Marafiki wasiokupenda wako hivi

Marafiki wasiokupenda wako hivi

Usiamini nafsi yoyote hata nafsi yako pia itilie mashaka..!!kwani ni mara ngapi nafsi yako mwenyew imekusaliti.?unaweza kufanya kitu badae ukabaki unajiraum,huu ni usaliti wa nafsi..hakuna rafiki wa kweli. wala rafiki muongo wote ni marafiki,ukimsikia mtu anakwambia flani ni rafiki yangu wa ukweli,jua huyo mtu anajiongopa na anajaribu kuubadilisha ukweli halisi ulioko ndami kabsa ya neno "rafiki"rafiki ni neno conclusive ukiongeza maneno mengine hapo mbele hayo ni yako...
 
hivi mtu asiekupenda anaweza kuwa rafiki yako??? sio kila anaecheka na wewe ni rafiki. rafiki wa kweli lazima mpendane.

tatizo linakuja pale ambapo unashindwa kugundua kama rafiki yako ni mkweli au vip je anakupenda kweli au kwa machale??? kuna watu wanafiki sana huwezi jua kama kweli anakupenda kama rafiki kumbe ni adui yako mkubwa fanikiwa tu uone anavyofura
 
Usiamini nafsi yoyote hata nafsi yako pia itilie mashaka..!!kwani ni mara ngapi nafsi yako mwenyew imekusaliti.?unaweza kufanya kitu badae ukabaki unajiraum,huu ni usaliti wa nafsi..hakuna rafiki wa kweli. wala rafiki muongo wote ni marafiki,ukimsikia mtu anakwambia flani ni rafiki yangu wa ukweli,jua huyo mtu anajiongopa na anajaribu kuubadilisha ukweli halisi ulioko ndami kabsa ya neno "rafiki"rafiki ni neno conclusive ukiongeza maneno mengine hapo mbele hayo ni yako...

Ni kweli hata nafsi yako inaweza kusaliti lakini ni bora nafsi yako kuliko swahiba ulomwamin looo
 
kama kila mtu ni adui wa mtu basi kila rafiki ni rafiki wa mtu
 
Apolinary

Imeandikwa "jihadharini na wanadamu'.
Hii kitu imenikumbusha miaka ya nyuma rafiki A.alimdanganya rafiki B amtukane bosi wake baada ya kunywa pombe.
Rafiki B akafukuzwa kazi,Rafiki A akamshauri rafiki B kumuuuzia nyumba zake rafiki b akaziuza nyumba na mnunuzi ni rafiki A.
Mwishoni rafiki A alikuja kumuoa mke wa rafiki B na wana watoto wakubwa leo hii.
Rafiki B yuko uswazi ni mywa gongo.

N.B.
Rafiki B alikuwa ni Mkurugenzi wa Wizara na Bosi aliyetukanwa ni Waziri.

Rafiki B ni taahira, alistahili alichokipata!!
 
tatizo linakuja pale ambapo unashindwa kugundua kama rafiki yako ni mkweli au vip je anakupenda kweli au kwa machale??? kuna watu wanafiki sana huwezi jua kama kweli anakupenda kama rafiki kumbe ni adui yako mkubwa fanikiwa tu uone anavyofura

hilo ndio tatizo....sasa tunajidanganya tuna marafiki kumbe ni nyoka tu wanafiki wakubwa wamekuzunguka
 
Life is full of suprises... so natarajiaga chochote muda wowote toka kwa yeyote... mm si muumini wa urafiki ila nna watu kibao waweza sema marafiki la hasha ni watu tunajuana na tumezoeana... "rafiki" ni neno kamili na lenye uzito trust knw one
 
Tulifungua biashara ya wawili mimi na rafiki yangu, biashara ikawa inaenda vizuri sana, nikapata safari nikamuacha yeye aendelee kuisimamia, nikiwa safarini akanipigia simu ohhh, mwenye nyumba kapandisha kodi na anataka ianze kulipwa baada ya mkataba wa kwanza kwisha, na hapo bado wiki 2 kodi mpya ianze, nikamwambia lipa tu ,akadai kodi kubwa sana bora tufunge tutafute pengine nikamwambia kuliko kufunga lipa halafu tutafute pengine taratibu, akaniambia haya. Baadae ananiambia nilichelewa kumpa jibu akaniambia kesha pata mtu mwingine nimerudisha chumba, nikamwambia o.k. mara nimerudi kaja tupige hesabu tu kila mtu achukue hela yake mi nataka kubadili biashara nikachukua changu. Baada ya muda naambiwa yupo palepale na biashara anafanya ileile. Sikumuuliza lolote ni mwaka sasa tunasalimiana tunacheka lakini sijawahi kumuuliza kitu, kapata msiba nimeenda mpaka kwao kuzika, mwisho kamuuliza ndugu yake hivi huyu ananifikiriaje? MIe kuja kuulizwa nikasema kwani kafanya nini? Hanielewi na maisha yangu yanasonga. Usiamini rafiki kabisa.
 
Marafiki zangu wa ukweli ni familia yangu tu.Hao wengine ni viumbe naishi nao tu duniani.Believe me!
 
Yaani mabinadamu ni manafiki sana. Na huku mjini ndiko unafiki umezidi kwa kiwango cha juu kabisa.
Alafu binadamu wanalimisha wengne kuwa wanafiki.

Mf: uko nae anaongea mwisho wa maongezi unagundua ni unafiki so lazima na wewe uwemnafiki kwa kumjibu kinafiki.

Baada ya kugundua usanii wake.
 
Unajua sio rahisi kumtambua mtu kwa Mara ya kwanza unapokutana naye ila mnapoendelea unamjua tu na ukishamjua njia yako unaiweka mbali naye ama unaishi naye kinafiki nafiki. Ninao wengi tu namna hii tena huwa wanatabia nyingine. Ukinunua tuseme gari, pikipiki, baiskel ama chochote huwa na wana wivu sana na hawaachi kikuomba ukiwapa lazima ije imeharibika sehemu hawatengenezi ila kujiombesha msamaha sasa. Mie nimekwisha wagundua wakiniomba nawaambia mbovu naiendesha kimungu Mungu tu hao wanasepa. Wajinga sana kama mtu u m feel achana naye na cha kwake pia usishikee.

hakuna k2 kbya kama dhalau yan cpend kbxa
 
Back
Top Bottom