JK leo tumekusikia ukijitetea kuwa watu wameanza kuzusha mitandaoni eti wewe ulikuwa unamchukia JPM na pengine ukawa mmoja wa maadui zake wakati wa utawala wake. Majibu yako yalikuwa mepesi mno kama kawaida yako "Mswahili" nanukuu "Eti kama kweli ningekuwa namchukia JPM nisingeweza kupitisha jina lake katika mchakato wa kuwania Urais 2015 kwani mimi (kama Rais na Mwenyekiti wa chama) ndiye niliyepeleka majina matano (5) Halmashauri" na ukaenda mbele zaidi ukasema katika kuchagua majina matano jina la kwanza lilikuwa la JPM alafu yakafuatia mengine manne. Umeenda mbele zaidi na kusema kuwa alikuwa jembe lako katika baraza lako la mawaziri huku ukijikanganya zaidi na kusema mlipokuwa mnatifuana JPM alikimbilia kupeleka mashtaka kwa kaka yako mkubwa ambaye ni marehemu sasa.
Maswali magumu:
(i) Je, kwani wewe ndiye uliyependekeza hayo majina matano au ni CC ya chama chako ndiyo iliketi na kukuletea wewe kwa ajili ya kuyawakilisha Halmashauri? Labda tusaidie kwani hayo majina ulitoka nayo nyumbani kwako kwa kushauriana na familia yako?
(ii) Je, si kweli JPM aliingizwa katika tano bora baada ya kuona "mamvi" hawezi kuaminika katika chama na wananchi wanataka mchapakazi asiyekuwa na doa ili kukikomboa chama kilichokuwa kinaelekea kuanguka na sio kwa mapenzi yako binafsi?
(iii) Hivi mashtaka aliyokuwa anapelekea JPM kwa kaka yako mara kwa mara yalihusu nini kama kweli alikuwa jembe lako katika baraza lako?
(iv) Mwisho japo sio kwa umuhimu. Unajuaje pengine watu wanasema chuki zako dhidi ya JPM zimeanza kuonekana zaidi baada ya yeye kuwa tayari ni "Mkuu" kwa maana ya kuwa hukuwa na jinsi tena ya kubatilisha maamuzi yako?
Maswali magumu:
(i) Je, kwani wewe ndiye uliyependekeza hayo majina matano au ni CC ya chama chako ndiyo iliketi na kukuletea wewe kwa ajili ya kuyawakilisha Halmashauri? Labda tusaidie kwani hayo majina ulitoka nayo nyumbani kwako kwa kushauriana na familia yako?
(ii) Je, si kweli JPM aliingizwa katika tano bora baada ya kuona "mamvi" hawezi kuaminika katika chama na wananchi wanataka mchapakazi asiyekuwa na doa ili kukikomboa chama kilichokuwa kinaelekea kuanguka na sio kwa mapenzi yako binafsi?
(iii) Hivi mashtaka aliyokuwa anapelekea JPM kwa kaka yako mara kwa mara yalihusu nini kama kweli alikuwa jembe lako katika baraza lako?
(iv) Mwisho japo sio kwa umuhimu. Unajuaje pengine watu wanasema chuki zako dhidi ya JPM zimeanza kuonekana zaidi baada ya yeye kuwa tayari ni "Mkuu" kwa maana ya kuwa hukuwa na jinsi tena ya kubatilisha maamuzi yako?