Marekani yasalimu amri kwa Magufuli

Marekani yasalimu amri kwa Magufuli

Safi waambie hao wa Lumumba. wamekaa kwenye key board tu. ombeni safari moja ya Marekani mbadilishwe akili zenu

Huwezi kumjua maskini mpaka umwone tajiri kwanza.

Kule Marekani kulipotokea kimbunga, kuna bandari moja ilifungwa. Mapato yake kwa siku bandari ile ambayo si moja ya bandari kubwa za Marekani ilikuwa ni dola milioni 400. Tanzania tuna nini mpaka sasa kinachokaribiana angalao na hicho? Umaskini wetu utaondoka kwa mipango thabiti siyo kwa kelele hizi za kusema sisi ni matajiri, Marekani imesalimu amri, n.k.

Ukiwa mjinga na unataka kuifurahisha nafsi yako, hata leo unaweza kusema, 'mimi ni tajiri kama Bakhresa, kuna siku Dangote atanipigia magoti', lakini hiyo haitabadilisha umaskini wako, na wala haitabadilisha utajiri wa Dangote au Bakhresa. Umaskini wako utaondoka kwanza kwa kukiri kuwa wewe ni maskini kuliko hao matajiri, na baadaye kwa kuwa na mipango thabiti ya kuondoka mahali ulipo.

Mpaka leo hii, hapa mahali tulipo, na kwa mwendo tunaoenda nao, kwa kadiri ya taarifa za UNDP, itatuchukua miaka 250 kuifikia Malaysia (wao wakiamua kubakia walipo!) ilipo leo ingawa miaka ya 1960 tulikuwa tunalingana kwa umaskini. Hiyo ni Malaysia wala siyo Marekani.
Safi waambie hao wa Lumumba. wamekaa kwenye key board tu. ombeni safari moja ya Marekani mbadilishwe akili zenu
Hata tukijitahidi vipi watakaoifikia Marekani siyo hiki kizazi chetu. Maendeleo ni process, hulali na kuamka ukashtukia umeendelea. Tulipotea njia mwanzoni. Hata tukiipata njia leo ni lazima tuanze safari, na baadaye tufike tunakotaka kwenda.
 
Balozi wa marekani akiwa na ujumbe wake leo wamekutana na viongozi wakuu wa serikali ya Tanzania na kuihakikishia nchi yetu kuwa wataendeleza uhusiano mwema kati ya nchi hizi mbili. Akiongea baada ya mkutani huo, waziri wa mambo ya nje, ushirikiano wa kikanda na kimataifa amesema kuwa Marekani imeahidi kuendelea kuisaidia tanzania na kuahidi Dola 750m kila mwaka kwa Tanzania. Pia ametolea maelezo swala la Mcc kwa maeneo ambayo hayakueleweka vixuri.

Source: TBC
Haijasalimu amri.... Imecommit kushirikiana

Mcc haiko chini ya balozi, mcc ni independent agency na maelezo aliyotoa balozi yako clear

Kitengo cha ptopaganda siku hizi kinahitaji watu wapya, it seems wote iq zao zilishuka ili wawe ka ari, nguvu na kasi za mtawala wao... Siwaoni mkisurvive kasi ya jpm
 
CIA ipo kazini, acha kuwa boya wewe, Marekani isalimu amri Kwa Tanzania?
Hebu tuambie inaogopa kuvamiwa na Tanzania hadi imesalimu amri?
akili za UVCCM ni za kuunga na superglue, narudia tena kukueleza kuwa CIA is carrying out its role, akili za kuambiwa changanya na za kwako.
Tembo ni mnyama mkubwa sana lakini sisimizi aweza mdondosha......Amini tu kuwa wao pia ni wanadamu na kuna mipaka ya nguvu zao. Cha msingi tuwe tu wastaarabu na kuacha kufanyiana ubabe siyo sisi au wao sote kwa pamoja we need each other.

Hili la Tanzania niliweke bayana, ile njema mpaka itokee hakuna wakupangua huu mchezo awe na nguvu au dhaifu. Nilisema narudia tena kwa nchi yangu Tanzania nitasimama kwa miguu yangu yote na kwahakika mpaka lile kusudi la moyo wangu mimi kama raia halali litimie, liwake jua inyeshe mvua. Kila mpango dhalimu kinyume na haya malengo utajisambaratisha wenyewe bila kujali mwenye kuuandaa ana akili na nguvu nyingi kiasi gani.

Kings rule by decrees......have I spoken so shall it be!
 
Mleta mada unachotakiwa kufahamu ni kwamba US ina-fund two types of projects! MCC infrastructure development project ambayo ndo tumepigwa za uso pamoja na social development projects hususani kwenye sekta ya afya. Haya mamilioni ya kwenye social development projects hawakuyaondoa.

