SI KWELI Masanja Mkandamizaji: Mama Samia malizia Code kwa Gwajima

SI KWELI Masanja Mkandamizaji: Mama Samia malizia Code kwa Gwajima

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kwa Sasa Kuna Chapisho Linalo Sambaa Kwenye Mtandao wa Kijamii Ususani Facebook Ikionesha Ukurasa wa Massanja Mkandamizaji ukitoa Pongezi Kwa Samia suluhu Hassan kumuweza Polepole.
Je Taarifa Hiyo ina Usahihi Kiasi Gani.
Sikweli Masanja Code.jpg
 
Tunachokijua
Kupitia mitandao ya kijamii kumekuwa na 'screenshot' ikiwa na jina la msanii/mchekeshaji na mchungaji, Masanja Mkandamizaji akimueleza Mama Samia kuwa amemuweza Polepole na sasa amebaki Askofu Gwajima tu na atampa Code za namna ya kumpata.

Uhalisia wa madai hayo

Ufuatiliaji wa JamiiCheck umejiridhisha kuwa Taarifa hiyo si ya kweli.

Utafutaji kwa kutumia maneno muhimu umejiridhisha kuwa ujumbe huo haujachapishwa na Masanja Mkandamizaji kupitia ukurasa wake wa X kama inavyoonekana kwenye 'screenshot' inayoonekana.

Aidha 'screenshot' hiyo ya kughushi haiendani na muonekano wa sasa wa kurasa za mtandao wa X, mathalani rejelea 'profile picture' imekaa katika pembe nne wakati muonekano wa sasa ni wa duara.

Hata hivyo 'handle' anayotumia Masanja ni @ mkandamizaji na si @mkandamizaj_masanja kama inavyoonekana kwenye screenshot.
Kwa Sasa Kuna Chapisho Linalo Sambaa Kwenye Mtandao wa Kijamii Ususani Facebook Ikionesha Ukurasa wa Massanja Mkandamizaji ukitoa Pongezi Kwa Samia suluhu Hassan kumuweza Polepole.
Je Taarifa Hiyo ina Usahihi Kiasi Gani.
View attachment 3487833
Hapa masanja kaongea pwenti japo naye ni wale wale wauzao roho za watu kwa kisingizio cha neno na roho mtakatifu wakati wana roho mchafu wa uroho na mtakakitu.
 
Back
Top Bottom