LAT,
Mimi nalidhani wakili kazi yake ni kumtetea 'mtuhumiwa'!?
Hoja ya 2015 (ID ya member) sio kwamba ni tatizo kisheria kwa Marando kutetea watuhumiwa wa ufisadi lakini anaona inaweza kuleta mkanganyiko (hasa kwa watu wa kawaida, me and you excluded!) na kushindwa kutofautisha role ya marando kama wakili na hapohapo kama mwanasiasa/mwanaharakati/mwanachama wa chama kinachojipambanua kuwa against ufisadi. Mleta hoja anaona mkanganyiko huu unaweza kuiathiri CDM (au Marando kama mwanasiasa).
Binafsi pia hili linanipa shida (pamoja na kwamba sioni tatizo la kisheria). Kwa mfano masuala kama ya EPA/Kagoda, Meremeta na mengine yamekuwa yakipigiwa kelele na CDM mara kwa mara na kuishurutisha serikali kuchukuwa hatua (kuchunguza na kuwashitaki watuhumiwa) na kuna watu kadhaa ambao CDM (including Marando) imekuwa ikiwataja kwa majina (viz, List of Shame).
Sasa let say watuhumiwa hawa itokee wapelekwe mahakamani halafu Marando kama wakili achukue assignment ya kuwatetea....kwangu mimi kimantiki nitaona kuna tatizo (nitatilia shaka credibilty ya Marando kama wakili au kama mwanasiasa). Inawezekanje kwenye jukwaa la siasa umtaje/umtuhumu mtu kuwa fisadi halafu wewe huyohuyo uende mahakani kumtetea kwamba sio fisadi? Kama hili linawezekana, by implication nalo linakuwa ufisadi....ni kama vile unatoa shutuma za uongo juu ya mtu ili baadae upate kazi ya kumtetea!
Kama kweli tunaipenda CDM, nadhani ni vema tukawa wakweli na kuwashauri ipasavyo (hata kama itawauma) ili kama chama kizidi kuimarika. Wakati mwinge sio rahisi kwa wanasiasa kuona conflicting interests walizonazo. Hivyo pamoja na kuwa ni haki ya Marando kufanya afanyacho na pia ni haki ya watuhumiwa kupara fair representation kwenye vyombo vya kisheria, lakini bado anaweza kuchuja ili kuepuka/kupunguza conflict of interest.