Mi huwa najua wanaokataa uwepo wa mungu huwa ni critical thinker kumbe mambo yenyewe ndo hivi basi ngoja twende sawa.
unaelewa unachokisema? deni linatokana na miradi mikubwa..
SI lazima hio hivyo selikali inapokumbwa na upunguzu kwenye recurrent expenditure na inaweza ikalazimika kukopa, na Deni ambalo linatokana kuekezwa kwenye mradi hill ni zuri kwa sababu linatengeneza economic activities ambazo itazalisha kiasi kingine cha hela.
miradi hiyo inahitaji hela, hela hizo inabidi tukope kwa sababu tu haturuhusiwi kuwa na mashine ya kutengenezea hela.. kwanini?
Unachokiandika hukijui kabisa, miladi ndio inahitaji pesa ila kuna mambo unapaswa uelewe hakuna nchi ambayo inazuiwa kutengeneza pesa hata wewe unaweza kuomba tenda serikalini ila tu kuna vitu lazima uzingatiwe hasa usalama wa hiyo pesa isiweze kukopiwa na kuingiza pesa isiyo halali kwenye mzunguko, kwenye uchumi pesa ni nothing kinachoangaliwa ni shughuli za uchumi ambazo nchi inaweza kuzalisha kwamba kwa kutumia hizo shughuri za kiuchumi ambazo nchi inazo inaweza kukusanya kiasi gani cha hela kufika lengo sasa hapo ndo uchumi wa nchi unapokuwa mdogo inabidi mkope pesa ama misada toka kwenye nchi zenye uchumi mkubwa. Hela unaweza ukatengeneza mengi Sana lakini kama uzalishaji na shughuli zingine za uchumi ni mdogo hazina maana mfano Zimbabwe walikuwa na mpaka na noti dola trillion moja lakini hiyo pesa unanunua mkate tu na nchi haijiwezi.
haijulikani.. mwisho wa siku wanatuletea theories za demand and supply... upuuzi mtupu
Tunakupa chance ya kuthibitisha theory ya demand and supply ni upuuzi mtupu ikizingatiwa nyie huwa mnapenda uthibitisho. Naomba uthibitishe hili dai lako.
huu ni unyonyaji wao wanakaa na hizo mashine kama nani?
Hata wewe unaweza kuwa na hizo na ukaomba tenda ya kutengeneza pesa benki kuu ila unakidhi vigezo? Pia elewa kinachozingatiwa kwenye uchumi ni shughuli za kiuchumi ambazo zitatoa picha ya GDP ya nchi na sio idadi ya pesa.
wao hayo mabilioni ya misaada wanayotugawia wanatoa wapi kama sio hizo hela wanazoprint watakavyo?
Wana uchumi mkubwa ndicho kinachowafanya wawe na uwezo was kutoa hayo mabilioni
1. USA USD trillion 17 gdp
2. China USD trillion 11 gdp
3. Japan USD trillion 4 gdp
Kwanini washindwe kukupa msaada kama nchi yako ni maskini.
nani amewapa mamlaka ya kukaa na hiyo mashine? wao kama nani? kwanini na sisi tusiwe nazo?? UKIRITIMBA HUU.
Hata wewe unaweza kuwa na hizo machine na ukaomba tenda ya kutengeneza pesa benki kuu ila unakidhi vigezo? Una teknolojia ya maana ya kupunguza ama kuzuia uharamia wa pesa feki?Pia elewa kinachozingatiwa kwenye uchumi ni shughuli za kiuchumi ambazo zitatoa picha ya GDP ya nchi na sio idadi ya pesa.