Marafiki wana msaada kuliko ndugu

Marafiki wana msaada kuliko ndugu

Salaam,

Watu wengi ukiwauliza juu ya michongo yao/mafanikio yao, watakuambia walipewa connection/support na marafiki zaidi kuliko ndugu.

Hata post za kazi zikitoka, ni rahisi sana kuona sim za marafiki zikimiminika kukujuza bt ni nadra kuona sim za ndugu.

Mungu wabariki marafiki popote walipo duniani.
Ukipigwa na JIWE FATUMA ndio utakumbuka msemo wa NYUMBANI NI NYUMBANI ,marafiki ni uhusiano fulani wa bandia uliokamatwa na nyakati nzuri nzuri za maokoto,undugu upo ukiwa hai na ukiwa mfu hata kama undugu haukupi hela
 
Ndo angekua na akili timamu angereason pia kwanini ipo hivyo.... na sio kuja kwa entitlement as if yeye kuna ndugu kibao amewabeba
Kutofautiana mitizamo ktk mambo ni jambo la kawaida hivo hakuna haja ya kutumia maneno makali ktk kuwasilisha mitizamo yetu.
 
Uko sahihi mkuu,mfano Mimi mjomba wangu alitaka nimsaidie biashara zake,kweli tumeenda miaka4 siioni Faida kwangu,mbali tuu na kupata uzoefu na kula.Nikajiongeza kusoma C.B.E _Dodoma huko nikakutana na jamaa anafanya kazi kampuni flani nzuri Katika kuzoeana akawa rafiki yangu mkubwa!Kazi zikatoka wa kwanza kunitafuta ilikuwa Mimi Ahsante rafiki,Sasa Nina wajukuu.
Wewe umesaidiaje ndugu zako baada ya kupata kazi? Au nawe ndio ndugu washenzi? Miaka minne kwa uncle wako huoni ni msaada? Acheni kueneza ujinga
 
Tatizo la marafiki uwepo wao ni wa muda tu.

Undugu hauishi Kamwe.

Watu wanaopoteza madaraka na fedha watakusimulia vizuri kuhusiana na marafiki.
Mada ilijikita zaidi kutambua mchango wao na si uwepo wao wa muda.

Wanaopoteza madaraka na fedha pia ukiwauliza kuhusu mchango wa marafiki ktk mafanikio yao pia watakueleza.
 
Mada ilijikita zaidi kutambua mchango wao na si uwepo wao wa muda.

Wanaopoteza madaraka na fedha pia ukiwauliza kuhusu mchango wa marafiki ktk mafanikio yao pia watakueleza.
Unapost halafu unatupangia cha kujibu??

Si ungeliacha hili jambo libakie kwako kuliko kushirikisha watu??
 
Back
Top Bottom