Masaa 24 yameshapita

Masaa 24 yameshapita

Tangu marekani itoe taarifa yao yameshakatika masaa zaidi ya 24 bila kusikia kikohozi wala chafya ya kiongozi yeyote wa kiserikali akiongelea jambo lolote lile. Kwa kifupi mpaka muda huu hakuna aliyeonekana akijaribu hata ile kujifanya anajikuna.

Nchi ni kama imepigwa ganzi, ndugu watanzania wenzetu wamekufa huko Moshi kwenye ajali ya Mafuta hatujasikia kauli ya viongozi hadi hivi sasa zaidi ya Kamanda Hamduni na mkuu wa Wilaya Moshi.

Je, tuamini serikali imejichimbia ikifanya rehersal ya kuja na majibu? Au Our Numero Uno amestushwa na taarifa hizo kufahamika na dunia au alikua hazifahamu na sasa yupo kupata briefing!!

Vipi viongozi ambao hata hawasikiki wakiendelea kuyaongelea maeneo yao kama tulivyozoeshwa?
Kwani hao siyo viongozi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kuna mambo mawili yaliobakia, either serikali yetu itutoe kafara raia million zaidi ya 50 au atolewe kafara mmoja aliezua hili balaa lote.
Walala hoi amabo mnaona kwenda marekani ni dili ndio imekula kwenu. Hakuna cha serikali kutoka tamko wala nini hebu rudini vijijini tulime mvua zinanyesa

God save us
 
Tangu marekani itoe taarifa yao yameshakatika masaa zaidi ya 24 bila kusikia kikohozi wala chafya ya kiongozi yeyote wa kiserikali akiongelea jambo lolote lile. Kwa kifupi mpaka muda huu hakuna aliyeonekana akijaribu hata ile kujifanya anajikuna.

Nchi ni kama imepigwa ganzi, ndugu watanzania wenzetu wamekufa huko Moshi kwenye ajali ya Mafuta hatujasikia kauli ya viongozi hadi hivi sasa zaidi ya Kamanda Hamduni na mkuu wa Wilaya Moshi.

Je, tuamini serikali imejichimbia ikifanya rehersal ya kuja na majibu? Au Our Numero Uno amestushwa na taarifa hizo kufahamika na dunia au alikua hazifahamu na sasa yupo kupata briefing!!

Vipi viongozi ambao hata hawasikiki wakiendelea kuyaongelea maeneo yao kama tulivyozoeshwa?
Kumekuwepo na taarifa ya Mzee Mkapa kwenda kumwona Jiwe pale Ikulu.

Kama ni kweli, nahisi lazima kuna taarifa hao "Mabeberu" wamempenyezea amfikisie Jiwe kabla hawajafanya wanalo kusudia. Kumpiga STOP Makonda si sawa na kufanya hivyo kwa Waziri wa Foreign Affairs!

Wanayofanyiwa wapinzani hapa ndani huwezi kuwafnayia watu wa nchi nyingine na Tanzania si kisiwa. Kama mataifa ya Ulaya Magharibu wanaufyata kwa Marekani, sembuse Tanzania!

Na tusije tukajidanganya kwamba hawajui yote wafanyayo viongozi wetu. Wanajua fika nani aliwatuma waliokusudia kumuua Tundu Lissu.
 
CCM ya sasa hivi!
Screenshot_20200128-075300-picsay.jpeg
 
Tangu marekani itoe taarifa yao yameshakatika masaa zaidi ya 24 bila kusikia kikohozi wala chafya ya kiongozi yeyote wa kiserikali akiongelea jambo lolote lile. Kwa kifupi mpaka muda huu hakuna aliyeonekana akijaribu hata ile kujifanya anajikuna.

Nchi ni kama imepigwa ganzi, ndugu watanzania wenzetu wamekufa huko Moshi kwenye ajali ya Mafuta hatujasikia kauli ya viongozi hadi hivi sasa zaidi ya Kamanda Hamduni na mkuu wa Wilaya Moshi.

Je, tuamini serikali imejichimbia ikifanya rehersal ya kuja na majibu? Au Our Numero Uno amestushwa na taarifa hizo kufahamika na dunia au alikua hazifahamu na sasa yupo kupata briefing!!

