Matapeli wa kisiasa waliopoteza chanzo cha mapato wanatafuta msaada kwenye tuta

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Tunajua fika CHADEMA na Act wazalendo ni vyama ambavyo kwa ushahidi wa wazi kabisa ambao hauna chembe kuwa ni vyama vya wasaka matonge. Wao kuweka pesa mfukoni ndio lilikuwa jambo la kwanza kuliko maslahi ya Tanzania na raia wake.

Tulishuhudia Zitto Kabwe akizurula Ulaya na Usa na kunadi kuwa hakuna demokrasia nchini,na hata haki ya watoto wa kike kusoma wakiwa na mimba inaminywa,akaandika barua tunyimwe mkopo. Hakuwa na muda wa kutumikia wananchi wa Kigoma, muda wote alikuwa anazurula nje ya nchi kusaka ufadhili wa mabeberu ili ajinufaishe kwa madai ya kutetea demokrasia kama vile Tanzania hakuna Demokrasia.

Chadema wao ndio wananchi walisha wachoka na siasa zao za kishamba za harakati zisizo na mashiko, kudai maandamano, kuvamia magereza, kupinga maendeleo ya wananchi huku nao wanayafaidi, wananchi waliwachoka hata kabla ya kupiga kura. Na kwenye boksi la kura wamepata wanacho stahili.

Act wazalendo na Chadema walizoea kupata ruzuku na michango ya wananchi bure kabisa, sasa kimoja kimekufa mende style hakuna ruzuku ya mil 360, hakuna michango ya wabunge zaidi ya mil 100 kwa mwezi.

Kilichobaki wanasaka msaada kwenye tuta, Eu iinyime misaada Tanzania ili wao wafurahi! Watanufaika nini? Tril 2 ambazo ni msaada wa EU kwa Tanzania mimi naona ni kitu kidogo sana kwa nchi ambayo inakusanya tril 1.5 kwa mwezi, achana na mapato mengine.

Watanzania tunajua siasa ni mtaji wenu, mlikuwa mnakula kwa kupitia vyama vyenu sasa wananchi wamewakataa, kuomba dua mbaya kwa Tanzania ni kupoteza muda.
 
Kimsingi umeandika upumbafu tu..ulitaka wayasemee wapi haya yanayoendelea nchini..ilihali taasisi zote nchini ziko hoi taabani kusimamia haki.

Kama kweli tuko vzr hatutaki misaada yao tokeni wazi mbele muwaambie usoni kua hatutaki waache tutajiendesha wenyewe.

Kwanza hiyo 1.5tr kwa mwezi tunayokusanya kumbuka mishahara tu ni zaidi ya 900b kwa mwezi hiyo ilo baki ndo itatakayo ivusha nchi..?achiliambali matumizi mengine ya serikali na taasisi zake..

Ebu kua na akili ya kufikiri hata kidogo ufiche aibu yako ya jinsi ulivyo mjinga.

Kimsingi tuna hitaji sana mosaada yao..na pia tunahitaji kujitegemea ambalo ndilo suala la msingi..ila tatizo approach yetu iko hasi.

Kumbuka ukitaka kula lazima uliwe kidogo..unataka kula bila kuliwa haiwezekani.

La mwisho ila sio kwa ulazima toeni majibu ya hela zao za korona zilitumikaje?..au warusishieni tu mana sisi ni dona kantre.

#MaendeleoHayanaChama
 
Wewe ndio huna akili kwani serikali ina chanzo kimoja cha mapato? Mishahara ni kama bil 600, deni la nje linalipwa na mambo yanasonga. Ila kumbuka serikali ina vyanzo vingi vya mapato,usikariri makusanyo ya TRA pekee.

Kuhusu misaada yao jana wamepewa majibu hata wewe kibaraka wao ulisikia.
Majibu gani..?we uliona majibu pale au makasiriko na macho kutumbuliwa..kwanza kumbuka tangu nchi ipate uhuru hii serikali ndio iliyokopa zaidi na inaendelea kukopa..?na hili deni litalipwa na watanzania ambao ni mimi na wewe.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Kama EU wanataka hiyo 27m Euro yao ya Corona warudishiwe tu, hela za masimango hazina faida. Waendelee na mishe zao watuache na nchi yetu. Misaada ya EU ni kwenye 100m Euro kwa mwaka ( 600m kwa miaka 6 ), makampuni yao makubwa yapewe nchini hasa hasa kwenye mining wapigwe tu unfair tax invoice pesa hiyo ije kwetu kwa njia nyingine.
 
Nashauri ARV nazo zisitolewe bure ili tuzinunue ghali kama yalivyo madawa ya Cancer!
Mbinyo uwe mkali mpaka kila mwananchi ausikie umegonga mfupa!Pengine tutakumbuka kutenda haki!

ARV sio mpango wa amsterdam.
 
Trillion 2 ambazo nchi inapata kama msaada toka EU Mimi naona ni kidogo sana kwa nchi inayokusanya 1.5 t kwa mwezi....
Haya ni maoni ya mtu Zuzu fala, mbumbumbu wa uchumi anayejua hesabu ya kujumlisha pekee.
 
Trillion 2 ambazo nchi inapata kama msaada toka EU Mimi naona ni kidogo sana kwa nchi inayokusanya 1.5 t kwa mwezi....
Haya ni maoni ya mtu Zuzu fala, mbumbumbu wa uchumi anayejua hesabu ya kujumlisha pekee.
Kwa mwezi unakusanya 1.5tr?????
Tangia lini?
 
Nashauri ARV nazo zisitolewe bure ili tuzinunue ghali kama yalivyo madawa ya Cancer!
Mbinyo uwe mkali mpaka kila mwananchi ausikie umegonga mfupa!Pengine tutakumbuka kutenda haki!
Una uhakika ni wangapi wanatumia ARV? Je, unayegombana naye hata kama anatumia hawezi kuzinunua? Acha utoto na mawazo mfilisi
 
Back
Top Bottom