1. VYOMBO VYA HABARI VILIVYOFUNGWA
Katika mkutano wa Oslo Forum, Maria Sarungi ametoa madai ya kupotosha kuhusu uhuru wa vyombo vya habari nchini, akieleza kuwa kuna vyombo vingi vya habari vimefungwa na Rais Samia ili kujitengenezea njia rahisi ya ushindi wa Mwezi Octoba. Hakuna chombo cha habari kilichofungiwa kwa sababu ya kutoa maoni huru au kwa kuikosoa serikali. Kama vipo avitaje! Siku ya uhuru wa vyombo vya habari sote ni mashahidi wadau wote walipongeza uhuru uliopo.
2. NGO'S ZILIZOFUNGWA
Kuhusu asasi za kiraia (NGO’s), ni vyema kuweka wazi kuwa mashirika yanayofanya kazi zao kwa mujibu wa sheria yanafanya kazi bila bughudha yoyote. Mashirika yasiyo karibishwa nchini ni yale yanayokiuka masharti ya usajili au kuendeleza ajenda zisizokubalika kama kuhimiza ushoga na usagaji. Hakuna NGO iliyofungiwa kwa sababu ya kumkosoa Rais, kama Maria Sarungi anavyodai kwa lengo la kuchafua taswira yetu kimataifa.
3. RUHUSA YA SHUGHULI ZA KISIASA
Katika uwanja wa kisiasa, Tanzania imepiga hatua kubwa. Vyama vya siasa vina uhuru wa kufanya mikutano, kampeni na kushiriki kwenye chaguzi kwa haki na usawa. Chadema kama chama cha upinzani kimekumbwa na migogoro ya ndani ambayo imedhoofisha nguvu zake za kisiasa. Mwaka huu chama hicho hakijaonesha maandalizi yoyote kuelekea uchaguzi. Ni wazi kwamba hakuna tishio la kweli la ushindani linaloibua hofu kwa serikali kama Maria anavyotaka kuonesha.
4. UHALIFU NA KUTEKWA
Kuhusu madai ya utekaji na kupotezwa kwa watu, ni lazima tuyachukulie kwa uzito unaostahili kwa kuzingatia ushahidi. Tanzania ni nchi ya sheria, na vyombo vya usalama vinafanya kazi kwa weledi kuhakikisha usalama wa raia. Uhalifu na matukio ya kihalifu hutokea sehemu nyingi duniani, ikiwemo mataifa yaliyoendelea kama Marekani, ambako watu hupotea au kuuawa bila serikali kuhusika. Hivyo basi, kuyahusisha matukio ya kihalifu na serikali kwa lengo la kisiasa ni upotoshaji wa makusudi.
5.MKAKATI WA KUJIPATIA FEDHA KWA ULAGHAI
Ni wazi kuwa Maria Sarungi ameendelea kutumia majukwaa ya kimataifa kama njia ya kujipatia mashiko ya wafadhili kama Ford Foundation, kwa kutengeneza picha mbaya ya Tanzania. Badala ya kuisemea Tanzania kwa uhalisia na kujenga, amechagua kuwa sehemu ya ajenda za nje zinazolenga kupandikiza chuki na kupunguza imani ya Watanzania kwa taasisi zao. (Hivi karibuni alipewa $400,000 zaidi ya TZS Bilioni 400 kwaajili ya Kampeni dhidi ya Tanzania kupitia Mwanzo org)
Katika mkutano wa Oslo Forum, Maria Sarungi ametoa madai ya kupotosha kuhusu uhuru wa vyombo vya habari nchini, akieleza kuwa kuna vyombo vingi vya habari vimefungwa na Rais Samia ili kujitengenezea njia rahisi ya ushindi wa Mwezi Octoba. Hakuna chombo cha habari kilichofungiwa kwa sababu ya kutoa maoni huru au kwa kuikosoa serikali. Kama vipo avitaje! Siku ya uhuru wa vyombo vya habari sote ni mashahidi wadau wote walipongeza uhuru uliopo.
2. NGO'S ZILIZOFUNGWA
Kuhusu asasi za kiraia (NGO’s), ni vyema kuweka wazi kuwa mashirika yanayofanya kazi zao kwa mujibu wa sheria yanafanya kazi bila bughudha yoyote. Mashirika yasiyo karibishwa nchini ni yale yanayokiuka masharti ya usajili au kuendeleza ajenda zisizokubalika kama kuhimiza ushoga na usagaji. Hakuna NGO iliyofungiwa kwa sababu ya kumkosoa Rais, kama Maria Sarungi anavyodai kwa lengo la kuchafua taswira yetu kimataifa.
3. RUHUSA YA SHUGHULI ZA KISIASA
Katika uwanja wa kisiasa, Tanzania imepiga hatua kubwa. Vyama vya siasa vina uhuru wa kufanya mikutano, kampeni na kushiriki kwenye chaguzi kwa haki na usawa. Chadema kama chama cha upinzani kimekumbwa na migogoro ya ndani ambayo imedhoofisha nguvu zake za kisiasa. Mwaka huu chama hicho hakijaonesha maandalizi yoyote kuelekea uchaguzi. Ni wazi kwamba hakuna tishio la kweli la ushindani linaloibua hofu kwa serikali kama Maria anavyotaka kuonesha.
4. UHALIFU NA KUTEKWA
Kuhusu madai ya utekaji na kupotezwa kwa watu, ni lazima tuyachukulie kwa uzito unaostahili kwa kuzingatia ushahidi. Tanzania ni nchi ya sheria, na vyombo vya usalama vinafanya kazi kwa weledi kuhakikisha usalama wa raia. Uhalifu na matukio ya kihalifu hutokea sehemu nyingi duniani, ikiwemo mataifa yaliyoendelea kama Marekani, ambako watu hupotea au kuuawa bila serikali kuhusika. Hivyo basi, kuyahusisha matukio ya kihalifu na serikali kwa lengo la kisiasa ni upotoshaji wa makusudi.
5.MKAKATI WA KUJIPATIA FEDHA KWA ULAGHAI
Ni wazi kuwa Maria Sarungi ameendelea kutumia majukwaa ya kimataifa kama njia ya kujipatia mashiko ya wafadhili kama Ford Foundation, kwa kutengeneza picha mbaya ya Tanzania. Badala ya kuisemea Tanzania kwa uhalisia na kujenga, amechagua kuwa sehemu ya ajenda za nje zinazolenga kupandikiza chuki na kupunguza imani ya Watanzania kwa taasisi zao. (Hivi karibuni alipewa $400,000 zaidi ya TZS Bilioni 400 kwaajili ya Kampeni dhidi ya Tanzania kupitia Mwanzo org)