Kwahiyo kudai eti Marekani kasalimu amri ni porojo.

Ingawaje
 
Seriously? Mbona kama US representatives wamepanic flani hivi amazing.. Watu wa diplomasia watanielewa.

sisi ndio tumepanic,kama uhusiano ungekuwa umevunjika kabisa si wangeondoa ubalozi wao kabisa.kitu kidogo ishipa inatutoka kwamba USA imesalimu amri,wabongo bhana tumezidi
 
wamarekani haeawezi kuacha kuosaidia tz wazungu wanajua wanachokifanya hawatoi msaada wa bure.

lazima kuna maslahi yao tz kama yapo hawawezi kukubali kuyapoteza.
 
Huwezi kumjua maskini mpaka umwone tajiri kwanza.

Kule Marekani kulipotokea kimbunga, kuna bandari moja ilifungwa. Mapato yake kwa siku bandari ile ambayo si moja ya bandari kubwa za Marekani ilikuwa ni dola milioni 400. Tanzania tuna nini mpaka sasa kinachokaribiana angalao na hicho? Umaskini wetu utaondoka kwa mipango thabiti siyo kwa kelele hizi za kusema sisi ni matajiri, Marekani imesalimu amri, n.k.

Ukiwa mjinga na unataka kuifurahisha nafsi yako, hata leo unaweza kusema, 'mimi ni tajiri kama Bakhresa, kuna siku Dangote atanipigia magoti', lakini hiyo haitabadilisha umaskini wako, na wala haitabadilisha utajiri wa Dangote au Bakhresa. Umaskini wako utaondoka kwanza kwa kukiri kuwa wewe ni maskini kuliko hao matajiri, na baadaye kwa kuwa na mipango thabiti ya kuondoka mahali ulipo.

Mpaka leo hii, hapa mahali tulipo, na kwa mwendo tunaoenda nao, kwa kadiri ya taarifa za UNDP, itatuchukua miaka 250 kuifikia Malaysia (wao wakiamua kubakia walipo!) ilipo leo ingawa miaka ya 1960 tulikuwa tunalingana kwa umaskini. Hiyo ni Malaysia wala siyo Marekani.

Hata tukijitahidi vipi watakaoifikia Marekani siyo hiki kizazi chetu. Maendeleo ni process, hulali na kuamka ukashtukia umeendelea. Tulipotea njia mwanzoni. Hata tukiipata njia leo ni lazima tuanze safari, na baadaye tufike tunakotaka kwenda.

Kati ya leo na 1960 imepita miaka zaidi ya 250? Kama kweli unachosema umekiamini then kama Malaysia iliwachukua hiyo miaka michache kufikia hapo leo iweje sisi tuchukue 250? Pengine ingekuwa vyema hata kwa uchache kuzipitia tu theory walizotunga wao za development kabla ya kuamini kila unachoambiwa.....Intimidation ni strategy pia ya kukuondolea wewe confidance ili usiweze kuthubutu na kuweza kuendelea pasipo vikwazo.

Ebu tujenge kujiamini kwanza kama nchi then yanatakayofuata ni matokeo.....hata kama itachukua bilions of years let us START now to walk our talks.

Tukumbuke kuwa poverty is nore of an attitude than anything else.....elimu kandamizi wanazotupatia zisizo zingatia context na culture zetu ni silaha pia ya kuendelea kututoa katika mstari wa maendeleo.

Tanzania njema ni lazima apende au asipende mtu....hapa kazi tu....hata tukiharibu ni sawa kama dhamira yetu ni njema!
 
Hii inchi ngumu kweli kuiongoza.

Kuna baadhi wamefurahi sanaa juu ya haka ka juhudi ka jpm kuna baadhi wanatamani ashindwe kabisaaa wapate cha kuongea,,

Swali akishindwa sijui wewe utaenda wapi???
Kuna wana ccm mpaka sasa hawataki kumsikia jpm kabisaaa na kuna wapinzani ndoo hawataki hata kuliona jina lake mahali,, kwani anafanya mambo ambayo walitamani kuyafanya kwa wana inchi,, ña kwa jinsi wanavyowajua wabongo wanajua tayari hili tufani litaondoka nao kama si wote basi weengi


Swali sasa huyu rais ni wa upande gani???
jibu:Jpm ni raisi wa watanzania wote wenye vyama na wasio na vyama.
 
CIA ipo kazini, acha kuwa boya wewe, Marekani isalimu amri Kwa Tanzania?
Hebu tua
mbie inaogopa kuvamiwa na Tanzania hadi imesalimu amri?
akili za UVCCM ni za kuunga na superglue, narudia tena kukueleza kuwa CIA is carrying out its role, akili za kuambiwa changanya na za kwako.

Mbona unabadili kilichoandikwa?
 
Hii inchi ngumu kweli kuiongoza.

