Matapeli wa miaka ya 90's walikuwa balaa sana

Matapeli wa miaka ya 90's walikuwa balaa sana

Hii ya watu kujifanya wasanii tumepigwa nayo sana hasa huku mikoani. Mi nakumbuka miaka michache iliyopita tumeenda kwenye show fulani sikumbuki ni msanii gani alikua anakuja kuperform. Sasa kuna wale ma underground hua wanatangulia mwanzoni, basi akapanda dogo mmoja akaimba wimbo wa "moyo wangu" ile kwaito ya diamond. Huo wimbo ulikua umetoka kama sio siku hiyo ni jana yake so watu wengi walikua hawaujui na kipindi icho kwaito ndio imekamata hatari. Unaambiwa dogo aliamsha bonge la shangwe ukumbini watu wakijua ni wimbo wake akaombwa urudiwe zaidi ya mara 2! Mashabiki acha tumiminike jukwaani kumtunza misimbazi [emoji1]. Baada ya siku mbilitatu ndio tunakuja kugundua kumbe tulipigwa.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji419][emoji1787]daaah
 
Ndio maana wanamuziki na wachezaji mpira wa zamani UKIMWI uliwatafuna sana maana pesa walikuwa hawana ila viburudisho nje nje[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ndio yalikuwa marupurupu yao....Hawa wachezaji wa siku hizi ndio wameshtuka; wao wanataka pesa kwanza.
 
Na-comment kuhusu mstari wa mwisho. Hata siku hizi watu bado wanaiba kirahisi mno. Bado kuna watu wanapigwa kirahisi mno na hata ukisimuliwa huwezi kuamini kama kuna watu wajinga kiasi hiki. Mtu anaweza kuambiwa wekeza sh milioni moja baada ya wiki zitazaa na kuwa sh milioni mbili na akakubali bila hata kutafakari. Utadhani ni bado tuko enzi za Abunuasi za sufuria kuzaa.
Me naona kwa saivi watu wengine wana tamaa ya mafanikio ya muda mfupi bila kutaka kuumiza kichwa ndio maana wanatapeliwa.
Shortcut zinawaponza wengi
 
Mimi bado najiuliza wale jamaa waliokua wanabadilisha karatasi kuwa pesa walikua wanatumia ujanja gani maana ni kweli pesa zilikua zinatokea baada ya karatasi kuwekewa dawa pia usisahau wale jamaa wa mkanda kuzungusha wametapeli sana raia
 
Kuna jamaa yangu anatoka Tanga likizo kipindi kile mabasi ya mikoani yanaanzia mnazi mmoja,alikuwa anakuja na begi la spear za magari kwao kulikuwa na magari mabovu kwa hiyo kufanya jambo ili aje tupige mpunga,kufika maeneo ya Kariakoo akakutana na wazee wa kanyaboya,likadondoshwa waleti mwana akaliokota jamaa mwizi akajifanya na ameliona waleti kama vipi wakagawane minoti,huku nyuma kuna jamaa analalamika kapotea waleti yake yenye mifeza kibao,jamaa yangu akaingia mazima,akaambiwa nipe begi nikushikie harafu tukutane maeneo flani tukafawane..jamaa akaachia begi akabaki na waleti yenye mikaratasi.
Nilisalimika pale Msimbazi maeneo ya Makao Makuu ya SSC. Wakati huo mabasi yanaingia alfajiri sana hapo Dar. Wakapita mbele yangu na kudondosha hilo furushi la fedha. Machale yakanicheza nikahamia upande wa pili wa barabara na kuona nini kinaendelea. Walipogundua nimestukia michezo wao, yule aliyetoka nyuma akaangalia kushoto na kulia na kuliokota like burungutu la mchongo na kutokomea nalo haraka. Nilibaki nacheka kimoyomoyo lakini ndo hivyo, walikuwa kazini!
 
Hii ya watu kujifanya wasanii tumepigwa nayo sana hasa huku mikoani. Mi nakumbuka miaka michache iliyopita tumeenda kwenye show fulani sikumbuki ni msanii gani alikua anakuja kuperform. Sasa kuna wale ma underground hua wanatangulia mwanzoni, basi akapanda dogo mmoja akaimba wimbo wa "moyo wangu" ile kwaito ya diamond. Huo wimbo ulikua umetoka kama sio siku hiyo ni jana yake so watu wengi walikua hawaujui na kipindi icho kwaito ndio imekamata hatari. Unaambiwa dogo aliamsha bonge la shangwe ukumbini watu wakijua ni wimbo wake akaombwa urudiwe zaidi ya mara 2! Mashabiki acha tumiminike jukwaani kumtunza misimbazi [emoji1]. Baada ya siku mbilitatu ndio tunakuja kugundua kumbe tulipigwa.

[emoji23][emoji23]
 
Neno "kanyaboya" lilitokana na bondia flani wa Burundi alikuja Tanzania kuzichapa alikuwa ba mikwara saana unaambiwa kabla ya pambano alikuwa anakimbia akiwa na gloves na mikwara kibao pale kariakoo.

Siku ya pambano yule bwana aitwae kanyaboya kilimkuta Kama bwana Mandonga.

Ndo watu wakaanza kusema kanyaboya kwa kitu Cha ubabaishaji au utapeli.

