Marekani yazishtukia Urusi na Korea Kaskazini, yadai zina mazungumzo ya siri

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
Ikulu ya White House ya Marekani, imesema kuwa Urusi inaendelea na mazungumzo ya siri na Korea Kaskazini ili kupata risasi na nyenzo nyingine za kivita dhidi ya Ukraine.

Mtandao wa BBC umeripoti kuwa msemaji wa usalama wa taifa hilo, John Kirby, amesema kuwa pamoja na vifaa vya kijeshi, Moscow inaweza pia kuingia katika mikataba ya kununua malighafi ili kuipatia sekta yake ya ulinzi.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Linda Thomas-Greenfield alizikosoa Urusi na Korea Kaskazini.

“Katika harakati zake za kutafuta silaha hizi, Urusi itakiuka maazimio ya Baraza la Usalama, yakiwemo yale ambayo Urusi yenyewe iliyapigia kura.

Mkataba wowote wa silaha kama huo utakuwa ukiukaji mkubwa wa azimio la Baraza la Usalama lililopitishwa kwa kauli moja baada ya majaribio ya nyuklia ya Korea Kaskazini na kurusha makombora ya balestiki," Linda Thomas-Greenfield amesema.
 
Ikulu ya White House ya Marekani, imesema kuwa Urusi inaendelea na mazungumzo ya siri na Korea Kaskazini ili kupata risasi na nyenzo nyingine za kivita dhidi ya Ukraine....
Mbona huyo mnaa hajashtuka mateso anayowapa washirika wa huyo mnaa huku bara la giza, Anahangaika na Mrusi ilhali Mrusi ana wanyonge vibaraka na washirika moja baada ya mwingine 🤸🤸🤸
 
Supa-pawa amepatwa na nini tena? Mpaka kugeukia kwa Kiduku kuomba 'nipige tafu' ?

T14 Armata dudus Yoda MK254 Aleyn
Mwaka huu Shoigu alikuwa Pyongyang kwenye maadhimisho ya miaka 70 ya vita ya Korea.
Hapo walikuwa na mazungumzo makubwa kuhusu ushirikiano wa kijeshi. Ni vigumu kwa Russia kuwa na war production kubwa hasa vitu vya kawaida visivyohitaji teknolojia kubwa sana kama artillery na shells.

Kama Russia iko overstretched kwenye production inaweza omba msaada kwingineko kama Iran. Sasa Iran nako Russia haijakubali kuuza Su-35 fighters, bado mazungumzo hayajulikani yamefikia wapi kuna mkwamo ulikuwepo. Mara nyingi Russia huwa inasumbua kuiuzia Iran silaha sasa wamebanwa Iran ikawasaidia kidogo nayo inataka mambo yake yaende. Hivyo Iran inaweza isitoe kitu kingine sababu inahatarisha sanctions nyingine na kelele za kimataifa bila kupata faida labda fedha ambazo sidhani kama ndio shida yao kubwa. Wao military production ya teknolojia kubwa kuzidi North Korea wanayo.

China ipo haitaki kuharibu biashara na West kisa maamuzi binafsi ya Putin. Hao wana production kubwa sana na teknolojia ya juu kuliko hata Urusi kwa sasa ila hawajaona haja kuvamia mambo wasiyo na maslahi nayo.

Hao wengine wanaweza toa msaada kidogo kwa timing na ndipo anabaki North Korea ambaye kila kitu anaweza toa. Sababu kuu kwake ni FEDHA, North Korea hata uwe nani ukiwa na hela tu yeye anakuuzia chochote alichonacho.
Alishafanya biashara za makombora na kina Iran, Libya ya Ghadaffi, Iraq ya Saddam Hussein na wakorofi wengine. Sababu hana cha kupoteza, ana sanctions kila kona na ana majirani wawili China na Russia wanaomtosheleza na kumlinda, jirani yake wa Kusini mipaka imefungwa senyenge na mabomu, Japan huyo wanashare maji na hawaelewani.

Kwanza North Korea huwa inatumia forced labour na ikijitahidi sana cheap labour, cost of production kwao ndogo sana. Ila wana production technology ya zamani ambayo kwenye silaha inaleta reliability ndogo.
Muhimu zaidi maghala yao ya silaha yana artillery shells na maroketi in millions sababu ndicho kitu pekee wanajua sana na wanapenda saturation attack. Hata cannons, self propelled guns, howitzers na rockets launchers wanazo hata 20,000 zinafika
20230822_170029.jpg


Alafu sasa, rockets na artillery shells huwa zina expiration usipozitumia miaka kadhaa kwenye makumi, mostly ni propellant kuisha muda. Mwisho wa siku wanataka swapping ila wakizitoa hela ya replacement hawana. So let's say badala usubiri shells ulizotengeneza mwaka 1970 ziishe muda mwaka 2030, ziuze 2023 utengeneze nyingine labda zenye improvement zidumu miaka 60 ijayo. But, Russia inaweza taka mpya, sijaona supplies zao za Iran na Sudan zikiwa ni za zamani zinakuwa nyingine ni batch ya 2023, hii ni kukwepa wear & tear ya guns.

So as long as Russia ina hela itauziwa chochote alichonacho North Korea. Ila sina imani kwamba watafikia terms za kuwapa military tech au kuwauzia silaha. Wao seriously wana shida sana na Air Force yao kuchoka kuliko maelezo, ila kwa njaa waliyonayo si lazima wapewe silaha ndio wakubali wao sio Iran.
 
Anapokera wengi wapenda uhuru ndio hp Mmarekani, Yan analotakaga yeye ndio lipewe kipaumbele Ila wenginne wakiamua ya kwao bila ya yy kushirikishwa inakuwa nongwa
Ndio maana yakua superpower hio ukiwa kiranja mkuu huwez kuruhusu vijana wengine wabweke hovyo
 
Walisema wapi weka evidence.
Sidhani kama kuna sehemu yametajwa masaa 72, alichosema ni wanajeshi wa Ukraine waweke silaha chini warudi kwa familia zao wakati majeshi yake yakiwa kwenye msafara kuvamia nchi. Jambo ambalo halijafanywa mpaka leo hii.

Ref kwenye speech yake kuhusu kuivamia ukraine.
 
Marekani na NATO na washirika wake kushirikiiana na Ukraine kuishinda Urusi ruksa
Urusi kua na washirika Marekani haitaki.
Aisee hili taifa kama angekua ni kiumbe basi agekua ni binadamu lakini mchawi.

Kwa maana Nina uhakika hakuna wanayama wachawi.
 
Back
Top Bottom