Masogange na Melisa kuachiwa huru!!!!!!

Masogange na Melisa kuachiwa huru!!!!!!

Nchaby

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2013
Posts
797
Reaction score
259
Wana Jf habari ni kuwa wale vinara waliokamatwa na mzigo mkubwa wa sembe huko SA wenye thamani ya 6.8 bilion sasa wataachiwa huru kwani imeonekana kuwa mzigo huo haukuwa ni madawa ya kulevya bali ephedrine ambazo haziko kwenye kundi la dawa za kulevya

Habari zinasema ephedrine ambayo inasemekana ndiyo waliyoisafirisha akina dada hao inaangukia ktk kundi la vibashirifu yaani dawa ambazo malighafi yake inaweza kutumika kutengeneza dawa za kulevya.

Hivyo basi kesi yao haina nguvu tena na wanatarajiwa kupewa dhamana wakati wowote kutoka sasa.
Source:Gazeti la Raia Mwema Sep.18, 2013

Huu ni mweleka wa hali ya juu sana aliopigwa Dr.Mwakyembe!!
Hakika imeniacha na maswali mengi pasipo
majibu!!!

Ikumbukwe kabla ya taarifa hizo mkuu wa kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya Alfred Nzowa alienda SA kwa kile alichodai kwenda kuangalia kama watanzania hao wanatendewa haki ktk kesi yao!!!
Mimi nikajiuliza hivi wako watanzania wangapi wanaotuhumiwa na sembe China, Hong Kong na kwingineko, kwa nini huyu mkuu aende SA tu?????

Ni Nzowa huyo huyo baada ya kutoka SA alisema kuwa watuhumiwa wamewataja watu waliowatuma mzigo huo na ni mnyororo mrefu sana. Hivyo ataufanyia kazi. Ina maana watuhumiwa walitaja majina ya wauza apples!!!!

Lakini taarifa za nyuma zilisema kuwa watuhumiwa waliingizwa katika chumba cha mateso baada ya kutoonyesha ushirikiano kwa polisi SA wa kutaja wahusika wa mzigo. Lakini baada ya kuingizwa ndani ya chumba hicho walisema kila kitu!!!!!
Najiuliza, inamaana watuhumiwa waliteswa kabla ya kuthibitisha kwa uhakika mzigo walioubeba ndani kulikuwa na nini?

Hakika vita ya kupambana na madawa ya kulevya ni ngumu mno. Wampambanaji ndio wanaomiliki,wanaoratibu,wanaosafirisha,wanaosimamia na kuendesha biashara hiyo ya sembe.

Ni lini Tanzania italivalia njuga kwa dhati tatizo la dawa za kulevya????

========================
UPDATE
========================

View attachment 112868
WATANZANIA wawili Agness Gerard ‘Masogange' na Melissa Edward wameachiwa huru na Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg baada ya kutakiwa kulipa faini ya Sh 4.8 milioni (Randi 30,000) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumiwa kutengeneza dawa za kulevya.
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai cha Afrika Kusini (hawk) Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya bali kemikali aina ya ephedrine.
Hata hivyo mahakama ilibaini kuwa Melissa hana hatia kwa kuwa ilionekana amemsindikiza Masogange, aliyemuomba amsaidie kubeba mzigo huo.
Mosagange alilipa faini ya Shilingi 2.5 milioni (R15, 000), huku akiahidi kumaliza nusu yake ambayo juhudi zilikuwa zinafanyika amalize kulipa jana Ijumaa.
"Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa tu kusaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini haikuwa mizigo yake. Mizigo yote iliandikwa jina la Agness Masogange na si Melissa," alisema Kapteni Ramaloko.
Kapteni Ramaloko alisema, Melissa alijitetea kuwa hakuwa amesafiri na Masogange bali walikutana ndani ya ndege na Masogange alimuomba amsaidie mizigo hiyo kwani ilikuwa mikubwa.
Kwa sheria za Afrika Kusini kubeba kemikali zozote ambazo zimepigwa marufuku ni kosa la jinai kisheria hivyo mahakama iliamuru Masogange ahukumiwe kwenda jela miezi 30 (miaka miwili na miezi sita) au alipe faini ya R30, 000(Sh 4.8 milioni).
Hata hivyo alilipa faini na nusu ya fedha hizo ilishalipwa na nyingine ilikuwa inakaribia kulipwa.
Ingawa Kamishana Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa alipoulizwa juzi Alhamisi alisema mzigo walioubeba Masogange na mwenzake haukuwa ni dawa za kulevya bali ni kemikali za dawa za kulevya, lakini Msemaji wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini, (SARS) Marika Muller, alieleza kuwa timu ya SARS ina uhakika kuwa mabegi sita yaliyokamatwa Julai 5, mwaka huu ni methamphetamine.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Mfululizo wa kukamatwa, kesi, hukumu na kuachiwa huru kwa Agnes Masogange kwenye kesi ya Madawa ya kulevya
Masogange ajisalimisha mwenyewe Mahakama a Kisutu
Kupandishwa kizimbani na kusomewa shitaka
Yaliyojili wakati wa kesi ya Masogange
Masogange kupelekwa kwa Mkemia Mkuu
Kesi kusikilizwa
Tetesi za kuachiwa huru
Hukumu
 
Aisee......nafikiri hata hiyo ephedrine wamekosea, haukuwa unga wa ngano kweli ila vipimo vyao vikapima vibaya?


Hii vita kweli mwisho wake ni kwenye tanuru la giza.....
 
Kama sio madawa yakulevya kwa nini waliyapitisha kwa siri? Na yule mwenzao kwa nini altoroka? Huu udhaifu ni wa SA sio Tz. Mapapa wa SA wana Nguvu sana!!
 
