Maswali 16 ya Mchungaji

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Ni katika kuitafuta haki, kuondoa fitina, majungu au habari zisizo na mshiko na za kusadikikasadikika.

1. Ufisadi wa Richmond ukoje? Je tunaupembua kama rushwa, kukiukwa sheria & taratibu za uzabuni au ni matumizi Mabaya ya mamlaka & madaraka?
2. Kama Richmond ni Rushwa, ilitolewa namna gani, kwa nani na kwa nini mpaka leo hakuna ushahidi kamili ili suala lifuate mkondo kisheria[DN1] ?
3. Kama Richmond ulikuwa ni wizi, ni fedha gani ziliibiwa? Ni nani aliiziba au khidhinisha wizi? Ni nini hasa kilichoibiwa?
4. Kama Richmond ulikuwa ni Mkataba hewa, mkopo uliotolewa na CRDB umerudishwa? Mitambo iliyoletwa na mkataba kwanini vilihanishiwa Dowans?
5. Kama Richmond ni ukiukwaji wa kanuni, kuvunja sheria, kutumia madaraka vibaya, vipi wahusika hawajapelekwa mahakamani kama Mramba ?
6. Kama kwenye Richmomd, kamati ya bunge ilisema PCCB walifanya udhaifu na ujanjaujanja kufunika kweli, kwa nini Hosea bado yu madarakani?
7. Kama mkataba wa Richmond ulikuwa na walakini, hata kukiukwa na Richmond, kwanini uliuzwa kwa Dowans kisha Symbion badala ya kufutwa?
8. Kama Serikali kupitia CRDB waliweza kuikopesha Richmond, walete turbines, kwanini hatukuipa Tanesco huo mkopo wanunue mtambo uwe wao?
9. Je ni hasara ya kiasi gani iliingia Taifa kwa ujumla kwa Richmond kushindwa kuwa makini na imara kuzalisha umeme Kama ilivyotakikana?
10. Kama Richmond walishindwa na kuchelewa kuanza uzalishaji kwa mujibu wa mkataba, kwanini mkataba huu haukusitishwa mara moja?

11. Baada ya kashfa ya Richmond, ripoti ya Mwakyembe, kujiuzulu Lowassa, Serikali (PCCB, DPP, AG) walifanya nini kuendeleza uchunguzi?
12. Kwenye hili la Richmond, kwanini limeendelea kuwa jambo la utata na minong'ono ya tuhuma za ufisadi mpaka sasa? Rais kwanini yu kimya?
13. Kama CCM kweli ilitaka kuondokana na zimwi la Richmond, ufisadi wake na hata Lowassa, kwanini hadi leo tope na doa hili halijaondolewa?
14. Haki na ukweli lazima vifahamike na ukiri wa udhaifu na aibu uIshike CCM. Hatiwezi kuwa waadilifu na wawajibikaji tusipotatua Richmond!
15. Ili tuendele, kashfa, tuhuma na tetesi za IPTL, RAdar, Meremeta, Richmond, Loliondo nk, lazima zitatuliwe, sheria na haki zifanye kazi !
16. Tanzania Mpya, yenye matumaini na mabadiliko ni ndoto tuu, kama jinamizi la ufisadi na hizo kashfa zitazikwa bila ukweli kufahamika!
 
..hata Dr.Mwakyembe aliwahi kusema kwamba kuna mambo tume yake iliamua kuyafunika ili serikali isiaibike.

..Mimi Nina wasiwasi Ccm itampitisha Lowassa, na Mwakyembe will come up with an explanation kumtetea Lowassa.
 
Mkuu Kishoka

Maswali yako hayana jibu la moja kwa moja. Wataalamu wameelezea rushwa katika makundi tofauti.

Mfano ipo rushwa ndogo(petty corruption) inayohusisha hongo ndogo ndogo.
Hii ndiyo tunaona watu wakifikishwa mahakamani au wakiwajibishwa

Ipo Grand crorrption, kiwango cha juu cha rushwa katika serikali ikitumia mifumo yote ya kisiasa, kisheria na kiuchumi

Na pia ipo systemic corruption ambayo inakuwepo tu kama kitu cha kudumu kutokana na udhaifu wa mifumo.
Kwamba rushwa inakuwa sehemu ya taratibu za maisha ya kila siku.


