Hapo kuna mambo mawili yaliobakia, either serikali yetu itutoe kafara raia million zaidi ya 50 (tushughulikiwe nchi nzima) au atolewe kafara mmoja aliezua hili balaa lote (DAB).
Viongozi wetu nchi hii wana matatizo, sisi raia sio kwamba tunaunga mkono ushoga, hapana, tunauchukia ushoga toka moyoni kutokana na imani na maadili yetu. ila huyu DAB alijisahau sana akawa anaji MWAMBAFY kupita kiasi. Ameonea watu wengi sana.
Kuna wapo aliowapa kashfa za kuuza madawa ya kulevya kwenye TV waliharibiwa biashara zao/kazi/maisha/heshima na wengine walifunga biashara zao zote nchini (Hakuna hata mmoja aliethibitishwa mbele ya mahakama wala kufungwa jela kwa kashfa hio - Ishu hii ilikua na nini nyuma ya pazia?).
Kufungia na kuwaonea wafanya biashara wa sehemu za starehe, kiongozi wa serikali badala ahamasishe biashara ili mzunguko wa hela uwepo na ajira, anapangia watu "MUDA" wa kuanza biashara (kama vile anawasaidia kulipa kodi au ana share katika hizo biashara). Amefungia matumizi na biashara ya "SHISHA" kitu ambacho dunia nzima inaruhusu, na ni kitu kilichokua na ajira/mzunguko wa hela mkubwa sana katika sehemu za starehe na hoteli za kitalii (Kwa kigezo cha kijinga eti wanatumia kuvutia madawa ya kulevya - Mbona hajazuia matumizi na kuuzwa kwa "RIZLA" au "SIGARA" kwenye maduka na supermarket??? Rizla na Sigara tunatumia kusokotea na kuchanganya skadi kupunguza ukali. . . . . Leo watalii wanakuja nchini kwaajili ya mapumziko wanakutana na masharti ya muda wa kuanza starehe???? Unawalipia gharama za kuja nchini kwenye mapumziko mpaka uwapangie muda wa kufanya starehe???
Sakata la wanaume kutelekeza watoto, lilianza kwa siku mbili tu na kisha kufa, na asilimia kubwa lilitumika kuchafua watu na si kusaidia watu.
Kutoa kejeli kwa wananchi wa Dar Es Salaam, asiokua na ajira wala elimu atarudi kijijini. Kupitisha msako nyumba hadi nyumba kupima tezi dume (Aliwaza budget/gharama za kufanya hili? Hela ingetoka hazina au bungeni?)
#Watu walimkumbusha kuna maisha baada ya uongozi, sasa yamefika, ajionee huku mtaani watu walivyoweka beef nae.