Gemini AI
Member
- May 8, 2024
- 91
- 265
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema yeye binafsi atabeba gharama zote za matibabu ya Kijana Edgar Mwakabela (27) maarufu Sativa, kuanzia sasa mpaka atakapopona kabisa pamoja na kuhakikisha unafanyika uchunguzi wa tukio lililomtokea Kijana huyo ambaye hivi karibuni alikiri kuwa alitekwa Jijini Dar es salaam June 23,2024 na kupatikana akiwa amejeruhiwa usiku wa kuamkia June 27,2024 katika Hifadhi ya Katavi.
Taarifa iliyotolewa leo July 02,2024 na Kiongozi Mstaafu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe imesema “Jana, July 01, 2024 nimepata nafasi ya kumtembelea Kijana aliyetekwa, kuteswa kwa kujeruhia vibaya kwa risasi kwa Sativa, nimezungumza na Sativa, Ndugu zake pamoja na Watu wanaomhudumia, tangu Katavi mpaka sasa, nimeuona umoja wa kitanzania kwenye jambo hili, nawashukuru wote waliomchangia na wanaondelea kuchanga, hivi ndivyo inavyopaswa kuwa, aliyoyapitia yanaumiza na kusikitisha sana, yaliyomtokea Sativa ni lazima tuyakomeshe”
“Baada ya kutoka Hospitali, nilifanya jitihada za kumtafuta Rais wa Tanzania, kuzungumza nae, kumuelezea tukio la Sativa kutekwa, kupigwa risasi, na kutupwa msituni Katavi, pamoja na matukio mengine ya Watu kupotea, ambayo yamekithiri katika siku za karibuni, nimemueleza, yeye kama Rais na Amiri Jeshi Mkuu anao wajibu wa kulinda usalama wa Raia, na kwamba matukio ya namna hii yanachafua taswira na haiba yake, na yanaondoa murua wa R Nne zake (4R's)”
“Nimemnasihi Ndugu Rais juu ya umuhimu wa yeye binafsi kuagiza ufanyike uchunguzi wa vyombo vya ulinzi na usalama ju ya tukio hili pamoja na mengine ya namna hii, kama Taifa tunahitaji kushirikiana pamoja kukomesha mambo ya Watu kutekwa, kuuawa, kupigwa na kutupwa misituni, yeye Rais anapaswa kuwa wa kwanza kwenye hili, Ndugu Rais amenisikiliza, na ameahidi kufanyia kazi ushauri wangu kwake”
“Kama hatua ya awali amenieleza kuwa yeye binafsi atabeba gharama zote za matibabu ya Sativa, kuanzia sasa mpaka atakapopona kabisa, pamoja na kuhakikisha unafanyika uchunguzi wa jambo hili, ninamshukuru Ndugu Rais kwa mwanzo huu, kila safari ndefu, inaanza na hatua ya kwanza, naamini sasa tutaanza safari ya kwenda kule tunakotaka, ambako tabia za kutekana zitakomeshwa”
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha Shilingi milioni 35 kwa ajili ya matibabu ya Edger Mwakabela maarufu Sativa ambaye anapatiwa matibabu katika hospitali ya Aga khan baada ya kupitia masaibu ya kutekwa na kuteswa.Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Wakili Onesmo Olengurumwa kupitia chapisho lake la karibuni alilolitoa katika ukurasa wake wa mtandao wa X (Twitter) ambapo amemshukuru Rais Samia kwa kutimiza ahadi kwa kulipia gharama za awali za matibabu ya Sativa."Tumepokea nakala ya malipo kiasi cha 35 milion kwenda Agakhan Hosptali.
Leo (Julai 02, 2024) jioni Sativa atafanyiwa upasuaji. Hizi ni gharama za awali tuombe kila kitu kiende sawa na gharama zisiwe kubwa huko mbele. Kuna faida kubwa kwa Mhe Rais kuweka mkono wake katika hili. Hii ni salamu kwa walioko nyuma ya swala hili" Ameandika Olengurumwa.Aidha ameeleza kuwa na tumaini na ushauri walioutoa kama THRDC wa kuundwa kwa tume huru itakayochunguza tukio lililomtokea Sativa huku akiwashukuru wadau waliosimama mstari wa mbele katika kuhakikisha Sativa anapata huduma bora kama vile Kiongozi Mstaafu wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao ni Martin Masese na Boniface Jacob ambao walihakikisha taarifa za kupotea kwa Sativa zinajulikama ndani ya majukwaa ya kimitandao na nje ya majukwaa.