Kwa upana wake, inatosha kusema rushwa ipo katika maeneo yote, iwe ufujaji(emblezzlement), wizi, udanganyifu au ushawishi na si lazima iwepesa tu

Msingi mkubwa unaotengeneza rushwa ni madaraka makubwa(discretionary power)

Lakini pia tukumbuke rushwa si lazima iwe haramu, kuna rushwa halali (legal corruption) zinazotumika kutengeneza rushwa katika mfumo mzuri kabisa na wa kisheria.

Kwa mfano, mkataba mbovu si lazima uwe haramu.Unakuwa ni halali ukiwa umeandikwa kwa njia halali , kupitia taratibu halali nakupatikana kwa uhalali ukiwa umetengenezwa kwa njia haramu.


Itakapotokea kuuvunja mkataba huo bila kufuata taratibu halali tayari ni tendo haramu.
Kwamba aliyeandika ameweka mazingira yatakayombana anayedhulumiwa.

Na hapa ndipo tunaona wanasiasa (kama mawaziri) wakitumia taaluma zao( kama wanasheria) katika kujipatia mafao binafasi ya kiuchumi(personal gain)


Suala la Richmond lipo katika hali hii.

Ni syndicate,iliyotumia systemic corruption kutengeneza grand corruption iliyofanya legal corruption kwa kutumia discretionary power


Pengine tunaweza kujibu hoja zako kwa kujaribu kutumia maelezo haya mafupi.
 
Ni katika kuitafuta haki, kuondoa fitina, majungu au habari zisizo na mshiko na za kusadikikasadikika.

8. Kama Serikali kupitia CRDB waliweza kuikopesha Richmond, walete turbines, kwanini hatukuipa Tanesco huo mkopo wanunue mtambo uwe wao?

Yaani hicho kipengele cha nane ni balaa kabisa, Mwekezaji anaingia nchini hana kitu, "watu" wanamsimamia mwekezaji aweze kukopeshwa kiasi kikubwa cha pesa na banki za ndani ili awekeze

kwa kweli Tanzania naona tuko mbio mno kumnyanganya Nigeria sifa zake kuu za uhujumu uchumi, wizi, ufisadi nk
 
Yaani hicho kipengele cha nane ni balaa kabisa, Mwekezaji anaingia nchini hana kitu, "watu" wanamsimamia mwekezaji aweze kukopeshwa kiasi kikubwa cha pesa na banki za ndani ili awekeze

kwa kweli Tanzania naona tuko mbio mno kumnyanganya Nigeria sifa zake kuu za uhujumu uchumi, wizi, ufisadi nk


Kama CRDB waliweza kuikopesha Richmond U.S. $30 million, iweje washindwe kuikopa Tanesco kununua Turbine za uhakika kutoka GE, Siemenes na wengine mabingwa wa Turbines (gesi, maji, jua, hewa)?

Utapeli wa IPTL ulitufanya wengine tujifunze kwa kina mambo ya mitambo ya umeme na procurement zake, na ndio maana kamwe sitaelewa ni kwa nini tuliamua kutoa zabuni kwa watu watuzalishie umeme, tuwalipe marudufu, kisha tununue kutoka kwao mitambo chakavu!

It doesn't make any single ounce of sense!
 
..hata Dr.Mwakyembe aliwahi kusema kwamba kuna mambo tume yake iliamua kuyafunika ili serikali isiaibike.

..Mimi Nina wasiwasi Ccm itampitisha Lowassa, na Mwakyembe will come up with an explanation kumtetea Lowassa.

Kitendo cha Mwakyembe na kamati yake kufanya cover-up, na cha Sitta kukataza kuichunguza Dowans, ni vigezo tosha kuonyesha utata wa hali ya juu na kukosekana kwa uwajibikaji, ufuataji wa kanuni na sheria, kuvunjwa kwa haki na bottom line ni kulea ugonjwa wa Satarani kwa kumwambia mgonjwa upasuaji au kuchoma miale/mionzi kutaharibu ngozi hivyo mgonjwa anywe panadol na maji ya madafu!

JInamizi la magamba na ufisadi lililelewa na kina Mwakyembe walipoionea haya Serikali na kulifanya Bunge linunulike kirahisi kisa kuiepusha Serikali aibu!

