Marafiki wana msaada kuliko ndugu

Marafiki wana msaada kuliko ndugu

Uongo ,marafiki watakuwepo kama wananufaika au wana mategemeo ya kunufaika na wewe,
Ndugu atakiwa na wewe kwa hali zote,kuwa makini hakuna watu wanafki kama marafiki
Kiujumla ndugu ni muhimu kuliko rafiki bt linapokuja suala la utafutaji na michongo ya kazi marafiki wanajitoa sana kuliko ndugu na ndo nilichokusudia kwenye mada yangu.
 
ndugu zetu ni marafiki wa watu wengine ko wanawasaidia pia

hata sisi ni ndugu wa nduguzetu ko tuna tabia za kibwege pia

ndugu atabaki kuwa ndugu hasa kwenye nyakati ngumu mno za magonjwa na vifo

marafiki wapo kwa nyakati za raha na vishida vidogo vidogo, wenye husimama na wewe kwenye shida kubwa ni wale marafiki ambao tumesha kuwa ndugu nao.
Mjadara ufungwe.
 
Kuna huu mfano nilisimliwa nikiwa mdogo. Kwamba jamaa mmoja alitaka kujua ndugu yake na rafiki nani anaweza kuwa naye wakati wa shida. Hivyo, siku moja alimchinja mbuzi, kisha akamfunika shuka jeupe. Ilipofika usiku, akaenda kwa rafiki yake, akamwambia "nimeua mtu na naogopa muda wowote naweza kukamatwa. Akamwambia kwamba anamwomba waende kuvuta mwili ya yule sliyeuliwa na kuutupa porini ili polisi wasije wakamhusisha kwamba amemuua mtu." Baada ya kusikiliza simulizi zima, rafiki yake akaona hiyo ni murder case, hivyo akishiriki kuvuta kwenda kumficha porini, mambo yakifichuka naye atakuwa kwenye hatia. Kwa kuona hivyo, akamwambia huyo rafiki yake kwamba huo ni msalaba wake mwenyewe, asimwingize kwenye matatizo maana familia yake inategemea. Jamaa baada ya kuona hivyo, akaenda kwa ndugu yake (brother) akasimulia kisa kizima cha kuua kama alivyofanya kwa rafiki yake. Ndugu yake akamwambia hilo ni tatizo kubwa, na kwamba asingeweza kumwacha ndugu yake kwenye tatizo kama hilo alibebe peke yake. Hivyo, alikubali kwenda kumsaidia kuvuta maiti kwenda kutupa porini. Walipofika sehemu husika huyo ndugu mtu akafunua shuka na ndugu yake huyu akakuta siyo mtu, bali ni mbuzi. Yule aliyedai kamuua mtu akamwambia "sasa naamini damu ni nzito kuliko maji, na kwamba ndugu yako hawezi kukuacha uingie kwenye matatizo." Ni simulizi linalofikirisha, lakini halitoi jibu linalofanana kwa watu/ndugu wote.
Mwisho wakamla mbuzi!
 
Ndg kamwe siwezi mbeza pamoja na mapungufu yake mengi siwezi na siwezi kweli.
Moja ya vitu nilivyoona kwa mzee wangu ni kuishi na watoto wandugu zake.

Ikitokea umekufa na una watoto wadogo hakuna rafiki atakae wachukua watoto wako.
Bali watachukuliwa na ndg zako haijarishi watalelewa malezi mazuri au ya manyanyaso
yote hayo ni mapito yao ktk maisha.

Marafiki ni kweli tunasaidiana sana kwenye connection maana mara zote hatuogopani na pia hatuoneani kijicho
lkn kwenye shida kati ya marafi zako 10 unaweza baki na mmoja tu nae hataenda muda anakuacha.


Urafiki wa kweli kuwahi kutokea ni wa Daudi na Jonathani Mtoto wa mfalme sauli huu ndo nilishuhudia urafiki mzuri na mtamu kuwahi kutokea.
 
Salaam,

Watu wengi ukiwauliza juu ya michongo yao/mafanikio yao, watakuambia walipewa connection/support na marafiki zaidi kuliko ndugu.

Hata post za kazi zikitoka, ni rahisi sana kuona sim za marafiki zikimiminika kukujuza bt ni nadra kuona sim za ndugu.

Mungu wabariki marafiki popote walipo duniani.
Mara nyingi marafiki mnakuwa na common interests, ndugu ni kama kaskazini na kusini saa nyingine. Kwahiyo hata baadhi ya mambo huwezi kulaumu sana
 
Marafiki wanasolve issue za Maokoto subiri uwaze kuharisha utaona Kama kuna rafiki atasafisha uharo wako....🐒
Ukiwa na maokoto unaajiri wajuzi wa kuhudumia mgonjwa,choka mbaya uhudumiwa na ndugu huku wakisimangwa na kuombewa dua la kifo cha haraka.
Pesa inaratibu mambo mengi hapa duniani kuliko ndugu.
Maskini siku zote huwasubiria ndugu waumwe hili wawanange wanapowauguza.
 
Salaam,

Watu wengi ukiwauliza juu ya michongo yao/mafanikio yao, watakuambia walipewa connection/support na marafiki zaidi kuliko ndugu.

Hata post za kazi zikitoka, ni rahisi sana kuona sim za marafiki zikimiminika kukujuza bt ni nadra kuona sim za ndugu.

Mungu wabariki marafiki popote walipo duniani.
Wewe ulishalikoroga huko umeanza lawama.

Hao wanaoitwa amarafiki ni bado tu hawajaonja joto lako la jiwe.

Mnaharibu mahusiano kwenye familia zenu wenyewe baadae mnaanza kulalamika wanapowaacha na ujeuri wenu.
 
Punguza matarajio mkuu,kila mtu ana hali anayoipitia na hana majibu,usiweke imani na nguvu zako kwa binaadam, maana wao hubadilika pasipo taarifa.
Uko sahihi.

Shida ya watu wengi wanataka wakishapata hizi miambili miambili wanatarajia waabudiwe na kupigiwa magoti.

Mambo yanapoenda kinyume wananza kuona ndugu ni wabaya.
 
Back
Top Bottom