Vipi viongozi ambao hata hawasikiki wakiendelea kuyaongelea maeneo yao kama tulivyozoeshwa?

Ana apisha wateule......hajaongea? uswahilini wanasema wapenda Mic wanzikimbia siku hizi
 
USA akisema ana ushahidi wa kutosha ujue hatari. Nadhani Serikali walikuwa relax hakuna uchunguzi wa nje kumbe jamaa kimya kimya. Na kawaida USA hapo ubalozini majasusi kibao na utakuta hata huku watumishi wa serikali kuna informers. Utajibu nini lazima ukae kimyaa labda umalize chinichini kuwa tufanyeje? solution watatoa USA wenyewe.
Mbona hata kwa Saddam Hussein wa Iraq walisema kua wana ushahidi kua Saddam ana silaha za WMD? Je walizikuta hizo silaha mpaka leo? Wameua watu na hakuna kilichopatikana mpaka leo hii!
 
Usiombe
Ukiwa maskini
Mwaka wa uchaguzi
Ushindi wako ... bao la mkono

Halafu kiranja mkuu ndie anakuambia
Unaua
Unatesa
Unazulmu haki za mijadala
Lazima kutengeneza tume huru ya uchaguzi

Kwa kweli kizunguzungu, kiebrania, kitakuzunguuka kichwani mpaka upoteze mwelekeo...... wamepoteana.
Hakika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi yule ROMA msanii wetu yuko wapi
Mshana hofu yangu hawa US tukiwaletea ujuaji wanaweza kutuletea undava tuka sambaratishana wenyewe.
Imagine wanatoa picha za setelite zikimuonyesha Oclock-8 kapigishwa magoti mbele ya kiti cha enzi huku pembeni Paulo kasimama na mjeledi tutasemaje zaidi ya kuchukiana zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hao hao wameiweka Libya kwenye machafuko na leo Libya wanatamani yule gwiji Gadafi afufuke nasi tunataka kuwasujudu wamarekani amini ipo siku tutalia na kuwatolea maneno machafu hao wamarekani kwa kusema kuwa tungejua
Mbona hata kwa Saddam Hussein wa Iraq walisema kua wana ushahidi kua Saddam ana silaha za WMD? Je walizikuta hizo silaha mpaka leo? Wameua watu na hakuna kilichopatikana mpaka leo hii!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa wamarekani wamekua chanzo kikubwa cha machafuko katika mataifa mengi duniani hasa katika bara la Africa tufikili zaidi nasi pia juu ya kile walicho lenga kwani hata katika VISA yao wamesema kuwa nchi zilizo zuiliwa wanapaswa kukubaliana na maafisa wao wa usalama kufanya kazi kwa ushilikiano na nchi husika kwangu naamini si bure kunakitu kimelengwa hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona hata kwa Saddam Hussein wa Iraq walisema kua wana ushahidi kua Saddam ana silaha za WMD? Je walizikuta hizo silaha mpaka leo? Wameua watu na hakuna kilichopatikana mpaka leo hii!
Suala la Saddam ni suala la kisiasa zaidi alikuwa anatishia maslahi yao mapana ya kiuchumi na watu waote wanajuwa ilikuwa ni hali ya kutafuta idhini ya kimataifa na mbaya zaidi Saddam alikuwa anawatisha kuwa anazo silaha kwa kukataa kuruhusu wakaguzi kwa kudhani itamsaidia ila hilo sio suala la Makonda hawana maslahi naye na zaidi siku nyingi wanasema fanyeni uchunguzi kimyaa haiwezekani matukio kibao eti asishikwe mtu hata mmoja inaweza kuwa sio yeye lakini lazima majibu yapatikane ni nani huyo anafanya upuuzi huu. kumbuka kuna watu kibao wamepotea au kutekwa wakati fulani lakini kweli hakuna mtu hata kushukiwa?? hapa wamemtaja mtu mmoja hawajasema nchi sasa usiniambia Mkuu wa mkoa anatishia maslahi yao. hapana kuna mambo hayasemwi na ni lazima yasemwe. Serikali ina mtandao mkubwa ukitishia maslahi ya nchi utajulikana kabla ya matukio.
 
Back
Top Bottom