Tungelitilia maanani jambo hili na si ushabiki wa kuitana mafisadi na kumkomalia Lowassa pekee, kuanguka kwa Serikali ya Kikwete kungekuwa ndio chachu ya kuleta mabadiliko ya msingi.

Mapinduzi si lazima yawe ya nguvu, mabavu au utovu wa nidhamu, CCM na JK wangeweza kuanguka kwa kukupigiwa kura ya kutokuwa na imani na ushahidi upo mkubwa sana kuwa wajibu huo na dhamana hiyo ilifukiwa kinyemela.

Sishangai Msabaha kusema ya UBangusilo! Kafara ikatolewa, Lowassa akabwagwa, leo kaamka ndani ya Tanuru la kondoo wa sadaka na kila mtu pale Dodoma anatafuta pa kujificha .

Heri kina Yona na Mramba wamebambikwa mvua ya kuchakachua kura, watatoka kwa rufaa na kufanyiwa fidia!
 
Rev. Kishoka,

..umesema kweli kabisa hapo juu.

..leo nimesikia Mzee Butiku analalamika kuhusu siasa za wana mtandao zilizoanza wakati wa uchaguzi mkuu wa 95.

..lakini ktk kauli zake hizo unaona kabisa kwamba anataka kushughulikia wanamtandao wote, isipokuwa JK.

..wengine kama Humphrey Polepole wanadai kwamba hawawezi kuhama CCM kwasababu wanaamini ktk misingi iliyoanzisha chama hicho. lakini imeshadhihirika kwamba chama hiki kimebadilika 100%. Wanamtandao ndiyo wameshika hatamu, na hawaheshimu tena misingi iliyokianzisha chama hicho.

..anayeamini ktk misingi iliyoanzisha CCM ni bora akaanzisha chama kipya kitakachofuata misingi hiyo. kwasababu hii CCM ya wanamtandao ni tofauti kabisa kabisa na CCM ile ya Mwalimu Nyerere, Rashidi Kawawa, Edward Sokoine, Daudi Mwakawago, na wenzao.

..kuna tatizo la watu waadilifu ktk nchi yetu kuwa ktk state of denial wakiamini kwamba CCM inaweza kurudi ktk misingi yake. wengine nadhani ni uoga tu unawasumbua.

..SAMAHANI KWA KUTOKA NJE YA MADA.

cc Humphrey Polepole, ZeMarcopolo, Nguruvi3, Mag3, Mkandara
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JokaKuu wanamtandao walipoteka chama,kwanza walikuwa kuvunjanguvu za wazee.

Hoja ya kuwaondoa katika vikao vya maamuzi (NEC na CC)ikakubaliwa.


Wazee wakawa nje, wanamtandao wakipanga yao. Tunakumbuka, Mangula alifanyiwa nini kule Iringa.

Wazee wakatoa benefit of doubt' mbele ya safari huenda mamboyakawa sawia.

Nguvu ya CCM ya akina Mwl, Moringe, Kawawa n.k. ilijengwakatika ukweli na uzalendo.
Waliambazina bila haya kwasababu walikuwa watumishiwa umma.


Hawakuruhusu wafanyabiashara, na utakumbuka wakati huohakukuwa na mfanyabiashara anayeingia chama kutumia mapesa yake.

Ni kweli watu walikuwa katika denial, kwa bahati mbayawanaona matokeo ikiwa ''too little too late'
Wanateseka na mizimu waliofugamiaka mingi


Kama CCM itakufa sidhani historia itamwacha JK. Ameruhusu wanamtandao ambao hadi leo tunasikia wanampeleka mbio.

Saahani tuechepuka katika mada
 
Nguruvi3,

..Lowassa na JK ndiyo waasisi wa mtandao.

..kuna jitihada za kujaribu kumtenganisha JK na mtandao.

..wanaofanya hivyo ama wanaficha ukweli, au wako kwenye denial.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kishoka

Tukirejea katika mada

1 Zilikuwepo fununua za mchezo Mchafu wa Richmond. Serikali ikakabidhi kazi PCCB.
Bunge halikuridhia likaunda kamati ndogo ya Shelukindo.
Kamati ikabaini kuna tatizo, ndipo ikaundwa ya bunge ya Mwakyembe


2. Waziri mkuu wakati huo akasimama bungeni na kusema taarifa ya PCCB ilikuwa sahihi.
Hapa akiwa kiongozi wa serikali aliridhika na kila ushahidi ulioletwa na vyombo vya umma kama PCCB n.k.


