Marando na watuhumiwa wa ufisadi

Marando na watuhumiwa wa ufisadi

Ni kweli, pia aelewe kuwa wale ni watuhumiwa si haki kuwabagua kwa utuhumiwa wao
hadi pale haki itakapojibainisha.
Marando na Dr Slaa wote ni CDM na kila siku wanasimama kwenye majukwaa ya siasa wanapinga Ufisadi.
Tukija kwenye suala la EPA Dr Slaa, anawatambua Mafisadi kina Jeetu Pater, Marando hawatambui?
Hii kweli sinema ya kihindi
 
hapa ndo ninapokuwa na doubt na uelewa wa wanaJF wengi. hivi kutibu mtu ndo kumtetea na kuhalalisha wizi wake? Marando anawatetea. hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. nashangaa wengi wanaokusifu kwa utumbo wako huu. Mleta mada unamantik. marando is threat to chadema than any. even shibuda is less. mark my words.
Ni threat kwa CCM na mafisadi sio kwa wananchi hata kiongozi wa waasi Libya Mustafa Abdel Jalil alikuwa waziri wa sheria wakati wa Gaddafi.
 
Tutafute namna ya kumtetea Marando jamani,hv kusema wale ni watuhumiwa tu maana yake Marando anapigania kumprove wrong Dr slaa? Tuseme vidagaa or whatever lakini fisadi ni fisadi na hao tunawajua hivyo!
 
Mimi nilishagasema humu kuwa kisiasa afanyacho Marando hakitaeleweka hata kama hakuna makosa kwenye maadili ya fani yake. Ni heri achague moja tu...siasa ama aendelee na fani yake bila kujiingiza kwenye siasa.
 
Wana JF

Kwanza na-declare interest mm ni mfuasi na mwanachama wa CHADEMA, Hili swala la Marando kuwa wakili wa baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi km vile manji na mahalu litakuja kuwa na madhara makubwa sana hapo badae ktk harakati za chama za kuchua dola natambua kabisa ile ni professional yake na ni vigumu aache kazi aliyoisomea kwa muda mrefu, lakini kabla ya kuchua kazi lazima mtu ufanya client assessment.

Kwa kuwa ameamua kuwa ktk siasa na kufanikiwa kuwa mjumbe wa cc ya cdm ni wakati wake muafaka wa kuhakikisha kimoja kati ya professional yake na siasa hakuna kinacholeta madhara kwa kingine. Kwa hiyo moja ya criteria ya kutumika kwake kum-accept client iwe ni asiwe mtuhumiwa wa ufisadi. Nionavyo mm professional yake kwa sasa inaleta madhara ktk siasa si kwake tu bali kwa Chadema kwa ujumla coz ni vigumu sana mtu kupinga ufisadi majukwaani na kuukubali mahakamani na watu wote wakaamua kukuamini ww ni mpiganaji wa kweli wa ufisadi.

Swala kubwa la sisi wana-chadema tunalotakiwa kulielewa ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawawezi kutofautisha professional na siasa kiasi kwamba point tutakayoitumia kuuelezea uma ya kuwa hii ni siasa na hii ni professional haitaweza kuzaa matunda yeyote. Marando na uongozi wa juu ulitazame hili kwa mapana na marefu ili nguvu iliyokwisha tumika kukifikisha chama hapa isije kupotea kirahisi kisa mtu mmoja ambae ana uwezo wa kuchua kesi zingine na kuendelea na maisha.

Tujiulize swali dogo kwa mfano leo ROSTAM amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa KAGODA na marando akafanya km anavyofanya kwa wale wa EPA itakuwa sahihi? Au kuwatetea wa EPA itakuwa halali na kumtetea Rostam itakuwa haramu wakati wote ni mafisadi?

Nawasilisha

Ni kweli hili suala la Marando linatakiwa kuangaliwa kwa undani zaidi na viongozi wa chama. Kwa upande mwingine linaathiri chama kusonga mbele. Wanaoijua issue ya Mahalu kwa kweli hawaamini mtu kama Marando kumtetea.Tunamwomba kabla ya kuchukua kesi aichunguze kwanza tunataka awe anawaadabisha hao mafisadi ili tabia hiyo ikome. Tanzania imeshatafunwa vya kutosha na ndio maana vijana tunateseka, hatuna ajira.
 
Zamani tulikuwa na majibu ktk kila swali na viongozi wetu walikuwa wanajibu kila hoja kwa ufasaha.tusirundike malalamiko akina Tumbo ndio kazi zao hizi!
 
Hivi Tundu Lissu akianza kuwatetea akina Rostam na mafisadi wenzie ataeleweka kweli?
 