Kuna baadhi wamefurahi sanaa juu ya haka ka juhudi ka jpm kuna baadhi wanatamani ashindwe kabisaaa wapate cha kuongea,,

Swali akishindwa sijui wewe utaenda wapi???
Kuna wana ccm mpaka sasa hawataki kumsikia jpm kabisaaa na kuna wapinzani ndoo hawataki hata kuliona jina lake mahali,, kwani anafanya mambo ambayo walitamani kuyafanya kwa wana inchi,, ña kwa jinsi wanavyowajua wabongo wanajua tayari hili tufani litaondoka nao kama si wote basi weengi


Swali sasa huyu rais ni wa upande gani???
Yaani kwa maneno rahisi ni nyumbu wajipange 2030 au 2035 huko... Waombe sana JPM apate atakayempokea mbovu 2025.. Nyumbu mkubali tu
 
Mate yanawatoka kuhusu Nuclear yetu....
Majuzi nilipata communication fulani nikajichekea tu.....ebu tujiulize upo jangwani na hakuna source ya maji lakini mfukoni kwako una bilioni moja ya kuweza kununua maji lakini huna mawasiliano wala jinsi ya kuondoka hapo kwani ulidondoshwa na ndege uka survive.....je hiyo bilioni yaweza kukupatia maji? Kwa mfano huo huo mliodondoshwa ni zaidi ya moja mka survive lakini miongoni mwenu yupo mwenye mawasiliano mtamkatalia msaada kwakua ni adui yenu au nyakati hizo uadui utakuwa pembeni?

Kuna njia ionekanayo njema mbele ya mwanadamu lakini mbele ni mauti.....tazama kuna njia mbili mbele yako yenye uzima na mauti, chagua uzima.....haya ni maneno ya imani unfortunately ukiwa na uzima na kukosa utambuzi huchagua mauti lakini katika no option au near to death experience scenarios kila mtu hupenda kuchagua uzima bila kuhubiriwa....Kwa hakika Tz is strategically placed to determine the future of many countries eleweni hilo.....mengine yote ni jinsi tutakavyochanga karata zetu. Mimi binafsi nilibahatika kuujua ufunguo wa kufunga na kufungua usiniulize maswali sinauwezo wa kuyajibu sawia jambo moja nalifahamu kwa hakika ......Tanzania njema ni lazima!
 
Sio Balozi amesalimu amri hayo ni maagizo kutoka White house kwa President Obama, Magufuli amekubaliwa na ameonekana yuko serious kupambana na ufisadi na kutaka utawala wa sheria. Very soon kabla hajaondoka madarakani mtegeeme President Magufuli ataalikwa Oval Office kama mgeni rasmi wa President Obama.
Bravo Mzee wa hapa kazi tu Dunia inakukubali.
 
Marekani isalimu amri kwa magufuli? Hehe waafrica tunapenda kujipa moyo kweli! Nchi yenyewe bajeti yake inapitwa na kampuni moja tuu za kimarekani...mfano google, amazon, apple, microsoft etc
Bavicha cjui magu awafanyie nn ili mtulize vidomo?
 
Si mlisema hamtaki misaada? Sasa mnapifariji ya nini? kwani gesi ya Tanzania imepotea? TRA wameacha kukusanya kodi? Hamtaki tena na sie tutoe misaada? Hata kama wamesema wataleta kataeni waambieni na nyie mnasubiri kuwapa wao.. sizitaki mbichi hizi kumbe ilikuwa inauma eee.
 
Kweli kabisa kitengo kinahitaji watu wapya wenye uwezo wa kuelewa mambo ya kidunia yanavyokwenda
 
Balozi wa marekani akiwa na ujumbe wake leo wamekutana na viongozi wakuu wa serikali ya Tanzania na kuihakikishia nchi yetu kuwa wataendeleza uhusiano mwema kati ya nchi hizi mbili.

Akiongea baada ya mkutani huo, waziri wa mambo ya nje, ushirikiano wa kikanda na kimataifa amesema kuwa Marekani imeahidi kuendelea kuisaidia tanzania na kuahidi Dola 750m kila mwaka kwa Tanzania.

Pia ametolea maelezo swala la Mcc kwa maeneo ambayo hayakueleweka vizuri.


Chanzo: TBC
Sasa hapa Marekani kasalim amri kwa lipi? kwa kutupa msaada wa afya na elimu ili tusiendelee kufa ovyo kwa ukosefu wa dawa muhimu na kuondoa ujinga ili tukatae kutawaliwa na CCM? Ni ujuha wa mtoa kichwa cha habari.Marekani kamuonea huruma Magufuli. MCC inabaki kwa vile inahusu zaidi miundombinu, hivyo itainyukua serikali zaidi ya wananchi wasiokuwa na hatia
 
Back
Top Bottom