka components.Na hii Ndiyo sababu hasa ya kutoleta Spea zake na badala ake kad nzma(circuit)..
 
Kwa uelewa wangu. Hizi flat tv mpya zinakuja na dc adapters zake. Mara nyingi vyombo vyenye adapter ni vigumu kuungua. Kunapokuwa na shoti huungua adapter sa sio aC YA MASHINE. HII NINSAWA NA LAPTOPS. ZINAZOUNGUA NA ADAPTER MARA NYINGI NA SIO AC
Mara nyingi flat huungua mbele wala cyo power supply hasa zle unakuta standby inawaka.na kumbuka cyo flat. zote znatumika adapter,hata zenye sehemu zote unapewa mara nyng bla adapter.
 
Mimi nina Samsung serie 5 inchi 40 ina miaka 3 ila kuna mistari imeanza kwa chini kulia, horizontally...sijajua ni nini ila inaonyesha vizuri hiyo michirizi kwa mbali inakera
Hlo tatzo inapona cyo screen, wap upo?
 
Ukinunia la mtumbaa ndo yanaharibika mapema m nnnayo Samsung nmeeka store n ya mtumbaa
 
Ninayo sumsang niliitumia kama miaka 4 hivi. Baadae haikutumia kama miezi mitatu. Nilivyokuja kuiwasha ikawa haitoi picha vizuri kama ina ukungu ndani sijui tatizo ni nini.
 
Labda inategemea na brand ya TV, mimi ya kwangu nilinunua mwaka 2011 hadi leo haijawahi kuleta shida yoyote ukiiona kama mpya vile
 
Mm nilinunua Sony BRAVIA LCD, mwaka 2012. Kwa sasa imechora mstari katikati ambao unatenganisha picha baada ya kuiwasha kama dk 5 inabadilika rangi. Upande wa juu wa screen inakuwa na rangi ya kawaida na upande wa chini inakuwa rangi tofauti. Mfano, kama mtu amevaa gauni la rangi ya blue,upande wa juu ya screen utaonyesha blue na upande wa chini utaonesha rangi ya kijani. Nijqjaribu kupeleka kwa kundi wakaniambia tatizo ni IC inayo onesha picha ikipata moto ndio inasababosha hayo. Na hizo IC hamna hazipatikani.
 
Ukitaka kujua vitu gani vibovu au vinaharibika mara kwa mara hata kama ni gari tembelea kwa mafundi au garage utapata picha. Chogo zimejaa sana kwa mafundi kuliko flat. Flat nyingi ni original brand hata kama ni mchina. Chogo ziko sokoni mda mrefu hivyo zimeforgiwa sana hivyo nyingi ni mbovu. Nilikua na machogo mawili dah hadi nilikonda, kila week fundi anakula hela. Nikaamua kumzilia fundi sasa nina flat mwaka wa pili singsung mchina. Yuko poa sana. Mwisho vitu vya electronics vinaharibika haraka sababu ya current zetu za umeme wetu uko irregular. Hivyo ni muhimu kuwa na stabilizer
 
Sonny bravia 40" nilichukua 1.2 mlimani city 3yrs ago bado brand new
 
Back
Top Bottom