Ni kweli lakini maadili ya uwakili yanasemaje? Tusipende kuhukumu pasipo kujua tunachokihukumu.

Mimi sijui hayo maadili ya uwakili kwa sababu mimi siyo wakali. Pia hakuna mtu anayelazimika kujua maadili ya kazi yangu. Hata hivyo kutojua maadili ya kazi mtu hakutunyimi haki ya kuona mambo katika mtazamo wa kawaida (hata kama mtazomo wetu unatokana na ujinga wetu). Na ni kutokana na mtazamo wetu, wengi wetu tunaamini kuwa Marando hana sababu ambayo anaweza kuitoa akatushawishi kwamba anaweza kuendelea kuwatetea mafisadi na wakati huo huo akaendelea kutuhubiria kuwa ufisadi ni mbaya...Wakati huo anakula na kusaza kwa sababu ya malipo ya uwakili wa kuwatetea mafidi ...It doesn't make sense at all!

Labda nikuulize...Unaweza kusimama kama wakili ukamtetea mteja anayetuhumiwa kumuua baba yako???
 
quote_icon.png
By ritz
Comrade Ngwendu, ni kweli kabisa hawa Pro-CDM-JF,uelewa wao ni mdogo sana kama huo mfano wa mgonjwa na Wakili.
Tatizo hawataki kujifunza na kukubali mawazo kutoka kwa watu wengine wao ni CDM tu mpaka imewapa upofu na akili zimedumaa kabisa tena zimefunikwa na blanketi jeusi,
hawa Pro-CDM-JF ni pumba sana mpaka wanatia huruma
Unataka CDM wajifunze toka kwa wengine wepi CCM? au kutoka kwako ha ha ha teacher.
 
si kosa kutetea maana ya uwakili ni kutetetea au kurekebisha kwenye makosa, ndio maana kuna kushinda kesi na kushindwa , Marando aliwahi kusema kuwa kesi hizi za ufisadi zimeisaidia CDM kujua kwa mapana zaidi wizi wa maliza walalahoi(Watz) kwa hiyo naona tumuache na taruma yake tutajua mengi, wezi wengi wanatumwa na mafisadi papa wakigundulika wanawaachia msara fisadi dagaa, tusubiri la kagoda kama CCM haikuhusika!!!
 
si kosa kutetea maana ya uwakili ni kutetetea au kurekebisha kwenye makosa, ndio maana kuna kushinda kesi na kushindwa , Marando aliwahi kusema kuwa kesi hizi za ufisadi zimeisaidia CDM kujua kwa mapana zaidi wizi wa maliza walalahoi(Watz) kwa hiyo naona tumuache na taruma yake tutajua mengi, wezi wengi wanatumwa na mafisadi papa wakigundulika wanawaachia msara fisadi dagaa, tusubiri la kagoda kama CCM haikuhusika!!!

Hapana mkuu,

Kwani Slaa kapata wapi taarifa? Kama ni kujua taarifa haina haja ya kuwatetea mafisadi. Ana njia nyingi sana za kupata taarifa ukingatia kuwa yeye (Marando) ni shushu mwenye uzoefu wa kutosha!!
 
Nakubaliana na wewe, lakini je ni wananchi wangapi wenye kulijua hili? kumbuka mpaka leo ccm mtaji wake mkubwa ni ujinga wa watz walio wengi, km hadi leo hawajaona madhara ya ccm unadhani ni lini watagundua marando anaongozwa na maadili ya uwakili? pia sisi km wanachama hatuweza kuwa busy kuhakikisha marando mmoja maadili yake ya uwakili hayaharibiki wakati huo huo chama chenye watu wengi ndo kiharibike,
Hii hoja ni vyema mkaitazama kwa undani kwa kuzingatia idadi kubwa ya uelewa mdogo waliyonayo wananchi wengi.

Nakubaliana na wewe kabisa, ninachotaka kusema ni kwamba kila mtu ana mtazamo wake
katika jambo hili na sidhani kama ni dhambi kutofautiana maana mwisho wa siku ukweli
utadhihirika. Hapa hatuhukumu bali tunajaribu kuangalia possibilities zote kuhusiana na
kile ulichokiita uelewa mdogo wa wananchi...
 
Mimi sijui hayo maadili ya uwakili kwa sababu mimi siyo wakali. Pia hakuna mtu anayelazimika kujua maadili ya kazi yangu. Hata hivyo kutojua maadili ya kazi mtu hakutunyimi haki ya kuona mambo katika mtazamo wa kawaida (hata kama mtazomo wetu unatokana na ujinga wetu). Na ni kutokana na mtazamo wetu, wengi wetu tunaamini kuwa Marando hana sababu ambayo anaweza kuitoa akatushawishi kwamba anaweza kuendelea kuwatetea mafisadi na wakati huo huo akaendelea kutuhubiria kuwa ufisadi ni mbaya...Wakati huo anakula na kusaza kwa sababu ya malipo ya uwakili wa kuwatetea mafidi ...It doesn't make sense at all!

