Marafiki wasiokupenda wako hivi

Marafiki wasiokupenda wako hivi

Alvin Slain

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
6,375
Reaction score
3,668
Habari za jukwaa hili.
Nadhani hamjambo kabisa.

Mara nyingi watu kwa maelfu hudhani kuwa na marafiki wenye mtizamo chanya,
lakini wengine huangukia katika kundi la marafiki wasio na upendo ndani yao.

Hizi ni baadhi ya ishara zitakazo kuonesha kuwa rafiki zako ni bora ama laa.


(1)Marafiki walio wanafiki mara nyingi hawatakualika katika shughuli yoyote watakayoifanya.

(2)Mtapiga picha ya pamoja iwe watu kumi na kuendelea lakini katika mitandao wataweka picha ambayo wewe haumo.

(3)Mara nyingi wanakufanya kuwa kichekesho kwao

(4)Ukiongea pointi za hali ya juu watacheka na hujui kwanini.

 
(5) watachukua mawazo yako iwe ya biashara au chochote chema na kufanya pasipo kukushirikisha
(6) watakuwa nawe wakati wa raha na kukukimbia( nduki) pindi unapohitaji msaada wao.

unadhani ni wangapi wanayajua haya?
 
Apolinary

Imeandikwa "jihadharini na wanadamu'.
Hii kitu imenikumbusha miaka ya nyuma rafiki A.alimdanganya rafiki B amtukane bosi wake baada ya kunywa pombe.
Rafiki B akafukuzwa kazi,Rafiki A akamshauri rafiki B kumuuuzia nyumba zake rafiki b akaziuza nyumba na mnunuzi ni rafiki A.
Mwishoni rafiki A alikuja kumuoa mke wa rafiki B na wana watoto wakubwa leo hii.
Rafiki B yuko uswazi ni mywa gongo.

N.B.
Rafiki B alikuwa ni Mkurugenzi wa Wizara na Bosi aliyetukanwa ni Waziri.
 
Last edited by a moderator:
Unajua sio rahisi kumtambua mtu kwa Mara ya kwanza unapokutana naye ila mnapoendelea unamjua tu na ukishamjua njia yako unaiweka mbali naye ama unaishi naye kinafiki nafiki. Ninao wengi tu namna hii tena huwa wanatabia nyingine. Ukinunua tuseme gari, pikipiki, baiskel ama chochote huwa na wana wivu sana na hawaachi kikuomba ukiwapa lazima ije imeharibika sehemu hawatengenezi ila kujiombesha msamaha sasa. Mie nimekwisha wagundua wakiniomba nawaambia mbovu naiendesha kimungu Mungu tu hao wanasepa. Wajinga sana kama mtu u m feel achana naye na cha kwake pia usishikee.
 
hivi mtu asiekupenda anaweza kuwa rafiki yako??? sio kila anaecheka na wewe ni rafiki. rafiki wa kweli lazima mpendane.
 
haiwezekani....wewe unamuona rafiki kwasababu anakuchekea sio rafiki huyo ni mnafiki tu mwisho wa siku utajua rangi zake halisi......phonebook yangu ina majina karibu 50 lakini hapo kuna marafiki watatu tu ingawa watu wa kunywa na kucheka nao wako zaidi ya 50

Ukitaka kuhakikisha angalia Facebook ndio utajua nini wanasema. Unakuta mtu alikuwa rafiki yako ila kwa sababu ya maisha mnapotezana Mara unakutana naye fb unamtumia friend request mwezi au miezi inapita unadhani labda huwa log in ila kukicha unakuta post zake ana respond kwa furaha unamtumia ujumbe hajibu ng'o nini unafanya mnaendelea kuchunguliana tu. Una marafiki 100 ila unakuta wanakoment au Ku like ni Wawili tu wengine wanapita tu. Unafiki huu.
 
Ukitaka kuhakikisha angalia Facebook ndio utajua nini wanasema. Unakuta mtu alikuwa rafiki yako ila kwa sababu ya maisha mnapotezana Mara unakutana naye fb unamtumia friend request mwezi au miezi inapita unadhani labda huwa log in ila kukicha unakuta post zake ana respond kwa furaha unamtumia ujumbe hajibu ng'o nini unafanya mnaendelea kuchunguliana tu. Una marafiki 100 ila unakuta wanakoment au Ku like ni Wawili tu wengine wanapita tu. Unafiki huu.

kupotezana kupo,majukumu na mambo kama hayo.....lakini rafiki yako, i mean RAFIKI YAKO afanye harusi ya mwanae au yake mwenyewe asikualike? mkae sehemu akufanye kichekesho?[according to this thread] huyo sio rafiki.... ila kama mnazungumzia 'rafiki' zenu wa facebook sawa.
 
Apolinary

Imeandikwa "jihadharini na wanadamu'.
Hii kitu imenikumbusha miaka ya nyuma rafiki A.alimdanganya rafiki B amtukane bosi wake baada ya kunywa pombe.
Rafiki B akafukuzwa kazi,Rafiki A akamshauri rafiki B kumuuuzia nyumba zake rafiki b akaziuza nyumba na mnunuzi ni rafiki A.
Mwishoni rafiki A alikuja kumuoa mke wa rafiki B na wana watoto wakubwa leo hii.
Rafiki B yuko uswazi ni mywa gongo.

N.B.
Rafiki B alikuwa ni Mkurugenzi wa Wizara na Bosi aliyetukanwa ni Waziri.

bora anakunywa gongo nilidhani alijinyonga.
 
Mpaka nazeeka sasa sinaga hiyo kitu marafiki , sijui BFF Akuuu nina Wafanyakazi wenzangu mwisho Getini , Nina Marafiki mwisho FB kukumbiasha vya shule na chuo tu , nina marafiki wasiojulikana kwenye Mitandao ya Kijamii kama hii Full stop !
 
Ukitaka kuhakikisha angalia Facebook ndio utajua nini wanasema. Unakuta mtu alikuwa rafiki yako ila kwa sababu ya maisha mnapotezana Mara unakutana naye fb unamtumia friend request mwezi au miezi inapita unadhani labda huwa log in ila kukicha unakuta post zake ana respond kwa furaha unamtumia ujumbe hajibu ng'o nini unafanya mnaendelea kuchunguliana tu. Una marafiki 100 ila unakuta wanakoment au Ku like ni Wawili tu wengine wanapita tu. Unafiki huu.

Unaongea ukweli kabisa.
Mimi mwenyewe Fb nina Marafiki Elf tano na ninaowajua ni kama hamsini tu.
Cha kushangaza wale ninawajua hatakoment hawalike wanaolike na coment ni wale nisiowajua huku wale ninawajua nikiwaona Online.
 
Mpaka nazeeka sasa sinaga hiyo kitu marafiki , sijui BFF Akuuu nina Wafanyakazi wenzangu mwisho Getini , Nina Marafiki mwisho FB kukumbiasha vya shule na chuo tu , nina marafiki wasiojulikana kwenye Mitandao ya Kijamii kama hii Full stop !

Ina maana hata sim yako haina contact za watu?
 
Mpaka nazeeka sasa sinaga hiyo kitu marafiki , sijui BFF Akuuu nina Wafanyakazi wenzangu mwisho Getini , Nina Marafiki mwisho FB kukumbiasha vya shule na chuo tu , nina marafiki wasiojulikana kwenye Mitandao ya Kijamii kama hii Full stop !

sure hii iko njema
 
Back
Top Bottom