Niliposikia tu kuwa polisi wa Tz wanaelekea huko SA kwenda kufanya nn sijui, nikajua jamaa wanataka ku-lidoctor sakata hili kwa maslahi ya watu wakubwa,na hakuna cha maana kitakachofanyika ktk kesi hii. Kwann waliingilia mapema na kwa haraka hivyo.
 
baada ya kusoma hii thread, nimechoka kabisa.... ngoja 2subiri wawe huru kabisa.
 
nilijua lazima watatoka. kuna mtu aliwai kuniambia wanatoaga pesa. harafu unga unabadilishwa kuua ushaidi.
na uyo kamanda alivyoenda south nikajua kaenda kuweka mambo sawa.
mbona akwenda hongkong.brazil.etc
 
Tuliambiwa issue za bwimbwi ziko juu kabisa pale
 
mhhh mimi nilisha patwa na mashaka nilipo soma taarifa ya nzowa ya kusema kuwa kaenda kuhakikisha kuwa watanzania wanapewa haki?
mara sijui madawa ya kutengenezea dawa za kifua ??
ila hapo mimi bado na swali kidogo kutokana na maelezo aliyo eleza nzowa nikuwa usafirishaji wa ephedrine ambazo hutumika kutengenezea dawa ya kifua inabidi uwe na kibari maalum kutoka serikalini.
swali la kujiuliza inamaana hao mabinti walisafirisha hayo madawa bila kuwa na kibali hicho cha serikali??

na kama ndio hivyo kwanini kulikuwa na sinto faham uwanja wa ndege mpaka kufikia hatua ya mwakyembe kulivalia njuga ? au ndio kusema kama habari ilivyo andikwa hapa jamvini kuwa kikwete aliruka faster na kwenda SA aliwapelekea hicho kibali cha kusafirisha hayo madawa??
au nzowa ndio alikwenda kule ??

wakina kaniki na matumla nao pia wamekamatwa mbona hatuja sikia kuwa raisi au nzowa au serikali haijatuma wachunguzi na wataalam waende kuwahoji nao pia ??
au kuna baadhi tu ya mkondo wa wahusika??
mbona mnatuchanganya sana juu ya hii makitu??

harafu kwa nini raisi amekuwa akijihusisha sana na haya mambo ama amekuwa akitajwa tajwa sana na kwa nini jina lake na sembe havikai mbali?
mara sijui mwanae alikamatwa faster akawasha ndege tena kwa garama za pesa ya wa tanzania mbio china ?mara sijui kagaramikia matibabu ya ray c huku tena mara kakutana na wabwia unga ikulu leo tena south kwa masogange??

hakika IKULU si salama tena
 
Hivi hili jina la dawa ephedrine ndio lilitumika tangu mwanzo au ni generic na trade names???!!
 
Good news well come home Masogange wivu tu kila mtu na bahati yake south africa karibu sana ndio mana askari wa tz wamekwenda huko brazil ethiopia ni mbali I can't wait to see u
 
Sasa ngoja na mimi nikaombe hiyo ajira pale chini, sifa nisaidieni, wanaojua sifa za kupiga hii kazi! kumbe ni ephedrine???
 
Nimeiona hiyo stori kwenye Raia Mwema na gazeti moja la udaku(silikumbuki)kwenye meza za magazeti,lakin kwa hili linalojadiliwa hapa,wauza unga wamepiga bao muhimu sana kwenye game muhimu mno na ndo bao la pekee na la kihistoria,ila pia naweza kusema sasa (kisirisiri) biashara ya unga imehalalishwa Afrika,acha wazungu wapambane tu,Nzowa pale ofisini (kwa mujibu wa kauli zake)ni kama taasisi yake ya kujichumia mapesa,nadhan hayo makaratas ya Orodha ya wauza unga yamemzunguka ofisini na hata pakukaa hana,,,,,
ameshindwa kupambana na biashara ya dawa za kulevya si tu kwa mizigo isyokamatwa hata inayokamatwa,pamoja na kwamba anadai ana orodha ya wauza unga manguli,inaonesha hana nia na washirika wake kuwafanyia uchunguz hao jamaa na kuwakamata,leo hii wanakuja na wimbo wa mahakama ya wauza unga,they r buying time,wasituhadae,sheri hii iliyopo inaweza tu kusaidia kupambana na wauza unga na watu wa aina hiyo,vilevile matukio yanayofanywa na KIRANJA MKUU nayo yanahalalisha hii biashara jamani,kumtibu ray-C na kukaa kimya bila kutia neno ni sawa na kukubaliana na hii bizness,kukutana na mateja na kuongea nao bila kutoa wito kwao na wauza unga pia ni kama amekubali,watanzania hatutak list ya wauza unga,watanzania tunataka ukomeshaj wa hii biashara kwa kuwakamata na kuwapoteza wauza unga,,,wakubwa,wadogo mpaka hawa wauza kete,jaman polisi wanawafahamu hawa,huwez uza unga au gongo bila kujulikana na polisi,,,,kuna utaratibu(sio rasimi)wa kupeleka pesa kwa mapolisi,sasa kwa Tanzania na nchi nyingi za afrika hakuna mpango madhubuti wa kupambana na wauza unga,na kwa sasa wanafanya makusudi kuwakomoa wale wanaojifanya wanapambana na hii bizness(akina mwakyembe),kwanza rais haonesh kukerwa kabisaaa
 
wakifika bongo tutajua zaidi, je wakipata dhamana wakarudi, nani atakuwa analipia gharama za kesi ( freight to and fro SA) au maboss wao?
hapo ni zaidi ya tujuavyo
SP
 
Back
Top Bottom