Labda nikuulize...Unaweza kusimama kama wakili ukamtetea mteja anayetuhumiwa kumuua baba yako???

Naweza endapo nadhani kuna jambo limefichika nyuma ya pazia kama vile mtuhumiwa kubambikiwa
mashtaka ambayo hakuhusika, nitafanya hivyo ili kuujua ukweli zaidi. Mbona imeshatokea hivyo Marekani
kwa wakili kumtetea mtuhumiwa aliyetuhumiwa kumuua mtoto wake, mwisho wa siku ukweli ukajulikana
kuwa hakuhusika bali alitolewa kafara na vigogo ili kulinda maslahi yao... tusiangalie jambo hili kwa upande mmoja tu
 
Marando kigeugeu na miongoni mwa mafisadi makubwa. Anang'ata na kupuliza, atachukiaje ufisadi halafu unatetea ufisadi wakati chama chake ambaye ni miongoni mwa vigogo wanajidai mapambano yao ni dhidi ya ufisadi? walewale wanakataa posho bungeni baada ya kulamba za miaka sita na kupewa mrabaha Barrick.
 
Role ya Marando ni kubwa sana hasa upande wa kotini kwa maslahi ya wapinzani wote nchini. Siku zote amekuwa akisema hakubaliani na aina ya watu wanaoletwa kotini kwa tuhuma za ufisadi kwakuwa ni dagaa tu, mapapa hayaletwi. Hivi karibuni aliulizwa swali hilo kwenye mdahalo na akina Nape akaeleza hivyo hivyo. Kwa maneno rahisi ni kuwa washitakiwa wa ufisadi wanabambikwa kesi. Fikiria kubambikwa kesi na machungu yake? Ulishawahi kufuatilia au hata kuiskia kesi ya Mahalu? Umeshaskia mashahidi wanaotakiwa Mahakamani kumtetea mshitakiwa? Dogo, TAFAKARI!
MARANDOO hakupaswa kuingilia hata kidogo kesi ya MAFISADI. jeetu ni fisadi mdogo?? MANJI je ni fisadi mdogo? Uwepo wa MANJI YANGA umepelekea yanga nao waitwe mafisadi(BISHA) Wapo wa TZ wengi mamilioni wenye kubambikiwa kesi akawasaidie hao kama alivyofanya LISSU ktk kesi ya kule SERENGETI NYAMUMWA. tena bule tutamchangia hela. Wale wazee wastaafu wa iliyokuwa jumuia ya Afrika mashariki wamekosa mtetezi mwenye nguvu MARANDO HUKUWAONA HAO BABU ZETU Tusijibu maswali magumu kwa majibu mepesi. LAKINI NANUKUU" UJINGA WA WAPIGA KURA NI MTAJI KWA WAGOMBEA(WANASIASA)
 
Mbona imeshatokea hivyo Marekani
kwa wakili kumtetea mtuhumiwa aliyetuhumiwa kumuua mtoto wake, mwisho wa siku ukweli ukajulikana
kuwa hakuhusika bali alitolewa kafara na vigogo ili kulinda maslahi yao... tusiangalie jambo hili kwa upande mmoja tu

Wapi Marekani imewahi kutokea hivyo? Na kama imewahi kutokea nina uhakika kabisa huo uamuzi ulikuwa ni controversial!
 
Marando kigeugeu na miongoni mwa mafisadi makubwa. Anang'ata na kupuliza, atachukiaje ufisadi halafu unatetea ufisadi wakati chama chake ambaye ni miongoni mwa vigogo wanajidai mapambano yao ni dhidi ya ufisadi? walewale wanakataa posho bungeni baada ya kulamba za miaka sita na kupewa mrabaha Barrick.
NAUNGA MKONO HOJA. Hao mafisadi dagaa wakiishinda kesi serikali na kuidai fidia je, hizo fedha sio za walipa kodi? Je MARANDO hawezi kulipwa kamisheni au gharama za kesi? ATAPOKEA??? njii hii bwana wajinga do waliwao. ukiwa mjinga lazima uliwe. NITAMSIFU SANA KAMA ATAFUNGUA KESI YA WANAFUNZI WALIOKOSA MKOPO MWAKA HUU(+14,000) DHIDI YA BODI YA MIKOPO.
 
MARANDO ANATAKA APROVE KWAMBA wale ni vijidagaa Wahusika WaPO
 
Back
Top Bottom