3 Ikabainika kuwa PCCB iliandika taarifa ya uongo. Haijakanushwa hadi leo

4 Kampuni ya Richmond haikuwepo, hadi leo hakuna anayesema ilikuwepo au kuonyesha wapi iliokuwa na makao. Serikali ilitoa fedha za manunuzi kwa kampuni isyokuwepo. Hapo ni wizi au udanganyifu

5 Baraza la mawaziri likavunjwa, waziri mkuu akajiuzulu.
Hili lilimaanisha kulikuwa na tatizo. Bila uwepo wa tatizo serikali ingesimama kidete kutetea kutokuwepo uhalifu


6 Serikali kulipa Richmond isyokuwepo badala ya Tanesco ndio wizi wenyewe

7 Mwakyembe akaomba taarifa ijadiliwe tena bungeni. Serikali ikakataa. Kwanini

8 Taarifa za wahusika zikatakiwa ziletwe bungeni. Spika na serikali wakafunika kombe

Richmond ni deal , wanaosema ni uzushi wanapaswa kutuonyesha utafiti, uchunguzi au njia nyingine waliofikia kusema ni uzushi. Wanaotuhumiwa hawatuelezi ni kwanini wanasingiziwa, na ukweli ni upi

Hadi leo hakuna independent investigation kuosha Richmond na wahusika. Tunaambiwa tu ilikuwa uzushi

Kwanini serikali ilikataa suala hilo lisijadiliwe zaidi?


 
rev. Kishoka,

..umesema kweli kabisa hapo juu.

..leo nimesikia mzee butiku analalamika kuhusu siasa za wana mtandao zilizoanza wakati wa uchaguzi mkuu wa 95.

..lakini ktk kauli zake hizo unaona kabisa kwamba anataka kushughulikia wanamtandao wote, isipokuwa jk.

..wengine kama humphrey polepole wanadai kwamba hawawezi kuhama ccm kwasababu wanaamini ktk misingi iliyoanzisha chama hicho. Lakini imeshadhihirika kwamba chama hiki kimebadilika 100%. Wanamtandao ndiyo wameshika hatamu, na hawaheshimu tena misingi iliyokianzisha chama hicho.

..anayeamini ktk misingi iliyoanzisha ccm ni bora akaanzisha chama kipya kitakachofuata misingi hiyo. Kwasababu hii ccm ya wanamtandao ni tofauti kabisa kabisa na ccm ile ya mwalimu nyerere, rashidi kawawa, edward sokoine, daudi mwakawago, na wenzao.

..kuna tatizo la watu waadilifu ktk nchi yetu kuwa ktk state of denial wakiamini kwamba ccm inaweza kurudi ktk misingi yake. Wengine nadhani ni uoga tu unawasumbua.

..samahani kwa kutoka nje ya mada.

Cc humphrey polepole, zemarcopolo, nguruvi3, mag3, mkandara
maslahi binafsi kwanza....
 
Mkuu Kishoka

4 Kampuni ya Richmond haikuwepo, hadi leo hakuna anayesema ilikuwepo au kuonyesha wapi iliokuwa na makao. Serikali ilitoa fedha za manunuzi kwa kampuni isyokuwepo. Hapo ni wizi au udanganyifu

6 Serikali kulipa Richmond isyokuwepo badala ya Tanesco ndio wizi wenyewe



Nguruvi3, Kampuni ya Richmond ipo, imesajiliwa kama kampuni ya uchapishaji/stationary (Masumin, Kiuta) na iko Houston Texas na Mwakyembe alikuja kutembea na kuiona. Tatizo ni kuwa kampuni hii, haikuwa na si kampuni ya kuzalisha umeme. Ilijitengenezea mazingira ya kilaghai kuwa inaweza kuzalisha umeme na kuleta mitambo ya kuzalisha umeme. Ubalozi wetu pale Washington DC, inasemekana uliafiki kuwa kampuni hii ni safi na inastahili (hizi ni tetesi, sina uhakika kama kweli Balozi Daraja au wafanyakazi wa Ubalozi waliafiki kuwa Richmond inafaa na ingepewa zabuni hiyo.
 
Back
Top Bottom