Kanyaboya
Hilo Kanyaboya nilishalivaa hapo Kariakoo Mtaa wa Kongo. Nilioneshwa Shati zuri Sana enzi hizo kutoka Uganda likiitwa la Juliana lina picha ya ndege. Tukakubaliana bei Ila huyo tapeli kanipeleka uchochoroni eti barabarani kuna njangu. Nikatoa pesa ndefu nikampa na yeye akasepa. Kwenda mbele nikafungua ule mzigo wangu. Nilistuka karibu nizimie kwa nilichokiona. Yaani niliuziwa vipande vya vitambaa ambavyo fundi cherehani huwa wamevikata!
 
Hii ya watu kujifanya wasanii tumepigwa nayo sana hasa huku mikoani. Mi nakumbuka miaka michache iliyopita tumeenda kwenye show fulani sikumbuki ni msanii gani alikua anakuja kuperform. Sasa kuna wale ma underground hua wanatangulia mwanzoni, basi akapanda dogo mmoja akaimba wimbo wa "moyo wangu" ile kwaito ya diamond. Huo wimbo ulikua umetoka kama sio siku hiyo ni jana yake so watu wengi walikua hawaujui na kipindi icho kwaito ndio imekamata hatari. Unaambiwa dogo aliamsha bonge la shangwe ukumbini watu wakijua ni wimbo wake akaombwa urudiwe zaidi ya mara 2! Mashabiki acha tumiminike jukwaani kumtunza misimbazi 😄. Baada ya siku mbilitatu ndio tunakuja kugundua kumbe tulipigwa.
Huko kwenu kulichelewa kukucha sana,huo wimbo wa moyo wangu au hata huyo Diamond si wa juzi tu hapa miaka ya 2010!
 
Kuna vitu vinafikirisha sana,hivi unawaza kufanya mapenzi na mtu ambaye unamsikia redioni tu

Hujawahi hata kumuona kwa sura duh

Mapenzi shikamoo!!!!!
Mkuu nenda kwenye uzi wa kula tunda kimasihara ndiyo utajua mapenz ni nyookoo
Daaah hatariiii Sana binadamu utashi umetuishia yaan tumekua kama bata kuku mbuzi kondooo yaan tunapandana ovyo ovyo no ustaarabu kabsaaa
 
Advance niko na mwanangu ye anasoma Sangu mi Meta, tulikuwa geto, kuna ticha mmoja wa hivi vi-Education center moja hivi mitaa ya karibu na Meta Sec achana na (Mbalepo ya Mbalizi Road).

Huyu ticha alikuwa anataka F-991 Calcukator, sasa tulikuwaga na "gaka" letu lipo kwenye box jipya na menu yake na "Og" mbili ambazo tulikuwa tunatumia. Tulivosikia mteja tukaenda na mwanangu asubuhi asubuhi, mwanangu kavaa kawaida mimi niko na Uniform, kufika pale Ticha akaitwa ,alikuwa anapiga pindi class hapo tuko na lile gaka kwenye box na menyu yake na Og kwenye box lake na menyu yake. Ticha alivokuja mwamba akaanza kumwambia tunauza caluculator, Akaomba aione mi nikampa Og(Ile feki mwamba ndo alikuwa nayo).

Jamaa kaiangalia pale akauliza bei, tukamwambia elf 30, akaomba atupe 25 tukamwambia hela haitoshi atupe elf 28, akawa anajivuta ,akasema ana 27, tukajifanya tunaondoka yeye akawa anarudi class, tulivofika getini ,mwanangu akanipasia gaka nikampa og, tukarudi fasta kabla hajaingia darasani tukamwambia tupe hiyo hiyo (27 elf) jamaa akatoa hela akachukua gaka tukatoweka haraka.

Haooo mpaka geto, nikatoa uniform tukaenda Kalobe kulewa ulanzi. Sikwenda shule kama siku 3, nikawa nawaza huenda Ticha alinikariri ataenda getini kwa kina Mng'ong'o kunivizia.
 
Advance niko na mwanangu ye anasoma Sangu mi Meta, tulikuwa geto, kuna ticha mmoja wa hivi vi-Education center moja hivi mitaa ya karibu na Meta Sec achana na (Mbalepo ya Mbalizi Road).

Huyu ticha alikuwa anataka F-991 Calcukator, sasa tulikuwaga na "gaka" letu lipo kwenye box jipya na menu yake na "Og" mbili ambazo tulikuwa tunatumia. Tulivosikia mteja tukaenda na mwanangu asubuhi asubuhi, mwanangu kavaa kawaida mimi niko na Uniform, kufika pale Ticha akaitwa ,alikuwa anapiga pindi class hapo tuko na lile gaka kwenye box na menyu yake na Og kwenye box lake na menyu yake. Ticha alivokuja mwamba akaanza kumwambia tunauza caluculator, Akaomba aione mi nikampa Og(Ile feki mwamba ndo alikuwa nayo).

Jamaa kaiangalia pale akauliza bei, tukamwambia elf 30, akaomba atupe 25 tukamwambia hela haitoshi atupe elf 28, akawa anajivuta ,akasema ana 27, tukajifanya tunaondoka yeye akawa anarudi class, tulivofika getini ,mwanangu akanipasia gaka nikampa og, tukarudi fasta kabla hajaingia darasani tukamwambia tupe hiyo hiyo (27 elf) jamaa akatoa hela akachukua gaka tukatoweka haraka.

Haooo mpaka geto, nikatoa uniform tukaenda Kalobe kulewa ulanzi. Sikwenda shule kama siku 3, nikawa nawaza huenda Ticha alinikariri ataenda getini kwa kina Mng'ong'o kunivizia.

Legend
 
Back
Top Bottom