Marekani yasalimu amri kwa Magufuli

Marekani yasalimu amri kwa Magufuli

kama barick peke yake alifanyiwa auditing anatakiwa kulipa kodi yetu ya bil 80 wameona tukiendeleza figisufigisu jamaa atachukua migodi yake wekeni mambo sawa balozi tanzania umesikia hakikisha acacia, barick nk wanafanya kazi vizur. Lazima waachie pesa, jeuri hiyo hawana kwa Mugabe wala Museven hapa kuna kitu wanajua wakizingua wameisha
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Seriously? Mbona kama US representatives wamepanic flani hivi amazing.. Watu wa diplomasia watanielewa.

Ni kweli wamepanic.Na sababu kubwa nadhani taarifa walizokuwa wakipeleka marekani kuhusiana na mambo mbali mbali hasa ya kisiasa ya Tanzania hazikuwa sahihi hivyo kusababisha marekani kuchukua hatua zisizo sahihi ambazo zimesababisha matokeo yasiyo sahihi.

Kuna uwezekano mkubwa sana wa marekani ikawaondoa kuanzia balozi mwenyewe na wengi wao wakaondolewa nchini wakaletwa wengine kushika nafasi zao.
 
Hii inchi ngumu kweli kuiongoza.

Kuna baadhi wamefurahi sanaa juu ya haka ka juhudi ka jpm kuna baadhi wanatamani ashindwe kabisaaa wapate cha kuongea,,

Swali akishindwa sijui wewe utaenda wapi???
Kuna wana ccm mpaka sasa hawataki kumsikia jpm kabisaaa na kuna wapinzani ndoo hawataki hata kuliona jina lake mahali,, kwani anafanya mambo ambayo walitamani kuyafanya kwa wana inchi,, ña kwa jinsi wanavyowajua wabongo wanajua tayari hili tufani litaondoka nao kama si wote basi weengi


Swali sasa huyu rais ni wa upande gani???
 
Mmmh huyu mtoa mada nawasiwasi nae .....marekan yasalimu amri????mweee halaf source Tbc labda vng"amuz vnatofautiana
Utake usitake ndio hivo sasa, wamesalimu amri tena kwa unyenyekevu mkubwa. Balozi w marekani ameenda na jopo la maafisa wake wote kuweka mambo sawa na serikali yetu.
Endelea na wasiwasi wako, JPM anawanyoosha tuu![emoji1]
 
Kichwa cha habari kimekaa kinafiki sana.!
 
Marekani haijawahi kuacha kuisaidia Tanzania katika maeneo yote. Mfuko wa PEPFAR pekee bado unatoa mabilioni ya dola kila mwaka katika sekta ya afya. Tuache kejeli zetu zisizokuwa na miguu wala mikono.....
 
Marekani isalimu amri kwa magufuli? Hehe waafrica tunapenda kujipa moyo kweli! Nchi yenyewe bajeti yake inapitwa na kampuni moja tuu za kimarekani...mfano google, amazon, apple, microsoft etc
Safi waambie hao wa Lumumba. wamekaa kwenye key board tu. ombeni safari moja ya Marekani mbadilishwe akili zenu
 
Serikali nayo inache ku flip-flop kwenye suala la misaada. Kama wameamua kuwa bold katika suala la kujitegemea waendelee hivyo. Sasa manaendelea kukubali usaidizi wao, mtapata wapi nguvu yta kukataa masharti yao?
 
Hii habari ingeweza kuandikwa vizuri zaidi kuliko ilivyoletwa. Kichwa cha habari kilekaa kipuuzi. Aliyeileta awe makini.
 
Marekani haijawahi kuacha kuisaidia Tanzania katika maeneo yote. Mfuko wa PEPFAR pekee bado unatoa mabilioni ya dola kila mwaka katika sekta ya afya. Tuache kejeli zetu zisizokuwa na miguu wala mikono.....
Kuna watu hata wakisikia hawaelewi, hata wakiangalia hawaoni. Pesa ya MCC siyo ya serikali, ni ya taasisi ambayo huitoa kwa masharti ya kuheshimu demokrasia na uhuru. Nchi yetu imekiuka, imenyimwa. Full stop.

Serikali ya Marekani haijawahi kutamka kuwa inasimamisha misaada kwa Tanzanaia. Marekani inatoa misaada mingi kwenye maeneo mbalimbali, misaada kwa serikali, misaada ya kisekta, misaada ya kiutu, na misaada ya kijamii. Marekani huwa inatoa misaada hata kwa tawala dhalimu kabisa ila inaamua itoe misaada ya namna gani kwa kutegemea aina ya serikali na utawala. Sekta ya afya ni kati ya maeneo yanayopokea msaada mkubwa toka Marekani.

Ninachoona hapa hakuna mabadiliko bali walichofanya ni kutoa ufafanuzi kwa watu ambao au walikuwa hawaelewi, au uelewa wao ni mdogo au walikuwa wakiwapotosha wananchi.
 
Kimahusiano ya kimataifa hii ni hatua njema kwa Serikali ya JPM
 
Back
Top Bottom