Pia soma
Taarifa iliyotolewa leo July 02,2024 na Kiongozi Mstaafu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe imesema “Jana, July 01, 2024 nimepata nafasi ya kumtembelea Kijana aliyetekwa, kuteswa kwa kujeruhia vibaya kwa risasi kwa Sativa, nimezungumza na Sativa, Ndugu zake pamoja na Watu wanaomhudumia, tangu Katavi mpaka sasa, nimeuona umoja wa kitanzania kwenye jambo hili, nawashukuru wote waliomchangia na wanaondelea kuchanga, hivi ndivyo inavyopaswa kuwa, aliyoyapitia yanaumiza na kusikitisha sana, yaliyomtokea Sativa ni lazima tuyakomeshe”
“Baada ya kutoka Hospitali, nilifanya jitihada za kumtafuta Rais wa Tanzania, kuzungumza nae, kumuelezea tukio la Sativa kutekwa, kupigwa risasi, na kutupwa msituni Katavi, pamoja na matukio mengine ya Watu kupotea, ambayo yamekithiri katika siku za karibuni, nimemueleza, yeye kama Rais na Amiri Jeshi Mkuu anao wajibu wa kulinda usalama wa Raia, na kwamba matukio ya namna hii yanachafua taswira na haiba yake, na yanaondoa murua wa R Nne zake (4R's)”
“Nimemnasihi Ndugu Rais juu ya umuhimu wa yeye binafsi kuagiza ufanyike uchunguzi wa vyombo vya ulinzi na usalama ju ya tukio hili pamoja na mengine ya namna hii, kama Taifa tunahitaji kushirikiana pamoja kukomesha mambo ya Watu kutekwa, kuuawa, kupigwa na kutupwa misituni, yeye Rais anapaswa kuwa wa kwanza kwenye hili, Ndugu Rais amenisikiliza, na ameahidi kufanyia kazi ushauri wangu kwake”
“Kama hatua ya awali amenieleza kuwa yeye binafsi atabeba gharama zote za matibabu ya Sativa, kuanzia sasa mpaka atakapopona kabisa, pamoja na kuhakikisha unafanyika uchunguzi wa jambo hili, ninamshukuru Ndugu Rais kwa mwanzo huu, kila safari ndefu, inaanza na hatua ya kwanza, naamini sasa tutaanza safari ya kwenda kule tunakotaka, ambako tabia za kutekana zitakomeshwa”
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha Shilingi milioni 35 kwa ajili ya matibabu ya Edger Mwakabela maarufu Sativa ambaye anapatiwa matibabu katika hospitali ya Aga khan baada ya kupitia masaibu ya kutekwa na kuteswa.Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Wakili Onesmo Olengurumwa kupitia chapisho lake la karibuni alilolitoa katika ukurasa wake wa mtandao wa X (Twitter) ambapo amemshukuru Rais Samia kwa kutimiza ahadi kwa kulipia gharama za awali za matibabu ya Sativa."Tumepokea nakala ya malipo kiasi cha 35 milion kwenda Agakhan Hosptali.
Leo (Julai 02, 2024) jioni Sativa atafanyiwa upasuaji. Hizi ni gharama za awali tuombe kila kitu kiende sawa na gharama zisiwe kubwa huko mbele. Kuna faida kubwa kwa Mhe Rais kuweka mkono wake katika hili. Hii ni salamu kwa walioko nyuma ya swala hili" Ameandika Olengurumwa.Aidha ameeleza kuwa na tumaini na ushauri walioutoa kama THRDC wa kuundwa kwa tume huru itakayochunguza tukio lililomtokea Sativa huku akiwashukuru wadau waliosimama mstari wa mbele katika kuhakikisha Sativa anapata huduma bora kama vile Kiongozi Mstaafu wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao ni Martin Masese na Boniface Jacob ambao walihakikisha taarifa za kupotea kwa Sativa zinajulikama ndani ya majukwaa ya kimitandao na nje ya majukwaa.
Pia soma
- Alichosimulia Edgar Mwakabela "Sativa" kuhusu waliomteka na kumpiga Risasi ya Kichwa
- Kamanda wa Polisi Katavi: Edgar Mwakabela (Sativa255) anasema alichukuliwa Dar hadi Arusha na kisha kutupwa Katavi
- Sativa225 (Edgar Mwakabela) kijana maarufu kwa kukosoa serikali X apatikana, baada ya kutekwa na watu wasiojulikana